Tanzania Constitution - (Swahili & English Versions)

Soma ukurasa wa 36
Kinga dhidi ya mashataka ya
na madai Sheria ya 1984
Na.15 ib.9 Sheria ya 1992
Na.20 ib…


(3) Isipokuwa kama ataacha kushika madaraka ya Rais
kutokana na masharti ya ibara ya 46A(10), itakuwa ni marufuku
kumshtaki au kufungua mahakamani shauri lolote la jinai au la
kumdai mtu aliyekuwa anashika madaraka ya Rais baada ya
kuacha madaraka hayo kutokana na jambo lolote alilofanya yeye
kama Rais wakati alipokuwa bado anashika madaraka ya Rais
kwa mujibu wa Katiba hii.

Kuna haja ya kuongeza kipengele kifuatacho

(4) Isipokuwa kama ataacha kushika madaraka ya Rais
kutokana na masharti ya ibara ya 46A(10), Raisi mstaafu atashtakiwa mahakamani itakapobainika kwamba alitumia madaraka kinyume na majukumu ya Uraisi, hususani katika maeneo yafuatayo:
(a) kwamba, alitumia madaraka yake kuhujumu utajiri wa Taifa
(b) kwamba, alitumia madaraka yake kuchochea aina zote za dhuluma, vitisho, ubaguzi,rushwa, uonevu au upendeleo
(c) kwamba, kwa kutumia madaraka yake, aliendesha shughuli za uchumi kwa njia zinazoweza kusababisha ulimbikizaji wa mali au njia kuu za uchumi katika mamlaka ya watu wachache
 
Kumbe watu wanaogopa mijadala pasua kichwa! Katiba ndiyo hii na kila siku tunalalamika kwamba ubovu wa katiba hii ndiyo chanzo cha nchi hii kuongozwa kibabaishaji,sasa kwa nini watu wemekimbia kujadili badala yake wote tumebakia kutumbua macho na kumwachia mwanamalundi peke yake kazi nzito kama hii?

Nilitegema kumuona Mzee Mwanakijiji na Mwafrika wa Kike wakimwaga sera hapa, lakini naona hoi..........

Au wanajiandaa kuja kuichambua zaidi, manake kila siku katiba ibadilishwe, Viongozi hivi mara vile, JK hivi, bunge vile na kadha wa kadha. Katiba hii hapa sasa, kwisha habari.

Big up MWANAMALUNDI.
 
Ukurasa wa 12, Utekelezaji wa shughuli za
Mamlaka ya Nchi Sheria ya 1984, Na.15 ib.6





Mahakama haziwezi kutoa haki chini ya mwamvuli wa idara za serikali. Kwa kifupi, hakuna uhuru wa mahakama hapa.

Mwanangu hili jiwe zito! Mi kwa sasa siwezi kufanya uchambuzi wa kina mpaka nikae chini ila nafuatilia.

Ninavyoelewa nguzo za nchi ni Executive (Serikali), Legislature (Bunge) na Judiciary (Mahakama)

Nguzo hizi tatu zinatakiwa kufanyiana "checks and balance" kwa kutotegemeana.Sasa kama Mahakama ni idara ya serikali kama ilivyo idara ya uhamiaji, majaji watawaadibisha vipi marais na mawaziri? Mbona kunakuwa na conundrum hapa kwamba idara hii inakwenda Wizara gani? au sehemu gani? Majaji na Waziri wa Wizara yenye Idara hii (kama iko chini ya Wizara) nani anakuwa mkubwa?

Kama hamna Wizara mbona inaonekana kama majaji wanakuwa chini ya executive badala ya kuwa independent katika judiciary?

Hiyo nyingine kuhusu immunity kila mtu anayejua sheria Tanzania anasema immunity siyo blatant na katiba imeeleza wazi kama ulivyopigia mstari hapo juu.
 
Nadhani vipingere kama hivi ambavyo vinahusu siasa au itikadi ya vyama ni lazima kuondolewa.

