Jackbauer
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 6,038
- 2,199
najua wengi wetu tunatamani kusikia tamko la serikali kuhusu mgomo wa madaktari.haieleweki kama serikali imewatimua madaktari waliogoma au la.haieleweki kama mgomo umekwisha au la.hatuelewi nini kinaendelea,je serikali imefanikiwa kudhibiti hali mbaya ya huduma kwenye mahospitali yaliyoko kwenye mgomo au la.pinda alisema tuvumilie sasa tunavumilia mpaka lini?mponda alisema yuko tayari kwa mazungumzo je madaktari wamekutana naye?ana makinda alisema tutarajie taarifa kutoka serikalini je tutasubiri mpaka lini?watanzania wanaendelea kufa au kuumia kwa kukosa huduma stahiki je tusubirie mpaka lini?tunawezaje kulazimisha tamko la serikali litoke ?je swala la mgomo wa madaktari sio kipaumbele kwa wabunge wetu?nahitaji tamko la serikali kama mwananchi niliyeathirika na mgomo huu.hatuwezi na kamwe tusikubali swala hili liende bila watu kuwajibika.mbunge wangu nifikishie ujumbe huu bungeni!wanajf na wananchi tushinikize kutolewa kwa tamko la serikali lenye muelekeo wa kuhitimisha mgogoro huu.