Tamko la Wabunge wa Jiji la DSM Kuhusu Kashfa ya Shirika la UDA

Wabunge wa DSM. Kwa hili la UDA angalau tunawapongeza lkn hatuwasifu sana mpaka tuone mwisho wake kama ya UBT. Tunahitaji kujua ukweli wa mradi wa Maji (DAWASCO) uliofadhiliwa na ADB maarufu Mradi wa Wachina wakati ni mkopo kwetu. Tupewe ukweli kwa nini ulikabidhiwa/haujakabidhiwa wakati maeneo mengine maji hayatoki? Miundombinu ya mabomba yaliyotandazwa bila maji inayoharibika kila siku itakarabatiwa na nani. Je miradi ya kusambaza maji kwa magari ni dili za madiwani hao waliouza UDA kiharamu? Kumbukeni sasa kumekucha. Agenda hizi usafiri na barabara, maji, viwanja n.k, msipozishughulikia kwa uzalendo uliotukuka tutawazomea na kuwadhalilisha kwenye majukwaa na barabarani.
 
makongoro mahanga ni rafiki wa karibu wa Didas masaburi na wote ni wajaruo wa Rorya kwa hiyo hawezi kusign. huyu ni Mbunge Bogas kuliko wote Dar
 
Ndugu zangu,


Bunge letu limeanza kuchangamka. Ndio, nimeanza kulifuatilia Bunge kwa muda mrefu. Sasa naiona tofauti. Na jana tu, nimemwona David Kafulila akishambulia bungeni kwa kujiamini. Ni kwenye mjadala wa bajeti ya Wizara ya Usafirishaji na Uchukuzi.


Kafulila anasimama na kutamka; ” Wabunge wenzangu tukomae bila kujali itikadi zetu. Tukomae jamani, hawa jamaa fedha wanayo ya kuimarisha usafiri wa reli.” Anasema Kafulila wa NCCR- Mageuzi.


Na hiyo ndio maana ya Bunge- wawakilishi wa wananchi kuongea kwa kutanguliza maslahi ya umma, maslahi ya nchi. Na Bunge lina maana ya kulonga kwa maana ya kuongea. Bunge halina maana ya kunong’ona na kulala.


Na pengine wengine hawajui, kuwa neno la Kiingereza ’Parliament’ kwa maana ya Bunge linatokana na neno la Kifaransa ’ Parle’ kwa maana ya kuongea. Hivyo, ’Le Parleament’ kwa Kifaransa ina maana ya jengo ambamo waliomo wanaongea kwa niaba ya waliowakilisha.

Ndio, tunahitaji Bunge kama Kariakoo na Buguruni na si Oysterbay na Masaki. Kariakoo , Buguruni na kwingineko ndiko waliko Watanzania wengi. Wanaamka saa kumi alfajiri na wanalala usiku wa manane. Si kwa kupenda- wanahangaika na shida za dunia. Ndio, kule Kariakoo na Buguruni watu wanaongea kuanzia saa kumi alfajiri mpaka saa saba za usiku. Na wanakerwa sana wanapowaona wabunge wao wanalala bungeni, au wananong’ona.


Tuje kwa Wabunge wa Dar es Salaam. Wamenifurahisha sana. Hili ndio Bunge ninalotaka kuliona. Kwamba, kwenye maslahi ya taifa, wabunge wasiendekeze ushabiki wa vyama. Nina hakika Watanzania wengi wamevutiwa na hatua hii ya Wabunge wa Dar es Salaam. Kwamba bila kujali ushabiki wa vyama vyao, wameamua kwa pamoja, kama timu ile ya Barcelona kushambulia kwa pamoja kwa kuivalia njuga kashfa ya mauzo ya hisa za UDA.


Na wabunge wa Dar es Salaam wameweka wazi; wanaotuhumiwa kuhusika na ufisadi ule wa fedha za umma wabingirishwe mchangani. Na hawakuuma maneno, wamemtaja Idi Simba, Meya Masabuli na wengine. Kwa hatua ile ya Wabunge, bila shaka, watu wa Dar es Salaam wamefurahi sana. Lakini wanasubiri kuona hatua zinazochukuliwa kwa watuhumiwa hao wa ubadhirifu wa mali ya umma.