Ujenzi wa Ujamaa na Kujitegemea Sheria ya 1984 Na.15 ib.6 Sheria Na.4 ya 1992 ib.6

9. Lengo la Katiba hii ni kuwezesha ujenzi wa Jamhuri ya Muungano na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar au wa chochote kati ya vyombo vyake na udugu na amani kutokana na kufuata siasa ya Ujamaa na Kujitegemea, amabyo inasisitiza utekelezaji wa misingi ya kijamaa kwa kuzingatia mazingira yaliyomo katika Jamhuri ya Muungano. Kwa hiyo, Mamlaka ya Nchi na vyombo vyake vyote vinawajibika kuelekeza sera na
shughuli zake zote katika lengo la kuhakikisha:
  • ) kwamba utu na haki nyinginezo zote za binadamu zinaheshimiwa na kuthaminiwa;
  • ) kwamba sheria za nchi zinalindwa na kutekelezwa;
  • ) kwamba shughuli za Serikali zinatekelezwa kwa njia ambazo zitahakikisha kwamba utajiri wa Taifa unaendelezwa, unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya wananchi wote kwa jumla na pia kuzuia mtu kumyonya mtu mwingine;
  • )kwamba maendeleo ya uchumi wa Taifa yanakuzwana kupangwa kwa ulinganifu na kwa pamoja;
  • ) kwamba kila mtu mwenye uwezo wa kufanya kazi anafanya kazi, na kazi maana yake ni shughuli yoyote ya halali inayompatia mtu riziki yake;
  • ) kwamba heshima ya binadamu nahifadhiwa na kudumishwa kwa kufuata Kanuni za Tangazo la Dunia kuhusu Haki za Binadamu;
  • ) kwamba Serikali na vyombo vyake vyote vya umma vinatoa nafasi zilizo sawa kwa raia wote, wake kwa waume, bila ya kujali rangi, kabila, dini au hali ya mtu;
  • ) kwamba aina zote za dhuluma, vitisho, ubaguzi, rushwa, uonevu au upendeleo inaondolewa nchini;
  • ) kwamba matumizi ya utajiri wa Taifa yanatilia mkazo maendeleo ya wananchi na hasa zaidi yanaelekezwa kwenye jitihada ya kuondosha umaskini, ujinga na maradhi;
  • ) kwamba shughuli za uchumi haziendeshwi kwa njia zinazoweza kusababisha ulimbikizaji wa mali au njia kuu za uchumi katika mamlaka ya watu wachache binafsi;
  • ) kwamba nchi inatawaliwa kwa kufuata misingi ya demokrasia na ujamaa.
 
ukurasa 89,Mamlaka ya Mahakama Maalum ya Katiba Sheria
ya 1979 Na.14
ib.9
na Sheria ya
1984 Na.15
ib.36


126.-(1) Kazi pekee ya Mahakama Maalum ya Katiba ya
Jamhuri ya Muungano ni kusikiliza shauri lililotolewa mbele yake,
kutoa uamuzi wa usuluhishi, juu ya suala lolote linalohusika na

tafsiri ya Katiba hii iwapo tafsiri hiyo au utekelezaji wake
unabishaniwa kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano na
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Then...,

(2) Katika kutekeleza kazi yake kwa mujibu wa masharti ya
ibara hii, Mahakama Maalum ya Katiba haitakuwa na mamlaka
ya kuchunguza au kubadilisha uamuzi wa Mahakama Kuu au
uamuzi wa Mahakama ya Rufani
uliotolewa kwa mujibu wa
masharti ya ibara ya 83 ya Katiba hii au uamuzi wa Mahakama
ya Rufani uliotolewa kwa mujibu wa ibara ya 117 ya Katiba hii.

Sasa kuna haja gani ya kuwa na Mahakama ya katiba isiyo na mamlaka ya kubadilisha maamuzi ya mahakama kuu/rufani???Haya ni matumizi mabaya ya pesa za wananchi. Hakuna haja ya hii mahakama. Hii mahakama ni redundant!!!
 
Ukurasa wa 104

(3) Itakuwa ni marufuku kwa mwanajeshi yeyote kujiunga na
chama chohote cha siasa, isipokuwa tu kama atakuwa na haki
ya kupiga kura iliyotajwa katika ibara ya 5 ya Katiba hii.

Inapingana na Sheria ya Na.4 ya 1992 ib.8 Sheria ya 2000 Na.3 ib.5

(2) Ni marufuku kwa sheria yoyote iliyotungwa na mamlaka
yoyote katika Jamhuri ya Muungano kuweka sharti lolote ambalo
ni la ubaguzi ama wa dhahiri au kwa taathira yake.
 
Baraza la Mawaziri Sheria ya 1984 Na.15
ibara 9
Sheria Na.4
ya 1992 ib…
Sheria Na.34
ya 1994 ibara
12


54.-(1) Kutakuwa na Baraza la Mawaziri ambalo wajumbe
wake watakuwa ni Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Rais wa
Zanzibar na Mawaziri wote

Kuna haja ya kuongeza kipengele kinachotaja idadi ya mawaziri na wizara husika. Maana kinachoendelea sasa hivi ni vituko. Raisi anaunda wizara ya uvuvi???
 
Soma ukurasa, 29
Utekelezaji wa kazi na shughuli za
Rais, n.k
Sheria ya 1984 Na.15
ib.9
Sheria ya 1992Na.4 ib …
Na.20
ib.12,
Sheria yua
1994 Na.34 ib
.

(5) Endapo kiti cha Rais kitakuwa wazi kutokana na Rais
kufariki dunia, kujiuzulu, kupoteza sifa za uchaguzi au kutomudu
kazi zake kutokana na maradhi ya mwili au kushindwa
kutekeleza kazi na shughuli za Rais, basi Makamu wa Rais
ataapishwa na atakuwa Rais kwa muda uliobaki katika kipindi
cha miaka mitano
na kwa masharti yaliyoelezwa katika ibara ya
40, kisha baada ya kushauriana na chama cha siasa anachotoka
Rais atapendekeza jina la mtu atakae kuwa Makamu wa Rais na
uteuzi huo utathibitishwa na Bunge kwa kura zisizopungua
asilimia hamsini ya Wabunge wote.

Swali: Kama makamu wa Raisi hajafikisha umri wa miaka 40 itakuwaje? Maana katiba hii hii inasema mtu yeyote hawezi kugombea urais kama hajafikisha umri wa miaka 40. Kwa hivi, miaka 40, pamoja na sifa nyingine ndivyo hasa vigezo vya raia wa Tanzania kukalia kiti cha urais.

Suala la umri ni la kibaguzi. Tunaomba liondolewe. Raia mwenye umri wa miaka 90 ana haki ya kuwa raisi, wakati mwenye miaka 38 anapoteza haki ya kuwa rais. Hii haijakaa sawa hata kidogo.Hiki kipengele kifutwe.
 
Hiyo nyingine kuhusu immunity kila mtu anayejua sheria Tanzania anasema immunity siyo blatant na katiba imeeleza wazi kama ulivyopigia mstari hapo juu.

Mkuu, hicho kipengele hakimo ndani ya katiba. Nimependekeza hayo marekebisho.
 
TANZANIA: KEY HISTORICAL AND CONSTITUTIONAL DEVELOPMENTS


From 1961 at the time of her independence up to 1977, when she got her permanent Constitution, Tanzania had 5 new constitutions namely; the Independence Constitution 1961,The Republican Constitution 1962, The Interim Constitution of the United Republic of Tanganyika and Zanzibar 1964, The Interim Constitution 1965, and the permanent Constitution of the united Republic of Tanzania of 1977.

1958: United Tanganyika Party (UTP) was formed

1958: African National Congress was formed

1961: Independence Constitution of Tanzania:

- was based on the West Minister model except that it had no bill of rights.

- provided for a Governor General representing the Queen as the Head of

State; an executive prime minister from the majority party in parliament; a cabinet of ministers collectively an individually responsible to parliament and an independent judiciary.

1962: The Republican Constitution of Tanzania marked the beginning of the presidential system and lay a foundation for “ imperial presidency”, in that it combined in the president the powers of head of state and government and all the previous powers of the Governor General and prime minister. He was Head of State and head of government, commander in Chief of the army and part of parliament, without whose assent a bill would never become law. He appointed ministers and the Vice President, and chaired cabinet.

-The collective and individual responsibility of ministers shifted from the national assembly to the president. Parliament could not impeach the President though the President could under certain circumstances dissolve parliament.

The president inherited all the powers of the governor by the colonial legislation such as the Deportation Ordinance, the Collective Punishment Ordinance, the Emergency Powers Order in Council to which the independent government added its own repressive laws such as the notorious Preventive Detention Act, which gave the president powers to detain a person without trial.

An existing national assembly which converted to a constituent assembly by an Act of parliament passed the new Republican Constitution. The 71 elected members of the national assembly, all elected members of TANU passed a law that allowed them to convert the national assembly into a constituent assembly with powers to adopt the new constitution. The procedure sided lined people and thus lacked political legitimacy or force of law from the people.

1964: The Union Constitution between Zanzibar and Tanganyika was a modification of the Republic Constitution of 1962.

