Tanesco imeshindwa kununua mafuta ya kuendeshea mitambo...? Tujiandae kwa mgawo mkubwa wa umeme

Mkeshaji

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
4,262
1,415
Wanabodi,
Inasemekana kuwa Shirika la Ugavi wa Umeme nchini Tanesco limeshindwa kununua mafuta kwa ajili ya mitambo ya kuzalisha umeme wa dharula.

Kwa mujibu wa mikataba ya uzalishaji wa umeme wa dharula ambayo shirika hilo limeingia na makampuni kadhaa ya kuzalisha umeme wa dharula ni kuwa Tanesco inawajibika pamoja na kulipia gharama za matengenezo, pia itatakiwa kununua mafuta ya kuendeshea mitambo ya kuzalisha umeme kwa makampuni hayo.
Makampuni hayo ni pamoja na Symbion, Aggreko na IPTL.

Kutokana na ukata huo, hadi sasa mitambo ya makampuni kadhaa ya kuzalisha umeme wa dharula imesimamisha shughuli za uzalishaji wa umeme huo wa dharula.
Mitambo ambayo imesimamishwa hadi sasa ni Symbion Dodoma (50MW), Aggreko Dar (50MW) na IPTL Dar (100MW).

Kutokana na mitambo hiyo kusimamisha uzalishaji, tayari maeneo kadhaa yameshaanza kuonja machungu ya mgawo wa umeme. Mgawo huu unatarajiwa kuwa mkali zaidi kwa kadri siku zinavyozidi kwenda kwani hata hali ya kina cha maji kwenye mabwawa ya kuzalishia umeme ya Mtera na Kidatu si nzuri sana.

Pamoja na kuwa Tanesco inakaribia kukamilisha ujenzi wa mtambo mwingine wa kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia pale Ubungo-Dar (100MW), lakini mtambo huo huenda usiweze kuzalisha umeme kwani inasemekana kuwa gesi iliyopo haitoshi kuweza kuongeza mtambo mwingine labda kama baadhi ya mitambo ya Symbion ambayo sasa inatumia gesi itaanza kutumia jet fuel. Tatizo linarudi tena palepale, mafuta hayo ni gharama kubwa sana na Tanesco inaonekana kushindwa kumudu gharama za ununuzi wa mafuta hayo.

Miradi mingi ya ujenzi wa vituo vya kuzalisha umeme ilikuwa inategemea ule mradi wa ujenzi wa bomba la gesi kutoka Mtwara hadi Ubungo Dar es Salaam. Lakini inaonekana kuwa mradi huo wa gesi tayari umeshaingia mushkeli. Mipango ilkikuwa bomba hilo liwe limekamilika ifikapo Desemba 2012. Hadi sasa hakuna kazi yoyote iliyoanza katika utekelezaji wa mradi huo.

My take:
Huu ni mwiba mwingine kwa watanzania.
 
Hio kitu mbona nilishaipost tangia jumatatu,aliyasema hayo january alipohojiwa na SupaMix(Zembwela&Baruti) mgao uliopo unasababishwa na aggreko na iptl washindwa kununua mafuta ya kuendeshea mitambo,mgao si tunapata huku kwetu mabwepande!!!!
 
naomba nisahishishwe kama kumbukumbu zangu hazipo sahihi.

Tarehe 15/02/2012 Tanesco walipandisha rasmi bei ya umeme kwa 40% baada ya kukubaliwa na EWALA. hiyo parcentage iliyoongezeka ni kwa ajili gani?

Mwaka jana bajeti ya wizara ya nishati na madini ilipokataliwa kupitishwa na bunge iliposomwa kwa mara ya kwanza ,walienda na kuirekebisha na kuweka hela nyingi sana kwenye tanesco ndipo wabunge vilaza wetu walipoipitisha kwa kelele, au zile namba walizoongeza kwenye bajeti ni za uongo?

Je? Suluhisho ni mgao? ikishondikana tunakoenda ili kutupunguzia kulaumu, wauze unit moja ya umeme hata kwa Tshs. 5,000 ili wenye pesa waendelee na maisha na asiye nayo awe anatumia umeme kwa ajili ya taa tu ili tujue moja nchi haina umeme.

Na hizi dharura watanzania tulishazikataa, sijui kwa nini wanaendelea kulala nazo tu nakuzaa nazo hadi zinatuzidishia matatizo namna hii

Nimechoka kulaumu uzembe wa watu wengine jamani, hivi hakuna mtu kweli wa kutimiza wajibu wake?
 
Hio kitu mbona nilishaipost tangia jumatatu,aliyasema hayo january alipohojiwa na SupaMix(Zembwela&Baruti) mgao uliopo unasababishwa na aggreko na iptl washindwa kununua mafuta ya kuendeshea mitambo,mgao si tunapata huku kwetu mabwepande!!!!
Kama January ndo aliyasema hayo basi kumbe hata Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge haielewi mikataba ya Tanesco na makampuni ya kuzalisha umeme.
Kimsingi, kwa mujibu wa mikataba hiyo anayepaswa kulipia gharama za matengenezo na uendeshaji ni Tanesco na wala siyo makampuni husika. Kama hayo makampuni yamekosa mafuta ni kuwa Tanesco imeshindwa kuwalipa hao jamaa pesa za ununuzi wa mafuta hayo.
 
Looh! huku Tabata mgao kama kawaida. Mimi nimechoka kuwazia juu ya maisha na hatima ya Tanzania ktk kila nyanja kwani kila jambo lipo hovyohovyo tu na ukisema upinge kwa njia ya maandamano basi wajinga wengine nao watakupinga kwa maneno..."eti ooh nchi yetu ni ya amani, hatutaki vita". Basi tuendelee kuumia na kulia vivyo hivyo!
 
naomba nisahishishwe kama kumbukumbu zangu hazipo sahihi.

Tarehe 15/02/2012 Tanesco walipandisha rasmi bei ya umeme kwa 40% baada ya kukubaliwa na EWALA. hiyo parcentage iliyoongezeka ni kwa ajili gani?

Mwaka jana bajeti ya wizara ya nishati na madini ilipokataliwa kupitishwa na bunge iliposomwa kwa mara ya kwanza ,walienda na kuirekebisha na kuweka hela nyingi sana kwenye tanesco ndipo wabunge vilaza wetu walipoipitisha kwa kelele, au zile namba walizoongeza kwenye bajeti ni za uongo?

Je? Suluhisho ni mgao? ikishondikana tunakoenda ili kutupunguzia kulaumu, wauze unit moja ya umeme hata kwa Tshs. 5,000 ili wenye pesa waendelee na maisha na asiye nayo awe anatumia umeme kwa ajili ya taa tu ili tujue moja nchi haina umeme.

Na hizi dharura watanzania tulishazikataa, sijui kwa nini wanaendelea kulala nazo tu nakuzaa nazo hadi zinatuzidishia matatizo namna hii

Nimechoka kulaumu uzembe wa watu wengine jamani, hivi hakuna mtu kweli wa kutimiza wajibu wake?
Mkuu hili shirika limebebeshwa mzigo mkubwa sana kutokana na maamuzi ya watu wachache ya kuingia mikataba ya kipuuzi. Kwa kuona mzigo huo Tanesco nao wakatafuta pa kuutulia. Na sehemu waliyoiona ni kwa mwananchi maskini.
Kwa hiyo pamoja na kuongeza hiyo 40% lakini bado pesa hiyo yote inakwenda kuwalipa makampuni yanayozalisha umeme. Shirika linaendeshwa kwa hasara lakini pia mwananchi maskini anabebeshwa mzigo mkubwa kwa uzembe/tamaa ya watu wachache.

Bajeti ya wizara ya nishati na madini iliposomwa kwa mara ya pili tuliahidiwa kuwa mgawo wa umeme utakuwa historia, na tukasomewa mipango lukuki ambayo kwa mujibu wa ile hotuba mingine ilitakiwa sasa hivi iwe imekamilika. Cha ajabu hakuna hata mmoja ulioanza utekelezaji wake na badala yake tunashughulikia "DHARULA" ambayo na yenyewe inatushinda.

Hivi hii nchi ina tatizo gani?
 
Mkuu hili shirika limebebeshwa mzigo mkubwa sana kutokana na maamuzi ya watu wachache ya kuingia mikataba ya kipuuzi. Kwa kuona mzigo huo Tanesco nao wakatafuta pa kuutulia. Na sehemu waliyoiona ni kwa mwananchi maskini.
Kwa hiyo pamoja na kuongeza hiyo 40% lakini bado pesa hiyo yote inakwenda kuwalipa makampuni yanayozalisha umeme. Shirika linaendeshwa kwa hasara lakini pia mwananchi maskini anabebeshwa mzigo mkubwa kwa uzembe/tamaa ya watu wachache.

Bajeti ya wizara ya nishati na madini iliposomwa kwa mara ya pili tuliahidiwa kuwa mgawo wa umeme utakuwa historia, na tukasomewa mipango lukuki ambayo kwa mujibu wa ile hotuba mingine ilitakiwa sasa hivi iwe imekamilika. Cha ajabu hakuna hata mmoja ulioanza utekelezaji wake na badala yake tunashughulikia "DHARULA" ambayo na yenyewe inatushinda.

Hivi hii nchi ina tatizo gani?

Mkeshaji tukiacha kushughulikia dharura ina maana kuna watu watakosa mkate wao ( capacity charges). Haingii akilini kwa nini kwa kipindi chote hiki serekali imeshindwa kununua mitambo kama hiyo wanayoikodisha kwenye makampuni binafsi na kuwapa Tanesco ili iweze kuepukana na hizo capacity charges ambazo hutozwa kila siku kwa hizo kampuni 4 karibu milioni 600.
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom