TANESCO board split on MD Rashidi's fate

Hii unaitoa wapi ? Tumeingia vita ya Kagera dola ikiwa kati ya sh. 7.00 na sh. 8.00. na tumemaliza vita dola ikiwa bado sh. 8.00. Miaka mitano baadaye 1984 dola ilikuwa bado ni chini ya sh. 10.00. Haya madai yako unayatoa wapi ? Kama kuna kitu alikitaa Mwalimu kata kata ni misaada yenye masharti na sharti mojawapo lilikuwa ni kushusha thamani ya fedha yetu. Unajua kwa nini alituomba tufunge mkanda ? Utanisamehe huu ni mchango wangu wa mwisho, kwaheri.

- Mkulu Mag3, hapa tupo ukurasa mmoja, unajua kwa kawaida huwa situpi risiti ya anything katika maisha yangu, hoja yako ni nzito na ninataka kuweka ushuhuda kwamba Mwaka 1983 nilisafiri kwenda majuu na nilinunua dola za US hii benki ya NBC karibu na Sanamu, dola moja kwa Shillingi 8.00,
Mwaka 1987 miwishoni nilisafiri tena kwenda majuu, benki hiyo hiyo nikanunua dola moja kwa shillingi 16.00, na ninazo risiti mpaka leo, ninakumbuka Mwalimu akilalamika kwenye hotuba yake ya Mbeya, kuhusu kupanda kwa bei ya matrekta ya kilimo kufikia Shillingi Laki Sita za Tanzania then,

- Balaa la kupanda kwa dola kulinganisha na shillingi, lilianzia kwenye Utawala wa Miwnyi na alipokuja Mkapa, ikawa a free fall!

Respect.


FMEs!
 
- Mkulu Mag3, hapa tupo ukurasa mmoja, unajua kwa kawaida huwa situpi risiti ya anything katika maisha yangu, hoja yako ni nzito na ninataka kuweka ushuhuda kwamba Mwaka 1983 nilisafiri kwenda majuu na nilinunua dola za US hii benki ya NBC karibu na Sanamu, dola moja kwa Shillingi 8.00,
Mwaka 1987 miwishoni nilisafiri tena kwenda majuu, benki hiyo hiyo nikanunua dola moja kwa shillingi 16.00, na ninazo risiti mpaka leo, ninakumbuka Mwalimu akilalamika kwenye hotuba yake ya Mbeya, kuhusu kupanda kwa bei ya matrekta ya kilimo kufikia Shillingi Laki Sita za Tanzania then,

- Balaa la kupanda kwa dola kulinganisha na shillingi, lilianzia kwenye Utawala wa Miwnyi na alipokuja Mkapa, ikawa a free fall!

Respect.


FMEs!

Bluray

Karudi kinyemela huyu sort him
 
Bluray

Karudi kinyemela huyu sort him

- Mkuu acha hizi, huu mfupa ulikushinda hata wewe sasa usiponze wenzio, jamani tafadhalini hebu nipeni nafasi nijadili taifa langu kwa amani, kwa nini ninawakosesha raha hivi? WHY? Wewe mwenyewe umeanzisha mjadala ambao huuwezi sasa umekabwa unajaribu kupoteza lengo as if wote humu hatuna akili, Bwa! ha! ha! jibu maswali hayo unayorushiwa!

- I mean give me a break, kila mtu analia lia tu hamna hoja, imebaki viroja tu, hapa kwetu ni masilahi ya taifa tu, hatuna peremende wala pipi, pleaaase! Bwa! ha! ha! aaaaagggggrrrrr! this is fun!


es!
 
- Mkuu acha hizi, huu mfupa ulikushinda hata wewe sasa usiponze wenzio, jamani tafadhalini hebu nipeni nafasi nijadili taifa langu kwa amani, kwa nini ninawakosesha raha hivi? WHY?

- I mean give me a break, kila mtu analia lia tu hamna hoja, imebaki viroja tu, hapa kwetu ni masilahi ya taifa tu, hatuna peremende wala pipi, pleaaase! Bwa! ha! ha! aaaaagggggrrrrr! this is fun!


es!


Sasa mbona ulikimbia mawe ya Bluray?

Mkuu Bluray karudi huyu.
 
Sasa mbona ulikimbia mawe ya Bluray?

Mkuu Bluray karudi huyu.

- Sikukimbia mawe ya mtu yoyote, hakukuwa na majibu ya swali moja tu ambalo to me ndilo lilikuwa the key to the debate likijibiwa ipasavyo sina noma kuendelea na debate anytime, na huko nyuma niliwahi ksuema kwamba furaha yako ni kuona vichwa vinavurugana hapa, wasiokuelewa vizuri ndio wanaohangaika, mimi hapana ninakujua vizuri sana na all your! games

- Sasa vipi wewe mbona unashindwa kuwajibu wakuu hapo juu au ndio unajaribu kutoka unyoya? Bwa! ha! ha!


es!
 
- Sikukimbia mawe ya mtu yoyote, hakukuwa na majibu ya swali moja tu ambalo to me ndilo lilikuwa the key to the debate likijibiwa ipasavyo sina noma kuendelea na deabte anytime,

- Sasa vipi wewe mbona unashindwa kuwajibu wakuu hapo juu au ndio unajaribu kutoka unyoya? Bwa! ha! ha!


es!

Sawa mzee wa sauti ya umeme kumbe Bluray ndie kashindwa kujibu swali moja tu.

Hat off mzee wa umeme kumbe Bluray si lolote wala chochote. Kama naaongopa aje hapa.

Nakukubali mzee wa sauti ya umeme bahari mdhoefu.

Peace
 
Hii unaitoa wapi ? Tumeingia vita ya Kagera dola ikiwa kati ya sh. 7.00 na sh. 8.00. na tumemaliza vita dola ikiwa bado sh. 8.00. Miaka mitano baadaye 1984 dola ilikuwa bado ni chini ya sh. 10.00. Haya madai yako unayatoa wapi ? Kama kuna kitu alikitaa Mwalimu kata kata ni misaada yenye masharti na sharti mojawapo lilikuwa ni kushusha thamani ya fedha yetu. Unajua kwa nini alituomba tufunge mkanda ? Utanisamehe huu ni mchango wangu wa mwisho, kwaheri.

Sasa wewe unadhani uamuzi wa nyerere ulikuwa wa busara kukataa mkopo wa masharti??? ulidhani uchumi ulivyo sasa hivi nani aliyasababisha? Nyerere alikuwa hana ubinafsi, mwenye mapenzi ya nchi but alikuwa na mtazamo finyu wa nchi angeliruhusu sekta binafsi, tukachimba mafuta, madini na uongozi imara aliouweka tusingelikuwa na matatizo ya kiuchumi tuliyonayo sasa halafu wewe unamfagilia!!! I mean come on!!!

Tuje kwenye mada husika Tanesco ni example of the failed governance structure za parastatals za Tanzania. ATC, Tanesco, TCC unakuta shirika linaendeshwa kihasara but unakuta matatizo tunayasababisha wenyewe. malimbikizo ya madeni, matumizi mabaya ya fedha, boards mbovu, wafanyakazi vihiyo, unakuta mashirika yanakufa. Idrissa hana makosa yeyote ni kwamba kakuta lisystem libovu lenye kuwa mtiririko wa matatizo unadhani anaweza kuyaondoa kwa kipindi kifupi alichokuwa Tanesco? Hata maximo aliwaomba watanzania muda sembuse Idrissa come on give him a break!!!
 
.............. Wakati wa Kasambala nakumbuka mzee wangu alilipa laki 7 kuunganishiwa mita hapo bado akaja kulipa 35000 ya mita yenyewe na kuhonga juu. haya nani msafi.......!!!

Halafu

..............inawezekana kabisa Kasambala hakuwapo kipindi hicho but it does preclude who was in charge (ambaye si Idrissa) kutumaliza sisi walalahoi kwa kutucharge laki saba tuunganishiwe mita kisa eti ziko haba..............

