TANESCO yaisamehe Zanzibar deni la bilioni 50/-

TANESCO wana madeni makubwa halafu wanafutia wengine madeni kisa Muungano wakati wazanzibari wanasema tunawanyonya, kama ni hivi bora Muungano ufe
 
WaBara kama imewauma Kwanini msiende mahakamani kama mlivyofanya kwa ile kuzuia TUZo ya Dowans kulipwa mabilioni na Tanesco?

Acheni kulalama. Kama imewauma mahakama zipo wazi kwa ajili yenu.
 
TANESCO wana madeni makubwa halafu wanafutia wengine madeni kisa Muungano wakati wazanzibari wanasema tunawanyonya, kama ni hivi bora Muungano ufe

Yaani nchi hii kwa uozo imelaanika. Kila kukicha ni ufisadi nauozo tu.
Afadhali kujitenga na uozo huu na kuanzisha nchi mpya.
 
Kwa hili ngeleja alipaswa kuondoka,tanesco inakopa lakini yenyewe inasamehe wanaotuita wakoloni weusi.
 
Walichokuwa wanakidai Zanzibar kina uhalali, na wala hawajafanyiwa hisani. Walikataa kupandishiwa bei ya umeme kwa hoja ya kwamba ongezeko hill limechangiwa zaidi na uzembe, ufisadi na kutokuwajibika kulikofanywa na Tanesco na wadau wake, na si kutokana na mfumuko wa bei. Niliwahi kumsikia mwakilishi mmoja akihoji kuwa vipi madhara ya rushwa iliyoliwa na mtendaji wa Tanesco ailipe mzanzibari??? Hivyo wakataka iwekwe unit cost ya kuzalisha umeme bila ya kuingiza fidia wanazolipwa Richmond na gharama nyenginezo wanazopata Tanesco kwa kuingia mikataba mibovu

Ikumbukwe katika mikataba kuna kipengele kinachoeleza kuwa upande mmoja hautowajibika kutokana na uzembe (negligence), uharibifu (damages) au ufisadi (corrupt practices) utakaofanywa na upande wa pili au washirika wake. Kimantiki Zanzibar wanahoji uhalali wa ongezeko la bei ya umeme kuanzia mwaka 2008 na wako tayari Tanesco walete mchanganuo wao wa gharama za matumizi ili ibainike kwa kiwango gani ongezeko limechangiwa na mfumuko wa bei na kuongezeka kwa gharama za maisha, na kwa kiasi gani limechangiwa na ubadhirifu na utendaji mbovu, ili kila upande ubebe msalaba wake mwenyewe
Lini Zanzibar walilipa umeme tangu umevushwa? Je, bilioni 50 wamelipa kiasi gani wanachodhani ni halali? wamesamehewa zote. Zbar hawajalipa umeme, wanalipiwa na mkulima na manyakazi wa Tanganyika. Hawajalipa elimu ya juu wanalipiwa na mMtanganyika! Mishahara inatoka hazina muulize Mramba na Mkulo. Kama hawawezi kulipa mshahara watawezaje kulipa umeme? Hiyo ya Richmond n.k ni kutafuta sababu tu kwasababu mgao hawaujui. Wamewahi kusamehewa umeme hata kabla ya Richmond.
Unafiki wao haya huyasikii katika makongamano, unachosikia ni Nyerere na Ukristo wakati nyuma ya pazia wanaalika wajomba kutoka Tel Aviv. Wanafiki hawa waambienei msiowaonea haya!

Narudia onyesha lini umeme ymelipwa na SMZ tangu uvushwe!
 
Shirika halina pesa mpaka limeomba mkopo, badala ya kudai madeni linatoa msamaha haya wawasamehe watanzania wote basi ili tuikubali huruma yao. Hii yote kubebeleza urafiki wa JKN na Karime? na pengo hili wataliziba vipi kuongeza kodi kwa watumiaji wake na kwa wale wasio na luku hapo ndo pa kubambikiwa kama wewe ni Zero.
 
Ukiwa mjinga ni bora unyamaze,

Kwa wasiofahamu, ngoja niweke wazi.

Tanesco haijaisamehe zanzibar isipokuwa ni mkataba baina ya nyerere na Karume waliokubaliana kuhusu nishati ya umeme.

Ikumbukwe kuwa zanzibar ilikuwa na vyanzo vyake vya umeme kama generator na mashine maalumu zilizopo ndani ya meli, na umeme ililetwa toka nchi za arabuni. Baada ya kuungana Nyerere akamuomba karume asitishe ule mpango na kumuahidi kuwa watapata umeme wa gharama nafuu kama ule wanaoupata znz.

Kama hamjui ulizeni sio mkurupuke.. HUU NI MKATABA NA SIO FADHIRA.
 
1. kama sii kuwa na nhi moja ni bora Tanganyika na Zanzibar zikawa huru na kujiunga na Afrika Mash ....ni tija kubwa kuliko Muungano wa sasa!
2. Bara wanaburuzwa ...angalia Mtoto wa Mwinyi mzanzibari NI WAZIRI WA AFYA BARA!!!

SASA KUHU BARA MUUNGANI INATUSAIIA NINI?
 
Ukiwa mjinga ni bora unyamaze,

Kwa wasiofahamu, ngoja niweke wazi.

Tanesco haijaisamehe zanzibar isipokuwa ni mkataba baina ya nyerere na Karume waliokubaliana kuhusu nishati ya umeme.

Ikumbukwe kuwa zanzibar ilikuwa na vyanzo vyake vya umeme kama generator na mashine maalumu zilizopo ndani ya meli, na umeme ililetwa toka nchi za arabuni. Baada ya kuungana Nyerere akamuomba karume asitishe ule mpango na kumuahidi kuwa watapata umeme wa gharama nafuu kama ule wanaoupata znz.

Kama hamjui ulizeni sio mkurupuke.. HUU NI MKATABA NA SIO FADHIRA.

mkataba huu mzuri kweli,maana unawanufaisha wazenj,,,,,bora tuchukue bahari yao,,,maana nao ni mkataba,,,,,,PATAMU HAPO,NA MAFUTA JE???,NA KOD ZA TRA TUWATOZE
 
Kibera nae?????
1. kama sii kuwa na nhi moja ni bora Tanganyika na Zanzibar zikawa huru na kujiunga na Afrika Mash ....ni tija kubwa kuliko Muungano wa sasa!
2. Bara wanaburuzwa ...angalia Mtoto wa Mwinyi mzanzibari NI WAZIRI WA AFYA BARA!!!

SASA KUHU BARA MUUNGANI INATUSAIIA NINI?
 
WaBara kama imewauma Kwanini msiende mahakamani kama mlivyofanya kwa ile kuzuia TUZo ya Dowans kulipwa mabilioni na Tanesco?

Acheni kulalama. Kama imewauma mahakama zipo wazi kwa ajili yenu.
Hili si deni la leo au jana. Tangu umeme uvushwe Wazanzibar wamekuwa wanatumia bure Baru baru! Kinachouma si wao kupewa zawadi, ni kauli zao za kinafiki kuwa hawafaidiki na muungano huku wakijua umeme wanaotumia ni zao la muungano.
Hili halisemwi hata kidogo. Tena umeme huo umepelekwa na Nyerere, sasa sikiliza wanavyomtukana yeye binafsi na ukristo wake! Kwa siri unamsikia makamu wao wa rais yupo Israel kwa nduguze Yesu wa damu! Unafiki ni kitu kibaya sana.

Lakini twende mahakani kwa mangapi? Mishahara ya Wazanzibar inachotwa hazina, wanaosoma elimu ya juu ni bureee!
Wabunge wa Zanzibar wanalipwa na kodi za Mtanganyika.

Haya huyasikii katika malalamiko yao, kama sehemu nzuri ya muungano. Utakachosikia ni 'uhaini na uhalifu wa Nyerere' Unafiki wa aina hii unatisha.

Haya ndiyo wanayotaka yawe katika mkataba, yaani vitu vya buree. Ikigusa kwao utasikia 'mafuta si ya muungano' unafiki huu. Kama mafuta si ya muungano ambayo ni nishati kama umeme, kwanini umeme uwe wa muungano! manafiki

Utasikia marufuku Mtanganyika kupata ajira, wasichosema ni kuwa wao wamepata ajira ndani ya Tanganyika kuliko sehemu nyingine yoyote wanaoishi duniani. Unafiki

Mtanganyika marufuku kumiliki ardhi, wao wana mapande ya kutosha tu bila bughudha kuanzia marais wao hadi mvuvi. Unafiki huu!
Huku wakiwa wamejaa kila kona ya bara wanachokifanya ni kuwachoma moto Watanganyika waishio kwao. Yaani adui yao ni Mtanganyika kuliko mwadamu mwingine katika uso huu wa dunia.
Hukumu ya kuchoma binadamu wanaipata wapi? Sikiliza makongamano wanavyonukuu aya za mwenyezi mungu! wakitoka hapo wanamtafuta Mtanganyika wamtie kibiriti.

Wameunda baraza lao la mitihani, lakini viwango vya kujiunga na elimu ya juu wantaka viwe 'special kwao' unafiki !

Mimi ni mpenzi wa muungano wa vinchi hivi vidogo na masikini kama vyetu. Lakini muungano wa kinafiki na kelele za kinafiki sikubaliani nazo. Tumechoka kusikia matusi huku Wasukuma, Wangoni, Wanyaturu n.k wakiendelea kulipa kodi kwa ajili ya watu kusema hovyo! watu wasio wakweli na wasio na shukrani hata kwa chema kidogo
 
Yaani huo mkataba ni kwa Zenji peke yake si wateja wote wa TANESCO?
Mkivunja muungano tuu mturudishie ela yetu
 
Usipokubali kuliwa kidogo huli wewe unataka kula tu bila kuliwa! Haiwezekani! Hawa jamaa ni honey wetu so lazma tuingie gharama kidogo kuwaweka sawa
 
Wilaya ya Maswa wamekosa maji takribani wiki moja sasa baada la idara ya maji wilayani humo kushindwa kulipa deni la mil 25 leo hao wanasamehewa mabilion..kwanini tusidai Tanganyika yetu
 
Kwani ndani ya TANESCO hakuna waZNZ? Kwani wizara ya nishati na madini hakuna waZNZ, Je serikali yote ya JMT hakuna waZNZ?. Hamuoni upendeleo wote mnaofanyiwa na TZ bara ila nyie kila kukicha mnalalama kero za muungano..
huku mnasahau hiyo serikali mnayoilalamikia wamo pia viongozi wenu


Walichokuwa wanakidai Zanzibar kina uhalali, na wala hawajafanyiwa hisani. Walikataa kupandishiwa bei ya umeme kwa hoja ya kwamba ongezeko hill limechangiwa zaidi na uzembe, ufisadi na kutokuwajibika kulikofanywa na Tanesco na wadau wake, na si kutokana na mfumuko wa bei. Niliwahi kumsikia mwakilishi mmoja akihoji kuwa vipi madhara ya rushwa iliyoliwa na mtendaji wa Tanesco ailipe mzanzibari??? Hivyo wakataka iwekwe unit cost ya kuzalisha umeme bila ya kuingiza fidia wanazolipwa Richmond na gharama nyenginezo wanazopata Tanesco kwa kuingia mikataba mibovu

Ikumbukwe katika mikataba kuna kipengele kinachoeleza kuwa upande mmoja hautowajibika kutokana na uzembe (negligence), uharibifu (damages) au ufisadi (corrupt practices) utakaofanywa na upande wa pili au washirika wake. Kimantiki Zanzibar wanahoji uhalali wa ongezeko la bei ya umeme kuanzia mwaka 2008 na wako tayari Tanesco walete mchanganuo wao wa gharama za matumizi ili ibainike kwa kiwango gani ongezeko limechangiwa na mfumuko wa bei na kuongezeka kwa gharama za maisha, na kwa kiasi gani limechangiwa na ubadhirifu na utendaji mbovu, ili kila upande ubebe msalaba wake mwenyewe
 
Wilaya ya Maswa wamekosa maji takribani wiki moja sasa baada la idara ya maji wilayani humo kushindwa kulipa deni la mil 25 leo hao wanasamehewa mabilion..kwanini tusidai Tanganyika yetu

....Mkuu Crashwise hii nafasi ya kuchangia nini kiwemo katika katiba mpya ni nafasi nzuri sana kwa Watanganyika kuitumia ili kudai Tanganyika yetu, tukiipoteza hii sidhani kama tutapata nafasi nyingine kama hii.
 
Kama kweli huo mkataba wa namna hiyo upo basi wapaswa kufutwa haraka. Wanaopendelewa hawaridhiki na zaidi wanaleta madharau. Ingelikua busara wasamehewe na wateja wa TZ bara pia.


Ukiwa mjinga ni bora unyamaze,

Kwa wasiofahamu, ngoja niweke wazi.

Tanesco haijaisamehe zanzibar isipokuwa ni mkataba baina ya nyerere na Karume waliokubaliana kuhusu nishati ya umeme.

Ikumbukwe kuwa zanzibar ilikuwa na vyanzo vyake vya umeme kama generator na mashine maalumu zilizopo ndani ya meli, na umeme ililetwa toka nchi za arabuni. Baada ya kuungana Nyerere akamuomba karume asitishe ule mpango na kumuahidi kuwa watapata umeme wa gharama nafuu kama ule wanaoupata znz.

Kama hamjui ulizeni sio mkurupuke.. HUU NI MKATABA NA SIO FADHIRA.
 
Back
Top Bottom