Tanzania baada ya uchaguzi je ni kweli haitatawalika?

Mzee wa Rula

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
8,171
3,346
Uchaguzi wa urais na wabunge uliofanyika 31 Oct, 2010 umeiacha nchi yetu katika wakati mgumu sana. Hii ni kutokana na madonda yaliyozaliwa na MATOKEO ya uchaguzi huo ambao ulilalamikiwa sana na vyama vya upinzani, waangalizi wa kimataifa, NG'Os na wananchi kwa ujumla wakilalamikia ucheleweshwaji wa utangazwaji wa matokeo hususani maeneo ambayo upinzani ulikuwa na nguvu kidogo.
Nini hatma ya Tanzania yetu mara baada ya uchaguzi huu kwa kuangalia mlolongo wa matukio haya:-

  • Chama cha CDM kupinga kutomtambua JK na kisha baadae kumtambua kulivuta hisia kubwa kutokana na madai yao ambayo leo hii ndiyo dira ya madai ya katiba mpya. Madai yao ni tume huru ya uchaguzi, katiba ambayo imempa madaraka makubwa rais na wizi wa kura katika uchaguzi ambao CDM walisema wanaandaa ushahidi lakini walijua wazi ushahidi huo hauwasaidii chochote kwani sheria inabana kuhoji matokeo ya urais na chombo chochote kile.

  • Kutokana na hoja hapo juu ni kama CDM walikuwa kimya kama wanatunga sheria, sasa uchaguzi wa mameya umekuwa kama ni weak point ya kutoa duku duku lao. Waliandaa maandamo ambayo jeshi la polisi liliyazuia pasi kuangalia kuwa kuyazuia kulikuwa na gharama kubwa kuliko kutoyazuia. Athari ya maandamano hayo ndiyo msingi wa thread hii, kutokana na maneno ya Dr. Slaa kuwa tukitaka nchi hii isitawalike basi inawezekana na Ndesamburo alipokuwa anamwambia JK kuwa haujui vurugu zangu basi ngojea nianze.
Nijuavyo mimi Dr. Slaa ni mtu mweledi kutokana na taaluma yake hivyo endapo akitaka kusimamia maneno yake sijui hali itakuwaje maana nyuma ya kiongozi huyu kuna nguvu kubwa ya umma inayomsupport.

  • Ninatilia mashaka endapo nao CDM wataamua kuanza siasa ya maji machafu mf tu wakiandaa documentary yao nao inayothibitisha kuwa jeshi la polisi ni waongo maandamano yale yalikuwa halali ila kutumika kwao kisiasa ndiko kulikoletea hali ile nadhani yao itakubalika kuliko ya polisi, sasa nini kitajengeka hapo?

  • Kutokana na CCM kushindwa kuwajibishana kumeleteleza mambo mengi ambayo sasa wananchi wanayajua kwa msaada wa viongozi wa vyama vya upinzani, media n.k Mambo hayo ni UFISADI, AHADI ZISIZOTEKELEZEKA, KUTOWAJIBIKA KWA VIONGOZI, UKOSEFU WA VIPAUMBELE VYA TAIFA VYA KUELEWEKA hivi vyote vimetumiwa na vyama vya upinzani kuongeza joto la mabadiliko.

  • Sambamba na hili, migomo kila kona ambayo sasa CCM ina amini CDM ina mkono wake vinazidi kuichanganya serikali. Ni kama mtu anayewashwa mwili mzima hajui ajikune wapi aache wapi.
Mwana JF kutokana na haya ambayo ni machache kwa lengo la wewe nawe ujizie, je kwa picha hii na ile uliyonayo kichwani JE NCHI ITATAWALIKA KWA MIAKA 5 IJAYO?
Nawakilisha.

 
Nina mashaka sana kama inatawalika hata sasa. Watu hawana Imani na serikali hata kidogo ndiyo maana migomo kila kona kelele na vilio ambavyo hata hivyo hakuna wa kuvisikiliza. Rais ni kama amesafiri akaacha mji usio na mchunga!
 
