Tanzania: Adui yetu ni nani na tuna fursa gani za kumshinda? Tunamlenga au tunamkwepa?

Mkandara kila la kheri! Umefika wakati wa kutafsiri maneno kwa vitendo tangulia nasi twaja.. mie nasubiri Kitila akiwa Mwenyekiti tutakuwa wote.

Anyway back to the issue, ruzuku ni Saratani mbaya SANA inayomaliza vyama vya upinzani kidogo kidogo. CCM wanalijua hilo na wanalifanyia kazi kisawa sawa (rejea sakata la Mrema Vs Marando, Mrema Vs Lwekama, Mrema Vs Tado etc) na ukitafakari kwa undani utaona haya yaliyojadiliwa hapa Ujinga, upumbavu, ushamba, ujuha nk ni nadharia ambazo ukitaka kuziona kwa vitendo kinyang'anyiro cha ruzuku kitakupa jibu.

Mtego wenyewe upo pale kwenye sheria isiyo tambua muungano wa vyama, hivyo kama mtakubaliana kuungana ni kivyenu tume inatambua mgombea wa chama kimoja tu. Huko Chadema unakoenda waulize walipoiunga mkono CUF mwaka 2000 yaliwakuta yepi. Baya zaidi mbali na ruzuku kuna fitna ya viti maalum kwa kina mama, ambavyo navyo hugawiwa kulingana na viti vya kuchaguliwa ktk baraza la madiwani na Bunge. Kwa msingi huo kitendo cha kumuunga mkono mwenzio mbali na kumuongezea ruzuku bali pia kunamuongezea viti maalum.

Kwa msingi huo basi utaona suala zima la muungano limegubikwa na vipingamizi kadhaa wa kadhaa vya kisheria na vya kimaslahi, by the time wapinzani watakapogundua hili (walau kudai sheria ibadilike) CCM watakuwa washatawala kwa miongo kadhaa.
 
Safi kabisa ndugu wananchi wenzangu. Mjadala huu ni mzuri. Wakati tukiendelea kujadili ni vizuri tukatofautisha kati ya mambo ambayo tuna uhakika nayo na yale ambayo tunabuni katika kujaribu kutafuta majawabu ya matatizo tuliyo nayo, yaani hypotheses. Kwa maoni yangu dhana kwamba hata vyama vya upinzani vikipewa nafasi ya kutawala vitashindwa kwa sababu ni dhaifu ni hypothesis kwa sababu vyama vya upinzani havijawahi kupata nafasi ya kutawala tukaviona. Kwa hiyo kimsingi woga tulio nao ni woga wa jambo tusilolijua (fear of unknown).

Kwa maoni yangu pia mambo yafuatayo ni halisi na ya uhakika:
i)jambo ambalo tunauhakika nalo na ushahidi tunao ni ukweli kwamba CCM imeshindwa kufanya kazi ya kuleta maendeleo kama ilivyotarajiwa. Hili ni jambo ambalo hatubahatishi, tumeliona na tumelishuhudia kwa macho na akili zetu. Kwa hiyo hata kama vyama vya upinzani vingekuwa ni dhaifu, CCM inastahili kufukuzwa kazi kama adhabu ya kushindwa kutekeleza wajibu wake.
ii)Vyama vya upinzani vilivyopo bungeni vimethibitisha kupitia bajeti yao mbadala kuwa viongozi wa vyama hivi wana uwezo wa kufikiri na kubuni njia za kufanikisha maendeleo ya nchi yetu kwa ubora zaidi kuliko CCM. Maoni ya wananchi na wataalamu mbalimbali nchini mwetu na sisi wenyewe hapa JF yanathibitisha hivyo.
iii)Wananchi wa Tanzania ni woga wa mabadiliko. Hili linathibitishwa na ukweli kwamba 80% ya watu wetu walikataa mfumo wa vyama vingi. Kimsingi sisi ni woga wa mambo tusiyoyajua (fear of unkown)-this maybe good or bad, but that is our identity as a people and as a nation. Kwa hiyo tukiangalia kwa jicho la kihistoria na kimantiki tutagundua kwamba tatizo letu la wananchi walio wengi ni kuogopa mabadiliko in the first place. Ukweli ni kwamba ukiongea na watu wengi wenye nafasi zao ukiwauliza kwa nini hawajiunga na vyama vya upinzani-majibu wanayotoa sio udhaifu wa vyama vya upinzani-watakwambia wanaogopa kufukuzwa kazi, biashara zao kuyumba, n.k. Kwa hiyo at the end of the day uwoga na kukosa ujasiri ni jambo la msingi sana katika kutafakari sababu za wananchi kutoviunga mkono vyama vya upinzani.

Kwa wale wanaosema kuwa vyama vya upinzani havina uwezo kwa kigezo cha kuwa na viongozi wachache kwa kuangalia tu wale wanaoonekana majukwaani, naomba niwatoe wasiwasi katika mambo mawili muhimu:
a)Viongozi wa vyama nvya siasa wapo wengi. Kimsingi kila mwanachama wa chama cha siasa ana haki na wajibu wa kukamata uongozi wa chama na wa serikali. Kwa hiyo kweli kwamba wanauvuma zaidi baharini ni papa, lakini hii haimanishi kwamba samaki, nyangumi na viumbe wengine hawapo.
b)Tunapoongelea kubadilisha uongozi wa nchi hatusemi kwamba nchi itaanza upya. Tunachoongelea hapa ni kubadilisha sera za nchi na executive ikiwa na maana ya Rais na mawaziri wake pamoja na baadhi ya maofisa wakuu katika vyombo fulanifulani vya kiutawala. Kwa hiyo dola itabaki kuwa ile, majeshi yetu na maafisa wengi ni haohao, walimu ni haohao, maprofesa ni haohao, n.k. Kwa hiyo hoja kwamba hatujaona watu wengine katika vyama vya upinzani zaidi ya akina Zitto, n,k., haina uzito. Cha kujiuliza hapa ni kama tumeona falsafa na sera mbadala zilizotolewa na vyama upinzani. Nami jibu langu ni ndio. Ushahidi mojawapo, soma bajeti yao mbadala.
Two specific comments kwa Kyoma: Mosi, Maybe you are right kwamba wananchi wetu ni werevu wa kujua kwamba vyama vya upinzani hamnazo na hivyo havipaswi kuchaguliwa, of course hii nayo ni hypothesis. Kinachonishangaza mimi ni huu werevu wa kujua ubaya wa vyama upinzania tu halafu wasijue ule wa CCM! Kama wananchi kweli wana werevu huo kwamba vyama vya upinzani ni fake, naamini watakuwa na werevu huohuo wa kutambua kuwa CCM imewaangusha na inapaswa kuadhibiwa na kwa hivyo wangepaswa waikatae katika uchaguzi. Kwa kuendelea kukichagua chama ambacho kimewasaliti kwa kiwango chochote unachoweza kufikiria ni ujuha kama ambavyo Mzee Mwanakijiji katuelezea. Hapa tulipo CCM wanawatumia wananchi kama katapila, wananchi wakishamaliza kuchonga barabara wanawekwa pembeni kama vile katapila linavyofanywa na haliruhusiwi hata kupita katika barabara walilochonga wenyewe. Pili, mimi katika huu mjadala najaribu kuwa katika hali ya uhalisia wa mazingira yetu ya kisiasa. Kusema kuwa wananchi wa Tanzania wanaweza kuonesha nguvu yao nje ya vyama vya siasa ni nadharia kwa sababu mfumo wetu wa siasa unapitia katika vyama vya siasa. Hii inafanya hata mifano yako mizuri ya Marekani isiwe na uzito na relevance katika context yetu.

