Mama Mdogo
JF-Expert Member
- Nov 21, 2007
- 2,962
- 2,138
Wiki chache zilizopita nilikuwa safarini kutoka Ushirombo/Bukombe kuja Dar kwa bus. Muda mwingine nikiwa macho nilikuwa naangalia mandhari nzuri ya njiani na kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kutupa nchi nzuri. Hata hivyo kuna kero mbili nilizoshuhudia zinazohusiana na hawa wadau wetu TANROADS.
Kwanza, barabara ya Mlima wa Sekenke iko katika hali mbaya, imechimbika na kubomoka. Ni miaka minne tu tangu imekamilika na kukabidhiwa serikalini lakini hali ndivyo hivyo. Je imejengwa chini ya kiwango na hao wajenzi wa Kichina au mizigo inayopita pale inazidi kiwango??
Pili, katika kipande cha barabara kutoka Chalinze hadi Vigwaza sikuona vile vigingi vya alama ya hifadhi ya barabara, je vimengolewa na wananchi wenye hasira kali? vimehujumiwa? Au Tanroads bado hawajaviweka. Je katika maeneo hayo mtu akijijengea banda lake hadi mita tano kando ya barabara ni nani wa kulaumiwa.
Kwa haya machache namuomba Injinia Mfugale (CEO wa Tanroads) afunguke!!! Nawasilisha
Kwanza, barabara ya Mlima wa Sekenke iko katika hali mbaya, imechimbika na kubomoka. Ni miaka minne tu tangu imekamilika na kukabidhiwa serikalini lakini hali ndivyo hivyo. Je imejengwa chini ya kiwango na hao wajenzi wa Kichina au mizigo inayopita pale inazidi kiwango??
Pili, katika kipande cha barabara kutoka Chalinze hadi Vigwaza sikuona vile vigingi vya alama ya hifadhi ya barabara, je vimengolewa na wananchi wenye hasira kali? vimehujumiwa? Au Tanroads bado hawajaviweka. Je katika maeneo hayo mtu akijijengea banda lake hadi mita tano kando ya barabara ni nani wa kulaumiwa.
Kwa haya machache namuomba Injinia Mfugale (CEO wa Tanroads) afunguke!!! Nawasilisha