Kwa Tanzania ya leo, ni upuuzi wa kupindukia kwa mtu kujilipua kama wale madaktari walijidai wanaomba msamaha. Sijui kama wanaelewa the real magnitude ya walichokifanya kwa maisha yao huko mbeleni. Mchezo wa 'mamluki' umekuwepo kwa miaka mingi mno kiasi kwamba watanzania wanaweza kabisa kutabiri watawala watafanya nini! They have never updated their game! Lakini aibu ni pale watanzania -vijana wanapoamua kucheza hizo zilipendwa!
2015 wataangalia upande gani? Na hata kwa sasa, nani atawaamini? Within their own community (medical profession) watakuwa wageni wa nani?
Mimi nafikiri Madaktari wetu wanakosa Uongozi bora tofauti kabisa na enzi za kina Sarungi. Nilisema toka mgomo w akwanza kuwa PR yao mbovu halafu hawajui wanachokidai isipokuwa kila siku walibadilisha ama kuongeza matakwa ili mradi ilidhihirika wazi kwamba hawakujipanga vizuri toka mwanzo.. Inaonyesha kuna makundi ndani ya madaktari wenyewe na pengine kosa kubwa ni kuwa na UNION nyingi na tofauti wakati wanasimamia profession moja...Mimi nilikuwa nasubiri kusikia kauli ya MAT ama jumuiya ya madaktari iliyokuwa chini ya Dr. Ulimboka.
Usaliti umekuwa ni sehemu ya maisha ya kawaida ya mtanzania. Madaktari wameasalitiana kama waandishi wa habari wanavyosalitiana juu ya kifo cha mwenzao marehemu Daudi Mwangosi. Walikubaliana kwamba wasiripoti habari za polisi walau kwa siku hizi arobaini lakini wapi kesho yake tu wengine wakaanza kutiririka na kauli za marpc.
Mimi nafikiri Madaktari wetu wanakosa Uongozi bora tofauti kabisa na enzi za kina Sarungi. Nilisema toka mgomo w akwanza kuwa PR yao mbovu halafu hawajui wanachokidai isipokuwa kila siku walibadilisha ama kuongeza matakwa ili mradi ilidhihirika wazi kwamba hawakujipanga vizuri toka mwanzo.. Inaonyesha kuna makundi ndani ya madaktari wenyewe na pengine kosa kubwa ni kuwa na UNION nyingi na tofauti wakati wanasimamia profession moja...
Inawezekana CCM wameitumia njia hii makusudi.. Zipo Jumuiya ya wanawake wa CCM, Chadema na sijui kila chama ili mradi kuwasambaratisha na kuondoa nguvu na ushirika wa wanawake wote nchini. Wametumia kutugawa hivi ktk makundi tofauti ili sisi wenyewe tusiwe na UMOJA hivyo basi ni muhimu sisi wenyewe kufikiria nje ya kabati hili..
mkandara unajua kwenye hii field kuna madaktari wanaopiga hela si mchezo mfano ni wale wakuu wa department, miradi na wenye majina makubwa mjini na kundi la pili ni wale wanaopigika na maisha mawilayani na mikoani ndani ndani huko. Kwenye hii migomo front line walikuwa ni wale wanaopigika lakini yale madon yalikuwa pembeni yakiangalia watoto wa juzijuzi kina ulimboka wakipiga kelele kwenye screen.. Hawa watu hawakuwa wamoja tangu awali
Full confusions!