Narudia tena hoja yangu ya msingi kuwa: dhana ya kwamba vyama vya upinzani haviwezi ni nadharia (hypothesis) kwa sababu hatuna ushahidi huu kutokana na ukweli kwamba havijawahi kupewa nafasi vikathibitisha hivyo au vinginevyo. Lakini ni ukweli ulio bayana kwamba, pamoja na CCM kupewa nafasi tele za kuongoza nchi yetu, wameshindwa na kuwasaliti wananchi wetu na ushahidi wa hili upo tele kwa kuona, kusikia, kunusa na kugusa! Kama wananchi wetu kweli ni werevu hili peke yake linatosha kuwaadhibu CCM.

Mwisho,bwana Kyoma nikukumbushe kuwa wananchi wa Tanzania hawakuunga mkono TAA na baadaye TANU kwa sababu vyama hivi vilikuwa na uwezo au vilikuwa vikongwe; wananchi waliviunga mkono vyama hivi kwa sababu vyama hivi vilikuwa vinapigania uhuru ambacho ndicho kitu wananchi walikuwa wanakitaka. Kama wananchi wa Tanzania wa leo wana werevu wa kiwango cha wananchi wa kizazi cha uhuru wanawajibu wa kuviunga mkono vyama vya upinzani sio kwa sababu tu vinaweza, bali pia kwa sababu ni vyama hivi vinavyotetea maslahi yao dhidi ya waporaji katika CCM.

Nawatakieni usiku mwema.
 
Leo hii rasmi natangaza kuomba kadi ya Chadema!...
Mh. Freeman, Zitto, J.J.Mnyika, Mwanasisa naomba tuwasiliane!
Mkandara sina kuficha wala mpango wa kupitia mlango wa nyuma.Nataka kutiwa maji ya ubatizo..
Ila tu kumbukeni Mkandara nina sifa moja!.......BABU UBISHI!

Tupo pamoja 2010!


Karibu sana mkuu; hivi ndivyo tutakavyotekeleza haya tunayoyasema hapa. Twendeni uwanjani tukacheze ball, tushirki kuyabadilisha mawazo yetu kuwa sera za vyama hivi.
 
Safi kabisa ndugu wananchi wenzangu. Mjadala huu ni mzuri. Wakati tukiendelea kujadili ni vizuri tukatofautisha kati ya mambo ambayo tuna uhakika nayo na yale ambayo tunabuni katika kujaribu kutafuta majawabu ya matatizo tuliyo nayo, yaani hypotheses. Kwa maoni yangu dhana kwamba hata vyama vya upinzani vikipewa nafasi ya kutawala vitashindwa kwa sababu ni dhaifu ni hypothesis kwa sababu vyama vya upinzani havijawahi kupata nafasi ya kutawala tukaviona. Kwa hiyo kimsingi woga tulio nao ni woga wa jambo tusilolijua (fear of unknown). Kwa maoni yangu pia mambo yafuatayo ni halisi na ya uhakika:
i)jambo ambalo tunauhakika nalo na ushahidi tunao ni ukweli kwamba CCM imeshindwa kufanya kazi ya kuleta maendeleo kama ilivyotarajiwa. Hili ni jambo ambalo hatubahatishi, tumeliona na tumelishuhudia kwa macho na akili zetu. Kwa hiyo hata kama vyama vya upinzani vingekuwa ni dhaifu, CCM inastahili kufukuzwa kazi kama adhabu ya kushindwa kutekeleza wajibu wake.
ii)Vyama vya upinzani vilivyopo bungeni vimethibitisha kupitia bajeti yao mbadala kuwa viongozi wa vyama hivi wana uwezo wa kufikiri na kubuni njia za kufanikisha maendeleo ya nchi yetu kwa ubora zaidi kuliko CCM. Maoni ya wananchi na wataalamu mbalimbali nchini mwetu na sisi wenyewe hapa JF yanathibitisha hivyo.
iii)Wananchi wa Tanzania ni woga wa mabadiliko. Hili linathibitishwa na ukweli kwamba 80% ya watu wetu walikataa mfumo wa vyama vingi. Kimsingi sisi ni woga wa mambo tusiyoyajua (fear of unkown)-this maybe good or bad, but that is our identity as a people and as a nation. Kwa hiyo tukiangalia kwa jicho la kihistoria na kimantiki tutagundua kwamba tatizo letu la wananchi walio wengi ni kuogopa mabadiliko in the first place. Ukweli ni kwamba ukiongea na watu wengi wenye nafasi zao ukiwauliza kwa nini hawajiunga na vyama vya upinzani-majibu wanayotoa sio udhaifu wa vyama vya upinzani-watakwambia wanaogopa kufukuzwa kazi, biashara zao kuyumba, n.k. Kwa hiyo at the end of the day uwoga na kukosa ujasiri ni jambo la msingi sana katika kutafakari sababu za wananchi kutoviunga mkono vyama vya upinzani.