The Union was constituted by signing of a treaty called the Articles of Union by the respective heads of state Mwalimu Nyerere and Karume. It was ratified by the respective legislative bodies and became part of the municipal law called the Acts of Union. Main features of the Acts of Union were the following:

- The Acts of Union were a constitutional instrument controlling both the Union and Zanzibar Constitutions.

- They established a 2-government Union . 11 items were placed under the jurisdiction of the Union legislature and executive and remained matters under the exclusive jurisdiction of the Zanzibar government. The Union executive was to operate in Zanzibar in relation to union matters through the Zanzibar president who by virtue of his position was also vice president of the Union.

- The Acts provided for a procedure for the adoption of a permanent constitution through the appointment of a constitutional commission followed by a constituent assembly, in order to allow some people participation in the making of the Union. Unfortunately the one-year period that was specified in the original articles came to some 13 years, when a constitutional commission and Constituent assembly were formed albeit in a fashion that almost sidelined people participation. The people have never had opportunity to debate the needs, structure and division of power of the union.

1964: The Interim Constitution of the United Republic of Tanganyika and Zanzibar (The Third Constitution of Tanzania)

It was a modification of the Republican Constitution and renamed by presidential decree. This presidential authority to make the constitutional changes was derived from the Acts of Union. It was never passed by a constituent assembly but was adopted like an ordinary act of parliament. This constitution laid the foundation for the two-government union.



1965: The Interim Constitution 1965: formalized the one party state and re-enacted all changes brought about by the Union. The Constitution declared the Afro-Shirazi the party for Zanzibar and TANU for Tanganyika. The Constitution of TANU was made a schedule to the Constitution thus legally endorsing the emergence of a party state. The 1965 Constitution was enacted by an ordinary Act of parliament an equivalent of an amendment of the Constitution repealing an existing Constitution and establishing a new one. It was yet another example of lack of constitutionalism and participation of the people.

1965-1977: Several amendments were made to the Interim Constitution before the permanent Constitution was adopted. Notable were 2 amendments.

- There was an increase in the number of matters under the jurisdiction of the Union government, which led to further constriction of the autonomy of Zanzibar.

- The second amendment was the consolidation of one party state and the undermining of the National Assembly in favour of the National Executive Committee of the Party. The 1975 amendment (Act 8 of 1975) for instance declared the supremacy of the party by providing that all functions of the all state organs were to be performed under the auspices of the party, a formalisation of what had already happened de facto.

-The 1977 Permanent Constitution / The Fourth Constitution concentrated state power in the executive within the party state under an imperial presidency it was made with no public debate or consultation. It for the first time recognized the monopoly of politics vested in the CCM, which by then emerged as single party in the whole union. The 1977 constitution rests on the 3 pillars namely imperial presidency, the two-union government and the one party state.

5 February 1977: The two existing political parties Tanganyika Africa National Union (TANU) and Afro Shirazi Party (ASP) merged to form Chama Cha Mapinduzi (CCM)

16 March 1977: After the merger of the TANU on the mainland and ASP in Zanzibar; the President of the United Republic of Tanzania appointed a 20-person joint party committee headed by Thabit Kombo to propose a new constitution. The same party Committee was appointed as the constitutional commission in accordance with the Acts of Union on March 25, 1977. It within a short time made and sent proposals to the NEC of the party, which adopted them in a day, in camera.

16 March 1977: The president appointed the Constituent Assembly was on the same day as the Committee, to discuss and enact the new constitution. The bill for the new constitution was published 7 days before the Constituent assembly met to discuss it and the constituent assembly enacted the Constitution in 3 hours after it was presented to it.

Amendments of the 1977 Constitution: The Fifth Constitutional amendment as an exception to the rule. This 1983-4 constitutional debate was a fine example of public participation in constitution making because it was initiated by the NEC of CCM contrary to the usual practice where the NEC made decisions and asked government to implement them. Secondly, contrary to previous practice, a public debate on the party’s proposals was invited and a year assigned for the purpose. Thirdly although having a bill of rights had not been part of the proposals, it was included as a result of public demand. The debate was therefore the only one of its kind in the constitutional history of Tanzania. As a result of the debate there demands for more autonomy of Zanzibar which threatened the party and led to announcing a “ pollution of political atmosphere forcing the then leadership of Zanzibar to resign.

1985: Mwalimu Julius Nyerere stepped down voluntarily as Head of State of Tanzania and Ali Hassan Mwinyi succeeded him as Head of State.

