Tanzania belongs to all Tanzanians

Mzalendo80

JF-Expert Member
Oct 30, 2010
2,508
1,338
Tanzania ni ya Watanzania sio ya CCM au chama chochote, kauli ya Nape aliyoitoa pale Manzese nakusema Tanzania inawenyewe na wenyewe ni CCM, He is wrong. Utawala wa kifisadi uliojaa rushwa na ukandamizaji wa Wanachi zidi ya utawala huo utafikia mwisho wake, kwani hakuna marefu yasio na ncha. Kwa muda mrefu sana tumewavumilia sana Mafisadi lakini sasa wanatuweka sisi Wananchi kwenye wakati mgumu wa kutovumilia tena. Vitendo vya kuuza rasilimali zetu kwa Wageni, kuingia mikataba feki ya 10% na kutuibia Kodi zetu kwa manufaa yao, tumeyavumilia sana, na wala wasituone tupo kimya wakadhani tunawaogopa. Sasa wameamua kuuza Ardhi yetu ambayo ndio nchi yenyewe hatutakivumilia tena ni bora kufa kutetea nchi yako kuliko kufa ukiwa mnafiki. Watanzania wenzangu Muda umefika wa kuungana pamoja bila ya kujali itikadi ya vyama au dini zetu ili tuweze kulikomboa hili taifa, watoto na wajukuu zetu waje walifaidi na Rasilimali zake. Watanzania Kama tusipo simama kidete kulikomboa hili taifa chini ya Utawala wa Kifisadi nani atatusimamia? Ifikie Mahala tusemeni sasa INATOSHA sio tunaburuzwa na Kundi lisilofika hata Watu 200.

Tanzania ni nchi yetu sote sio ya Mafisadi au Chama chochote bali ni ya Watanzania
 
Back
Top Bottom