Tamko la Jumuiya ya Madaktari Tanzania

sidhani kama unaweza kuepuka makundi au wasaliti katika umoja wowote duniani.
hao madon unaowasema hawakuunga mkono mgomo ni kina nani?unakumbuka kamati iliyoenda kumuona rais ilijumuisha watu gani?nitakusaidia mmoja ....ni profesa wa magonjwa ya njia ya mkojo anaitwa Yongolo.nitajie waliobaki mkuu.

haturuhusiwi kuandika majina ya watu humu ... mkuu trust me kwenye mgomo wenu kuna watu walikuwa wakishiriki ilimradi tu msiwaone wasaliti lakini mioyoni hamkuanao walikuwa wakiwaza zaidi hatima ya kazi zao za ziada mbali na kutibu ... jaribu kuchunguza mwenyewe ushiriki wa wakuu wa department, miradi, DMO, RMO na wale wenye majina makubwa mjini
 
ccmweli bhana, wameona njia pekee ya kutatua madai yao ni kuwagawa!

Wakadhani watanyamaza
Lazima tutasikia mengi na bado.
 
Kiukweli yule mwenyekiti famba wa jana sio dakitare,yule ni askari wa usalama wa taifa na wale wengine ni makanjanja tu wachumia tumbo!! Yani ilikua full maigizo matupu.
 
Wameshagawanyika hawa watu sasa,haya yetu macho tu aisee!Lakini ningependa kuuliza kipindi chote hiki cha miezi miwili MAT wamechukua hatua gani kwa hawa vijana wa Intern wanaohaha mtaani hasa kufuatilia ni lini wataanza kuhojiwa na MCT?

Mkuu MWILI NYUMBA, ..MAT ni chama cha KITAALUMA, ..katika kipindi hicho chote,kimekuwa kikitoa updates, kupitia vikao, na taarifa mbali mbali...zikiwa
1. Kuwapa moyo(kuwatia shime)

2.Kutoa matangazo ya kazi yatokayo sehemu mblimbali(kazi zinazohusiana na TAALUMA)..mfano Tafiti (Research) n.k

3.Ikiomba UMOJA, SUBIRA na kutokubali kupotoshwa au kudanganywa kwa wanachama waliofukuzwa( Intern doctors).

4. Ikifuatilia kesi dhidi ya Mwenyekiti wa MAT

5.mengineyo


Shida inapokuja katika hoja namba Tatu(3), niluyoitaja hapo juu, baadhi ya wanachama kusahau hiki ni chama cha kitaaluma, na si kisiasa, kutokuwa WAVUMILIVU (kuhitaji mambo yao yawe solved kwa uharaka hata kama WATAJUTIA), kutofuata uongozi na kauli za viongozi...kwani i can tell you Mkuu,
-Si intern hao tu wenye shida.
-Hata maaumuzi YASIYO SAHIHI waliyoyafanya hawakuujulisha uongozi wa MAT, wala jumuiya ya madaktari angalau kupata ushauri.

Na hapa ndipo yanapoonekana haya yanayoonekana na kusikia tunayoyasikia.
 
Yani wale watotow janawaliokuwa wanasoma sijui hotuba au risala iliyoandikwa na Ramadhan Ighondu ndo mnaijadili hapa??!!

Cut this craap. Hiini staged play ya kipuuzi sana.
 
naona 'fushi'limeanza upya kabisa.niliwahi kusema migogoro haiishi kwa propaganda za kisisasa.

Ni kweli kabisa! Busara ilikuwa ni kuwasikiliza madaktari na kutekeleza madai yao! Hizi propaganda zao zitawagawa hawa madaktari na kitakchofuatia ni huduma mbaya kwa mwananchi!! Ingawa kwa ulevi wa siasa wapo wasomi wazuri tu wanafurahia na kushabikia Tamthilia hii!!Jamani maigizo yao ni mauti kwetu!!!
 
haturuhusiwi kuandika majina ya watu humu ... mkuu trust me kwenye mgomo wenu kuna watu walikuwa wakishiriki ilimradi tu msiwaone wasaliti lakini mioyoni hamkuanao walikuwa wakiwaza zaidi hatima ya kazi zao za ziada mbali na kutibu ... jaribu kuchunguza mwenyewe ushiriki wa wakuu wa department, miradi, DMO, RMO na wale wenye majina makubwa mjini

Nakubaliana nawe, nilikuwa lindi, alikuja RMO mzee mmoja anaitwa machibya, na Mkuu wa mkoa wake wakaja na kauli ya kuwapongeza madaktari wa mkoa wao kwa kutoshiriki mgomo!!!

shida ya hivi vyeo vya kisiasa vya kupewa!!!
 
Nakubaliana nawe, nilikuwa lindi, alikuja RMO mzee mmoja anaitwa machibya, na Mkuu wa mkoa wake wakaja na kauli ya kuwapongeza madaktari wa mkoa wao kwa kutoshiriki mgomo!!!

shida ya hivi vyeo vya kisiasa vya kupewa!!!
hata hawa ma DMO na RMO hawako salama na maslahi yao yameminywa ndio maana hukumbwa na kashfa za kifisadi.wanajua ugumu unaowakabili katika kuboresha huduma za afya lakini hawasemi wazi wazi.
Ni hivi majuzi DMO wa lushoto kadhalilishwa na mkuu wa mkoa lakini yuko kimya tu.
 
naamini serikali ingekua na nia ya dhati ya kutatua mgogoro wa madaktari ingefanya hivyo kwani muda iliopewa ni mrefu sana.sasa tunaelekea kwenye mgomo mwingine tena.tusubiri tuone.
 
Nahisi jama wa jana waliandaliwa mpaka ile press release. Yale siyo maneno ya mpiganaji.
 
Kwa nini CCM na Ikulu mnawalazimisha kuwaomba msamaha wakati madai yao yote bado hayajatekelezwa? Hamuoni kuwa haiwezekani? Na watu wenye timamu tulijua tangu jana tamko la Jana halikuwa lao bali Lenu CCM na Ikulu ya akina RAMA
 
Mimi nilikuwa nasubiri kusikia kauli ya MAT ama jumuiya ya madaktari iliyokuwa chini ya Dr. Ulimboka.
Usaliti umekuwa ni sehemu ya maisha ya kawaida ya mtanzania. Madaktari wameasalitiana kama waandishi wa habari wanavyosalitiana juu ya kifo cha mwenzao marehemu Daudi Mwangosi. Walikubaliana kwamba wasiripoti habari za polisi walau kwa siku hizi arobaini lakini wapi kesho yake tu wengine wakaanza kutiririka na kauli za marpc.

.
Njaa mbaya sana. Inaweza kabisa kuuondoa utu.
.
 
Back
Top Bottom