tamko na picha CHADEMA DODOMA yalaani mauaji ya Arusha

kweleakwelea

JF-Expert Member
Nov 29, 2010
3,066
1,535
Wandugu wapendwa,

Maandamano ya Jumamosi Dodoma yalikuwa mazuri. shukurani za pekee kwa jumuiya ya wana UDOM kwa kujitokeza kuyapamba. maandamano haya yalitokea ofisi za mkoa Dodoma, yakaenda hadi soko la Majengo, yakapita independence square, hadi stand ya mkoa...toka hapo yakaelekea njia ya bungeni hadi CBE na kushika barabara ya makole. Yakanyoosha moja kwa moja hadi viwanja vya barafu.

Mkurugenzi wa organaizesheni Ben Kigaila ndiye aliyaongoza na ndiye aliyepokea tamko na kuhutubia. pamoja naye wagombea mbali mbali waliochakachuliwa na kiongozi wa wanafunzi wa udom waliopata nafasi ya kuzungumza na wananchi. Sam Kigaila naye akapewa nafasi ya kuzungumza...Sam ni soo!! sisiemu lazima wamejifunza kuwa hawataweza kuzuia nguvu ya umma kwa kumuangamiza Slaa kwani kuna topaz za uhakika nyuma yake....

Katibu wa mkoa aliweza kutamka rasmi kuwa polisi vihiyo mfano aliyekuwa karani wa mahita akipata cheo ndio mwanzo wa shida. inasemekana wakati maandamano yanaendelea mashuzi yaliwatoka wana ccm na kumpigia RPC kumuuliza kwanini ameruhusu maandamano. Naye aliwajibu kuwa ni ya amani. Polisi waliongoza maandamano yooote kwa uzuri.

Baada ya hapo kamanda kigaila alionana alifungua tawi la chadema kata ya uhuru, akapata kuzungumza na halafu akaonana na wanachadema tawi la UDOM ambao walimueleza mengi yakiwamo manyanyaso wanayofanyiwa na baadhi ya walimu kwa kuwa tu ni wanachadema. Aliahidi kuyafanyia kazi malalamiko hayo..

Baada ya hapo akaenda george town miyuji kuonana na wanafunzi wa chuo cha mipango. akiwa huko alionuyeshwa orodha ya papo kwa papo ya wanafunzi 300 ambao wanatyaka kadi. alihakikishiwa kuwa asilima 95 % ni wana chadema. Uongozi wa muda ulichaguliwa na kuambiwa utafute ofisi na uendelee kuandikisha wanachama. Mheshimiwa Mbowe atakuja kuzindua tawi na kukabidhi kadi..

Wakiwa na wanachuo hao wa mipango, mhenshimiwa dada kunti ambaye ni diwani aliyechakachuliwa wa ipagala aliwataka wanafunzi kuhimiza wanawake na kuanzia magirlfriend wao kuingia CHADEMA kwani ndio tofali lililobaki. Alisisitiza kuwa wanawake wana uwezo mkubwa wa kukinyanyua chama...

Picha za mwisho zinamwonyesha kijana akisimika bendera nyumbani mwa kweleakwelea!

Natuma picha hizi kubatilisha uwongo wa TBCCM kuwa maandamano hayakupata kibali cha wananchi na yalihudhuriwa na watu wachache!

Vyombo vya habari, kazi kwenu!

Naomba kuwasilisha!

IMAG0025.jpg

IMAG0029.jpg

IMAG0030.jpg

IMAG0033.jpg

IMAG0038.jpg

IMAG0046.jpg

IMAG0047.jpg
 
hakuna kitu itafanana na nguvu ya umma! huwezi amini gharama zooote zimekuwa zikilipiwa kwa mtindo wa papo na wananchi wenye nia ya kukomboa nchi yao! Tamko naona halijaonekana. nimeliposti hapa!

clip_image001.gif

clip_image003.jpg

TAMKO LA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO
CHADEMA MKOA WA DODOMA KULAANI MATUMIZI MABAYA YA NGUVU ZA POLISI MKOANI ARUSHA NA KUSABABISHA MAUAJI YA RAIA WASIO NA HATIA.

UTANGULIZI.
Ndugu Mgeni rasmi, awali ya yote tunamshukuru Mwenyezi Mungu kwa rehema na uzima anaozidi kutujalia. Tumekusanyika hapa leo hii kwa Amani, ili kuweza kuunga mkono Tamko la CHADEMA Taifa juu ya mauaji ya Raia watatu (1) Denis M. Shirima (2) Ismail Omari (3) Paulo Njuguna (Mkenya) wasiokuwa na hatia yaliyofanywa na Serikali dhalimu kupitia Jeshi la Polisi Mkoani Arusha. Lakini pia tunawapa pole wale wote waliofikwa na maafa mbalimbali yaliyosababishwa na vurugu zilizoanzishwa na Jeshi la Polisi

TUSIMAME KWA DAKIKA 1 KUWAKUMBUKA MASHUJAA HAO WATATU WALIOPOTEZA MAISHA.

MSIMAMO WA CHADEMA DODOMA JUU YA MAUAJI YA RAIA ARUSHA.

Ndugu Mgeni rasmi, CHADEMA (Mkoani Dodoma) tunaamini kabisa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ibara ya 20 (1) na Tamko la haki za binadamu la umoja wa Mataifa ya mwaka 1948, (yaani Universal Declaration of Human Rights) kuwa ni haki ya msingi ya kila Raia kuandamana kwa Amani ndani ya Nchi yake. Na Jeshi la Polisi kuwa kama nyenzo ya kulinda Amani na si kuvuruga Amani. Hii ni haki ya kikatiba ya wananchi wa Tanzania.

Ndugu Mgeni rasmi, imekuwa tabia ya CCM na Serikali kupitia Jeshi la Polisi kuwapora Raia wa Tanzania haki zao za msingi na za Kikatiba kwa kisingizio cha kuvurugika kwa Amani,jambo ambalo halivumiliki na halikubaliki. Watanzania wamejua na wanaamini kuwa Jeshi la Polisi ni chombo cha kuwalinda wao (Wananchi) na mali zao. Jeshi la Polisi kwa sasa limekuwa chombo cha kuvuruga Amani na kupora mali za Watanzania kwa kisingizio cha maono ya "kiintelijensia". Je Intelejensia" hiyo haiwezi kutumika kwa kutazama madhara ya kuzuia maandamano hayo ya Amani? Maandamano ya mazishi ya wahanga wa mauaji ya Arusha ni ushahidi tosha kuwa dhana ya inteligensia ni fikra potofu na hupikwa na kikundi kidogo cha watu kwa ajili ya maslahi yao.



Ndugu Mgeni rasmi, CHADEMA Dodoma, Tunawapa pole Ndugu na jamaa za mashujaa waliopoteza maisha katika harakati za kudai haki zao na za Watanzania wote kwa ujumla. Vilevile tunawapa pole majeruhi wote walioumizwa na Jeshi la Polisi linalotaka kuingiza Tanzania katika machafuko makubwa. Tunawaombea majeruhi wote wapone haraka na kuwataka wasikate tamaa badala yake waendeleze mapambano mpaka kufikia lengo.

Ndugu Mgeni rasmi, Tunawapa pole na pongezi za dhati Viongozi wetu makini wa chama kitaifa Mwenyekiti Freeman Aikaeli Mbowe, na Katibu Mkuu Dr Wilbrod Peter Slaa, (Katibu Mkuu Taifa), na Wabunge wa majimbo na wa viti maalumu wa CHADEMA walioongoza mapambano dhidi ya Serikali dhalimu inayotumia nguvu nyingi na kodi za Watanzania waliopigika kupora haki zao.

Ndugu Mgeni rasmi, CHADEMA DODOMA tunalaani nguvu za kivita zilizotumiwa na Jeshi la Polisi Mkoani Arusha KUPAMBANA NA RAIA WASIO NA SILAHA WALIOBEBA MAJANI NA VITAMBAA VYEUPE, jambo lililopelekea mauaji ya watu watatu wasiokuwa na hatia na kupelekea wengine wengi kubaki vilema na majeraha yasiyokuwa ya lazima. Tunaungana na Viongozi wetu wa CHADEMA Kitaifa kulitaka Jeshi la Polisi kwanza kuwaomba radhi Watanzania kwa kusababisha majonzi makubwa yaliyogharimu maisha ya Ndugu zao, pili kuwataka wahusika wakuu waliosababisha vurugu hizo kuwajibika wakiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nchi Ndugu

Shamshi Vuai Nahodha, akifuatiwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Said Mwema au Bwana "Intelijensia" na Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha (RPC) Thobias Andengenye.

Ndugu Mgeni rasmi, Tunalitaka Jeshi la Polisi nchini kutoendeleza tabia ya kuwanyanyasa Wana wa nchi hii (Watanzania) kwa sababu ya maslahi ya watu wachache hasa Viongozi wa CCM, kinyume na hapo wao watakuwa wa kwanza kuhukumiwa kwa tabia hiyo, kwani Watanzania watashindwa kuvumilia. Tunalisihi Jeshi la Polisi kutoa Ulinzi na kuhakikisha usalama wa Watanzania hasa pale wanapotaka kupaza sauti zao kwa njia ya maandamano ya Amani. Polisi kamwe hawajapata mamlaka ya kisheria ya kuzuia mikutano ya hadhara na maandamano bali kuweka ulinzi na kuhakikisha sauti za watanzania zinafika mahali husika. Kupitia hadhara hii tunatangaza kusimamia haki zetu.

Sisi kama Watanzania tunaliagiza Jeshi la Polisi kuacha mara moja tabia ya kukurupuka na kutumia silaha nzito kwa Watanzania

wasiokuwa na hatia (vurugu) pindi wanapodai haki zao. Maandamano kama yale ya Arusha na ya wanavyuo mfano Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) yalikuwa ya amani na hayakustahili kukambiliana na mashambulizi ya kivita! Tunawapa pole watanzania wote waliokumbana na mikikimikiki kutoka kwa Jeshi la Polisi.
NINI CHANZO CHA JEURI YA JESHI LA POLISI.
Ndugu mgeni rasmi , CHADEMA DODOMA tunaamini kabisa kuwa jeuri ya jeshi hili la polisi linatokana na mambo makuu matatu:-
· Kwanza ni kutokuwa na katiba inayoeleza wazi zile haki za msingi za mtanzania na nguvu zake katika kutetea haki hizo.
· Pili ni kutokuwa na viongozi makini na wenye uwezo wa kuthubutu kuheshimu haki za watanzania, wakiongozwa na viongozi wa CCM .
· Tatu ni dharau na ukatili wa viongozi wa jeshi hilo waliokengeuka na kujengeka kifikra kwamba vyeo au madaraka wanayoyapata yametokana na uswahiba wao na viongozi wakuu wa serikali ya Chama Cha Mapinduzi!

Ndugu mgeni rasmi , sababu hizo, msingi wake hasa ni ubovu wa katiba yetu inayotoa mwanya kwa viongozi wa serikali na jeshi la polisi kutokuheshimu UMMA wa watanzania kwa kuwa katiba hiyo ilitungwa na watu wachache, kwa maslahi ya watu hao wachache na si watanzania wote.

Hivyo basi tunaisihi Serikali na kuitaka kuanzisha mara moja mchakato wa katiba mpya ( siyo marekebisho ) itakayotoa fursa kwa kila mwana wa nchi hii kueleza wazi hasa wanahitaji katiba ya aina gani kwa mstakabali wa Taifa hili.



Ndugu mgeni rasmi, tunapenda kutoa angalizo kwa Serikali kuwa, kutowashirikisha watanzania katika maamuzi juu ya katiba mpya kunaweza kulifikisha Taifa hili katika historia chafu ambayo haijawahi kutokea. Dalili za uchafu huu wa historia zimeanza kuonekana kwa kuwa ni tabia ya Serikali ya CCM kuwapuuza watanzania. Tunasisitiza hili " Maamuzi ya watanzania yaheshimiwe".

