Wana Jf Wenzangu kuna tangazo jipya huwa nalisikia radioni la kutolazimisha penzi hata kwa mke wako. Kimsingi naona kama kila siku zinvyokwenda maadili yanapungua hata kwa vyombo vya serikali kama vile wizara. Tangazo hili silikubali na halisikiliziki ndani ya familia zetu. Kila siku asubuhi inanibidi nizime radio ya gari kulikwepa kwani ninakuwa na watoto nawapeleka shule. Wahusika nawaomba hata kama hi fedha ya wafadhili basi tuone na maadili yetu yanachukua nafasi gani.