Tanesco/serikali wanatumaliza

Magezi

JF-Expert Member
Oct 26, 2008
3,359
692
SHIRIKA LA UMEME TANZANIA


TANGAZO KWA WATEJA NA WANANCHI KWA UJUMLA:
MALIPO YA USHURU KWA AJILI YA MFUKO WA UMEME VIJIJINI

  • Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kuwatangazia Wateja Wake na wananchi kwa ujumla kwamba, kuanzia tarehe 1 Septemba, 2009, Wateja wote wanaotumia umeme watatakiwa kulipa ushuru kwa ajili ya mfuko wa umeme vijijini.

  • Ushuru huu unatozwa kwa mujibu wa Tangazo la Serikali (GN) la tarehe 1 Agosti, 2008 na kama inavyoainishwa katika sheria ya Bunge kuhusiana na Wamlaka wa Umeme Vijijini (Rural Energy Act of 2005) Kifungu namba 19 (3) (c) na (d).

  • Ushuru huu ni kwa ajili ya mfuko wa Umeme Vijijini ambao matumizi yake ni pamoja na kuongeza kasi ya usambazaji Umeme Vijijini na mafunzo kwa wajasiliamali ili kuboresha maendeleo ya jamii kwa kutumia nishati bora vijijini. Ushuru huu utakuwa ni asilimia tatu (3%) ya thamani ya umeme uliotumiwa katika mwezi husika, yaani juu ya gharama ya matumizi ya Umeme.

  • TANESCO ni mkusanyaji tu wa ushuru huu ambapo makusanyo yote yatakabidhiwa kwa wakala wa Umeme Vijijini (REA).

  • Ushuru huu utaonekana katika Ankara ya umeme kama ifuatavyo: VAT 18% + EWURA 1% X REA 3% hii inatokana na upungufu wa nafasi katika fomu ya Ankara, hata hivyo kwa sasa tunatengeneza fomu mpya ambayo itaonyesha kila gharama peke yake, tunategemea fomu hii itakuwa tayari kabla ya mwisho wa mwaka 2009.



Imetolewa na: OFISI YA MAWASILIANO
TANESCO MAKAO MAKUU
 
Upumbafu tu wa Tanesco na serikali, hivi hela yote ya richmond, kiwira, IPTL mbona imepotea bure leo mnaanza kutubebesha mzigo sisi watumiaji wa umeme??

Yaani utafikiri tanesco hakuna watu walio enda shule, kwa sababu uwezo wa kufikiri njia mbadala ya kuweka umeme vijijini.

Hivi ni kwa nini kampuni binafsi zisipewe wilaya moja moja au mbili kulingana na uwezo wa kampuni wakazalisha umeme na kuuza kwa wananchi?? Hili linashindikana nini?? au ndo maslahi binafsi??
 
mzigo wote unakwenda kwa mtumiaji wa mwisho. OK tutawasha vibatari.

Na vipi sisi wa huku Utete na kibiti, mnatuwashia umeme lini?
 
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) linapenda kuwatangazia Wateja Wake na wananchi kwa ujumla kwamba, kuanzia tarehe 1 Septemba, 2009, Wateja wote wanaotumia umeme watatakiwa kulipa ushuru kwa ajili ya mfuko wa umeme vijijini.


Eti Shirika LINAPENDA! As if ni jambo la kupendeza. Nilitegemea wangesema shirika LINASIKITIKA. Wataalam wa lugha, hiyo imekaaje? Grrrrrrrrrrrrrrrrrrrrrr!!!!
 
Hivi hawa Tanesco wataendelea kutupandishia bei ya umeme mpaka lini ?.Kila siku wanatafuta misamiati na kujenga hoja za kijinga kama sababu za kupandisha umeme.
 
Hivi hawa Tanesco wataendelea kutupandishia bei ya umeme mpaka lini ?.Kila siku wanatafuta misamiati na kujenga hoja za kijinga kama sababu za kupandisha umeme.

Ndo maana mimi nasema uwezo wa kufikiri wa viongozi wa tanesco/serikali ya CCM umekwisha. Husikii hata siku moja wana mkakati wa kujipatia mapato au kurahisisha kazi zao bila kutegemea bill za umeme.

Halafu Ngeleja sijui anafanya nini pale wizarani, pamoja na kuwa alipongezwa na Pinda.
 
CCM inatafuta pesa za kampeni jamani...

inawezekana mkuu make huwa ndo zao, zamani walikuwa wanashurutisha mashirika yote ya umma kutoa pesa za kampeni bila maelezo nadhani sasa wanatumia mbinu za kuuhadaa umma.
 
Huu ni ufisadi mtupu watu wanatafuta jinsi ya kula hela za wananchi, Kodi mle nyie sasa mnatafuta kodi nyingine kupitia umeme? Yale mamilioni ya richmond mmemega kimiakimia sasa mnatafuta mfuko wa kutunyonya tena hakika hii nchi imelaaniwa toba yarabi nyie mafisadi ipo siku yenu tu. Wadau hebu hili swala tafuteni jinsi ya kulisitisha maana ni ufisadi mwingine unanyemelea kwani hao tanesco wanapata shilingi ngapi kwetu mpaka watuongezee kodi ya kizushi? Walikuwa wanalipa kampuni hewa mamilioni kwa siku leo hii kupeleka umeme vijijini watukate sisi? Sasa wakishapeleka na wakaanza kukamua hela kwao watafuta au ndo itakuwa ya kudumu? Na wakishapeleka je watakuwa wanaturudishia pesa zetu walizopelekea au ndo tutakuwa tumejila?

Wadau tusaidiane
 
polen sana mnaonekana mwaumia na hilo lakini sidhan kama mwanishindwa. hivi inawezekana kupika pombe usionje? unajua nauliza hili kwa sababu kianzi mlimba morogoro wanazalisha umeme lakini kuna watu wanatumia koroboi. hilo tangazo lao la umeme vijiji ni umbea tu, kampeni zao hizo. kanzi na idodi ilikoungua shule ni ulimi na pua hivi community concern za haya makampuni ni zip?
 
polen sana mnaonekana mwaumia na hilo lakini sidhan kama mwanishindwa. hivi inawezekana kupika pombe usionje? unajua nauliza hili kwa sababu kianzi mlimba morogoro wanazalisha umeme lakini kuna watu wanatumia koroboi. hilo tangazo lao la umeme vijiji ni umbea tu, kampeni zao hizo. kianzi na idodi ilikoungua shule ni ulimi na pua hivi community concern za haya makampuni ni zip?
 
Back
Top Bottom