Tanzania Daima lamshambulia Zitto?

PICHA SI TATIZO: TATIZO SIASA ZA ZITTO za 'opportunism and facemongerism' - siasa za uuza sura ambazo CDM si mahali pake. CDM ni hoja kwa hoja, hoja kwa hoja ...

SIASA za 'gizani' ambazo zimefanywa na wanamtandao tangu miaka ya 1970 ndizo zimeifikisha nchi hii hapa ilipo: PABAYA, MBELE HAIENDI NYUMA HAIRUDI. MTANDAO ulianzisha siasa za gizani kwa sababu moja kuu, nayo ni kwamba NDANI YA CCM kwa kufuata utaratibu wa chama mafisadi hawa hawakuwa na nafasi ya kupata uongozi wa juu. WAO WANAMTANDAO wakaliona hilo, wakabuni mbinu (1) siasa za pesa tena chafu, na (2) publicity, vyombo vya habari kuwatangaza kwamba wao ndio wakombozi, messiah, wetu. KUMBE PUUUUUUUUUUU. WATANZANIA walipokuja kuwagundua mambo yakawa yameisha, wako IKULU.

SASA KWA BAHATI NZURI AU MBAYA MH. ZITTO nae anakabiliwa na mazingira yaleyale yaliyokuwa yakiwakabili WANAMTANDAO, nae ameamua kutumia mbinu zilezile zilizotumiwa na WANAMTANDAO, na yeye ZITTO ameongeza mbinu nyingine CHAFU ZAIDI (kwani ni bidhaa inayogombaniwa na wajinga wengi) ya kwamba ANAONEWA ndani ya CDM, na silaha yake ni eti kwa kuwa ni 'muislamu' na ni 'maarufu'. Gazeti LISIPOMTANGAZA anavyotaka yeye KWAKE LIMETANGAZA vita. KWA TARATIBU ndani ya CDM ZITTO 'si mzito' kama yeye anavyofikiri, siyo kwamba anabaniwa ila kuna 'VICHWA' zaidi yake. KWA MFANO alipokuwa MBUNGE 2005 - 2010 ALIKUWA maarufu kama pop star MICHAEL JACKSON, na sababu ni kwamba, alikuwa peke yake kijana (akisaidiwa na vijana wengine kwa kweli kama MDEE) upande wa CDM na alikuwa na hiyo platform BUNGE. SASA vijana ni wengi BUNGENI na wengi wao kwa uwezo wako mbali sana, wanamzidi. KUPAMBANA NA HILO ZITTO ameanzisha siasa mpya tofauti na alizozifanya 2005 - 2010, kwamba anachukua MSIMAMO wake binafsi tofauti na ule wa chama CDM. KWA MFANO CDM inakuwa na hoja na wabunge wao wanajipanga kwa pamoja kwamba, nani kati yao je, ni MH. MNYIKA au TUNDU au MDEE au MSIKA au ZITTO nk atayesimama kupambana na CCM na SERIKALI YAO. Sasa hapa ndipo tatizo kwa ZITTO anapochaguliwa MH mwingine, yeye atasimama na msimamo wake, na hapa sasa ndipo matatizo yanapoanzia KWA CDM kwani lazima MBUNGE wa namna hiyo ashughulikiwe (lakini kwa silaha ya ZITTO ya uislamu CDM wanajikuta mikono yao imefungwa kwa kiasi fulani).

MIMI napenda kushauri (1) KUWA WANANCHI WATAMBUE KUWA watu wa namna hii wapo wengi kwenye siasa (angalia siasa za KENYA); (2) CDM iongeze juhudi za kutambua 'true characters' za watu wao na 'watu WALIO NYUMA YAO'; (3) hizo characters zioneshwe wazi kwa wananchi ili watu hao WATAKAPOCHUKULIWA HATUA madhara kwa chama yawe madogo; na (4) lazima chama kiendelee kuwalea na kuwaonya vijana kama akina ZITTO kwani wanaamini kuwa wao ni maarufu sana, kitu ambacho siyo kweli, ili waweze KUZINGATIA MSIMAMO wa CHAMA: kama kila mtu atafanya kile anachoona yeye kinafaa, basi chama hakitakuwepo. CHAMA ni msimamo wa pamoja, kama imeamuliwa na CHAMA kwa vikao halali ambamo mhusika alishiriki na kujenga hoja zake ambazo hazikuungwa mkono, basi hana namna bali ni kuunga mkono msimamo wa CHAMA la siyo njia nyeupeeeeeeeeeeeeeeee.

haumjui Zitto wewe,unajaribu kumfananisha zitto na hao watoto wachanga!!udini unauingiza ww na wala sio Zitto..kakojoe ukalale hauna jipya zaidi ya majungu na wivu kwa kijana Zitto.
 
