Tamko la Kafulila kwa Umma (kufuatia mbunge wa Bahi kukamatwa kwa Rushwa)...

Alichokifanya Kafulila sioni kama ni kosa,kama alikwisha sema na umma mzima ukasikia na spika akafumba macho bila kutaka kusoma na kutaka uthibitisho toka kwa Mh.Kafulila mlitaka yeye fanye nini zaidi ya kuwalikisha fikra na mawazo yake.

Pili bunge hii limekuwa la kulindana pasi na sababu za msingi.Tumeona aliyekuwa mbunge wa Arusha bwana Godbless Lema alivyouliza hatua gani kwa kutumia kanuni za bunge zitachukuliwa kama mbunge atathibitika amelidanganya bunge.Maamuzi ya kukurupuka badala ya kujibu swali la msingi lilipelekea spika wa bunge kumtaka atoe maelezo kimaandishi,maandishi yametolewa kama alivyoagiza lakini hakuna hat stahiki alizochukuliwa mpaka mahakama inatengua matokeo yake ya ubunge.

Mawazo yako mh.Kafulila yanafaa kufanyiwa kazi ikithibitika kanunu na sheria zinazoliongoza bunge zichukuwe mkondo wake.Esma kweli daima fitina kwako iwe mwiko kwa maslahi ya taifa.



Siungi mkono tamko la Ndugu Kafulila.
Siungi mkono kwa sababu nafahamu ,pamoja na matatizo yetu ya kimfumo na kitaasisi ,bado tunaamini katika utawala wa sheria ambao ni moja ya misingi na viashiria vya dhana ya demokrasia.
Hadi hapo mahakama itakapotamka vinginevyo ,mbunge mtuhumiwa asitendewe kama mtu aliyepatikana na hatia.Kwa sasa bado ni mtuhumiwa tu.
Vinginevyo,kwa siasa zetu za ajabu ,zinazoratibiwa na CCM & washirika wake,tunaweza kupoteza wabunge wetu wengine mahiri kama tukikubaliana na hoja iliyoletwa.Eti mtu avuliwe ubunge kwa kutuhumiwa tu!Hata mahakama hazifikii hukumu bila kuzingatia na kupima ushahidi.
Hata hivyo,ni juu ya mbunge anayetuhumiwa kutafakari na kufuata kile dhamira yake inamuelekeza.
Kama kweli anafahamu ametenda kosa husika,hana sababu yoyote ya kusubiri hukumu ya mahakama kuweza kufanya uamuzi.Alipaswa awe amkwisha kujiuzulu nafasi yake tangu jana alipokamatwa.
Nataka kueleweka wazi kuwa matazamo wa kisheria (legality) usiwekwe katika fungu moja na mtazamo wa kimaadili (morality) ingawa dhana hizi mbili,aghalabu, huhusiana katika mazingira mahususi.Hoja hii inaimarishwa na ukweli kuwa mtuhumiwa anaweza kuwa alitenda kosa kabisa ,dhamira yake ikimshuhudia,lakini hatimaye, mwenendoo & hukumu /ushahidi wa kimahakama ukaaamua kutomtia hatiani.
Ni kwa kuzingatia ukweli huu, bado Ndugu Kafulila anaendelea na majukumu yake ya kibunge,licha ya kuwa na kesi mahakamani na chama chake kuhusiana na uanachama wake.Vinginevyo,asingetoa tamko lake kama mjumbe wa kamati ya bunge, bali kama mwanachi anayewajibika!
 
