Tangu JK aapishwe ni machungu tu kwa Watz

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
233

Nimelitafakari sana hili, na nimegundua kwamba tangu kuapishwa kwa JK mwezi uliyopita, Watz wamekuwa wanaonja machungu tu: Mgao wa umeme na maji, habari za kupanda bei za umeme, ongezeko la bei ya mafuta, ongezeko la bei ya bidhaa mbali mbali, wanafunzi wa vyuo kuandamana kudai haki/posho zao, uharamia katika chaguzi za mameya wa halmashauri…….

Listi ni ndefu mno, na mwanzo ndiyo huonyesha ishara ya tunakokwenda. Ni bora wananchi wakasahau kabisa uwezekano wa hata kutimiza asilimia 0.000001 ya ahadi lukuki alizotoa JK wakati wa kampeni – iwapo mwanzo ni wa namna hii.

Nasikia yeye yuko majuu kwenye matanuzi.

 
vasco dagama anajivinjari tu USA, hajui hayo mnayoyapata coz its none of his bussiness.
 
Jumapili liyopita nimesali pamoja na Jaji Makame....yaani haonyeshi dalili kuwa alihusika na wizi wa kura kabisaa
 
Hawezi tena kutawala vyema kwa sababu huko majuu aloko, wazungu hawalitaki tena bakuli lake analetembeza kwa sababu ya yaliyojiri katika Wikileaks!
 
Hujiulizi soda kupanda baada ya uchaguzi instead of baada ya bajeti kwa maana ya kodi kuwa wamepandishiwa? CCM walichukua hela makampuni mengi tu, na wakaambia mjue mtarudishaje faida zenu. Kwa hiyo huko kupanda ni katika kufidia na ku-maintain faida zao ktk walichochangia. Na things will get more worse mwakani maana hata wafadhili wengi wamegoma kuchangia. Wekeni akiba bandugu, maana things will get worse come 2011.
 
Ulitaka JK awape wakristo wa Tanzania zawadi gani zaidi ya kuwatangazia heri njema ya GIZA (blackout!)?
 
ujue ccm bado wanadhana kua kuongoza wananchi wa Tz ni raisi sana kuliko hata kuongoza mbwa wa polisi.sasa wajue tu watz wameshaamka ndio maana mining'ono imekua mingi mtaani.
 
ARI ZAIDI,KASI ZAIDI ndio ulikuwa msemo wake nadhani umeshaanza kutimia, fungeni mikanda wandugu.
 
Si wote wanasikia machungu asimilia 62% wanaona mambo yao safi, asilimia 38% ndio wanaona machungu

Wengine Machungu tangu enzi za nyerere hadi leo...same shi.....t different day
 
Si wote wanasikia machungu asimilia 62% wanaona mambo yao safi, asilimia 38% ndio wanaona machungu

Wengine Machungu tangu enzi za nyerere hadi leo...same shi.....t different day

Umenifurahisha kweli........................ Umenikumbusha lile domna la njano tena unalipata kwa foleni. Nakumbuka tulikuwa Bukoba enzi hizo kabla ya vita. Hivyo inabidi kuchanganya na unga wa mihogo kutoka Kiambisi, wilaya ya Biharamuro.
 
mkwere na kundi la mabaradhuli wamedhamiria kutufilisi kabisa na kujitarisha kwa garama yoyote. Nashauri tuache kulalamika na tuchukue hatua, kila ambae hajui kutumia silaha aende mgambo au aombe aelekezwe na wanaofaham, tukikaa kimya watoto wa wajukuu zetu watatucheka kwanini tusifanye kama akina kinjekitile ngwale?,dedan kimath na wengineo? Mkoloni bado yupo na mapambano lazima yaendelee watu waache uoga.
 

Nimelitafakari sana hili, na nimegundua kwamba tangu kuapishwa kwa JK mwezi uliyopita, Watz wamekuwa wanaonja machungu tu: Mgao wa umeme na maji, habari za kupanda bei za umeme, ongezeko la bei ya mafuta, ongezeko la bei ya bidhaa mbali mbali, wanafunzi wa vyuo kuandamana kudai haki/posho zao, uharamia katika chaguzi za mameya wa halmashauri…….

Listi ni ndefu mno, na mwanzo ndiyo huonyesha ishara ya tunakokwenda. Ni bora wananchi wakasahau kabisa uwezekano wa hata kutimiza asilimia 0.000001 ya ahadi lukuki alizotoa JK wakati wa kampeni – iwapo mwanzo ni wa namna hii.

Nasikia yeye yuko majuu kwenye matanuzi.


Mungu atuepushe tusijeletewa RICHMOND nyingine manake na original Richmond ilitanguliwa na mazingira kama haya wakati JK anaingia madarakani katika awamu ya kwanza!

MUNGU IBARIKI TANZANIA!
 
Back
Top Bottom