Tanzania Daima hamuitendei haki JamiiForums

JoJiPoJi

JF-Expert Member
Aug 8, 2009
2,907
3,261
Mara nyingi vyombo mbalimbali vya habari vimekuwa vikitegemea kupata habari kutoka hapa JF na kwa lugha nyingine wamekuwa wakifanya biashara ya kuuza habari ambayo tunazileta hapa bila idhini ya wamiliki wa habari husika.
Kwenye gazeti la Tanzania Daima la leo ukurasa wa mbele kuna habari “viongozi chadema kuhujumiwa” hii habari bila shaka ilijadiliwa hapa kwa kirefu sana, ila leo inatumika kuuza gazeti, inasikitisha, basi wahariri hata wangetumia busara kusema chanzo cha habari yao ni JamiiForums ili angalau hata kijijini ambako hawajui jamii forums waanze kutafuta na kujua ni nini, habari zetu mchukue bure basi mtusaidie kututangaza
 
Hakuna tatizo. Wamesaidia ujumbe uwafikie Watanzania wengi. Natamani kama magezeti na redio station zote wangechukua habari hapa jf ili ziwafikie Wananchi wengi.
 
Sioni shida maana wana grounds za kujitetea bado, kwamba wamesoma hiyo habari hapa then wakaanza uchunguzi wao wa kina kujua kinachoendelea..then ndo waka publish.
Pili, hili suala la kutumia majina anonymously .....linaweza kukufanya uhisi kwamba Tanzania daima wame copy and paste...kumbe muanzisha thread ni mwandishi wa Tanzania Daima.
 
Wanazidi kuipandisha chati! mimi niliifahami jamiiforum kupitia gazeti la Raia mwema. uzuri waliuwa wanasema jf ndio chanzo cha habari yao!
 
Mara nyingi vyombo mbalimbali vya habari vimekuwa vikitegemea kupata habari kutoka hapa JF na kwa lugha nyingine wamekuwa wakifanya biashara ya kuuza habari ambayo tunazileta hapa bila idhini ya wamiliki wa habari husika.
Kwenye gazeti la Tanzania Daima la leo ukurasa wa mbele kuna habari "viongozi chadema kuhujumiwa" hii habari bila shaka ilijadiliwa hapa kwa kirefu sana, ila leo inatumika kuuza gazeti, inasikitisha, basi wahariri hata wangetumia busara kusema chanzo cha habari yao ni JamiiForums ili angalau hata kijijini ambako hawajui jamii forums waanze kutafuta na kujua ni nini, habari zetu mchukue bure basi mtusaidie kututangaza
Je wewe unajuaje aliyeileta ndokaandika kwenye hilo gazeti???Think twice before provoke some one or something!!
 
Je wewe unajuaje aliyeileta ndokaandika kwenye hilo gazeti???Think twice before provoke some one or something!!

Naona hauelewi, hata kama aliyeileta hiyo habari hapa hata kama ni mwandishi wa gazeti hilo, bado jf inaendelea kuwa chanzo cha habari yake na alitakiwa awaambie wasomaji kuwa chanzo cha habari yake ni JAMIIFORUMS, au haujui kuwa kila unachoandika hapa kinabaki kuwa mali ya JF
 
Wanazidi kuipandisha chati! mimi niliifahami jamiiforum kupitia gazeti la Raia mwema. uzuri waliuwa wanasema jf ndio chanzo cha habari yao!

Na hilo ndilo linatakiwa, licha yakuwa jamiiforums hawazuhii kutumika kwa habari zake ila ni busara pia kuwajulisha wananchi kuwa habari kwa hisani ya JamiiForums
 
Sioni shida maana wana grounds za kujitetea bado, kwamba wamesoma hiyo habari hapa then wakaanza uchunguzi wao wa kina kujua kinachoendelea..then ndo waka publish.
Pili, hili suala la kutumia majina anonymously .....linaweza kukufanya uhisi kwamba Tanzania daima wame copy and paste...kumbe muanzisha thread ni mwandishi wa Tanzania Daima.

Ndugu ninachoelewa kuwa kila kilichomo au kinachoanzishwa hapa JF kinabaki kuwa mali halali ya JamiiForums kisheria, sasa kama unahisi ukianzisha thread na baadae uiamishe unakuwa umetenda kosa kisheria
 
Umesoma disclaimer notice ya JF? Wanasema wao wala third parties hawatawajibika kwa info zozote zitakazoandikwa humu. Sasa iweje kuwe na contradiction na sheria unayoisema?

Ndugu ninachoelewa kuwa kila kilichomo au kinachoanzishwa hapa JF kinabaki kuwa mali halali ya JamiiForums kisheria, sasa kama unahisi ukianzisha thread na baadae uiamishe unakuwa umetenda kosa kisheria
 
Unaweza kuita ukurasa wa maoni ya wasomaji katika gazeti "chanzo cha habari?". Jamii Forumns ni shirika la habari? Hiyo ni mosi. Pili ni kwamba huyo mtu aliyeleta "habari" hapa na kisha habari hiyo ikatoka gazetini amelalamilka? Kama hajalalamika kinakuudhi kitu gani?

Tuaaandika hapa kwa dhumuni la kuwafikishia wananchi wenzetu wengi maoni yetu, na hata wakati mwingine kuwapa kile tunachoona ni "habari". Kama kuna magazeti yanasaidia kusambaza kwa wengi zaidi basi hilo halina noma. Si lazima watutaje. Kwani tuko hapa kutafuta sifa?

Hongera Tanzania Daima. Tafadhali mtusaidie kusambaza zaidi mada zetu, ili tuiendeleze nchi yetu.
 
Naona hauelewi, hata kama aliyeileta hiyo habari hapa hata kama ni mwandishi wa gazeti hilo, bado jf inaendelea kuwa chanzo cha habari yake na alitakiwa awaambie wasomaji kuwa chanzo cha habari yake ni JAMIIFORUMS, au haujui kuwa kila unachoandika hapa kinabaki kuwa mali ya JF
Yani habari yake mwenyewe aombe rukusa??
 
Je wewe unajuaje aliyeileta ndokaandika kwenye hilo gazeti???Think twice before provoke some one or something!!

Unamwambia mwenzio 'think twice' wakati wewe mwenyewe huja-think twice! Kwa utaratibu wa haki miliki, hata kama ni wewe umeleta humu, basi sema imetoka JF ambako uliipeleka wewe kama sio kwamba chochote kinachoingia JF basi copyright ni ya JF.
 
Je wewe unajuaje aliyeileta ndokaandika kwenye hilo gazeti???Think twice before provoke some one or something!!

In the academic world, every fact must be cited and that is why you have authors referencing their old works in new ones (by mentioning name of the author-their name and year of publication). Tz daima were supposed to acknowledge the source of information regardless of whether the author is the same in all works.
 
Kwa vyovyo vile, Tz daima au mtu yeyote anayechukua habari kutoka JF anatakiwa kusema kuwa chanzo ni JF kama ambavyo wana-JF wamekuwa wakitaja vyanzo vyao!

Najua wanasaidia kutangaza habari hizo na kufikisha ujumbe kwa watu wengi zaidi, ila kama wangekuwa wametaja JF, kuna watu wengi zaidi wangevutiwa kuona original news na hata kuchangia!
 
Mimi nafikiri ni jambo jema kwa vyombo vingine vya habari kuiga Tanzania Daima sababu si Watanzania wote wanaoweza ku-access jamiiforum na ukjihabarisha,na ni vyema tukatambua kuwa wanajamiiforum ujitolea kwa kutafuta habari mbalimbali kwa vyanzo vyao na kuzileta jammiiforum ili umma wa Watanzania uhabarike,hata habari ya January Makamba na Barrick ingewafikia watanzania wengi kama ingetolewa kwenye magazeti ingawa hata hapa kwenye forum hatuioni tena.
 
JF ni zaidi ya HABARI...tutake tusitake watakuja na kuchukua habari tunazopost..
Ila kiungwana kama wamachukua humu ndani inabidi waseme..
 
Mara nyingi vyombo mbalimbali vya habari vimekuwa vikitegemea kupata habari kutoka hapa JF na kwa lugha nyingine wamekuwa wakifanya biashara ya kuuza habari ambayo tunazileta hapa bila idhini ya wamiliki wa habari husika.
Kwenye gazeti la Tanzania Daima la leo ukurasa wa mbele kuna habari “viongozi chadema kuhujumiwa” hii habari bila shaka ilijadiliwa hapa kwa kirefu sana, ila leo inatumika kuuza gazeti, inasikitisha, basi wahariri hata wangetumia busara kusema chanzo cha habari yao ni JamiiForums ili angalau hata kijijini ambako hawajui jamii forums waanze kutafuta na kujua ni nini, habari zetu mchukue bure basi mtusaidie kututangaza

Unajuaje kama aliyeleta hii habari hapa anauhisiano na Tanzania Daima?
 
JF ni zaidi ya HABARI...tutake tusitake watakuja na kuchukua habari tunazopost..
Ila kiungwana kama wamachukua humu ndani inabidi waseme..

Hilo ndili suala la muhimu ambalo binafsi naliona. Hata kama JF ni free access, si sawa mtu kukomba kitu hapa JF na kusambaza kana kwamba yeye ndiye source!

Unajuaje kama aliyeleta hii habari hapa anauhisiano na Tanzania Daima?

Inawezekana sana, ila kama hii habari ilitoka kwanza hapa JF kabla ya TZ daima, basi walitakiwa kusema hivyo ili waache kujichukulia ownership ya kitu ambacho tayari kiko kwenye public domain! Ndiiyo maana hata sisi (wana JF) tukichukua habari kutoka kwingine tunawajibika (sana sana morally and for credibility purposes) kuweka source ya habari tunazobandika hapa!

Kibiashara ni haki jf ilipwe huo ndo ukweli na wawe wanataja kuwa chanzo ni jf

Hili nadhani ni jambo jingine tena jipya.....Sina hakika kama JF imeweka vifungu vya kisheria ambavyo vinaiwezesha kudai malipo. Hata hivyo kuna sheria za free online documents ambazo inabidi sasa JF ianze kuziangalia kwa makini!

Hivi nikiweka hapa copywrite materials nani anawajibika?
 
Mara nyingi vyombo mbalimbali vya habari vimekuwa vikitegemea kupata habari kutoka hapa JF na kwa lugha nyingine wamekuwa wakifanya biashara ya kuuza habari ambayo tunazileta hapa bila idhini ya wamiliki wa habari husika.
Kwenye gazeti la Tanzania Daima la leo ukurasa wa mbele kuna habari "viongozi chadema kuhujumiwa" hii habari bila shaka ilijadiliwa hapa kwa kirefu sana, ila leo inatumika kuuza gazeti, inasikitisha, basi wahariri hata wangetumia busara kusema chanzo cha habari yao ni JamiiForums ili angalau hata kijijini ambako hawajui jamii forums waanze kutafuta na kujua ni nini, habari zetu mchukue bure basi mtusaidie kututangaza
Mkuu bahati mbaya humu hatujuani nani ni nani lakini kuna waandishi au kuna watu wenye uhusiano na waandhi wa habari si Tanzania daima tu hutusaidia kupata news na sisi kuzileta hapa sasa ukisema eti wasizitumie utakuwa unakosema......
 
Back
Top Bottom