Kwa wale wanaosema kuwa vyama vya upinzani havina uwezo kwa kigezo cha kuwa na viongozi wachache kwa kuangalia tu wale wanaoonekana majukwaani, naomba niwatoe wasiwasi katika mambo mawili muhimu:
a)Viongozi wa vyama nvya siasa wapo wengi. Kimsingi kila mwanachama wa chama cha siasa ana haki na wajibu wa kukamata uongozi wa chama na wa serikali. Kwa hiyo kweli kwamba wanauvuma zaidi baharini ni papa, lakini hii haimanishi kwamba samaki, nyangumi na viumbe wengine hawapo.
b)Tunapoongelea kubadilisha uongozi wa nchi hatusemi kwamba nchi itaanza upya. Tunachoongelea hapa ni kubadilisha sera za nchi na executive ikiwa na maana ya Rais na mawaziri wake pamoja na baadhi ya maofisa wakuu katika vyombo fulanifulani vya kiutawala. Kwa hiyo dola itabaki kuwa ile, majeshi yetu na maafisa wengi ni haohao, walimu ni haohao, maprofesa ni haohao, n.k. Kwa hiyo hoja kwamba hatujaona watu wengine katika vyama vya upinzani zaidi ya akina Zitto, n,k., haina uzito. Cha kujiuliza hapa ni kama tumeona falsafa na sera mbadala zilizotolewa na vyama upinzani. Nami jibu langu ni ndio. Ushahidi mojawapo, soma bajeti yao mbadala.
Two specific comments kwa Kyoma: Mosi, Maybe you are right kwamba wananchi wetu ni werevu wa kujua kwamba vyama vya upinzani hamnazo na hivyo havipaswi kuchaguliwa, of course hii nayo ni hypothesis. Kinachonishangaza mimi ni huu werevu wa kujua ubaya wa vyama upinzania tu halafu wasijue ule wa CCM! Kama wananchi kweli wana werevu huo kwamba vyama vya upinzani ni fake, naamini watakuwa na werevu huohuo wa kutambua kuwa CCM imewaangusha na inapaswa kuadhibiwa na kwa hivyo wangepaswa waikatae katika uchaguzi. Kwa kuendelea kukichagua chama ambacho kimewasaliti kwa kiwango chochote unachoweza kufikiria ni ujuha kama ambavyo Mzee Mwanakijiji katuelezea. Hapa tulipo CCM wanawatumia wananchi kama katapila, wananchi wakishamaliza kuchonga barabara wanawekwa pembeni kama vile katapila linavyofanywa na haliruhusiwi hata kupita katika barabara walilochonga wenyewe. Pili, mimi katika huu mjadala najaribu kuwa katika hali ya uhalisia wa mazingira yetu ya kisiasa. Kusema kuwa wananchi wa Tanzania wanaweza kuonesha nguvu yao nje ya vyama vya siasa ni nadharia kwa sababu mfumo wetu wa siasa unapitia katika vyama vya siasa. Hii inafanya hata mifano yako mizuri ya Marekani isiwe na uzito na relevance katika context yetu.

Narudia tena hoja yangu ya msingi kuwa: dhana ya kwamba vyama vya upinzani haviwezi ni nadharia (hypothesis) kwa sababu hatuna ushahidi huu kutokana na ukweli kwamba havijawahi kupewa nafasi vikathibitisha hivyo au vinginevyo. Lakini ni ukweli ulio bayana kwamba, pamoja na CCM kupewa nafasi tele za kuongoza nchi yetu, wameshindwa na kuwasaliti wananchi wetu na ushahidi wa hili upo tele kwa kuona, kusikia, kunusa na kugusa! Kama wananchi wetu kweli ni werevu hili peke yake linatosha kuwaadhibu CCM.

Mwisho,bwana Kyoma nikukumbushe kuwa wananchi wa Tanzania hawakuunga mkono TAA na baadaye TANU kwa sababu vyama hivi vilikuwa na uwezo au vilikuwa vikongwe; wananchi waliviunga mkono vyama hivi kwa sababu vyama hivi vilikuwa vinapigania uhuru ambacho ndicho kitu wananchi walikuwa wanakitaka. Kama wananchi wa Tanzania wa leo wana werevu wa kiwango cha wananchi wa kizazi cha uhuru wanawajibu wa kuviunga mkono vyama vya upinzani sio kwa sababu tu vinaweza, bali pia kwa sababu ni vyama hivi vinavyotetea maslahi yao dhidi ya waporaji katika CCM.

Nawatakieni usiku mwema.

Touche! Hicho mimi ndio nimekuwa nikikisema siku zote. We can give the opposition a chance to show us what they got. If we are not impressed, we can bench them and bring back the old dog. But before we do that, they (the opposition) need to get it together first.
 
Leo hii rasmi natangaza kuomba kadi ya Chadema!...
Mh. Freeman, Zitto, J.J.Mnyika, Mwanasisa naomba tuwasiliane!
Mkandara sina kuficha wala mpango wa kupitia mlango wa nyuma.Nataka kutiwa maji ya ubatizo..
Ila tu kumbukeni Mkandara nina sifa moja!.......BABU UBISHI!

Tupo pamoja 2010!

Kupiga kura ni "Kutenda."

Sio sahihi kusema kwamba tuache maneno (tupu) kwa kujadili siasa humu bila ya kuchukua hatua ya vitendo kuyakamilisha hayo tunayoyajadili humu JF.

Tukumbuke pia kuwa "Mtendaji" kwenye mambo ya siasa si lazima mtu asimame jukwaani kwa kuomba kura za wananchi. Akina James Carville (Clinton campaign), Karl Rove (Bush 2004) n.k. wote walikuwa ni watendaji katika siasa.

Mkandara, usisahau kutafuta 'strategist' vinginevyo utakwama. Tunakutakia la kila kheri. Mmmmmh, lakini kweli CHADEMA Ujamaa wanaukubali?

Tukubaliane, katika ushabiki wa soka sio wote ni wachezaji. Mashabiki ni sehemu mhimu ya mchezo huo. Tusiwalaumu mashabiki kwa timu zetu kutofanya vizuri.
 
Kalamu,

Nimefikia uamuzi huu si kwa sababu ya kutafuta nafasi ya uongozi ndani ya Chadema. Elimu yangu ya madrasa haiwezi nipa nafasi hiyo wala sina kipaji cha uongozi zaidi ya kusimamia na kuongoza kikundi kidogo sana cha watu.

Nakwenda Chadema kwa sababu ya mada hii!... nimekuwa nikisita miaka hadi miaka kujitwika mzigo ambao sidhani kama nauweza. Lakini baada ya kutafakari sana na hasa kufikiria kuwa humu JF kuna vichwa sii mchezo ila kilichokosekana ni kuyaweka maneno yao ktk vitendo..

