Tangazo: Bash la Balozi NYC Haya Tukutane Wakuu!

Apr 27, 2006
26,588
10,374
Wakulu wote JF, na wananchi wenzangu wote mnaoishi US na hata nje, na hasa New York City na vitongoji vyake,

- Nina furaha kuwafahamisha kwamba kwa niaba ya Balozi wetu wa kudumu katika Umoja wa Mataifa, New York USA, Ofisi ya ubalozi wetu NY, imeniomba kuwafikishia ujumbe huu rasmi kuhusu bash zito la kuchoma nyama liltakalofanyika nyumbani kwa balozi, siku ya tarehe 15/8/2009 yaani Jumamosi ya mwisho wa wiki hii, ikiwa ni kufuatia ahadi iliyotolewa na Balozi mwenyewe kwenye ile Bash ya mwisho kule Wilson Woods Park.

- Kwa kifupi ni kwamba:-

1. The bash itafanyika:- Tarehe 15/8/2009, siku ya Jumamosi.

2. Kuanzia Saa Nane Mchana na kuendelea, yaani From 2.00PM.

3. Kutakuwa na nyama za kuchoma, kuku, mpaka nyama ya mbuzi, na pia kutakua na vinywaji kwa wingi sana.

4. Wananchi wote mnaalikwa na kukaribishwa na ni kwa wakubwa na watoto, wa umri wowote ule.

5. Baada ya kuchoma nyama kama kawaida kwa kushirikiana na Ma DJ's Mao & Freddy, ninawakaribisha wananchi wote kuelekea Alamo Club, 166 Gramatan Avenue, Mount Vernon NY 10552,

- Ambako tutakuwa na muziki wa Disco, mpaka asubuhi na pia kiingilo kitakuwa ni bure kwa kila mwananchi atakayejitokeza. This time ninategemea tutakuwa na shindano la kutafuta bingwa wa "Ndombolo ya solo", na Bingwa wa "Muziki wa Duara" yaani Taarabu iliyokwenda shule.

6. Anuani ya kufika Nyumbani kwa Balozi kwenye Bash ni:-

30 Overhill Road
MT. Vernon, NY 10552


Kwa maelezo zaidi wasiliana kwa simu na:-

1. Tanzania Embassy (NY):- 1-212-972-9160,

au

2. Mukulu William Malecela Cell #1-914-473-1033.

Ahsanteni wakuu na See You there na kama kuna marekebisho zaidi tutafahamishana.

William Malecela - CO (Community Organizer)
.
 

- Nina furaha kuwafahamisha kwamba kwa niaba ya Balozi wetu wa kudumu katika Umoja wa Mataifa, New York USA, Ofisi ya ubalozi wetu NY, imeniomba kuwafikishia ujumbe huu rasmi kuhusu bash zito la kuchoma nyama liltakalofanyika nyumbani kwa balozi, siku ya tarehe 15/8/2009 yaani Jumamosi ya mwisho wa wiki hii, ikiwa ni kufuatia ahadi iliyotolewa na Balozi mwenyewe kwenye ile Bash ya mwisho kule Wilson Woods Park.

Mahiga ameona bosi wake mwenyewe ni legalega mpenda safari, ameona na yeye ajifanyie mapati sasa.

Mara kamfanyia pati ya NBA draft mchezaji basket mpya wa Kitanzania. Balozi mzima wa UN.

Sasa anafanya pati ya kuchoma nyama, bila kichwa wala miguu. Watu wanakutana kula!

Na mwezi wa tisa tena Kikwete akija kwenye UN conference watachoma nyama, hela za kodi zipo za kufuja.

Ukiwa na bosi dhaifu kama Kikwete ndio unaanza ku freelance ovyo ovyo kama hivi, hawana kazi.
 
Vp mpwa Yo Yo hutaenda kujiachia?
Naamini Komredi Nyani Ngabu atatia timu tu kujiachia hapo.
 
Mahiga ameona bosi wake mwenyewe ni legalega mpenda safari, ameona na yeye ajifanyie mapati sasa. Mara kamfanyia pati ya NBA draft mchezaji basket mpya wa Kitanzania. Balozi mzima wa UN.

- Mkuu heshima mbele sana, ile party ya Draft kwa Hasheem Thabeet, iliyofanyika kule Madison iligharamiwa na Heinken, Maybach, pamoja na kampuni ya michezo inayomsimamia Thabeet, maofisa wote wa ubalozi, maofisa wote wa UN na wananchi wa kawaida tulialikwa kufuatana na matakwa na Thabeet mwenyewe, ndiye aliyetoa majina ya nani aalikwe au asialikwe, Ubalozi wala Balozi hawakuwa na anything to do na ile party kwa hiyo hii hard talk yako ni mis-informed, na ni uongo wa mchana!

Sasa anafanya pati ya kuchoma nyama, bila kichwa wala miguu. Watu wanakutana kula!
- Hii party inafanyika kutokana na michango ya mifukoni mwa maofisa na Balozi mwenyewe, na sio kitu cha ajabu kwa sababu toka alipokuwepo Balozi Rupia, chagula, Mwakawago na hata Nyakyi walikuwa wakizifanya hizi shughuli yaani kila Summer na mwisho wa mwaka walikuwa wakifanya party za namna hii, kwa hiyo sio kweli kwamba eti ni party zisizo na kichwa wala miguu, sometimes hizi hard talks zako mkuu huwa ndio hazina vichwa wala miguu, kwa sababu siku zote huwa uko mis-informed,

- Naomba kukupa darasa kidogo kuhusu Hard Talk ambazo unajaribu kuziiga toka kwa Conservative's Radio Hosts kama Rush Limbaugh na "The Great One" Mark Levin, ni kwamba wao hulipwa Millions of Dollars kwa kutoa hard talks wanapokuwa hewani huwa wamezungukwa na ma-side kicks wengi ambao nao huwalipa toka kwenye hizo Millions wanazolipwa na hizo Radio stations kama ABC, hawa Side kicks wengi wao ni ma-lawyer by professional kama vile alivyo Mark Levin "The Great One" na yeye ni lawyer pia,

- Hawa kazi yao ni kukusanya facts na dataz, ambazo huzisukuma kwa hawa watangazaji wanapokuwa mtamboni, yaani hewani na hawa kazi nyingine kubwa ni kuhakikisha kwamba kila linalosemwa linaambatana na mistari ya sheria za FCC yaani za utangazaji, as opposed na wewe na hii hard talk yako ambayo siku zote ni misinformed, backwards, na ni very low IQ kwa sababu how can you dare kuita mkusanyiko wa wananchi wa Tanzania walioko USA, ambao wamekuwa wakikutana kila mwaka toka wewe ukiwa bado BOT hata kabla hujaenda Soviet kwamba eti hauna kichwa wala miguu?

- Wakati unaoa, Balozi Mwakawago alipokufanyia party nyumbani hapo hapo kwa Balozi, ilikuwa ni ya nini hela za serikali au za kwake mfukoni? Halafu kichwa na miguu yake ilikuwa ni nini hasa mkuu? So much for the hard talk unh! kumbe unakimbia kivuli chako mwenyewe!

Na mwezi wa tisa tena Kikwete akija kwenye UN conference watachoma nyama, hela za kodi zipo za kufuja.Ukiwa na bosi dhaifu kama Kikwete ndio unaanza ku freelance ovyo ovyo kama hivi, hawana kazi.
- Mis-informed na uongo wa mchana when was the last time Rais amekwenda NY, akafanyiwa mambo ya kuchoma nyama? Mr. Hard Talk when was the last time that happened? Naomba umtaje rais yoyote wa Tanzania aliyewahi kwenda NYC, halafu akachomewa nyama na hela za serikali? Just mention one muongo mkubwa wewe, unaokota okota habari hazina vichwa wala miguu halafu unasimama mbele ya wanaume na kusema eti ni Hard Talk! Mkuu mtaje rais mmoja tu aliyewahi kuchomewa nyama na hela za serikali kule NYC, just mention one!

- Kama unataka kuongelea udhaifu na strength za rais wa jamhuri nenda ufungue thread kule kwenye siasa, sio kwenye kuhabarishana kuhusu kukutana kwa wananchi, hiyo hard talk yako ipo kwenye the wrong place bro, kwanza ni muongo, halafu hujui the history, kwa kifupi huna hoja period, your hard talk is simply a foolish talk kwa sababu ni mis-informed na ni backwards, I understand kwamba Soviet hamkuwa na haya mambo ya socialization, ambayo ni natural in nature ndio maana hata bongo wananchi wakivuna mavuno hucheza ngoma na kunywa pombe usiku kucha, watoto wakienda jando, mabadiliko ya misimu yote husherehekewa na kwa ngoma na pombe, na sio kwa hela za serikali au za walipa kodi kama Soviet, mkuu it is about time sasa ukaa-adjust kwa sababu you are not in the Soviet tena.

- Halafu nimeshawahi kukukumbusha kwamba kwa mila na desturi zetu wa-Tanzania na Waa-Africa, mtu mzima mwenye umri mkubwa kama Balozi, na kiongozi wa taifa haitwi hovyo hovyo kama unavyomuita, huwa tunatanguliza jina kama Dr. Mahiga, Balozi Mahiga, au Mzee Mahiga, ni ukosefu tu wa maadili kuropoka ropoka hovyo majina ya watu wanaokuzidi umri, elimu na mpaka madaraka, kama sio mpaka elimu.

Ahsante mkuu na unakaribishwa sana kwenye hii party, itakayotukutanisha wanyonge wengi kujuliana hali na kufahamiana zaidi kwa karibu, na ikibidi kusaidiana kwa hali na mali, na the party is on tena big time!

Ahsante.

William.
 
Nikimwita Ndugu yangu Mahiga..mimi kama Mtz na raia ni kosa?

Tuache utamaduni wa kutukuzana..wote tu Wanadamu tu!
 
bwana malechela hukutakiwa kuacha mistari miingi namna hiyo....weka tangazo anaetaka kuja aende asietaka ale kona.....sasa wewe nae bana
 
Nikimwita Ndugu yangu Mahiga..mimi kama Mtz na raia ni kosa?

Tuache utamaduni wa kutukuzana..wote tu Wanadamu tu!

- Total confused mkuu, yaani one minute unamuita ndugu yako ingawa sio lakini the next unasema tuache kutukuzana, kumuita mtu asiye ndugu yako ndugu kwa sababu ni balozi maana yake ni nini kama sio kutukuzana unakokukataa, na wewe exactly ni nini hasa hard talk!, Confused talk or what?

Ahsante.

William.
 
bwana malechela hukutakiwa kuacha mistari miingi namna hiyo....weka tangazo anaetaka kuja aende asietaka ale kona.....sasa wewe nae bana

- Ahsante Cousin, tupo pamoja sometimes ni vyema kuelimishana, lakini point taken.

Ahsante.

William.
 
Ni dhambi kubwa kutukuza wanadamu!! sisi tumezaliwa na iko siku pia tutachungulia kaburi..uwe tajiri, raisi, balozi!

Muhimu ni heshima tu! hapa duniani tunaishi mda mfupi saana!
 
1. Secretary of the Tanzania Basketball Federation Lawrence Cheyo confirmed the news, saying TBF are stitching together a welcome home bash for Hasheem.

2. But the US Embassy in Dar es salaam seems to have beaten TBF with a thunderous dunk - they are hosting a welcome reception for Hasheem on Monday August 17, 2009 at the Embassy, reliable sources have confirmed. Entrance by invitation only!!!


- Source Michuzi.
 
Nyie jichaneni na pesa zetu kwa kula hiyo minyama lakini mjue huku wenzenu majority hardly kupata mlo mmoja kwa siku!! Mnapofakamia hiyo minyama na UGIMBI/KIMPUMU mkumbuke hilo jambo.
 
Back
Top Bottom