Ndugu mgeni rasmi , CHADEMA DODOMA tunaungana na Viongozi wetu kitaifa kuwasihi na kuwahamasisha watanzania kudai katiba mpya itakayoweka bayana ni Taifa gani wanalolihitaji watanzania. Tunaungana na umma wa watanzania wote kudai uandikwaji wa katiba utakaoongozwa na BARAZA LA KATIBA na kupinga tume inayotaka kuundwa na Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete. Tunasisitiza kuwa zoezi hili lianze mara moja ili kuzuia uwezekano wa uharibifu wa maendeleo na ustawi wa jamii kuendelea kujitokeza. Haya ni maangamizi kwa taifa. Ndugu mgeni rasmi, ni dhahiri kuwa katiba hii tuliyonayo sasa hivi ni kikwazo kikubwa cha maendeleo ya Taifa letu!

Ndugu mgeni rasmi. Tunaomba watanzania waendelee kuwa imara pasipo kutetereka katika kudai haki zao za msingi na kuendelea

kuwakumbuka Ndugu zetu mashujaa walioandika historia katika nchi hii kwa kufa kishujaa walipokuwa wakitetea haki zao na za watanzania wote kwa ujumla. Tunaomba watanzania wote kuendelea


kudumisha amani tuliyonayo ijapokuwa Serikali na jeshi lake la polisi wanataka na wameanza kuvuruga Amani hiyo.

Ndugu mgeni rasmi, tunalisihi jeshi la polisi kuelekeza nguvu zake na silaha zake nzito nzito kupambana na wahalifu wanaosumbua nchi hii kama majambazi na mafisadi yanayofilisi nchi na siyo kuwa warahisi wa kuwapiga mabomu watanzania waliokuwa huru ndani ya nchi yao kwa kipindi kirefu.

Pia tunaliomba jeshi la polisi kuelekeza nguvu zake za "Kiintelijensia" katika kutabiri na kugundua madhara na athari za mikataba inayoingiwa na Serikali (hilo ndilo la msingi kwa watanzania). Kama vile Dowans, Meremeta, Kagoda kwa kutaja machache tu.

Tunalitaka jeshi la polisi lijenge utamaduni wa kusema ukweli na kuondokana na utamaduni wa kuwabambikia raia kesi mbalimbali ambazo haziwahusu. Mfano wa hili ni mbinu chafu ambazo zinaendelea chini ya jeshi la polisi kuhariri na kurusha kwenye runinga picha zinazoonyesha kuwa CHADEMA ndio chanzo cha vurugu za Arusha! Umma mzima umeshuhudia kuwa maandamano yalikuwa ya amani kwa urefu wa kilomita mbili hadi pale polisi kwa makusudi walipoamua kuanzisha vurugu kwa kuwashambulia waandamanaji kwa

mabomu na risasi za moto. Mkanda huu lakini haukuonyesha polisi walivyodhalilisha na kunyanyasa raia waliowapiga, kuvunja vioo vya

magari, na kupora mali za raia. Tunamtaka kamanda Paul Chagonja kwa niaba ya polisi kuuomba radhi umma wa watanzania kwa juhudi zake za makusudi za kupotosha ukweli na kutetea uovu mkubwa uliofanywa na jeshi la polisi. Tunasisitiza kuwe na tume huru ya kuchunguza mauaji haya. Pia tunasisitiza kuwa viongozi wa CHADEMA na watu wote waliobambikiwa shauri hili wafutiwe kesi, na waachiwe huru bila ya masharti yoyote.

Tunamtaka pia Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda atamke rasmi tarehe ya kufanyika kwa uchaguzi halali wa Meya wa Jiji la Arusha. Tunamtaka Mh. Pinda atumie wepesi ule ule alioutumia kusimamisha uchaguzi wa meya wa Manispaa ya Kigoma baada ya kulalamikiwa na Chama Cha Mapinduzi. Katika tukio hili Mh. Pinda aliweza hata kupora uhuru wa mahakama na kusimamisha uchaguzi. Maendeleo ya wananchi ni zaidi ya vyeo vinavyong'ang'aniwa na Chama Cha Mapinduzi.

CHADEMA inatoa rai kwa raia wote wa Tanzania kusimama kidete kwa ajili ya haki na maendeleo ya taifa lao. Watanzania wa kada mbalimbali wake kwa waume, wazee kwa vijana, wawe wanasiasa, wasomi, wafanyabiashara, wanafunzi, wakulima na wafanyakazi kuungana mkono na kuhakikisha ustawi wa nchi yetu hauwekwi rehani kwa maslahi ya watu wachache. Tunapaswa kuulinda na kuutetea ustawi wa nchi yetu kwa maslahi ya kizazi hiki na kile kijacho.



Ndugu mgeni rasmi, tunamalizia kwa kusema "Jeshi la polisi litambue kuwa kwa kupitia kodi za raia wa Tanzania, ndipo mishahara yao na posho zinalipwa, pia zana za kazi zao zinanunuliwa. Jeshi la polisi
liwaheshimu watanzania kwani lipo kwa ajili ya kuwalinda wao na mali zao na sio kuwatia ulemavu na kuwapotezea maisha.

Tanzania bila ubabe inawezekana!

Ndugu mgeni rasmi; tunaomba kuwasilisha hoja
MUNGU IBARIKI CHADEMA
MUNGU IBARIKI TANZANIA
MUNGU IBARIKI AFRIKA

"Mungu warehemu mashujaa wetu hawa ISMAL OMAR, DENIS MICHAEL na PAULO NJUGUNA (Mkenya ) wapumzike kwa amani.
TUNAJIVUNIA NGUVU YA UMMA.
PEOPLE'S POWER
__________________________
Steven E. Masawe
KATIBU MKOA
CHADEMA.
 
Tunashukuru sana kwa picha na tamko zuri. Adha,ni bora umefanya vema haraka kukanusha wanafiki TBC
 
Tatizo kubwa ni kwamba katika maandamano hayo wakazi au wenyeji wa Dodoma hawakuhudhuria wala hata kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya barafu wakazi au wenyeji wa mji wa Dodoma hawakuonekana. Wengi waliohudhuria walikuwa ni wanafunzi wa UDOM. Sababu kubwa ni nini? Wana Dodoma, badilikeni!
 
dhehebu la ccm lilijikita mapema zamani hapa dodoma na kuweka ngao. actually, dodoma kuwa makao makuu ya nchi ilikuwa ni proposal ya mjerumani. kitu kikubwa ambacho mjerumani alikiona miongoni mwa wenyeji ni loyalty kwa watawala. hivyo akajua patamfaa zaidi. pamoja na hivyo population kubwa ya waelewa ni wahamiaji ambao majorityy ni civil cervants. hawa huogopa kushow up japokuwa wana mapenzi makubwa na cdm. katika maeneo yote ya civilservants cdm ilishinda ikiwemo ene la jeshi la polisi.....dodoma kumekuwa na uccm kwa muda mrefu. kuna wakati mtu huonekana wa ajabu hata akiweka bendera ya chama kingine..au hata kushughulika na upinzani..maandalizi yalikuwa ni ya muda mfupi, matangazo pia hayakufika mbali.japo radio five walitangaza usiku kuamkia siku ya tukio...pia wengine walihofia kupigwa risasi....

all in all tumejifunza, mwitikio ni mkubwa miongozi mwa vijana na wasomi. tutaenda nao taratibu! kipindi cha bunge kuna haja kubwa ya sangara ya aina yake kufanyika hapa dodoma. point taken!
 
Mungu tusaidie Watanzania wako.
Hongereni Chadema kwa ujasiri na Ushujaa wenu.

Haki ya mtu yaweza kucheleweshwa lakini haipotezwi.
 
Back
Top Bottom