Na wabunge wa Dar es Salaam wakitaka waendelee kuheshimika na kuwa mfano kwa wabunge wengine, basi, katika hili la UDA na iwe ’ Bayankata’ kwa kwenda mbele. Waweke ushabiki wa vyama kando. Na kama ’ Barcelona’ .


Naam, tumewaona wabunge wa Dar es Salaam wakipanda kwa pamoja na kushambulia. Sasa kazi kwao ni kubaki katikati na kukomaa ' Kibayankata'- Ndio yenyewe! Na kama kuna kushuka na kujihami, basi, washuke kwa pamoja, A la’ Barcelona!
Maggid,


Msamvu, Morogoro
Ijumaa, Agosti 8, 2011
0754 678 252
http://mjengwa.blogspot.com
 
Halima Mdee ndie Messi wao, wakati John John Mnyika anaplay part ya Xavi Hernandez!
 
kudadeki iacheni dar iitwe dar ,wabunge wamefanya maamuzi critical mwenyikiti ccm katibu cdm imetulia saana ,go ahed tuko nyuma yenu
 
Safi sana Wabunge:
Sasa huu uwe mwanzo mwema. Simamieni vizuri mambo yafuatayo
Ubungo Bus Terminal
Maeneo yote ya wazi sehemu mbalimbali
DAWASCO
Na mengine yote mtazidishiwa
Siasa za Umwinyi, kwenda kwenye misiba, kwenda msondo na kugawa jezi sasa basi, pigeni kazi
 
Hii Inahitaji pongezi ya hali ya Juu SANA!! Ila kwa hao wawekezaji uchara nawaunga sana Mkono kwa nia yao Njema ya kutaka kuboresha usafiri Dar es Salaam ambao Hali ni Mbaya kupindukia!! Huwezi kabisa Kujivuni hali ya usafiri wa Public Kwa jiji la Dar es Salaam kwa Hali ya kawaida huu usafiri siku zote naufananisha na Jehadamu!! Huwezi kusema unaishi kwenye Ulimwengu wa Sayansi na Technologia halafu kuwezi hata kuplan kufika mahali fulani on Time!! Huku tukiona wanaotakiwa kufanya hizi planning wakineemesha Matumbo yao Bila kutumia akili zao KUFIKIRI!!
NAPENDEKEZA YAFANYIKE YAFUATAYO KWA WANA HISA WETU WAPYA
1: TATHMINI HALISI YA SHIRIKA IFANYIKE KWA KUSHIRIKISHA TAASISI ZINAZOHESHIMIKA NA KUJUA THAMANI HALISI YA SHIRIKA KWA SASA NA MALI ZAKE ZOTE
2:HAWA WABIA WETU UCHWARA WASHUKURIWE KWA KUONYESHA NIA YA KUWEKEZA NA KIASI CHA HELA WALICHOTOA KITAFSIRIWE KATIKA HISA NA WAPEWE PORTION YAO YA HISA HATA KAMA NI 6% NO PROBLEM ILA WATAKUWA NI SEHEMU YA WAWEKEZAJI
3:HILI SUALA LA IDDI SIMBA KUCHUKUA SEHEMU YA MALIPO NAONA LITAKUWA LA BINAFSI ZAIDI KWANI HAWA WAWEKEZAJI TUTAWATATHIMINI KUTOKANA NA KIASI WALICHOWEKEZA NDANI YA AKAUNTI YA UDA, NA KAMA HAWAJAWEKEZA CHOCHOTE TUACHANE NAO
4:NINGEWASHAURI TAKUKURU WAFUATILIE TARATIBU HUSIKA ZA MALIPO ALIYOYAPATA IDDI SIMBA KAMA YANA UHALALI WOWOTE AU NI SEHEMU YA RUSHWA NA AWEZE KUPELEKWA KUNAKO HUSIKA
5:pIA NDUGU ZANGU WA TRA WAJUE NDIO MUDA MUAFAKA WA KUCHUKUA KODI KWENYE MALIPO HAYA YA NDUGU SIMBA NA SIO KUFUATILIA MISHAHARA YA WATU NA HUKU KUNA WATU WANAMALIPO MAKUBWA BILA KUYALIPIA KODI!!
 
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni hiyo, Bw. Idd Simba amejibu tuhuma zilizoelekezwa kwake kuwa fedha zilizoingizwa kwenye Akaunti yake binafsi zilitokana na Ushauri wa Jumla wa Kibiashara aliotaka (Kisena) kutoka kwake, "alikuwa anastahili kulipa fedha zangu binafsi, Nilitoa amri ya kulipia katika akaunti yangu, alifanya hivyo kwa awamu tofauti kadri nilivyotoa maagizo"

Source: Majira 05/07/2011
 
hapa kuna mtu kaliwa.. Kisena kesho naye ataibuka na kusema alizompa Simba ni malipo ya committment fee kama alivyoelekezwa.. kitaivaaaa!!
 
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Kampuni hiyo, Bw. Idd Simba amejibu tuhuma zilizoelekezwa kwake kuwa fedha zilizoingizwa kwenye Akaunti yake binafsi zilitokana na Ushauri wa Jumla wa Kibiashara aliotaka (Kisena) kutoka kwake, "alikuwa anastahili kulipa fedha zangu binafsi, Nilitoa amri ya kulipia katika akaunti yangu, alifanya hivyo kwa awamu tofauti kadri nilivyotoa maagizo"

Source: Majira 05/07/2011

Kwa alivyo jieleza Mzee Iddi Mohamed Simba nakubaliana nae kabisa kuwa wamemlipa kama consultation fee kwani ana kampuni yake ya ushauri inayoitwa INTERFINAS (International Finance Advisory Services) na kwa wawekezaji wengi wanaifahamu kwani inajihusisha na kutoa ushauri mbalimbali wa kibiashara.
 
Wapi makongoro mahanga kwenye list ya MPs?
<br />
<br />





Makongoro anajua hatukumchagua kuwa Mbunge wetu sisi wakazi wa Jimbo la Segerea ,alichaguliwa na Jakaya kupitia NEC,NDIYO MAANA HAFANYI KAZI YEYOTE YA KUTETEA JIMBO HILI!!
Ni fisadi na Mshe*nz*!! We dnt need his bloody ****in Utetezi;Mbunge tuliyemchagua ni Mpendazoe!!
 
Mtoto wa Mkulima, yy ni mwanasheria anajua kanuni za bunge zinasemaje ktk uchunguzi wa sakata hili la kisanii......,
tunategemea kamati ya Mh Zitto K ndiyo inapaswa ku handle hii issue.

So imekuwaje PM kutaka kamati ndogo chini ya Kamati ya Bunge ya Mh P Serukamba kushiriki ktk uchunguzi..?
Haingii akilini Mh Prof Kapuya ahusishwe kumiliki hisa ktk Simon Group n then ndy awe mwenyekiti wake....!
kuna chain ya urafiki wa kisiasa hapa toka Bodi ya UDA, City Council na baadhi ya kundi la wabunge..!

Mradi DART ili uweze kufanya kazi vizuri na kupata ufanisi ni lazima kwa njia moja au nyingine uunganishwe na UDA,
na kama tunavyojua kuna fedha nyingi ya kumwaga toka mkopo wa World Bank.....,
so watu wanazihiitaji hizo fedha 4 preparation of 2015 election...., ndiyo maandalizi yake hayo!
UDA kwanza n then fedha ya mradi wa DART later....!

Inasikitisha kwa mtoto wa mkulima, nilitegemea achukue hatua kali pale UDA / City Council zilipokaidi barua toka Office yake...,
labda anajua ukweli khs hii kashfa...!
 
Wabunge wa Dar wamenifurahisha sana sina neno zuri zaidi ya kuwaombea kwa Mungu afya njema katika kutekeleza majukumu yao.
 
Damu nzito........

Kwa alivyo jieleza Mzee Iddi Mohamed Simba nakubaliana nae kabisa kuwa wamemlipa kama consultation fee kwani ana kampuni yake ya ushauri inayoitwa INTERFINAS (International Finance Advisory Services) na kwa wawekezaji wengi wanaifahamu kwani inajihusisha na kutoa ushauri mbalimbali wa kibiashara.
 
Myika onyesheni mshikamano na hao wabunge wa CCM kwa kuitisha maandamano ya kupinga uporaji huo wa UDA. hapo ndio tutajua hao wabunge sio wanafiki kwenye hili suala.
 
Back
Top Bottom