Hivi Wakuu bado mnaendelea tu kumuelimisha tu huyu jamaa.........!!
 
but alikuwa na mtazamo finyu wa nchi angeliruhusu sekta binafsi, tukachimba mafuta, madini na uongozi imara aliouweka tusingelikuwa na matatizo ya kiuchumi tuliyonayo sasa halafu wewe unamfagilia!!! I mean come on!!!

Katika hili ni muhimu kutambua mantiki ya Mwalimu kutotilia kipaumbele sekta binafsi, uchimbaji mafuta (kitu ambacho si kweli kwamba hakutaka) na madini..

Yote hayo yalikuwa yakifanyika lakini in a limited way. Kwa nini? Kwa sababu aliamini kuwa nchi bado haikuwa na INSTITUTIONS za kuweza kuhakikisha kuwa taifa linafaidikia na shughuli hizo....

Ukiangalia na hali iliyotokea baada ya wajuvi wengi kudharau mtazamo wake na kufakamia hayo, ni wazi alikuwa sahihi kabisa....

omarilyas
 
Kitu kimoja ninachosoma hapa ni umuhimu wa INTEGRITY. Na somo hili nadhani ni muhimu sana kwa vijana wote ambao wangelipenda hapo baadae kutumikia umma ama kuingia katika siasa. Ni wazi kuwa Dr Rashid ana mafanikio ya kujivuni katika Tanesco na ni wazi kuwa kati ya wanaompinga na hata kufikia kuandika magazetini habari zenye lengo la kumpa uzito Rais kumteua tena kuendelea na wadhifa wake huo wana maslahi yao wanayoyapiagania. Lakini kushindwa kwake kulinda INTEGRITY yake hapo kabla kunamfanya Dr Rashid kushindwa kutekeleza jukumu lake ipasavyo. He is vulnerable and so many of us in the near future we will find ourselves in that situation....

omarilyas
 
  • Dk. Idris Rashidi ampasua kichwa JK
  • Afunga virago TANESCO, mkakati waandaliwa kumrejesha

na Ratifa Baranyikwa

MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Umeme nchini (TANESCO), Dk. Idris Rashidi, tayari ameshafungasha virago baada ya mkataba wake kumalizika Novemba 30, mwaka huu, lakini serikali inafanya mkakati wa kumrejesha kisirisiri, Tanzania Daima Jumatano limegundua.

Mara ya kwanza Dk. Rashidi alipotaka kujiuzulu mwaka jana, Rais Jakaya Kikwete alikataa barua yake ya kujiuzulu, akidai kwamba angependa aendelee kutokana na utendaji wake ndani ya shirika hilo kuwa mzuri.

Vyanzo vya habari vya kuaminika vimeliambia gazeti hili kuwa tayari mkakati wa kumkatalia tena unaandaliwa, maana jina la Dk. Rashidi limepenyezwa miongoni mwa walioomba nafasi hiyo, ili kujenga mazingira ya kumrejesha katika nafasi yake.

Hata hivyo, mkakati huo unaweza kuigawa serikali kwa sababu kwa mujibu wa habari hizo, Dk. Rashidi anapingwa na watendaji wengi TANESCO na katika Wizara ya Nishati na Madini kutokana na msimamo wake wa kukabiliana na ufisadi ndani ya shirika hilo ambalo linajiendesha kwa kusuasua.

Hadi sasa nafasi ya Dk. Rashidi sasa inakaimiwa na Steven Mabada tangu Novemba 30, mwaka huu, baada ya kuondoka.

Septemba 18, mwaka huu TANESCO ilitangaza nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO na zaidi ya watu 50 walijitokeza kuomba ambako hatua za kuyachuja majina hayo na kubaki matatu zimekwishakamilika.

Alipoulizwa juu ya mchakato wa kumpata mrithi wa Dk. Rashidi, Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja alisema upo katika hatua za mwisho.

Ngeleja alikataa kuzungumzia mkakati unaoandaliwa kumrejesha Dk. Rashidi katika wajibu wake, lakini alisisitiza kuwa mchakato upo katika hatua za mwisho, na mtu atakayeshika nafasi hiyo atatangazwa wakati wowote kuanzia sasa.

