Nimelisoma tangazo la Wizara ya Nishati na Madini kuhusu kile kilichodaiwa kwamba Ngeleja amemkana Jairo na kilichojitokeza pale kikanikumbusha ule usemi wa kimombo usemao kwamba a fool who is quiet is considered wise. Taarifa hiyo imejaribu kukanusha na kufafanua kukosekana kwa Ngeleja bungeni na kuonekana kwake katika mapokezi ya Katibu Mkuu aliyesimamishwa (David Jairo).
Tangazo limetetea kwamba Ngeleja alikuja Dar kuhudhuria mikutano ya masuala ya umeme na masuala ya mafuta. Hata hivyo hakuna maelezo ya kwa nini alihusika na mapokezi hayo na kwa nini ilikuwa lazima waandishi wachukue tukio hilo na kuacha yale ya msingi yaliyomleta ambayo hata hivyo hayakutangazwa wala kuonyeshwa.
Je, isingewezekana wakakutana ofisini kwa waziri kimya kimya kama wanavyofanya siku zote. Waandishi wale waliitwa na nani na walijuaje kwamba waziri alikuwa anasubiri ili awepo kwenye tukio hilo? Na vipi wale wafanyakazi walioacha kazi za ujenzi wa taifa na kujihusisha na kazi hiyo ambayo haina taji kwa taifa na mwajiri wao.
Kwa ujumla tangazo hilo limeacha maswali mengi kuliko majibu na unajiuliza iwapo ilikuwa ni lazima tangazo hilo litolewe. Kwangu mimi, hakuna ambacho tangazo hilo imefanikiwa kukipata zaidi ya kupoteza fedha za walipa kodi maskini wa nchi hii.
Tangazo limetetea kwamba Ngeleja alikuja Dar kuhudhuria mikutano ya masuala ya umeme na masuala ya mafuta. Hata hivyo hakuna maelezo ya kwa nini alihusika na mapokezi hayo na kwa nini ilikuwa lazima waandishi wachukue tukio hilo na kuacha yale ya msingi yaliyomleta ambayo hata hivyo hayakutangazwa wala kuonyeshwa.
Je, isingewezekana wakakutana ofisini kwa waziri kimya kimya kama wanavyofanya siku zote. Waandishi wale waliitwa na nani na walijuaje kwamba waziri alikuwa anasubiri ili awepo kwenye tukio hilo? Na vipi wale wafanyakazi walioacha kazi za ujenzi wa taifa na kujihusisha na kazi hiyo ambayo haina taji kwa taifa na mwajiri wao.
Kwa ujumla tangazo hilo limeacha maswali mengi kuliko majibu na unajiuliza iwapo ilikuwa ni lazima tangazo hilo litolewe. Kwangu mimi, hakuna ambacho tangazo hilo imefanikiwa kukipata zaidi ya kupoteza fedha za walipa kodi maskini wa nchi hii.