Kama nilivyosema Ubishi wangu utakuwa mtihani mkubwa kwa Chadema na viongozi wake, jambo ambalo binafsi nafikiri litakuwa na msaada mkubwa kwa chama kuweza kuona upande wa pili wanafikira gani. Trust me sii rahisi kabisa kutazama upande wa pili ktk sura (shilingi) ile ile. Waswahili husema:- Nyani hucheka makalio ya mwenzake!...Lakini huyo nyani hata kama atapewa Kioo kujitazama bado sii rahisi kuamini kuwa matakalio yale ni yake.

Chadema wanahitaji mtu wa pembeni lakini yumo ndani kuweza kuyaona makalio ya pande zote... kazi hiyo naiweza sana!...
Huyo Strategist ndio akina nyie ambao mnakaa pembeni kusubiri kualikwa matanga ya Kifo cha CCM. Karibu sana na naanza kabisa kutanguliza kuomba msaada wako!

Ndugu yangu nakuomba soma vizuri mada hii kisha fikiria! kweli wewe na elimu yako unasubiri nani? nani kweli atakayeweza leta mabadiliko Tanzania ikiwa sii wewe, jirani yako, mshikaji wako na wote humu ambao nyote mnaona UHURU wa Watanzania umebebwa na baadhi ya watu wachache kama vile ndio halali ya urithi wao!

Nchi imerudi ktk kutawaliwa, na sidhani kama hapo ulipo unaweza nambia tofauti ya Utawala huu hasa baada ya Marehemu Mwl. Nyerere kufa na Ule wa Mkoloni kama sio tofauti za rangi za watawala....How can you sleep at night!

Mimi nachukua kadi tu sintagombea nafasi yoyote zaidi ya kufuata maelekezo ya wenye mji! Nitaweza kufahamu zaidi jitihada zinazofanyika kuliko kubeba mzigo wa dhana na kuchuma madhambi!...hali wananchi wazee na vijana wetu wanalia kama vile Darfur!.. Darfur iko bongo mjomba kama unayo huruma kweli basi shika jembe leo.

Unajua ktk safari yangu bara Tanzania, niliona watu ktk kila hali ya maisha na kuna wakati nilikaa na kujiuliza How can these people (leaders) go to sleep after their Up country Tour?

Yaani kuna watu maisha yao yamerudi miaka 40 nyuma!.. kuna mabanda ndugu yangu yamejengwa na makaratasi ya plasitic na watu wanalala humo tena vitongoji vya mijini. Vijiji vingi vimebaki vitupu watu wamekimbilia mijini ambako wizi na Ujambazi umekuwa sugu. Watoto wa kike wamelazimishwa kuuza miili yao kwa sababu ya kutafuta ada! ati msichana wa miaka 16 leo hii ni mama mzima anatakiwa kujitegemea.

Sasa ikiwa hawa wananchi wame - turn kuwa malaya , majambazi ni watu gani watakao kuwa hatarini kimaisha?. Jibu ni wenye nacho!.. na the first victim wa Ujambazi watakuja kuwa hawa viongozi wetu wamaolimbikiza mali kwani hakuna Jambazi atakaye taka kumuibia maskini.

Tazama South Afrika leo! kuna watu wanaujutia uhuru.. kwani leo hii maskini na matajiri wote hawana usingizi!.. soon hali hiyo itaingia Tanzania na kama sio sisi kuchukua muda wetu kuhakikisha hali hiyo haifikii basi mjomba hata pepo hutaweza kuiona. Mungu kakupa kipaji na elimu ambayo umegundua mapungufu yote haya lakini umeshindwa kutumia utume wako mdogo kuwasaidia maskini wanaokufa kila siku kwa njaa na malaria tu.

Tanzania sii nchi ya kutegemea mvua hata kidogo!...Tanzania sii nchi ya kukosa maji, Umeme wala kodi ya wananchi kufikia asilimia 15 hali makampuni ya kigeni (sio ya ndani) yanapata nafuu za kodi. Kibaya zaidi ni kwamba makampuni haya mengi hayazalishi kitu ndani ya nchi ila ni mawakala wa makampuni ya nje! - Tanzania ni sokoni! na kama mjuavyo soko halizalishi kitu zaidi ya ajira ambazo mishahara yake inalipwa kutokana na mauzo ya bidhaa yaani mfuko wa maskini mkulima.

Mimi sio Mjamaa kwa mrengo wa vita baridi bali mjamaa kwa imani ya kuwa UMOJA ni nguvu na Utengano ni udhaifu. Ukipanda juu usije wasahau wa chini lakini lazima mmoja apande! Na anayepanda juu awe na uhakika kuna watu chini wameshikilia ngazi!. WE all need each other!
 
Last edited by a moderator:
Kaka Mkandara:

U have made my sunday...

Karibu sana uwe wakala wa mabadiliko unayotaka kuyaona. Tunahitaji mpinzani kama wewe ndani ya upinzani hususani ndani ya CHADEMA. Ubishi wako ni asset kwa Taifa.

Ama kuhusu taratibu za kujiunga tuwasiliane kupitia mnyika@yahoo.com, unaweza kupitia pia masharti ya uanachama na mambo mengine basic kwa kuingia kupitia tovuti ya CHADEMA.

Ingawa umesema hutaki uongozi lakini kwa michango yako ambayo umekuwa ukiitoa toka BCSTimes inaonyesha dhahiri kwamba unaweza kuwa policy and law maker mzuri kuliko aina za wabunge wengi wa ndio mzee tulio nao hivi sasa. Nakuomba ujiandae kukamata kujiti!

Inshallah tutafika..

JJ
 
Last edited by a moderator:
Shukran,
Nimepitia tovuti ya chama na kusoma mengi sana ila kitu kimoja tu! sikuona template ya usajili kwa wanachama wapya. nadhani mnahitaji kuwa na ukurasa maalum wa Usajili na pengine kufanya interview kupitia mtandao. Pia jina la msajili na e-mail yake muhimu kutuwezesha kuwasiliana naye moja kwa moja.
For those who want to join!
 
Shukran,
Nimepitia tovuti ya chama na kusoma mengi sana ila kitu kimoja tu! sikuona template ya usajili kwa wanachama wapya. nadhani mnahitaji kuwa na ukurasa maalum wa Usajili na pengine kufanya interview kupitia mtandao. Pia jina la msajili na e-mail yake muhimu kutuwezesha kuwasiliana naye moja kwa moja.
For those who want to join!

