Tanesco Luku itakuwa offline kwa siku kumi!

Kang

JF-Expert Member
Jun 24, 2008
5,495
2,250
Kuna mtu ameniambia watu wanakimbilia kununua LUKU kwa kuwa system ya tanesco itakuwa offline hadi tarehe 16 kuanzia leo. Hii ni kwa ajili ya matengenezo ya system yao.

Kuna ukweli kwenye hii habari?
 
Hivi Hili Shirika halina back Up System? siku zote limekalia Ufisadi tu? Haliwezi hata kuwa Na back up system ina maana Wanashindwa kuwa na Mitambo ya Kisasa Server Za maana ili waeweze kuwa na Access kila kona ya nchi kama mfano wa ATM Mashine Mbona Leo Viji benki Uchwara vina Afford kuwa Na mitandao Kama Hiyo Wao Wanashindwa Wanachoweza ni ufisadi Wa IPTL <Net Group Solution,Richie Man Monduli Na Dowans> Nimesikitika Kukuta Foleni Zenye Mistari Mirefu Mno katika vituo vya Mafuta vilipo viji ofisi vya kuuzia LUKU aibu
 
Huyo ndio Rashid ameanza kutukomoa na muungwana antabasamu tu!! Anaogopa akimfukuza waislamu watamwambia unaona anamfukuza muislamu mwenzie; katika kuendesha mambo ya nchi hakuna udini wala undugu; Nyerere alimfukuza kazi mdogo wake Joseph alipokuwa RC Mwanza!!
 
Ni kweli kabisa ni aibu kutokuwa na redundancy server na system...ina maana zikifa ndio mchezo kwisha..hawa wana utani wajua hawa...sasa wanatukomoa kwa maana sio maana yake heri wangetupa option kuwa kwa kipindi hicho unaweza kwenda neg balance system zikirejea watakata pesa zao kwanza kwenye luku ya mwanzo utayonunua.wanatukomoa???poa tu ila tutaongea hatutakaa kimya...tena kizazi hiki kinajua haki yake
 
Hata mi naona kama hakuna maelezo ya maana kwa nini system nzima iwe offline. Wengine tumeshawahi kuona system overhaul katika mashirika makubwa na haiwezekani eti kazi zote zinasimama kwa siku 10, maximum ni time za uciku maybe siku moja kuanzia saa 2 uck hadi saa 1 asubuhi. Lakini si siku 10 mfululizo. Hii ni hatua ya Dr Idris thumbing his nose at us!
Alafu mbona hawajatoa taarifa wiki moja kabla? Kwa nini iwe kama rumours tu, mtu unasikia through word of mouth, official information inakuja 12 hours before deadline. Hatuko serious! Hii ni ishara ya kutukomoa, eti Dr Idris is flexing his muscles?! Ngoja aone wananchi watakapoamua kuflex their muscles itakuwaje!
 
Hili shirika lina ukiritimba..ligawanyike..ktk mashirika matatu (3 in One)..uzalishaji, usambazaji na uuzaji!

Actually hii ya kuuza umeme wangecontract out kwa watu makini TANESCO wangekusanya over 80% ya mapato! Nina wasi2 kuwa mikoani pesa nyingi haikusanywi watu wanatumia tu umeme kwa kujiunganishia bure tu! Kuna watu Moshi na Arushi Vijijini kwa miaka mingi hawalipi au hulipa tu % ndogo sana ..wao huwakatia tu posho ndogo jamaa wa TANESCO!

Taabu sasa wenyewe wanfanya kila kitu..ndo mawzo mgando hayo!
 
Hili shirika lina ukiritimba..ligawanyike..ktk mashirika matatu (3 in One)..uzalishaji, usambazaji na uuzaji!

Actually hii ya kuuza umeme wangecontract out kwa watu makini TANESCO wangekusanya over 80% ya mapato! Nina wasi2 kuwa mikoani pesa nyingi haikusanywi watu wanatumia tu umeme kwa kujiunganishia bure tu! Kuna watu Moshi na Arushi Vijijini kwa miaka mingi hawalipi au hulipa tu % ndogo sana ..wao huwakatia tu posho ndogo jamaa wa TANESCO!

Taabu sasa wenyewe wanfanya kila kitu..ndo mawzo mgando hayo!

Hapa umenena mkuu lakini sio kazi ndogo hii check ofgem wa uk wanavyoangaika to get competition into the grid and selling part of the network even though supply ya umeme huku ulaya sio issue..issue infrastructure za kusambaza na kuconnect na EU. Barriers for the new comers into these grids ambazo incumbents wameshikiria ndo tatizo lao kubwa..sisi tanzania tatizo letu lipo kwenye kwenye stage zoote (supply, transmission and selling). Yani kama nilvyowahi kutoa maoni mwanzo tukileta a competition regulator from EU aje bongo anaweza kuonekana racist kwa matusi atakayoyasema kuusu tunavyoendesha institution zetu ...TANZANIA TATIZO SIO TANESCO TATIZO ni SERIKALI KUTOK KUWA NA POLICY zAMAANA KWENYE UENDESHAJI WA KILA INSTITUTION. LEO TANESCO KESHO NSSF KESHO KUTWA TTCL etc etc etc ..WOTE WAMEOZA!! inasikitisha na kutuvunja moyo wa kurudi home :-(
 
This couldn't come at the worst possible time, too bad to customers, politicians, Tanesco na hata government.

CLASSIC EXAMPLE OF WHERE WE PUT OUR EFFORTS AS THE GOVERNMENT; RELI MAUTIUTI, UMEME IN THE MORTUARY, BANDARI IKO PSYCHIATRIC WARD, AFYA IMEPARALYSE KUANZIA SHINGONI KWENDA CHINI, AIR TANZANIA IMESHAOSHWA IKO MAKABURINI TUNAZIKA, MAJI NDIO USISEME... SIJUI SIJUI SIJUI

ANYWAY, NGOJA TUPATE VITAMBULISHO VYA URAIA LABDA VITASAIDIA KUWATAMBUA WAGENI WANAMENG'ENYA ARDHI YETU
 
Back
Top Bottom