Mungi
JF Gold Member
- Sep 23, 2010
- 16,975
- 9,566
Ndg, wana JF,
Katika kikao cha wilaya kilichofanyika katika Hoteli ya Stereo hapa Arusha, chadema wilaya ya arusha imetoa tamko kwamba haitambui muafaka wa madiwani, na kwa usaliti waliouonyesha hawatahitaji kuona katiba inapindishwa, wachukuliwe hatua kali za kinidhamu ili iwe fundisho kwa wale wote wenye nia mbaya na wasioendana na katiba ya chama.
Kikao hicho kilifanyika chini ya uongozi wa mkoa, ambayo ilikuwa chini ya mwenyekiti wake Ndg, Samson Mwigamba na Katibu wake wa mkoa pamoja na wajumbe wengine akiwepo mbunge wa jimbo la arusha ambaye ameingia kwa kofia ya kuwa mjumbe wa kamati kuu ya chama.
Msimamo huo uliungwa mkono na wajumbe wote, ambao kwa pamoja wamesema madiwani wote waliokiuka katiba wafukuzwe kabisa chamani wakatafute chama chao.
nawakilisha.
Katika kikao cha wilaya kilichofanyika katika Hoteli ya Stereo hapa Arusha, chadema wilaya ya arusha imetoa tamko kwamba haitambui muafaka wa madiwani, na kwa usaliti waliouonyesha hawatahitaji kuona katiba inapindishwa, wachukuliwe hatua kali za kinidhamu ili iwe fundisho kwa wale wote wenye nia mbaya na wasioendana na katiba ya chama.
Kikao hicho kilifanyika chini ya uongozi wa mkoa, ambayo ilikuwa chini ya mwenyekiti wake Ndg, Samson Mwigamba na Katibu wake wa mkoa pamoja na wajumbe wengine akiwepo mbunge wa jimbo la arusha ambaye ameingia kwa kofia ya kuwa mjumbe wa kamati kuu ya chama.
Msimamo huo uliungwa mkono na wajumbe wote, ambao kwa pamoja wamesema madiwani wote waliokiuka katiba wafukuzwe kabisa chamani wakatafute chama chao.
nawakilisha.