Nchi iko stable na yoyote atakae kaidi amri ya wanausalama atapelekwa kwenye vyombo vya sheria, muache tabia ya kutisha wananchi na kusambaza chuki
 
Nchi iko stable na yoyote atakae kaidi amri ya wanausalama atapelekwa kwenye vyombo vya sheria, muache tabia ya kutisha wananchi na kusambaza chuki
Vyombo vya sheria? Unaona vilivyoshindwa kufanya kazi Tunisia? People power is supreme.
 
Tanzania haina raisi pia haina mawaziri leo ni siku ya saba wauza mafuta waitawala Tanzania na kuipa serikali masaa 24 je nchi haina watawala.

My take:
Kauli hii ya Dr Slaa nchi haitawaliki imetimia kwani usalama wa taifa umeshikiliwa na watu wachache tena wenye viburi. Mafuta ni kila kitu katika kuendesha nchi ktk viwanda, usafirishaji na shughuli zinginezo. Uhuru wa nchi yetu umewekwa rehani.

Nawasilisha
 
Jamani hawa watu nimewashtukia, Kumbe wanapokuwa kimya sana ujue wanaandaa uongo ili kuusambaza kwenye mitandao ya kompyuta. Walikuja na uongo kwamba MAFUTA, LUKU, NA GESI vingekuwa adimu, Jana wameibuka na uzushi mwingine tena kwamba Serikali ya Zanzibar inaandaa musuada wa Sheria ya kuwalinda familia za marais pale inapotokea Ma-rais hao wamepoteza maisha. Mambo ya kizushi tu ambayo hata mtoto mdogo anapuuza akiyasikia. Sasa sijui watakuja na lipi?

Sijui kama na ninyi mlishalishtukia hili?. WAKO WAPI akina Maziwa Majani ya Maboga? (a.k.a MNM), Jisu kubwa? (TL), Huyu mama wa kawe yupo?. utawasikia watakapoibuka, watakuja na maneno utafikiri wameokota mstu wa MBANDE. Zamani nilikuwa nawahusudu sana,ila baada ya kugundua mambo yao yanayowaweka mjini sina hamu nao tena.

Nitafanyakazi sana ili mkono wangu uende kinywani. "KILA MTU ATAUBEBA MZIGO WAKE MWENYEWE"
 
Jamani hawa watu nimewashtukia, Kumbe wanapokuwa kimya sana ujue wanaandaa uongo ili kuusambaza kwenye mitandao ya kompyuta. Walikuja na uongo kwamba MAFUTA, LUKU, NA GESI vingekuwa adimu, Jana wameibuka na uzushi mwingine tena kwamba Serikali ya Zanzibar inaandaa musuada wa Sheria ya kuwalinda familia za marais pale inapotokea Ma-rais hao wamepoteza maisha. Mambo ya kizushi tu ambayo hata mtoto mdogo anapuuza akiyasikia. Sasa sijui watakuja na lipi?

Sijui kama na ninyi mlishalishtukia hili?. WAKO WAPI akina Maziwa Majani ya Maboga? (a.k.a MNM), Jisu kubwa? (TL), Huyu mama wa kawe yupo?. utawasikia watakapoibuka, watakuja na maneno utafikiri wameokota mstu wa MBANDE. Zamani nilikuwa nawahusudu sana,ila baada ya kugundua mambo yao yanayowaweka mjini sina hamu nao tena.

Nitafanyakazi sana ili mkono wangu uende kinywani. "KILA MTU ATAUBEBA MZIGO WAKE MWENYEWE"

Karibu JF wewe ni kati ya wanachama waliojiunga wakati wa uchaguzi wa Igunga kuleta porojo hapa JF...sikuelewi unachoongea mawazo yako hayana tofauti na mtoto wa shule ya msingi,akili zako fupi na zembe kufikiri....nakuomba uje DODOMA nitakupa ofa ya kwenda Mirembe Hospital bure...
 
Join Date : 27th October 2011Posts : 9
Rep Power : 0

Umetumwa!
 
Je Hayo unayosema wanazusha yangetokea kweli ingekuaje? Au unataka wanyamazie yote yanayotokea just because umewashtukia?
Mwambie alekutuma kuwa kakosea nenda kadanganye watoto kindagarten.
Alosema Slaa Pale mwembeyanga nayo ni uzushi??
Alowasema Mdee Bungeni kuwa wamejitwalia ardhi kubwa kiulaghai huko moro ni uzushi???

Kama sio Chadema lini ungejua kuna mafisadi kwenu wewe?

Nakushauri rudi kajiandae upya halafu ndio ukadanganye tena ukadanganye kindergaten, na uqe makini wasikushtukie
 
Mara tu baada ya kumalizika uchaguzi Mkuu CDM walikuja sijui sera au tuseme mkakati wakizunguuka nchi nzima wakiwashawishi watanzania wasikubaliane na ushindi wa Dk Jakaya mrisho kikwete hasa walipokuwa pale Arusha, Slaa na Ndesa waliwachochea wanainchi wafanye vurugu waende wakawatoe watu waliokuwa wameshikiliwa na police, Leo naona hali ni shwari, Je wameshindwa mkakati wao huo au ndio CDM nao wanaelekea shimoni?
 
Slaa Na Ndesa hawakuchochea wananchi wafanye vurugu. Embu nukuu maneno yao walosema watu wafanye vurugu uyaweke hapa.
 
Chadema kwishney!
Slaa hana jipya.
Mbowe kajificha.
Zito tena ndio hivyo
Safari anahangaika kujibu ishu za udini ndani ya chadema.
Lisu anahangaika na kesi!
Kwa kifupi uongoz wote wa chadema upo upo tu!
 
We acha uongo,unaushahidi gani kua Ndesa na Slaa waliwachochea watu?Kama huna cha kupost ni vema ukakaa kimya.Mijitu mingine mi MASABURI sana.
 

Karibu JF wewe ni kati ya wanachama waliojiunga wakati wa uchaguzi wa Igunga kuleta porojo hapa JF...sikuelewi unachoongea mawazo yako hayana tofauti na mtoto wa shule ya msingi,akili zako fupi na zembe kufikiri....nakuomba uje DODOMA nitakupa ofa ya kwenda Mirembe Hospital bure...

Wewe uliojiunga wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mbona pumba tupu
 
we mnafiki kweli, kwani mswada inayokataliwa huko z'bar unahusu niniii! Sasa we unayegeuza ukweli kuwa uzushi, bila shaka we ni shoga.
 
Slaa Na Ndesa hawakuchochea wananchi wafanye vurugu. Embu nukuu maneno yao walosema watu wafanye vurugu uyaweke hapa.

Tutaakikisha nchi aitawaliki tena "Ndesamburo"

Nendeni mkavamie kituoni cha polisi muwalete hapa kina Lema na wenzake "A loser Dr.Slaa"
 
Mara tu baada ya kumalizika uchaguzi Mkuu CDM walikuja sijui sera au tuseme mkakati wakizunguuka nchi nzima wakiwashawishi watanzania wasikubaliane na ushindi wa Dk Jakaya mrisho kikwete hasa walipokuwa pale Arusha, Slaa na Ndesa waliwachochea wanainchi wafanye vurugu waende wakawatoe watu waliokuwa wameshikiliwa na police, Leo naona hali ni shwari, Je wameshindwa mkakati wao huo au ndio CDM nao wanaelekea shimoni?

kweli nimeamini cuf na ccm dugu moja.Wewe kwenye uchaguzi Igunga ulikuwa unaunga mkono Cuf
 
Back
Top Bottom