Kaka:

Fomu ya kujiunga inapatikana hapa: http://www.chadema.net/maelezo/fomu/uanachama.php

Inapomahali pa kuandika email address, na taarifa zote zinaingia kwenye online data bank.(ambayo ni siri)

Ila ambacho nakubaliana nawe kuwa hakuna ni sehemu ambayo inaweza ku-display interviews na wanachama wapya ambao wako tayari kuwekwa wazi.Nitamwambia bwana tovuti wetu aongeze.

Asante kwa ushauri

JJ
 
Ha ha ha ha........................ Lakini wengine tulikuwa tunafahamu brother Mkandara ni CHADEMA damu.

Kila mafanikio katika wadhifa wako mpya wa umemba wa chama, kwa hiyo utaanza kujibu mawe yanayoelekezwa kwenye chama chako bila kificho. BRAVO!
 
Hayo maneno hapo juu ni mazito mno. Yanatia kila namna ya matumaini, hata mahali ambapo matumaini yalikuwa yameanza kufifia.

Unajua, waTanzania wanayo (au walikuwa) na matumaini makubwa na serikali ya ndugu Kikwete. Kwa namna fulani, nadhani wengi wao walipokuwa wanapiga kura walikuwa na hakika kuwa baada ya rais wetu kuwa mwanafunzi wa Mwalimu kwa miaka mingi, na hata lugha yake kushabihiana na ile ya Mwalimu, walijua kuwa mtetezi wa haki zao wamempata tena.

Rais alianza vizuri, hasa alipochukua uamzi wa kuondoa utata wa mauaji ya wafanya biashara haraka na kukomesha ujambazi ulioonekana kuchukua nguvu mpya.

Baada ya haya mambo mawili, nadhani tumekuwa tukienda katika mwendo wa 'auto-pilot.' Pengine ni kwa vile mengi mazuri yanayotendeka kila siku pengine sisi raia wa kawaida sio rahisi kuyaona haraka na kwa bayana.

Hata hivyo, hisia zinaendelea kujitokeza zinazoonyesha kuwa kuna udhaifu mkubwa katika serikali yetu; mambo ambayo nadhani yanaanzia kwenye chama kinachotawala na kuenea hadi katika mihimiri yote ya serikali.

Dalili mojawapo inayoonyesha kuwa maslahi ya mwananchi wa kawaida yanazidi kupungua nguvu ni uhitaji wa kuwa na nyenzo au influence fulani iliyo karibu na serikali ndipo mambo yamwendee sawa, tena haraka.

Watanzania kwa ujumla wao ni watu wanaojali waTanzania wenzao popote pale, bila ya kujali chama cha siasa, ukabila, udini, au hata cheo alichonacho mtu. Mambo haya yameanza kutoweka, tena kwa haraka sana. Watu sasa wanaanza kuhisiana kwa vyama vya siasa zao zaidi kuliko uTanzania wao kwanza. Hili ni jukumu la uongozi wa juu wa nchi yetu kuendelea kuupalilia na kuuwekea mbolea. Tusijidanganye kuwa mambo haya yanakuja hivi hivi tu, au yakishapatikana hayatoweki tena kama yanakosa msisitizo.

Nimeandika kiujumla mno, lakini nitapenda kutoa mifano michache ya baadhi ya mambo ambayo nadhani serikali yetu inaonekana kuyapuuza, au kama inayashughulikia, basi dalili hazionekani kwa nje.
Wanafunzi walioko Ukraine wamepata matatizo makubwa. Inawezekana kabisa hawa wanafunzi walikosea njia sahihi ya kuondokea nchini kwenda masomoni. Lakini kuna uwezekano mkubwa kuwa pengine wahusika wa jambo hili serikalini hawakuwa wawazi kabisa kuwaelekeza mambo halisi yalivyokuwa kabla hawajaondoka. Katika hali ya utata kama ulivyojitokeza hapa, nadhani serikali inao wajibu wa kuonyesha huruma. Mambo yanavyoonekana sasa hivi, ni kama serikali inawakomoa, na hasa kutokana na kujihusisha na vyama vya kisiasa. Si wajibu wa rais, au hata waziri mkuu kujihusisha na watu binafsi na hawa wachache hivi? Hata kuyatolea maelekezo tu kwa watendaji wahusika ndani kwa ndani?

Kujikwaa kwa maskendo kumezidi mno sasa. Kila kunapokucha kuna skendo mpya, ya utendaji usioridhisha katika vyombo vya serikali. Si Benki kuu, Tanesco, Migodi (yao) ya madini, n.k. Tunachokiona sisi wananchi ni juhudi za serikali zinazoashiria kujifanya yanashughulikiwa kwa kiaina ya kutufanya tuyasahau kadri ya siku zinavyozidi kwenda mbele, na mengine mazito na mapya zaidi yakitufanya tuyawekee uzito haya badala ya yale yaliyopita. Nasema tena, pengine serikali inayashughulikia yote haya kwa njia ambazo hazionekani kwetu sasa hivi.

CCM imezidi mno kuwa biashara ya kutafutia riziki - chukulia kwa maana yoyote uipendayo mwenyewe.

Narudi kwa mchango wa Mkandara#66 hapo juu:
Mkandara, mengi uliyoyasema katika mchango wako huo, ni wengi humu JF yanatufadhaisha na kutukosesha raha. Hata kama si wanachama wa chama chochote kile cha siasa, bado tunayo matumaini kwamba pengine hivi karibuni ndani ya CCM mambo yataanza kurekebishwa na kuwa mazuri kuliko mwelekeo unavyoonyesha sasa hivi. Lakini pamoja na yote hayo, itakuwa ni faraja kubwa sana kama vyama kama CHADEMA vitaimarika zaidi na kuwa mshindani wa nguvu kwa CCM. Nafahamu Swali ni lile lile linaloulizwa na wengi: tunasubiri nini? Na Tunamtegemea nani aweke mambo sawa huko kwenye upinzani kama si sisi ambao haturidhishwi na CCM. Jibu langu ni kwamba bado tunayo matumaini ya uwezo wa mwenyekiti wa ccm na wenzake katika chama chao kuweza kugeuza hali ya mambo kwenye chama na serikalini. Tuzidi kumpa muda kidogo. Kama mambo yakiendelea kuachwa yaendelee kama yanavyokwenda sasa, basi kura pamoja na 'intangible' support zetu mtavipata bila ya wasix2.
 