Septemba 18, mwaka huu Bodi ya Wakurugenzi ya TANESCO ilitangaza nafasi hiyo katika vyombo vya habari na kuwataka watu wenye sifa wawe wamewasilisha barua zao za maombi kabla ya Oktoba 2.

Nafasi hiyo ilitangazwa baada ya Dk. Rashidi kuwa katika hatua za mwisho za kumaliza mkataba wake wa miaka mitatu uliokuwa ukimalizika Novemba 30, mwaka huu.

Kumekuwa na madai kuwa tangazo la nafasi ya mkurugenzi huyo ilitangazwa kwa siri pasipo Dk. Rashidi mwenyewe au menejimenti ya shirika hilo kuwa na taarifa zozote, jambo ambalo hata hivyo liliwahi kupingwa na Ngeleja.

Waziri Ngeleja ambaye amekuwa akisemekana kutoelewana na Dk. Rashidi, alisema kwa mujibu wa mfumo na utaratibu, bodi iliunda kamati ndogo kushughulikia suala la kutolewa kwa tangazo ambako kwa upande wa TANESCO, aliyeshirikishwa katika kamati hiyo ni mwanasheria mkuu wake.

Bodi ya TANESCO inaundwa na Mwenyekiti, Peter Ngumbulu ambaye anateuliwa na rais pamoja na wajumbe wanane wanaoteuliwa na waziri mwenye dhamana wa nishati na madini ambao ni Adola Mapunda, Victor Mwambalaswa (Mbunge) na Vintan Mbiro.

Wengine ni Beatus Segeja, Semindu Pawa, Ngosi Mwihava, Juma Bakari (ambaye ni Mkurugenzi wa Shirika la Umeme la Zanzibar - ZECO) na Agnes Bukuku anayetoka Hazina.

Uteuzi wa Dk. Rashidi kushika wadhifa huo wa ukurugenzi wa shirika hilo ulitangazwa na bodi hiyo mwishoni mwa mwaka 2006 baada ya serikali kuamua kuachana na Kampuni ya Net Group Solutions ya nchini Afrika Kusini ambayo nayo ilimaliza mkataba huku ikiiacha TANESCO ikiwa taabani.

Utendaji wa Dk. Rashidi uliingia dosari mwaka jana alipotangaza kuwa taifa lingeingia gizani iwapo serikali isingeridhia ununuzi wa mitambo ya kufua umeme kutoka Kampuni ya Dowans ambayo ilirithi mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura kutoka katika kampuni tata ya Richmond.

Mbali ya hoja hiyo kuihusisha TANESCO na njama za kuibeba kinyemela Dowans, ambayo tayari mkataba wake wa kuzalisha umeme ulivunjwa Agosti mwaka jana, Dk. Rashidi alilaumiwa kwa kutangaza uamuzi huo pasipo kupata idhini ya Bodi ya Wakurugenzi.

Badala yake, Dk. Rashidi aliamua kwenda kwenye Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma hali ambayo ilizua mjadala mzito kutoka kwa wabunge na watu wa kada mbalimbali. Kauli iliyomponza ni ile ya kusema, “taifa likiingia gizani tusilaumiwe.” Kutokana na hali hiyo, baadhi ya wajumbe wa bodi wakati ule walidhamiria kwamba mara baada ya kumaliza muda wake wa miaka mitatu, kamwe wasingekubali kumpa kipindi kingine ili aiongoze tena TANESCO.
 
Ukiona wanamng'ang'ania asiondoke basi lazima ujue kwamba jamaa ni Fusadi Papa, wanaogopa akija mwingine hawawezi kumwendesha.
 
wana JF nimesikia mchakato wa kumpata Mkurugenzi Mtendaji wa Tanesco atakayemrithi Dr Rashid zimekamilika, hivi serikali inasita nini kumtangaza huyo alieshinda usaili. wenye data tupeni hapa
 
Back
Top Bottom