Tangazo la serikali linatosha kurasimisha J'mosi ya kila mwisho wa mwezi kuwa ya usafi kisheria?

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,011
144,371
Nimeona kupitia taarifa ya habari ya ITV saa 2 usiku huu kuwa sasa Jumamosi ya kila mwisho wa mwezi imerasimishwa kuwa ni siku ya usafi kisheria kupitia Tangazo la Serikali namba 139/2016 la tarehe 23/04/2016 na mtu yoyote ambae atakiuka agizo hilo atawajibika kulipa faini ya shilingi 50,000 (na kama sikosei kuna kifungo pia).Makampuni ambayo hayatashiriki katika usafi nayo yana adhabu yake ambayo ni kubwa zaidi.

Taarifa hii imetolewa na Naibu Waziri wa Mazingira,Luhaga Mpina na hii tunaambiwa ni sheria ya mazingira.

Sasa wadau,hasa wataalamu wa sheria,jambo hili ni sahihi kisheria?

Kama haitoshe,kuna sehemu abiria wameshushwa kutoka kwenye magari na wanajeshi ili wafanye usafi!!
 
Wasipo angalia 2020 watajikuta wanatumia nguvu nyingi sana kushinda uchaguzi: huku sasa ndio kukurupuka at best.
Ndio maana niliwahi sema 2020 hawa jamaa watapata kura za vijijinii tu na siyo mijini na hata huko vijijini wanaweza kutoswa pia.
 
Ndio maana nliwahi sema 2020 hawa jamaa watapata kura za vijijinii tu na siyo mijini na hata huko vijijini wanaweza kutoswa pia.
Mijini tayari washakosa tangia uchaguzi uliopita; naweza kuona wana nia njema ya kutaka kurekebisha lakini hizi mbinu za wasaidizi wa raisi zitawacost kisiasa wengi wa hawa watu wanaokuja na namna za kutekeleza maagizo awaendi kuomba kura come 2020 viongozi wa vyama inabidi warudi.

Kwa utaratibu huu wanajichimbia kaburi wenyewe; kwanza the whole thing is unconstitutional sasa huyo bwana Masaju sijui ana kazi gani kushindwa kuwaambia ukweli hili ni kinyume na katiba ya Tanzania as well as international human right act; tunapoelekea hata mimi nimeanza kuogopa kwakweli.
 
Huku kujipendekeza bila kumwambia ukweli ngosha wasipo angalia 2020 watajikuta wanatumia nguvu nyingi sana kushinda uchaguzi: huku sasa ndio kukurupuka at best wameshindwa mbinu za kusafisha miji kwa mipango ya serikari za mitaa sasa wanataka kutumia nguvu.
Mtu mchafu hutetea uchafu. Mpango wowote wa kufanya usafi ni jambo jema sana na huduma hii inafaa hata kuongezwa siku mbili zaidi. Huoni mitaa ilivyo chafuka?
 
Mtu mchafu hutetea uchafu. Mpango wowote wa kufanya usafi ni jambo jema sana na huduma hii inafaa hata kuongezwa siku mbili zaidi. Huoni mitaa ilivyo chafuka?
Kodi wanazolipa watu locally zinaenda wapi? au zipo kwa sababu ya kulipa mishahara ya hawa vilaza tu.

Serikari aiwezi kuendelea kuajiri watalaamu wapuuzi wasioweza kubuni wala kukopi mfumo wowote duniani matokeo yake watu wanatumia nguvu na kuanza huu utaratibu wa unyanyasaji kwa raia wake.
 
Ndio maana niliwahi sema 2020 hawa jamaa watapata kura za vijijinii tu na siyo mijini na hata huko vijijini wanaweza kutoswa pia.
Mmh weeeeeee usitadanganywe na comments za humu za mtu mmoja ana ID sita ukafikiri watu hawamkubali Magu, ongea tu wa kitaani kwako mjini wala hata usiende vijijini usikie Magu anavyokubalika. Tena wanakwambia tusifanye uchaguzi tena hadi atakapong'atuka mwenyewe kama Baba wa Taifa. Magu ni habari nyingine, wanaompinga ni wale wanaotumbuliwa na ukawa coz utendaji wake umewanyima hoja ya kujiuza kwa wananchi
 
Mmh weeeeeee usitadanganywe na comments za humu za mtu mmoja ana ID sita ukafikiri watu hawamkubali Magu, ongea tu wa kitaani kwako mjini wala hata usiende vijijini usikie Magu anavyokubalika. Tena wanakwambia tusifanye uchaguzi tena hadi atakapong'atuka mwenyewe kama Baba wa Taifa. Magu ni habari nyingine, wanaompinga ni wale wanaotumbuliwa na ukawa coz utendaji wake umewanyima hoja ya kujiuza kwa wananchi
Kwa taarifa yako,star tv wametangaza kuna mtendaji alitaka kupata kichapo kwa kulazimisha watu washiriki huu usafi katika eneo la soko(sikumbuki ni wapi).
 
Kwa taarifa yako,star tv wametangaza kuna mtendaji alitaka kupata kichapo kwa kulazimisha watu washiriki huu usafi katika eneo la soko(sikumbuki ni wapi).
Hiyo ni kwavile ilikuwa haijawa rasmi mkuu, sasa imerasmishwa subiri uone kama watu watamchukia Magu sababu ya usafi. Ujue humu tunadanyana sana na kuongea kishabiki, lakini ukweli ni kwamba huko kitaaani Magu anakubalika mno usipime
 
Nimeshangwa na tabia watu wapo kwenye mambo yao eti wanazuiliwa wafanye usafi
 
Udikteta katika ubora wake. Kusafisha mazingira yetu ni muhimu na zipo halmashauri za miji na Majiji na zinakusanya kodi chungu nzima hizi kodi wanazokusanya kwanini zisitumike kuajiri Wafanyakazi wa kuyaweka mazingira yetu katika hali ya usafi badala ya kutaka kuwashinikiza Wananchi.

Jumamosi ya mwisho wa mwezi iendelee kuwa siku ya usafi lakini si kwa kulazimishana na kutafutiana vifungo visivyohusu kitu, mtawafunga wangapi!?

Naanza kukumbuka maneno ya Tundu Lissu kuhusu huu utawala wa sasa.
 
Huku kujipendekeza bila kumwambia ukweli ngosha wasipo angalia 2020 watajikuta wanatumia nguvu nyingi sana kushinda uchaguzi: huku sasa ndio kukurupuka at best wameshindwa mbinu za kusafisha miji kwa mipango ya serikari za mitaa sasa wanataka kutumia nguvu.
Sisi tunatazama ya sasa, 2020 mwachie lowassa. Usafi mtafanya tu. Kama hukufunzwa na baba yako basi serikali itakufunza. Hata singapore walianza hivi.
 
Back
Top Bottom