MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 705
WanaJF
Sisi wakazi wa Mbezi Beach tumekuwa tukiumizwa bila kupewa sababu ya msingi na hawa "ndugu" zetu wa TANESCO, kwani wamekuwa - kwa takriban mwezi mmoja sasa - na desturi (si tabia) ya kukata umeme bila kutoa taarifa, wakati mwingine mara mbili au tatu kwa siku, kwa muda mfupi na kisha kurejesha, na kama wanakata mara moja, basi umeme unarejeshwa baada ya saa sita au zaidi.
Meneja Uhusiano wa TANESCO, "dada" yangu, Badra Masoud, alitamka rasmi wiki iliyokwisha kwamba "mgao" wa umeme sasa haupo tena. Je, kinachoendelea huku Mbezi Beach - KILA SIKU - nini, kama si mgao?
Mwenye habari zaidi atuelimishe. LAKINI INAKERA!
./Mwana wa Haki
Sisi wakazi wa Mbezi Beach tumekuwa tukiumizwa bila kupewa sababu ya msingi na hawa "ndugu" zetu wa TANESCO, kwani wamekuwa - kwa takriban mwezi mmoja sasa - na desturi (si tabia) ya kukata umeme bila kutoa taarifa, wakati mwingine mara mbili au tatu kwa siku, kwa muda mfupi na kisha kurejesha, na kama wanakata mara moja, basi umeme unarejeshwa baada ya saa sita au zaidi.
Meneja Uhusiano wa TANESCO, "dada" yangu, Badra Masoud, alitamka rasmi wiki iliyokwisha kwamba "mgao" wa umeme sasa haupo tena. Je, kinachoendelea huku Mbezi Beach - KILA SIKU - nini, kama si mgao?
Mwenye habari zaidi atuelimishe. LAKINI INAKERA!
./Mwana wa Haki