Siungi mkono tamko la Ndugu Kafulila.
Siungi mkono kwa sababu nafahamu ,pamoja na matatizo yetu ya kimfumo na kitaasisi ,bado tunaamini katika utawala wa sheria ambao ni moja ya misingi na viashiria vya dhana ya demokrasia.
Hadi hapo mahakama itakapotamka vinginevyo ,mbunge mtuhumiwa asitendewe kama mtu aliyepatikana na hatia.Kwa sasa bado ni mtuhumiwa tu.
Vinginevyo,kwa siasa zetu za ajabu ,zinazoratibiwa na CCM & washirika wake,tunaweza kupoteza wabunge wetu wengine mahiri kama tukikubaliana na hoja iliyoletwa.Eti mtu avuliwe ubunge kwa kutuhumiwa tu!Hata mahakama hazifikii hukumu bila kuzingatia na kupima ushahidi.
Hata hivyo,ni juu ya mbunge anayetuhumiwa kutafakari na kufuata kile dhamira yake inamuelekeza.
Kama kweli anafahamu ametenda kosa husika,hana sababu yoyote ya kusubiri hukumu ya mahakama kuweza kufanya uamuzi.Alipaswa awe amkwisha kujiuzulu nafasi yake tangu jana alipokamatwa.
Nataka kueleweka wazi kuwa matazamo wa kisheria (legality) usiwekwe katika fungu moja na mtazamo wa kimaadili (morality) ingawa dhana hizi mbili,aghalabu, huhusiana katika mazingira mahususi.Hoja hii inaimarishwa na ukweli kuwa mtuhumiwa anaweza kuwa alitenda kosa kabisa ,dhamira yake ikimshuhudia,lakini hatimaye, mwenendoo & hukumu /ushahidi wa kimahakama ukaaamua kutomtia hatiani.
Ni kwa kuzingatia ukweli huu, bado Ndugu Kafulila anaendelea na majukumu yake ya kibunge,licha ya kuwa na kesi mahakamani na chama chake kuhusiana na uanachama wake.Vinginevyo,asingetoa tamko lake kama mjumbe wa kamati ya bunge, bali kama mwanachi anayewajibika!

Pamoja na natural justice huyo mheshimiwa mtuhumiwa apime mwenyewe na kuchukua hatua hata kama hana hatia, ajiuzuru maana MKE WA KAIZARI HATUHUMIWI BILA SABABU!
 
Dah huyu muheshimimiwa imemkamatia pabaya,anyways ngoja tuone jinsi atakavyojipangusa hiyo dhambi maana wengine wataalamu bwana kwenye kunawa.
 
leo nina ombi moja kubwa. Hawa watuhumiwa wa kudai na kupokea rushwa tunawasikia na kuwaona wakipelekwa mahakamani, wachache sana wamepatikana na hatia. Hata hivyo hilo siyo tatizo langu, langu ni hili. Je, kuna mtanzania anaeweza kunitajia mtanzania ambaye hapokei wala kutoa rushwa? Ni vyema akatutajia ili tuige maisha ya mtu wa aina hiyo. Naomba sanasana jamani majina ya wasioomba wala kupokea rushwa.
mimi sipokei wala kutoa rushwa
 
serikali iikaa kimya au ni kwamba serikali ilikuwa inafuatilia kauli yako na hatimae mmoja wa uliowataja kafikishwa kizimbani?nilitaraji badala ya kulalamika,ungefurahi kuwa umefarijika kwa sababu kauli uliyotoa kuwa baadhi ya wajumbe wa kamati ya LAAC wanachukua rushwa,kwamba kauli yako imepewa uzito na hatua zimeanza kuchukuliwa!!!
 
kuvunja kamati,je wakiingia wajumbe wachafu kuliko hao?huoni kuwa suluhisho sio kuivunja kamati,bali wajumbe wanaotuhumiwa kuchukua mlungula watolewe,ili nafasi zao zizibwe!mimi naona mrema anafaa sanasana kuongoza kamati,ikivunjwa wanaweza kuingia tusiowatarajia!
 
Mtuhumiwa amepelekwa mahakamani hivyo naona ingekuwa busara zaidi kusubiri hukumu itolewe kuliko kuhukumu kabla, ikumbukwe kuwa hata yeye anayo kesi ambayo inamfanya awe na hadhi ya ubunge hadi sasa, hivyo naona tamko lake sio wakati mufaka kulitoa.
 
Kafulila onyesha uzalendo, kamat ya LAAC imeshachafuliwa pamoja na bunge kwa ujumla kwan bunge n mhimili wa muhmu sasa tena sana kwa maendeleo ya taifa! Bunge legelege huzaa serikal legelege, huyo mbunge anastahli kuvuliwa ubunge! For the good reputation ya bunge letu tukufu.
 
Pamoja na natural justice huyo mheshimiwa mtuhumiwa apime mwenyewe na kuchukua hatua hata kama hana hatia, ajiuzuru maana MKE WA KAIZARI HATUHUMIWI BILA SABABU!

Ndugu bullet,sikubaliani na wazo lako.
Kukubaliana na maoni yako ni kukaribisha vurugu,matatizo (social disorder).
Hivi kesho mtu moja mwenye malengo yake akisema Ndugu Kafulila amemwibia kuku wake wa mayai,ungependa kuona mtuhumiwa anachukua hatua ya kujiuzulu hata kama ni kwa mashtaka ya kutunga?
Maana pana ya hoja yako ni kuwa hata huku mitaani tutakuwa na uwezo wa kufikia hukumu dhidi ya watu tunaowatuhumu kwa masuala mbalimbali.Kama tunahimizwa kuzitegemea mahakama kama vyombo vya kutoa haki ,kwa kutafsiri sheria ,kwa nini hatutaki kuzitumia katika masuala yanayowahusu watunga sheria.
 
Kafulila nae kapata issue ya kutokea baada ya kuwa kimya siku nyingi.
Siasa bana!
 
Ni basi tu kwa vile Nchi yetu haipo serious.
Lakini hii kashfa ilitakiwa iwafute ubunge wabunge wote wa kwenye hiyo kamati.
 
Mbona mimi nasikia kuwa wbaunge wote wanaokaa kwenye hizi kamati ni wala rushwa na huwa wanasumbua sana Menejimenti za mashirika na taasisi nyingine za serikali wakienda huko kiukaguzi maana ni kama omba omba wakifika huko! duh aibu!

sio kusikia tu hawa jamaa wanakula rushwa kinoma yaani kila halmashauri inapopeleka vitabu vyake kukaguliwa lazima waende na fungu la kuwapa hawa wabunge la sivyo vitabu vitakataliwa.
Inauma sana ila wanakula rushwa kinyama mkuu.
 
sawa unaweza kujitoa,lakini kumbuka ...... chako akipendi movie za kivyokovyoko,kwa sasa tulia acha sheria ifanye kazi.
 
sawa unaweza kujitoa,lakini kumbuka ...... chako akipendi movie za kivyakovyako,kwa sasa tulia acha sheria ifanye kazi.
 
Mbona mimi nasikia kuwa wbaunge wote wanaokaa kwenye hizi kamati ni wala rushwa na huwa wanasumbua sana Menejimenti za mashirika na taasisi nyingine za serikali wakienda huko kiukaguzi maana ni kama omba omba wakifika huko! duh aibu!

Ni yupi uliyewahi kusikia kajiuzulu?
 
Hao waliotajwa na Kafulila mwaka jana na orodha nzima aliye nayo aiweke hadharani plz isijekuwa pumba zake.
 
Kwa principle za natural justice Kafulila umechemka, jamaa bado anabaki kama mtuhumiwa tu, hata Bunge haliwezi kumvua ubwege sorry ubunge bila kwanza kujiridhisha na tuhuma zinazomkabili je anafahamu presumption of innocence? Innocent until proven guilty, sasa utasemaje afukuzwe ubunge? Ushauri wangu kwake ni kwanza alitakiwa yeye ajitoe kwenye hiyo kamati kama anaamini ni ya waomba rushwa, pili atoe ushirikiano TAKUKURU kama shahidi ili kama kuna anachokijua kuhusu hizo rushwa then asaidie mashtaka ili haki itendeke, tusijenge taifa la washika sheria mkononi, misingi ya sheria lazima iheshimike ili kujenga taifa bora. Ni waty wangapi wanakesi za kubambikiwa wako mahakamani wakisota bila suluhu, ni wezi wangapi wako mtaani wakitanua bila kufanywa kitu? Mjomba usikurupuke. Nachukia waomba rushwa lakini bado naamini lazima waathibiwe na mahakama kwanza then mengine ndo yafuate.
 
Back
Top Bottom