1990: Salmin Amour replaced Abdul Wakil as President of Zanzibar and 2nd Vice President of the Union

February 1991: The Presidential Commission on Single Party or Multiparty System in Tanzania, 1991 popularly known as the Nyalali Commission, was established by President Mwinyi

March 1991: The Nyalali Commission was inaugurated. It was constituted of 22 Commissioners, with equal membership of ten members each from both the Mainland and the islands, and one Chairperson and a Vice Chairperson. Its main terms of reference were to collect people’s views on whether Tanzania should continue with the Single Party System or adopt a Multi-party system.

1992: the Nyalali commission made recommendations to amend both the Union and Zanzibar Constitutions, to make the whole of Tanzania a multi-party state.

The Eight Constitutional Amendment of 1992 paved way for a multi party political system, following the recommendation of the Nyalali Commission to adopt multipartism. The constitutional amendment changed the composition of the National Assembly, which consisted of elected members. Women representatives who were 15% of the total membership were to be appointed by their parties. There were to be 5 members elected from the Zanzibari House of Representatives from among themselves. The National Electoral Commission members were to be appointed by the President. Instead of being a member of CCM as before, parliamentary and presidential candidates could be nominated by any registered party, which meant that independent candidates could not stand for elections any more. Matters to do with the registration of political parties were added on the list of Union matters making them 22.

The Ninth Constitutional Amendment came six months later. It provided for the election of the president and his removal by way of impeachment. It also provided for post of prime minister and the passing of a vote of no confidence in him by the National Assembly.

The Eleventh Constitutional Amendment addressed the issue of vice –president, following the report of the Bomani Committee. The system of running mate was introduced that paired a presidential and vice- presidential candidate. This meant that the President of Zanzibar ceased being an automatic Vice president of the Union but became a member of the Union cabinet.

The Twelfth Constitutional Amendment 1995 was passed before parliament was dissolved before the October 1995 general elections. It declares the president of the Union, and the President of Zanzibar as the Vice President of the Union and the Prime Minister prime leaders required to take oath to defend, protect and nurture the union.

1995: Ali Hassan Mwinyi stepped down as Head of State having constitutionally completed two terms in office and Benjamin William Mkapa was elected as Head of State.

October 29, 1995: first presidential and parliamentary elections under multiparty system, 13 political parties contested.

November 1995: After irregularities at some polling station, National Election Commission of Tanzania annulled the election vote in seven Dar es salaam constituencies and arranged for a re-run.

November 13, 1995: Ten opposition parties announced a boycott of the repeat elections and all opposition presidential candidates withdrew.

November 17, 1995: A re-run of the elections took place and CCM emerged victor with 75% of the vote.

1998: the Union President appointed a 16 member Committee led by Justice Kisanga to look at the Union Constitution and make necessary recommendations.

April 2000: The Thirteenth Constitutional Amendment

It introduced the following changes:

- Prior, a candidate needed 50% of votes in presidential elections to be declared president of the United Republic; only a simple majority was required to be declared president

- Before, the President had no power to nominate any body to parliament all members of parliament except the Attorney General, women in special seats and representatives of the Zanzibar House, were elected form constituencies. The Constitutional amendment allowed the President to nominate up to 10 members of parliament

- Increased the number of special seats fro women from 15%- 20%, depending on the declaration of the National Electoral Commission from time to time, with the consent of the president

Hogera Mkuu lakini umesahau kuweka tarehe ya uhuru wa Zanzibar na tarehe ya Mapinduzi matukufu ya 64.
 
Mnahitaji kuipata sheria ya mabadiliko ya 14 ya Katiba.

Nafikiri hili jambo kwa sasa ndiyo wakati wake muafaka kuletwa mbele ya meza, na si hayo mabadiliko 14 pekee na ikiwezekana na mengineyo yaliyotokea hivi karibuni.
kuna hoja ya Mbatia kwamba mawaziri kikatiba ni lazima watokane na wabunge, lakini inakuwaje bunge linapovunjwa mawaziri wanaendelea na nyazifa zao?

Pia kuna utata wa kikatiba ambao kwa mazoea Rais ameendelea kuwa madarakani hata baada ya bunge kuvunjwa wakati katiba inatamka kwamba anatakiwa kujiuzulu bunge linapovunjwa, hebu tujadiliane na mwanakijiji naomba utuletee hayo mabadiliko 14.
 