Hayo maneno hapo juu ni mazito mno. Yanatia kila namna ya matumaini, hata mahali ambapo matumaini yalikuwa yameanza kufifia.

Unajua, waTanzania wanayo (au walikuwa) na matumaini makubwa na serikali ya ndugu Kikwete. Kwa namna fulani, nadhani wengi wao walipokuwa wanapiga kura walikuwa na hakika kuwa baada ya rais wetu kuwa mwanafunzi wa Mwalimu kwa miaka mingi, na hata lugha yake kushabihiana na ile ya Mwalimu, walijua kuwa mtetezi wa haki zao wamempata tena.

Rais alianza vizuri, hasa alipochukua uamzi wa kuondoa utata wa mauaji ya wafanya biashara haraka na kukomesha ujambazi ulioonekana kuchukua nguvu mpya.

Baada ya haya mambo mawili, nadhani tumekuwa tukienda katika mwendo wa 'auto-pilot.' Pengine ni kwa vile mengi mazuri yanayotendeka kila siku pengine sisi raia wa kawaida sio rahisi kuyaona haraka na kwa bayana.

Hata hivyo, hisia zinaendelea kujitokeza zinazoonyesha kuwa kuna udhaifu mkubwa katika serikali yetu; mambo ambayo nadhani yanaanzia kwenye chama kinachotawala na kuenea hadi katika mihimiri yote ya serikali.

Dalili mojawapo inayoonyesha kuwa maslahi ya mwananchi wa kawaida yanazidi kupungua nguvu ni uhitaji wa kuwa na nyenzo au influence fulani iliyo karibu na serikali ndipo mambo yamwendee sawa, tena haraka.

Watanzania kwa ujumla wao ni watu wanaojali waTanzania wenzao popote pale, bila ya kujali chama cha siasa, ukabila, udini, au hata cheo alichonacho mtu. Mambo haya yameanza kutoweka, tena kwa haraka sana. Watu sasa wanaanza kuhisiana kwa vyama vya siasa zao zaidi kuliko uTanzania wao kwanza. Hili ni jukumu la uongozi wa juu wa nchi yetu kuendelea kuupalilia na kuuwekea mbolea. Tusijidanganye kuwa mambo haya yanakuja hivi hivi tu, au yakishapatikana hayatoweki tena kama yanakosa msisitizo.

Nimeandika kiujumla mno, lakini nitapenda kutoa mifano michache ya baadhi ya mambo ambayo nadhani serikali yetu inaonekana kuyapuuza, au kama inayashughulikia, basi dalili hazionekani kwa nje.
Wanafunzi walioko Ukraine wamepata matatizo makubwa. Inawezekana kabisa hawa wanafunzi walikosea njia sahihi ya kuondokea nchini kwenda masomoni. Lakini kuna uwezekano mkubwa kuwa pengine wahusika wa jambo hili serikalini hawakuwa wawazi kabisa kuwaelekeza mambo halisi yalivyokuwa kabla hawajaondoka. Katika hali ya utata kama ulivyojitokeza hapa, nadhani serikali inao wajibu wa kuonyesha huruma. Mambo yanavyoonekana sasa hivi, ni kama serikali inawakomoa, na hasa kutokana na kujihusisha na vyama vya kisiasa. Si wajibu wa rais, au hata waziri mkuu kujihusisha na watu binafsi na hawa wachache hivi? Hata kuyatolea maelekezo tu kwa watendaji wahusika ndani kwa ndani?

Kujikwaa kwa maskendo kumezidi mno sasa. Kila kunapokucha kuna skendo mpya, ya utendaji usioridhisha katika vyombo vya serikali. Si Benki kuu, Tanesco, Migodi (yao) ya madini, n.k. Tunachokiona sisi wananchi ni juhudi za serikali zinazoashiria kujifanya yanashughulikiwa kwa kiaina ya kutufanya tuyasahau kadri ya siku zinavyozidi kwenda mbele, na mengine mazito na mapya zaidi yakitufanya tuyawekee uzito haya badala ya yale yaliyopita. Nasema tena, pengine serikali inayashughulikia yote haya kwa njia ambazo hazionekani kwetu sasa hivi.

CCM imezidi mno kuwa biashara ya kutafutia riziki - chukulia kwa maana yoyote uipendayo mwenyewe.

Narudi kwa mchango wa Mkandara#66 hapo juu:
Mkandara, mengi uliyoyasema katika mchango wako huo, ni wengi humu JF yanatufadhaisha na kutukosesha raha. Hata kama si wanachama wa chama chochote kile cha siasa, bado tunayo matumaini kwamba pengine hivi karibuni ndani ya CCM mambo yataanza kurekebishwa na kuwa mazuri kuliko mwelekeo unavyoonyesha sasa hivi. Lakini pamoja na yote hayo, itakuwa ni faraja kubwa sana kama vyama kama CHADEMA vitaimarika zaidi na kuwa mshindani wa nguvu kwa CCM. Nafahamu Swali ni lile lile linaloulizwa na wengi: tunasubiri nini? Na Tunamtegemea nani aweke mambo sawa huko kwenye upinzani kama si sisi ambao haturidhishwi na CCM. Jibu langu ni kwamba bado tunayo matumaini ya uwezo wa mwenyekiti wa ccm na wenzake katika chama chao kuweza kugeuza hali ya mambo kwenye chama na serikalini. Tuzidi kumpa muda kidogo. Kama mambo yakiendelea kuachwa yaendelee kama yanavyokwenda sasa, basi kura pamoja na 'intangible' support zetu mtavipata bila ya wasix2.
 
Kalamu,
Wakombozi wetu akina Mandela wangesubiri wakitegemea siku moja Kaburu atakuja kuwa na mawazo tofauti... mjomba wangesubiri sana na pengine leo hii Afrika ingekuwa bado Imetawaliwa kama Visiwa vingine vya Africa na Amerika ya kusini.
Hivi kweli unategemea mtu ambaye kisha onja tamu ya fedha kukubali siku moja watakuja badilika?
Kalamu kuna vitu viwili hapa, binafsi nimevifikiria sana hasa baada ya kuzitazama nchi kama Iraq, Sudan, Rwanda na hata Palestine!
Hizi ni nchi zilizosubiri sana namwisho wake wakachoka na badala ya kutafuta suluhu waliamua kuingia mwituni!.. Matokeo yake walijenga chuki kubwa ambayo haina kipimo wala subira. Sintapenda kuiona Tanzania katika hali hiyo na trust me kama tutasubiri zaidi ndivyo chuki inavyozidi kuweka hekalu ndani ya nyoyo yetu.
Wakati ni huu, mahubiri yabaki misikitini na makanisani, nimekwisha amua na nashukuru sana kwamba kwa mara ya kwanza nitakuwa na watu ambao wapo karibu na mimi toka hapa JF na nadhani ni muhimu kwangu kuwashukuru wote waliojitahidi kuiweka tovuti hii hai kwa muda wote huu.

Dua,
Sikuwa Chadema hata siku moja ila baada ya kusoma hoja nyingi ktk mada hii, kupima uzito wa mazungumzo, muda naopoteza humu bila hata kujitokeza kutoa mchango wa buree! nimejikuta sina Hila isipokuwa kujiunga na wakombozi. Tumejaribu vya kutosha upande wa CCM toka enzi ya bcstimes lakini ndio kwanza CCM wamezidi kujenga ngome kubwa kujitenga na wananchi. Sina mapenzi na CUF kwa sababu moja kubwa nayo ni Seif Shariff ktk swala la Zanzibar kuleta mtazamo wa Hizbu!.

Vyama vinginevyo sina kabisa mawasiliano na mtu yeyote na Chadema imekuja juu ya vyama vyote! Kwa sababu Chadema ni kizazi changu, watu ambao nina hakika wanaweza kunisikiliza kwa mchango wangu wa senti mbili tatu. CCM has to go na kama watakuja badilika basi ujuwe ni nguvu ya Upinzani sio watu waliokaa na kuweka matumaini hewa. Sisi wenyewe tunaubeba Usanii.

nakuomba soma tena maelezo ya ndugu yetu kalamu kisha fikiria wewe mwenyewe...
Kujikwaa kwa maskendo kumezidi mno sasa. Kila kunapokucha kuna skendo mpya, ya utendaji usioridhisha katika vyombo vya serikali. Si Benki kuu, Tanesco, Migodi (yao) ya madini, n.k. Tunachokiona sisi wananchi ni juhudi za serikali zinazoashiria kujifanya yanashughulikiwa kwa kiaina ya kutufanya tuyasahau kadri ya siku zinavyozidi kwenda mbele, na mengine mazito na mapya zaidi yakitufanya tuyawekee uzito haya badala ya yale yaliyopita. Nasema tena, pengine serikali inayashughulikia yote haya kwa njia ambazo hazionekani kwetu sasa hivi.
CCM imezidi mno kuwa biashara ya kutafutia riziki - chukulia kwa maana yoyote uipendayo mwenyewe
 
Ndugu wana JF,

Baada ya kufuatilia kwa karibu mjadala huu na mimi nimeona nitoe yangu machache.

Kwanza naomba wale wote wanaodiriki kusema kuwa watanzani ni wajinga ni vizuri wakajirudi Ndugu zangu, matamshi kama haya sio tu yanafadhaisha lakini pia ndio moja ya adui wetu mkuu. Kuendelea kuamini kuwa watanzania ni wajinga ni sawasawa na kujikata mguu na kuanza kuamini kuwa kamwe huwezi kujisaidia kupambana na adui ujinga, maradhi na umasikini.

Vilevile historia inatufundisha kuwa wengi waliothubutu kusema hivyo kufikia hivi leo watanzania wameweza kuwathibitishia kuwa nani ni mjinga kweli. Kumbukeni maneno ya Mzee wetu aliyewaambia "TO HELL WITH ........".

Vilevile ni wazi kuwa wengi wanaosema watanzania ni wajinga wanawalenga walalahoi walio zaidi ya asilimia themanini katika jamii yetu wakidhani kuwa wale waliopo katika tabaka la walahai kama wengi wetu hapa na wale walio katika tabaka la walaheri ndio werevu.

Sidhangai hili kwani ni wazi wengi humu wapo nje ya Tanzania na wakipita nyumbani kama watalii weusi kucritisize every reality and romanticise every fake progresses without taking any meaningful time kuinteract na walalahoi wetu ama wawe wa jijini Dar ama huko vijijini tutokako wengi wetu. Laiti kama kwa pamoja, wa ughaibuni na wabenzi (walalahai/walalaheri/waheshimiwa ama the so called corporate tanzania or intellectuals) wa nyumbani tungethubutu kuinteract na ndugu zetu hawa, wawe vijana wa kijuweni ama wazee wa barazani ama kilabuni, tungetambua ni vipi walivyo werevu kupita hata sisi tunaojiona tu werevu wa kuwaita wao wajinga.

Kwa ujumla watanzania ni werevu sana na ndio maana mwaka 1995 hawakumpa Mrema, 2005 wakamtosa Freeman na 2010 watawatosa kina "THE HAVARD GRADUATE" na mitume feki wengine watakaojitokeza "kuondoa" kile watakachodai kuwa uongozi hovyohovyo wa Kaka JK.

Ukitaka kung'amua uerevu wao toa wiki yako moja nenda nyumbani straight kijijini hata yombo dovya na tandale kama sio gazaulole halafu kaa na watanzania uwasikilize mawazo yao.

Kwa kifupi ndugu zangu watanzania sio wajinga na kama kuna wajinga basi ni wale wanaojiona ndio werevu kiasi cha kufikia hatua ya kuwatusi, kuwakejeli na kuwadhihaki kwa mikogo na vibweka vya kila aina........kama yule aliyewaambia TO HELL na yule aliyewaambia kuwa hata wakila majani mheshimiwa sana hawezi kupanda punda kusafiri nje ya nchi.....ama Mheshimiwa sana mwenyewe aliyewaita wapumbavu...

Kama ni upungufu basi ni utamaduni wa uvumilivu wa hali ya juu uliochanganyika na uoga wa kuthubutu ambao kamwe hausababishwi na ujinga bali uerevu wao kutokana na mafunzo ya kihistoria waliyoyapata tangia enzi zile za Mrema na "wanamageuzi" wenziwe hadi kufikia sasa.


Tanzanianjema
 
Kaka Mkandara,

Pongezi kwa uthubutu wako. Ni kweli ukereketwa wako na maumivu yanayowasibu watanzania unaweza ukasaidia kupeleka mbele hilo gurudumu la kizazi kipya ingawa kwa bahati mbaya hadi sasa bado lina utando wa fikira na nyendo za kizazi kilichopita na kilichopo.