Cha maana ni mchango wa Zitto kwenye future ya chadema siyo kwenye past! Watu hawaoni ile vibrance ya Zitto ya kuichana CCM hadharani! Pia kwenye eneo la uenezi wa chama amejitenga sana! Kwamfano Arusha pamoja na kuwa kitovu cha hamasa ya chadema nchini hajawahi kufika kuwatia moyo wanachama wa Arusha! Mimi Zitto nashindwa kumwamini siku hizi! Halafu inaniuma maana ni Jembe letu chadema!

zitto ataenda vipi Arusha wakati chama hawamuweki kwenye ratiba wala kumpa bajeti,Anayepewa bajeti ni Slaa,Mbowe na akina Lema.Zitto hata akijaribu kuomba bajeti wanamuambia chama hakina ele na akitumia pesa zake wanamuambia anaenda kutengeneza mtandao.
 
Kiujumla zito ni mnafiki na nikiongezi pekee nisiyependa cdm na huku nyanda ya juu kusini akipewa nafasi yoyote ile kat ya uwenyekt,ukatbu au uraisi wengi 2taamia chama kngne
 
Gazeti la The Guardian on Sunday pia lilishamwandika vibaya Zitto kuwa ana maslahi kwenye kampuni za madini lakini naona aliamua kukaa kimya maana waandikaji wengine wana headings za kuuvutia halafu mashiko kwenye makala hakuna wala ushahidi wala mantiki.
Picha mnayosema imepigwa na JOSEPH SENGA.
Ni imani yangu kuwa maneno MARAFIKI WA KWELI ni ya kisanii au kimaigizo zaiiidi.
Hata hivyo siku zote JK ana kicheko/tabasamu usoni hata kama hali ni mbaya.
Tena Marehemu Samora Machel amewahi kusema kuzungumza wala kula na adui siyo tatizo.Tatizo ni iwapo utalala na adui.Naamini Zitto hatafanya kosa la kulala na adui au kulala adui akabaki macho kwa maana falsafa ya Samora
 
Mwandishi amesema Marafiki wa Kweli sio Kufa na Kufaana ndio maana naona mleta mada ni mchonganishi
 
SEMA, sasa wewe unayemjua tuambie hicho unachokijua, mbona hujakisema unaishia kutukana. NIKO 'LANDMARK room namba 205' UBUNGO njoo nikukojolee

haumjui Zitto wewe,unajaribu kumfananisha zitto na hao watoto wachanga!!udini unauingiza ww na wala sio Zitto..kakojoe ukalale hauna jipya zaidi ya majungu na wivu kwa kijana Zitto.
 
Hoja hapa si kushirikiana mageuzi1992 bali maneno yaliyoandikwa chini ya Picha ya Zitto na Kikwete. Kama gazeti limeandika hivyo kusudio lao ni nini? Ina maana kama Slaa na Kikwete wangepiga picha hiyo maneno yangekuwa ni hayo hayo?

Naomba kuuliza,kipi cha ajabu Zitto kusemwa ni rafiki wa Kikwete?

Kama ni hivyo hatuitaji kubishana ila kuhakiki maneno yaliyoandikwa na kujua undani wake.

Malumbano yatatutoa nje ya ukweli.urafiki si dhambi,dhambi ni what do they share in common,hicho ndicho kinachoumiza.
 
Last edited by a moderator:
Maandamano ya wabunge wa CDM kupinga ushindi wa JK Zito alichomoa. Kabla yake JK alimteua huyu dogo kwenye kamati ya madini, Mei Mosi JK anaonyesha kufurahishwa na kazi ya Zitto bungeni kushinikiza WM apigiwe kura ya kutokuwa na imani, sasa Zitto kaenda ikulu kupata ghahawa wakati JK akiapisha timu yake....could these be the right dots to connect about JK-ZK friendship? If so should we be concerned that Zitto might be dancing to JK's tune while disguised? Just thinking loud!
 
Wanajaribu kumrudisha kwenye mstari

Wazee wa Chadema Na Bi.Shida Kabwe wameshindwa
 
Ccm tumeshawaelekezea KIBLA, 2015, tunawachinjilia mbali...
 
Hold on a minute; yaani muda wote huu watu wamekwazwa na nini picha? caption ya picha inasemaje maana hadi hivi sasa naona watu wana project their own fear, illusions, and passions kwenye picha. Binafsi nadhani picha inasema mengi kuhusu Kikwete kuliko Zitto.. think about it.
 
Tz daima ukiisoma kati kati ya mistari utagundua kitu.
Kuna watu ambao huwa iko hasi nao tu hata wafanyeje, nitaanza kuchunguza kama na Zito ni miongoni mwao.
 
Kama ulivyosema Zitto mwenyewe "ni kichwa", basi ujue hata yeye anaelewa vizuri sana kwamba hakuna mwanachama wa CHADEMA aliye maarufu zaidi ya chama. Kwa kifupi ni kwamba hakuna mwanachama au kiongozi wa CHADEMA - kuanzia mwenyekiti hadi kwenye "kapeti" - asiyejua kwamba nje ya chama hana umaarufu wowote - hata waliofanya kazi kubwa kukijenga kufikia kilipo hawana jeuri hiyo. Kama umekisoma hicho chama kwa makini, utagundua kuwa hakuna mwenye ubavu wa kutoka akategemea kuendelea bila kutetereka. Ni tofauti kabisa na CCM ambako ukitoka chati inapanda!
acha ubwege wewe zitto ni maarufu zaidi ya cdm.umaarufu wa slaa unashuka na zitto anaendelea kupanda kuanzia bungeni hadi uraini..huyo mbowe yupo pale kwa nguvu aliyonayo MTEI unless zitto would b a chairman
 
Naomba kuuliza,kipi cha ajabu Zitto kusemwa ni rafiki wa Kikwete?

Kama ni hivyo hatuitaji kubishana ila kuhakiki maneno yaliyoandikwa na kujua undani wake.

Malumbano yatatutoa nje ya ukweli.urafiki si dhambi,dhambi ni what do they share in common,hicho ndicho kinachoumiza.
Kufa kufaana. Ni ukweli usiopingika kuwa Zitto hapatani na Mbowe na Dr. Slaa kisiasa. Matter of fact, ni yeye anayeongoza hoja za CDM bungeni. Wengine wapowapo tu.
 
Siamini kama una ufinyu wa fikra kushindwa kuelewa dhamira ya mwandish kuweka habari kama hiyo tena frontpage,na usitawaliwe na ushabiki wa kupenda watu wako na cjui kama ni kigezo cha ukanda ama la wajua mwenyewe!tunaelewa propaganda inayofanzika na viongoz wa chadema kwa roho zao mbaya za ubaguzi ni kummaliza ZITTO kisiasa wanatumia muda mwingi ila nyota ya ZITTO hakuna mwenye kuweza kuifunika!dr. Slaa alienda kigoma na akaendesha kampen za kisirisiri ili ZITTO Akose ubunge na tulijua hilo wanakigoma walimpuuza na kumuona mbaguzi hata kura wakamnyima,tunaelewa wanakaskazin wote hawampendi zitto sababu ya umaarufu wake kuliko mwanachama yeyote ndani ya chadema na ndo kiongoz pekee mwenye sura ya kitaifa,mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni,
 
wote wanaopinga mada hiyo sio kuwa wana ufinyu wa fikra wanajua maana ya kuwekwa habari hiyo ni ajenda ya kumbomoa ZITTO kisiasa,ambayo inaendeshwa na uongozi wa chadema tena kwa makusudi kwa dhambi yao ya ubaguzi tu,dr. Slaa alithubutu hadi kuendesha kampen mbovu alipofika kigoma kutaka ZITTO Akose urais ila habari hizo tulizigundua na wanakigoma hawakutaka hata kumpa kura,sidhan kama chadema kuna mtu ana uwezo kama ZITTO!katufanza vijana weng tuamini katika siasa jitaidin kuthamin mchango wake,ndomana leo ukienda kaskazin hawamtaki ZITTO wanamwita msaliti kwa ujinga na propaganda za haya magazeti yanayotumwa na MBOWE kwa makusudi mazima,mnyonge mnyongen lakin haki yake mpeni
 
Back
Top Bottom