Hiyo 13th Amendment iliwekwa baada ya kuona kibano cha Mrema mwaka 1995 -- kulikuwapo hatari kubwa kwa Mkapa kutopata zaidi ya 50% ya kura zote safi na hivyo uchaguzi wa Rais kurudiwa kwa wagombea wawili wa juu. Ili baadaye kusiwepo wasiwasi huu ndiyo maana serikali ya CCM ikaleta hiyo requirement ya simple majority tu, na kuifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi chache sana katika Afrika (kama siyo pekee) kutokuwa na re-rerun ya kura ya rais iwapo mgombea hapati over 50%.

Wakati sisi tulianza na ulazima wa 50% or more kwa mshindi, jirani zetu Kenya walianza na hiyo simple majority requirement katika uchaguzi wao wa vyama vingi mwaka 1992 (ambapo Moi alishinda kwa kupata 35% tu ya kura zote.) Baadaye, wakati sisi huku tulipobadilisha na kuwa na simple majority, wenzetu Kenya wakabadili na kuwa na ulazima wa 50%! Tume-swap the requirement!!!

CCM inaogopa ulazima wa 50 % kwa sababu haijiamini kabisa mbele ya wapinzani -- mimi sioni sababu nyingine!
 
Hiyo 13th Amendment iliwekwa baada ya kuona kibano cha Mrema mwaka 1995 -- kulikuwapo hatari kubwa kwa Mkapa kutopata zaidi ya 50% ya kura zote safi na hivyo uchaguzi wa Rais kurudiwa kwa wagombea wawili wa juu. Ili baadaye kusiwepo wasiwasi huu ndiyo maana serikali ya CCM ikaleta hiyo requirement ya simple majority tu, na kuifanya Tanzania kuwa miongoni mwa nchi chache sana katika Afrika (kama siyo pekee) kutokuwa na re-rerun ya kura ya rais iwapo mgombea hapati over 50%.

Wakati sisi tulianza na ulazima wa 50% or more kwa mshindi, jirani zetu Kenya walianza na hiyo simple majority requirement katika uchaguzi wao wa vyama vingi mwaka 1992 (ambapo Moi alishinda kwa kupata 35% tu ya kura zote.) Baadaye, wakati sisi huku tulipobadilisha na kuwa na simple majority, wenzetu Kenya wakabadili na kuwa na ulazima wa 50%! Tume-swap the requirement!!!

CCM inaogopa ulazima wa 50 % kwa sababu haijiamini kabisa mbele ya wapinzani -- mimi sioni sababu nyingine!

Lakini hoja yangu hapa ni kwa nini sisi wanajamvi wa JF tuko keen sana kujadili matukio lakini hatuko makini kwenye kujadili kisababishi cha matukio yenyewe, yaani ubovu wa katiba yetu. Kwangu mimi CHADEMA,CCJ au CCM havina maana kama mfumo wa uendeshaji wa nchi yetu haujabadilishwa, na huwezi kubadilisha mfumo wa uendeshaji nchi kama katiba ya nchi haijabadilishwa!!
 
Mjadala umeanza rasmi....tuendelee bila kuacha mpaka tupate hii kitu mpya...bila hivyo tutaendelea na nyundo za kichwani na jembe la kuchimbia kaburi.
 
SEHEMU YA PILI
BARAZA LA MAPINDUZI LA ZANZIBAR
Baraza la Mapinduzi la
Zanzibar na kazi zake
105.-(1) Kutakuwa na Baraza la Mapinduzi la Zanzibar
litakalokuwa na wajumbe wafuatao:
(a) Mwenyekiti wa baraza la Mapinduzi;
(b) Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar;
(c) Mawaziri wote wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar;
(d) Wajumbe wengine watakaoteuliwa na Mwenyekiti wa
Baraza la Mapinduzi kwa mujibu wa masharti ya Katiba
ya Zanzibar.

KIPENGELE b) cha ibara 105(1) kimekiukwa na ndoa ya ccm na cuf kwa kufuta nafasi ya waziri kiongozi
 
Kuna umuhimu mkubwa sana kwa Waziri wa sheria na katiba Celina Kombani kuwa anajibu hoja za wana JF kuhusu katiba, asikae tu kutueleza kuwa hakuna umuhimu wa kuandika katiba kwa sasa, bali tuendelee kushonea viraka. CELINA please come out utueleze mapungufu yote haya ni kumkomoa nani. Au unasubiri mpaka tuandamane polisi watuue ndo mjue katiba mpya inahiatjika??
 
Itoshe kwangu kumshukuru aliyeleta hii hoja mezani, lakini pia nimshukuru Mwanamalundi kwa kazi nzuri ya uchambuzi. Angalau amenifunua kwa kiasi kikubwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom