Geza Ulole
JF-Expert Member
- Oct 31, 2009
- 59,202
- 79,433
Mie napenda kufahamu kutoka kwa kiongozi yeyote wa CUF humu ndani hata kama Mtatiro yumo, nikiwa kama mwanaharakati wa maendeleo na ustawi wa Watanzania wenzangu! Ninataka kuhudhuria haya maandamano, ila naomba kujua kama naweza vaa uniform ya chama changu kingine (aidha magwanda, bendera au kofia)! maana naskia huwa wana CUF hukataza hayo nakumbuka kuna wakati waliitisha maandamano kwa sharti ya kutobeba bendera au kuvaa uniform za chama kingine chochote! Naombeni kujua maana nina hofu nisije nikatimuliwa!