Tamko la Wabunge wa Jiji la DSM Kuhusu Kashfa ya Shirika la UDA

Pongezi kwa wabunge wa Dar es Salaam, wabunge wengine mikoani wanatakiwa kuiga huu mfano linapotea jambo la maslahi ya Umma mnaweka pembeni ukelekweta wa vyama
 
Bado ninauliza hivi ofisi ya waziri mkuu ilikuwa haijui jambo hili kweli!!
Kwanini isundwe kamati ya bunge kuchunguza, na kazi hiyo anapewa Hosea wa PCCB aliyeshindwa madudu ya Richmond!
Kwanini taairfa itolewe kwenye kamati ya miundo mbinu na si bungeni
Uchunguzi utaanza na kumalizika lini, isije ikawa utaanza Jan 2012 na kumalizika Dec 2015.
Kwanini viongozi wa jiji na mwenyekiti wa bodi ya UDA wanakiburi cha kukiuka maagizo ya ofisi ya PM, sijui ni kwa miujiza gani ofisi ya waziri mkuu haiujui au haihusiki!!!!!!!

Ninachowapongeza wabunge ni kukaa pamoja japo kuandika kitu lakini bila hatua zaidi, haya maandiko yenu yatabaki katika kumbu kumbu.
Tumeshaona tume na tume, uchunguzi na uchunguzi hakuna taarifa hata moja inayotoka wala watu kuchukuliwa hatua.

Sitawaelewa nitakaposikia mkisema tulitoa tamko na mengine ni ya serikali.
Hivyo vyombo vya dola mnavyopongeza sina imani navyo kabisa. Hivyo ni kwa ajili ya vibaka si Mafisadi wanaoogopwa na Mh Waziri mkuu Pinda(alitamka bungeni).

Ngoja tuone igizo hili litaishaje!
 
Kama huu ndiyo usanii basi uendelee tu, kwani ndani ya usanii kama huu sisis wananchi tunapata uelewa wa mambo ya sirini.
 
Ndugu zangu,


Bunge letu limeanza kuchangamka. Ndio, nimeanza kulifuatilia Bunge kwa muda mrefu. Sasa naiona tofauti. Na jana tu, nimemwona David Kafulila akishambulia bungeni kwa kujiamini. Ni kwenye mjadala wa bajeti ya Wizara ya Usafirishaji na Uchukuzi.


Kafulila anasimama na kutamka; ” Wabunge wenzangu tukomae bila kujali itikadi zetu. Tukomae jamani, hawa jamaa fedha wanayo ya kuimarisha usafiri wa reli.” Anasema Kafulila wa NCCR- Mageuzi.


Na hiyo ndio maana ya Bunge- wawakilishi wa wananchi kuongea kwa kutanguliza maslahi ya umma, maslahi ya nchi. Na Bunge lina maana ya kulonga kwa maana ya kuongea. Bunge halina maana ya kunong’ona na kulala.


Na pengine wengine hawajui, kuwa neno la Kiingereza ’Parliament’ kwa maana ya Bunge linatokana na neno la Kifaransa ’ Parle’ kwa maana ya kuongea. Hivyo, ’Le Parleament’ kwa Kifaransa ina maana ya jengo ambamo waliomo wanaongea kwa niaba ya waliowakilisha.

Ndio, tunahitaji Bunge kama Kariakoo na Buguruni na si Oysterbay na Masaki. Kariakoo , Buguruni na kwingineko ndiko waliko Watanzania wengi. Wanaamka saa kumi alfajiri na wanalala usiku wa manane. Si kwa kupenda- wanahangaika na shida za dunia. Ndio, kule Kariakoo na Buguruni watu wanaongea kuanzia saa kumi alfajiri mpaka saa saba za usiku. Na wanakerwa sana wanapowaona wabunge wao wanalala bungeni, au wananong’ona.


Tuje kwa Wabunge wa Dar es Salaam. Wamenifurahisha sana. Hili ndio Bunge ninalotaka kuliona. Kwamba, kwenye maslahi ya taifa, wabunge wasiendekeze ushabiki wa vyama. Nina hakika Watanzania wengi wamevutiwa na hatua hii ya Wabunge wa Dar es Salaam. Kwamba bila kujali ushabiki wa vyama vyao, wameamua kwa pamoja, kama timu ile ya Barcelona kushambulia kwa pamoja kwa kuivalia njuga kashfa ya mauzo ya hisa za UDA.


Na wabunge wa Dar es Salaam wameweka wazi; wanaotuhumiwa kuhusika na ufisadi ule wa fedha za umma wabingirishwe mchangani. Na hawakuuma maneno, wamemtaja Idi Simba, Meya Masabuli na wengine. Kwa hatua ile ya Wabunge, bila shaka, watu wa Dar es Salaam wamefurahi sana. Lakini wanasubiri kuona hatua zinazochukuliwa kwa watuhumiwa hao wa ubadhirifu wa mali ya umma.


Na wabunge wa Dar es Salaam wakitaka waendelee kuheshimika na kuwa mfano kwa wabunge wengine, basi, katika hili la UDA na iwe ’ Bayankata’ kwa kwenda mbele. Waweke ushabiki wa vyama kando. Na kama ’ Barcelona’ .


Naam, tumewaona wabunge wa Dar es Salaam wakipanda kwa pamoja na kushambulia. Sasa kazi kwao ni kubaki katikati na kukomaa ' Kibayankata'- Ndio yenyewe! Na kama kuna kushuka na kujihami, basi, washuke kwa pamoja, A la’ Barcelona!
Maggid,


Msamvu, Morogoro
Ijumaa, Agosti 8, 2011
0754 678 252

http://mjengwa.blogspot.com

Kaka Maggid, hapo kwenye red,hiyo kalenda ndo mnayotumia huko Msamvu?
 
Kwa alivyo jieleza Mzee Iddi Mohamed Simba nakubaliana nae kabisa kuwa wamemlipa kama consultation fee kwani ana kampuni yake ya ushauri inayoitwa INTERFINAS (International Finance Advisory Services) na kwa wawekezaji wengi wanaifahamu kwani inajihusisha na kutoa ushauri mbalimbali wa kibiashara.

Conflict of interest, huwezi kuwa mwenyekiti wa bodi halafu ukajipa kazi ya consultancy. Mwenyekiti wa bodi akishakuwa mmoja wa wazabuni, hivi kweli UDA wanaweza kumnyima kazi hata kama hakushinda? Jamani tuwe na uzalendo, hata kama ana kampuni hiyo ya ushauri akafanyie pengine sio UDA ambapo yeye ni mwenyekiti wa bodi.
 
Mokongoro ni mjomba wake masaburi na ni wabia wa chuo cha ugavi kule chanika
 
Hii Inahitaji pongezi ya hali ya Juu SANA!! Ila kwa hao wawekezaji uchara nawaunga sana Mkono kwa nia yao Njema ya kutaka kuboresha usafiri Dar es Salaam ambao Hali ni Mbaya kupindukia!! Huwezi kabisa Kujivuni hali ya usafiri wa Public Kwa jiji la Dar es Salaam kwa Hali ya kawaida huu usafiri siku zote naufananisha na Jehadamu!! Huwezi kusema unaishi kwenye Ulimwengu wa Sayansi na Technologia halafu kuwezi hata kuplan kufika mahali fulani on Time!! Huku tukiona wanaotakiwa kufanya hizi planning wakineemesha Matumbo yao Bila kutumia akili zao KUFIKIRI!!
NAPENDEKEZA YAFANYIKE YAFUATAYO KWA WANA HISA WETU WAPYA
1: TATHMINI HALISI YA SHIRIKA IFANYIKE KWA KUSHIRIKISHA TAASISI ZINAZOHESHIMIKA NA KUJUA THAMANI HALISI YA SHIRIKA KWA SASA NA MALI ZAKE ZOTE
2:HAWA WABIA WETU UCHWARA WASHUKURIWE KWA KUONYESHA NIA YA KUWEKEZA NA KIASI CHA HELA WALICHOTOA KITAFSIRIWE KATIKA HISA NA WAPEWE PORTION YAO YA HISA HATA KAMA NI 6% NO PROBLEM ILA WATAKUWA NI SEHEMU YA WAWEKEZAJI
3:HILI SUALA LA IDDI SIMBA KUCHUKUA SEHEMU YA MALIPO NAONA LITAKUWA LA BINAFSI ZAIDI KWANI HAWA WAWEKEZAJI TUTAWATATHIMINI KUTOKANA NA KIASI WALICHOWEKEZA NDANI YA AKAUNTI YA UDA, NA KAMA HAWAJAWEKEZA CHOCHOTE TUACHANE NAO
4:NINGEWASHAURI TAKUKURU WAFUATILIE TARATIBU HUSIKA ZA MALIPO ALIYOYAPATA IDDI SIMBA KAMA YANA UHALALI WOWOTE AU NI SEHEMU YA RUSHWA NA AWEZE KUPELEKWA KUNAKO HUSIKA
5:pIA NDUGU ZANGU WA TRA WAJUE NDIO MUDA MUAFAKA WA KUCHUKUA KODI KWENYE MALIPO HAYA YA NDUGU SIMBA NA SIO KUFUATILIA MISHAHARA YA WATU NA HUKU KUNA WATU WANAMALIPO MAKUBWA BILA KUYALIPIA KODI!!

Wabunge wa Dar kwa pamoja walau wameanza kufanya kazi kwa niaaba ya wananchi;

Waheshimiwa Myika na Mdee nafikiri mmo humu JF, naomba muwahurumie wana dar hasa wafanyakazi na wanafunzi, hili swala la usafiri dar ni issue inayoweza kutatulika tena mapema sana, hebu himizeni sio kila siku tupo kwenye mpango! ooo Mchakato mpaka lini!? wananchi wanataka kutatuliwa hizi kero zao on time, tunaomba muwabane wahusika waseme hadi sasa nini kimefanyika na ni lini usafiri dar utakuwa umeimarika, watoto wanaamka saa kumi na moja asubuhi! unategemea watasoma shule hawa?, watakua Vizuri hawa? hawajamaa wa waserikalini hawapati hizi taabu kwa sababu wana magari ya serikali; la kumpeleka baba kazini, la watoto shule na la mama Saloon, so hawajui balaa la daladala, hili ni tatizo kubwa sana tena huwa nahurumia sana watu mitaa ya Posta unakuta mtu anakimbilia daladala kama hana akili na jamaa wa serikali wapo kwenye V8 wanakula viyoyozi na sisi wengine wenye vimikweche tunaingia ghara za mafuta bila sababu kwa kuwa ukikiacha home utafika office shati lako jeupe lina tope, kwa nini watu wajazane kwenye daladala kama wanyama.

please wabunge unganeni kwenye kero za msingi za dar sio kuuza sura tu!, angalia masaki hakuna maji Chole road why? kisa miradi ya wakubwa ya malori ya maji!? amkeni tupendezeshe miji yetu uwezo tunao na pesa TZ ipo.

halmashauri zinashindwa hata kutengeneza mazingira safi! e.g weka vitofali kuzuia vumbi, tope nk, kuweni wabunifu jamani sio kunenepesha matumbo tu.
 
Tunashukuru kwa wakati kama huu wabunge wote kutoka vyama tofauti kushikamana kwa pamoja kwa maslahi ya Taifa hili TAJIRI,tuzidi kupamba na kushikamana kwa maslahi ya Taifa hili
 


Tamko hili limetolewa tarehe 4 Agosti 2011 na wabunge wafuatao wa mkoa wa Dar es salaam:

Abas Mtemvu-Mwenyekiti,
John Mnyika-Katibu,
Mussa Zungu,
Dr Faustine Ndugulile,
Philippa Mturano,
Mariam Kisangi,
Zarina Madabida,
Iddi Azzan,
Halima Mdee,
Eugine Mwaiposa,
Angellah Kairuki
Prof. Fennella Mukangara

Makongoro si Mbunge wa Dar es Salaam mbona simuoni kwenye tamko?
 
Mokongoro ni mjomba wake masaburi na ni wabia wa chuo cha ugavi kule chanika

Mkuu si angetoa tu tamko hata kama Masburi ni mjomba wake. Angedeclare tu kwamba Masaburi ni mJomba lakini alichokifanya ni batili. Duh nimesoma Gazeti la Majira Ndg Simba akijitetea na pia nimesoma Tamko la Kisena kwenye Gazeti la Mwananchi nimebaki nimeduwaa!! Hivi Nchi hii inaenda wapi sasa kila mtu anapora kilichokaribu naye. Kila kukicha huyu kapora hiki huyo kapora kile ili mradi tu nchi inakwenda shagilabagala!! MZAWA Simba anasema ati kalipwa kwa kutoa Consultancy kwa Simon Group na hivyo kulipwa million 300!! Simon Group ndio wananunua UDA wakati Simba ni Chairpeson of the Board of Directors; bonge la conflict of interest!! Sitaki kuamini kuwa Simba; msomi aliyebobea, mwanataaluma na mtumishi wa siku nyingi wa mashirika ya kimataifa hajui kwamba hapo kulikuwa na Bonge la conflict of interest. Nimeamini kwamba fedha mwanaharamu na inaweza ikakufanya ifanye chochote ambacho hukiamini!! Idd Simba a.k.a Mzawa amekula vya wazawa!!!
 
Conflict of interest, huwezi kuwa mwenyekiti wa bodi halafu ukajipa kazi ya consultancy. Mwenyekiti wa bodi akishakuwa mmoja wa wazabuni, hivi kweli UDA wanaweza kumnyima kazi hata kama hakushinda? Jamani tuwe na uzalendo, hata kama ana kampuni hiyo ya ushauri akafanyie pengine sio UDA ambapo yeye ni mwenyekiti wa bodi.

Mkuu hata mtoto mdogo asingekubali kuishauri kampuni ambayo inataka kununua shirika ambalo wewe ni kiongozi. Hapa kuna inside dealing ambayo inakatazwa!
 
Je serikali itawashitaki kweli?siku kumi za jairo bado hazijatimia?dpp ameshapata jarada la chenge ili ashitakiwe?au ndo funika kombe mwanaharamu apite?tusubili tuone japo kwa mfano nini kitatokea ingawa bado ninawasiwasi na hawa magamba.
 
Safi sana wabunge wa Dar. Utaifa kwanza. (Sijui kama yule dada yetu Faizafoxy na kaka yake Ms watachangia hii mada...!)
 
Kumbe kuna issues wapinzani na chama tawala mnaweza kukaa na kukubaliana? Safi

Ukisikia uwajibikaji wa namna hii kweli wabunge wengi mtaendelea kulinda hadhi kwenye majimbo yenu, Muungano na tamko la pamoja na ingelikuwa hivyo hivyo kwa mikoa mingine tunge iweka serikali yetu kati majibu ya kipuuzi na kutufanya sie ni watoto yasingelikuwepo kabisa
 
Back
Top Bottom