Tamko la Kamati Kuu ya CCM; Muda waongezwa kujivua gamba

Yani kwenye kikao cha baraza la mawaziri wameamua mafuta ya pande bei, kwenye halmashauri ya magamba wanasema bei ishuke eti inamuumiza mtu wa chini, vikao vyote hvyo mwenyekiti mmoja. Hakika bora tz bora hata tungempa DOVUTWA tujue moja.
 
Kumbe mafuta ya taa yamepandishwa bei kwa ajili ya kuzuia uchakachuaji? Yani baada kuwadhibiti wachakachuaji, wao wameona bora tuwaadhibu tu na wananchi wa kawaida.

Safari ndefu sana kwa taifa letu kama huu ndio uwezo wa kufikiria jinsi ya kutataua matatizo kwa viongozi wetu.
 
Kauli ya kujivua gamba ilikuwa ni usanii tu ndio maana sasa wanaikimbia kauli yao wenyewe. Lowassa na Chenge wamegoma kung'oka na hakuna mwenye ubavu wa kuthubutu kuwafukuza maana chama chote kimejaa mafisadi.
Tuache kupayuka,tusubiri kikao cha NEC.
 
CCM jamani, utani mwingine acheni.

Yaani watu wazima 33 wa ngazi ya Taifa wamekutana kwa masaa takribani 11 ili kujadili haya masuala hapa? Na miongoni mwa hao watu kuna ma-Rais wanne (Kikwete, Mwinyi, Karume, Shein), na mawaziri wakuu wawili (Malecela, Pinda), ukiacha vibosile wengine wengi, halafu wanatoka na white paper ya darasa la saba!

Huu utani mbaya.


Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM imemaliza kikao chake cha siku moja usiku wa tarehe 31/07/2011 mjini Dodoma chini ya uenyekiti wa Mwenyekiti wa CCM Taifa, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete. Pamoja na mambo mengine Kamati Kuu imeamua yafuatayo;

1. Imefanya uteuzi wa makatibu ishirini na saba (27) kujaza nafasi zilizokuwa wazi katika wilaya hizo. (majina na wilaya zao yameambatanishwa). Pamoja na uteuzi huo, Kamati Kuu imetengua uteuzi wa Makatibu wa Wilaya watatu (3) katika kuboresha ufanisi wa kazi katika wilaya hizo.(majina na wilaya zao yameambatanishwa).

Uteuzi na utenguzi wa makatibu wa wilaya na mikoa ni jukumu la Mwenyekiti na sekretarieti. CC inaridhia tu. Si suala la mjadala.

2. Kamati Kuu imepokea na kuridhia taarifa ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM kuwakilisha Mkoa wa Tabora, Ndugu Rostam Aziz. Aidha imempongeza kwa uamuzi huo uliozingatia maslahi mapana ya chama chake.
Maneno muhimu..."imepokea na kuridhia taarifa...", kwa maana kuwa hakuna mjadala wala tathmini. CC haikuagiza hilo lifanyike, kwa hiyo hakukuwa nachakufuatilia hapo.

3. Kamati Kuu imepokea pia taarifa ya kujiuzulu kwa aliyekuwa Mbunge wa Igunga, Ndugu Rostam Aziz na kuagiza chama kupanga ratiba ya mchakato wa kumpata mgombea ubunge wa Jimbo la Igunga itakayozingatia ratiba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi juu ya uteuzi wa mgombea. Aidha Kamati Kuu imeagiza shughuli zote za kampeni kutafanywa na CCM Mkoa, Wilaya na ngazi zote za chama wilayani Igunga. CCM Taifa watashiriki kuongeza nguvu. Chama kinatoa wito kwa wana CCM, wapenzi na wakereketwa wa chama chetu kushiriki kwa pamoja kuhakikisha jimbo linabaki kwa CCM.
Maneno muhimu..."imepokea taarifa...", kwa maana kuwa hakuna mjadala wala tathmini. Katibu Mkuu alikwisharidhia huu uamuzi wa Rostam na kumuarifu Spika kwa mujibu wa utaratibu. CC haikuagiza na wala hakuna mjadala.

4. Kamati Kuu haijaridhishwa na kiwango cha bei ya mafuta ya taa nchini kwa kuwa ndio nishati inayotumiwa na wananchi wengi wenye kipato cha chini. Aidha Kamati Kuu haikuridhishwa na maelezo ya kupandishwa kwa bei ya mafuta hayo kwa kisingizo cha kuzuia uchakachuaji wa mafuta mengine. Hivyo basi, Kamati Kuu imeiagiza Serikali kutafuta njia za kushusha bei ya mafuta ya taa na kuvitaka vyombo vya Serikali vinavyohusika na usimamiaji wa ubora wa mafuta, vihakikishe vinatimiza wajibu wake kuzuia kabisa mtindo wa uchakachuaji wa mafuta nchini na si kupandisha bei ya mafuta ya taa kama suluhisho.
Haijaridhishwa? Kiwango gani ndiyo kinaridhisha? Mwenyekiti wa CC ndiye mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri, na ndiye Rais (Mkuu wa Serikali). Kikwete anasimamia maamuzi ya CC kuagiza serikali ya Kikwete kuhusu kutekeleza uamuzi wa ........ (sijui uamuzi wa nani?). Mkanganyiko.
5. Kamati Kuu inasikitishwa na tatizo la umeme nchini kwani athari zake kwa uchumi wa Taifa na mtu mmoja mmoja ni kubwa. Hivyo basi imeitaka Serikali kutumia muda iliyopewa wa kurekebisha Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kuja na mpango wa dharura wa kunusuru hali hii na kisha kulimaliza kabisa tatizo la umeme nchini.
Inasikitishwa? Kweli hili ndiyo neno sahihi waliona katika ujumbe huu? Na pia, Mwenyekiti wa CC ndiye mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri, na ndiye Rais (Mkuu wa Serikali). Kikwete anasimamia maamuzi ya CC kuagiza serikali ya Kikwete kuhusu kutekeleza uamuzi wa ........ (sijui uamuzi wa nani?). Mkanganyiko mwingine.

6. Aidha Kamati Kuu imejadili masuala mengine kama; migogoro ya ardhi, tatizo la bei ya pamba, tatizo la uuzaji wa mahindi, migogoro migodini, masuala yanayohusu kero za Muungano na kuagiza Serikali kuyashughulikia kwani yanatatulika.
Kwa lugha nyingine, kulikuwa na mazungumzo kama ya kijiweni. Hakuna agenda wala azimio mahsusi. Ni kila mmoja kusema liwalo na mwisho kukubaliana kuwa ndiyo iwe hivyo. Yanatatulika haya, tusipoteze muda kutatua au hata kuagiza yatatulike.

7. Kamati Kuu imeipongeza Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa kwa kazi nzuri ya kutekeleza maamuzi ya NEC na kuitaka iongeze kasi katika utekelezaji huo, ili kuhakikisha mageuzi yaliyokusudiwa yanatekelezwa kwa wakati. Aidha imejadili na kupitisha miundo mipya ya Idara ya Itikadi na Uenezi na Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa.
Labda mie sijaelewa hapa. Wanapongezwa kwa kazi nzuri ya kutekeleza maamuzi ya NEC, kuwataka waongeze kasi katika utekelezaji huo. Kwa hiyo wametekeleza (wapongezwe?) au hawajatekeleza (waongeze kasi?)?

8. Kuhusu suala la maadili ndani ya Chama, Chama kinaendelea kusimamia maadili, na kuwataka wale waliotakiwa kujipima na kuwajibika watumie muda huo, kujipima na kuwajibika kwa masilahi mapana ya chama. Aidha Halmashauri Kuu ya CCM Taifa inatarajiwa kukutana wakati wowote mwezi Septemba, ambapo pamoja na mambo mengine itatathimini utekelezaji wa maamuzi yake.
Hapo sasa. Inawezekana wamejipima kwa siku 120 na wameamua kuwajibika kwa kubakia katika nafasi zao ndani ya chama na jamii, kwa masilahi mapana ya chama.....na yao pia. Je, CC mnasemaje? Taarifa wapeleke wapi?
 
nape nape tulikwambia hao watu hawakutakii mema hukusikia ona sasa unavyoumbuka, na huu ndio mwisho wako kisiasa sijui utapanda na lipi jukwaani labda urudie udini

mapacha wakiondoka nchi itatikisika
 
4. Kamati Kuu haijaridhishwa na kiwango cha bei ya mafuta ya taa nchini kwa kuwa ndio nishati inayotumiwa na wananchi wengi wenye kipato cha chini. Aidha Kamati Kuu haikuridhishwa na maelezo ya kupandishwakwa bei ya mafuta hayo kwa kisingizo cha kuzuia uchakachuaji wa mafuta mengine.

Hivyo basi, Kamati Kuu imeiagiza Serikali kutafuta njia za kushusha bei ya mafuta ya taa na kuvitaka vyombo vya Serikali vinavyohusika na usimamiaji wa ubora wa mafuta, vihakikishe vinatimiza wajibu wake kuzuia kabisa mtindo wa uchakachuaji wa mafuta nchini na si kupandisha beiya mafuta ya taa kama suluhisho.

Kweli haya sasa ni maigizo, Mhe. amepitisha bajeti na kukubali bei ya mafuta ya taa ipande akiwa kama mwenyekiti wa Baraza la Mawaziri, then huku akiwa kama mwenyekiti wa CC anasema hapana bei ya afuta ya taa ishushe tena anaiamuru serikali hiyo hiyo anayoongoza yeye!!
full kudata! nasikia na kale ka ugonjwa ka kisasa huwa kanaathiri uwezo wa kufikiria!
 
Is this what Nape classfies as 'taarifa kwa vyombo vya habari'?
Hivi ww Nape una uhusiano na ile pub ya Makumbusho inayojiita:.. (nimesahau nisipigwe bab) lakini kuna picha kuna simba kapakatwa.
 
Yani kwenye kikao cha baraza la mawaziri wameamua mafuta ya pande bei, kwenye halmashauri ya magamba wanasema bei ishuke eti inamuumiza mtu wa chini, vikao vyote hvyo mwenyekiti mmoja. Hakika bora tz bora hata tungempa DOVUTWA tujue moja.
Hapo naunga mikono na miguu 100%
 
Kweli nchi hii ukisikia kitendawili ndiyo hicho hao hao ndiyo mawaziri maraisi bada wanasema wataiagiza serikali kupunguza bei ya mafuta ya taa.
 
Wtz msishangae. Maamuzi ya utatanishi ya CCM na Skl yake yanatokana JK haketi na BLM kwa maamuzi ya pamoja. Kila suala linapitishwa kwa hati ya dharura. Ndiyo sababu kila wizara inatamka kivyake, lobbying kama za kijairo na kingeleja. CC inajifanya kuishangaa Skl yake. Tusitarajie mabadiliko ya dhati kutoka CCM na Skl yake.
 
Kwangu mimi gamba au bila gamba si hoja ya msingi. Jambo la msingi ni kuwa iwapo wanapovuliwa magamba nchi itanufaika na wizi uliotokea hapo ningeshangilia. Lakini mtu anatuhumiwa wizi halafu hakuna hatua zozote anachukuliwa...hayo ni maneno ya kisiasa tu yasiyo na tija na huenda ni wivu kwa walionacho.

Nionavyo mimi iwapo kuna dhamira ya kweli ya kuvuana magamba na kupongezana kwa kusemana kwenye vyombo vya habari, basi tuone kiasi cha fedha kilichorudishwa kikiingizwa hazina ili kisiaidie kwenye uchumi wa nchi.

Ushauri wangu ni kuwa, msiwasumbue watu bure kwa kelele zenu zisizo na msingi...tuambieni mmechukua hatua gani na tumepata faida gani kwa maamuzi yenu. Vinginevyo, ni utapeli tu!
 
Tafsiri pana ni kuwa kamati kuu haina imani na Kikwete , kwani hili ni agizo kwake kama mwenyekiti wa baraza la mawaziri kuwa aende akaitishe kikao cha baraza la mawaziri na kuangalia upya bajeti yake , na hivyo ameshindwa kuisimamia serikali yake katika kutengeneza bajeti.

Pili, kamati kuu haina imani na wabunge wa CCM kwaani wakati wabunge wa upinzani wote wakiikataa bajeti ya serikali wao wote wa CCM walisema kuwa wanaipitisha. Hivyo kitendo cha kamati kuu kukataa uamuzi uliopitishwa na wabunge wake ni kuwa hawana imani na Waziri mkuu ambaye ni msimamizi wa shughuli za serikali bungeni.

Tatu, kamati kuu haina imani na spika wa bunge kwani alilisimamia bunge kupitisha maamuzi ambayo chama alichotoka hakikubaliani na maamuzi hayo , na hivyo anapaswa kujipima mwenyewe kwani yeye aliwasimamia wabunge wa CCM kwenye caucus ya chama kukubaliana kuwa bajeti hiyo ipitishwe.

Nne, kamati kuu haina imani na baraza la mawaziri lililopitisha bajeti hiyo kwani kwa muono wao ni kuwa hawakuzingatia maslahi ya umma hivyo baraza linapaswa kujipima .

Tano, kamati kuu kuelekeza vyombo vya dola kuthibiti uchakachuaji ni wazi kuwa wamekosa imani na serikali ya chama chao katika kusimamia vyombo vyake vya dola na huu ni udhaifu mkubwa na wanapaswa kama serikali kujipima .

Mimi naona kuwa uamuzi huu wa CC ni katika kuonyesha udhaifu wa viongozi wa Serikali ya CCM na wabunge wake wote na hivyo wanakubaliana na wabunge wa Upinzani waliokataa kuipitisha bajeti hiyo kwani ilikuwa inawaumiza sana wananchi.
 
Sasa hivi hawa jamaa hawanamaamuzi ila wanafuata CDM wamefanya nini nao wanarandaranda humo humo, Hapo sijaona pointi yoyote ya msingi kwani tayari matatizo hayo yameshapigiwa kelele kipindi kirefu halafu isitoshe tatizo la umeme lilianza toka 2006 mpaka leo kamati ndo inaliona.

Sasa Nini way forward? Wameamua nini kukabiliana na mambo hayo? Au wamesema tu ili kutupumbaza sisi wananchi tuone kama CCM inashughullikia matatizo hayo? Wanavyosema kujipima kwa nini mwenyeketi wao asianze kujipima yeye kwanza na uwajibikaji? maana kila kukicha safari tu. Mbona NEC haijakemea hili?

NEC ya siku hizi haina nguvu kama enzi zile bwana wamejaa wasanii tu
 
loooh! CCM Magambaz, kweli mwisho wenu umefika, kisa nini hasa kukaa na kujifungia masaa yooote yale jana na hatimaye mnaleta taarifa ya kwenye khanga na maneno ya mipasho namna hiyo???
Kikwete, Marais wastaafu,viongozi waandamizi kama Nape, mukama n.k,wote ni wasanii wa jukwaani,wanawahadaa wananchi.
 
Amakwelii! Kama ni kaburi tayari limesha andaliwa na tuna karibia kutoa heshma za mwsho kwa marehem ccm* kama hali ndio hii Igunga sio yao tena waisahau. Kuwepo madarakani hadi 2015 kupo mashakani.
 
Back
Top Bottom