Ushauri wangu kaka ni kuwa kama kweli unaingia huko hakikisha hukubali ushawishi wa kuchukua madaraka yoyote hapo kwa muda wa mwaka mmoja ili upate kusoma undani wa jahazi hilo unalopanda na zaidi ukaweza kulinda uhuru wako wa kukosoa.

Zaidi usivunjike moyo kila utakapokutana na mafyongofyongo yaliyopo humo ndani kwani tofauti na jiti kavu CCM, uchanga wa huko unatoa nafasi ya wewe kuwa sehemu ya kurekebisha na kujenga taswira makini ingawa inahitaji uvumilivu mno.

Tanzanianjema
 
OK, nimerudi mjini na nimefurahi kukuta mawazo mapya mengi. Nakubaliana na mengine na sikubaliani na mengine. Nitatoa ufafanuzi zaidi baadaye lakini ngoja nirudie tena kumwelewesha Tanzanianjema na wengineo wanaoniambia kuwa mimi ndiye mjinga, siyo watanzania. Nilikwisha fafanua jambo hili kule nyuma, lakini kwa vile sijaambiwa msamiati sahihi wa kutumia ndiyo maana naendelea kutumia neno ujinga. Naona ndugu hawa wanalichukulia neno hilo kwa maana ya tusi la stupidity badala ya neo la kawaida ignorance. Ninaposema watu ni wajinga nina maana kuwa ni ignorant wa wajibu wao kama raia. Utakubalina nami kuwa ni kutokana na ignorance ndiyo maana huwa wanauza shahada zao za uchaguzi. Kwa hiyo tusiangalie neo hili kama tusi, siwezi kuwatukana watanzania kuwa ni wajinga kwa maana ya "stupi.d" kwani hiyo inajumuisha wazee wangu wengi tu, nadhani kuanzia hapa nitakuwa naandika ignorance kwa kiingereza moja kwa moja. Raia wasingekuwa ignorant, serikali isingekuwa inafanya upuuzi huu bila kuogopa. Siyo lazima raia wachague chama cha upinzani kuonyesha kuwa wanajua wajibu wao, kinachotakiwa ni kwa wao kuweza kuiwajibisha serikali inapokosea.

Baada ya ufafanuzi huo, napenda pia nieleze kuwa sikubaliani na wale wanaosema kuwa tatizo kuu ni viongozi wa upinzani; huwezi kuwahukumu kabla hujawapa madaraka na kuona kweli kama wataharibu. Kuna ushahidi kuwa viongozi wa upinzani wanapohamia CCM huwa anapewa nafasi ya uongozi na wanafanya vizuri: angalia akina Nsanzugwako, Limbu, Makanga, na wengineo. Kuwapima viongozi hao kutokana na migogoro kwenye vyama vyao pia siyo sahihi kwa vile migogoro kwenye vyama vya upinzani ni jambo la kawaida sana baada ya kushindwa uchaguzi: mlioko Uingereza nadhani mnakumbuka jinsi Conservative walivyovurugika baada kushindwa na Labor, walioko Australia pia mtakumbuka jinsi Liberal ilivyovurugika baada ya kupoteza kwa Labor na halafu baadaye kibau kikawageukia Labor baada ya kupoteza kwa Liberal uchaguzi uliofuata. Ingawa migogoro ya vyama haitokei sana Marekani lakini huwa ipo ya kichinichini baada ya uchaguzi.

Mimi bado nina imani kabisa kuwa tatizo letu ni ignorance na umaskini. Kosa la vyama vya upinzani ni kushindwa kuwasadia raia kuondokana na ignorance. Kudai kuwa wananchi hawataki kuruka kutupa maji na kuokota matope siyo sahihi kwa sababu kama CCM ikitolewa madarakani, basi ikiwa upande wa upinzani itakuwa kali sana kuibana serikali kiasi kuwa hayo matope hayatakuwapo. Tatizo ni kuwa miongoni mwa wananchi wengi wanadhani kuwa wapinzani ni wavurugaji; wanalichukulia neno hilo katika maisha ya jamii kuwa mpinzani ni mtu wa fujo. Vyama vya upinzani vinashindwa kuwaelewesha wananchi ukweli huo sawasawa. Umma mkubwa sana wa raia wetu walioko vijijini hawajui maana ya vyama vya upinzani na maana ya uchaguzi katika maisha yao, na lazima tukubali kuwa wao ndio wanaotuchagulia viongozi. Sisi tulioko mijini ambao ndio tunajua ukweli wa mambo ni asilimia ndogo sana. Vile vile nadhani unajua kuwa uchagzui wa majimbo ya mjini huwa ni motomoto sana kuliko yale ya vijijini, hata pale CCM inaposhinda jimbo la mjuini inakuwa ni kwa mapambano kweli kweli na mara nyingi wanashindwa kutokana na makosa ya upinzani. Tatizo hili hili letu ndilo lililoko Zimbabwe pia; majimbo ya mijini karibu yote yamechukuliwa na vyama vya upinzani lakini yale ya vijijini yote yako kwa Mugabe.

Mambo mengine yote yaliyoandikwa wakati sipo mjini nitayaunganisha na kuyajadili hapo baadaye.
 
Leo hii rasmi natangaza kuomba kadi ya Chadema!...
Mh. Freeman, Zitto, J.J.Mnyika, Mwanasisa naomba tuwasiliane!
Mkandara sina kuficha wala mpango wa kupitia mlango wa nyuma.Nataka kutiwa maji ya ubatizo..
Ila tu kumbukeni Mkandara nina sifa moja!.......BABU UBISHI!

Tupo pamoja 2010!

Ndugu Mkandara

Nilikuwa mbali kwa muda mrefu kidogo. Baada ya kupewa taarifa za maamuzi yako mazito nimelazimika kuja haraka hapa kukukaribisha. Naamini ubishi na umakini wako utakua chachu muhimu sana katika kujenga na kukikuza CHADEMA.

Nafarajika sasa, hatimae umeamua kupiga hatua moja kubwa, kushiriki moja kwa moja katika mapambano dhidi ya ufisadi na kuchochea ustawi wa Taifa letu.


Kwa wanabodi wengine,

Mjadala mzito huu. Nimeingia katikati. Ngoja niupitie kwa kina niwezi kutoa yangu mawili matatu.
 
wewe Eric unapotea sana bwana, halafu ile thread yetu ya udhuru hukuiona uage? karibu sana tena. Tunasubiri mawazo yako kwenye hii mada!
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom