Salary Slip
JF-Expert Member
- Apr 3, 2012
- 47,013
- 144,371
Mamlaka ya udhibiti wa manunuzi ya umma PPRA imeanza kufanyia uchunguzi mchakato wa zabuni wa kununua mafuta mazito uliosababisha mvutano kati ya TANESCO na wizara ya Nishati na Madini.
PPRA itachunguza mchakato uliotumiwa na wizara ya nishati na madini kuipatia kampuni ya PUMA zabuni ya kusambaza mafuta mazito wakati mchakato wa zabuni hiyo ulikwisha kamilika.
Lakini PPRA pia itachunguza utaratibu uliotumiwa na TANESCO kuipatia zabuni kampuni ya Oryx.Afisa mmoja wa PPRA amesema wizara nayo lazima ichunguzwe ni kwanini ilikubali kuipa zabuni kampuni ya PUMA nje ya taratibu zilizoanishwa kisheria.Afisa huyo alisema kuwa ktk swala la zabuni kuna taratibu na wao PPRA kinachowafanya waichunguze wizara ni kutaka kuona huyu mzabuni(PUMA) aliyekuja nyuma kushawishi ni taratibu gani zilitumika kumpa zabuni.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya mamlaka hiyo vinatilia shaka uadilifu wa kampuni hiyo ya PUMA ambayo seriali ina ubia kutokana na hatua yake ya awali kugoma kuuza mafuta kwa bei ambayo iliwekwa na serikali.
Source:Gazeti la habari leo la tarehe 06/08/2012.
PPRA itachunguza mchakato uliotumiwa na wizara ya nishati na madini kuipatia kampuni ya PUMA zabuni ya kusambaza mafuta mazito wakati mchakato wa zabuni hiyo ulikwisha kamilika.
Lakini PPRA pia itachunguza utaratibu uliotumiwa na TANESCO kuipatia zabuni kampuni ya Oryx.Afisa mmoja wa PPRA amesema wizara nayo lazima ichunguzwe ni kwanini ilikubali kuipa zabuni kampuni ya PUMA nje ya taratibu zilizoanishwa kisheria.Afisa huyo alisema kuwa ktk swala la zabuni kuna taratibu na wao PPRA kinachowafanya waichunguze wizara ni kutaka kuona huyu mzabuni(PUMA) aliyekuja nyuma kushawishi ni taratibu gani zilitumika kumpa zabuni.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya mamlaka hiyo vinatilia shaka uadilifu wa kampuni hiyo ya PUMA ambayo seriali ina ubia kutokana na hatua yake ya awali kugoma kuuza mafuta kwa bei ambayo iliwekwa na serikali.
Source:Gazeti la habari leo la tarehe 06/08/2012.