Tambaza Taifa Kubwa!!

Steve Dii

JF-Expert Member
Jun 25, 2007
6,402
1,254
Yep ni Tambaza. Kwani kuna shule gani tena nyingine inafua dafu?! Come on pipo, let's be honest...

Naongelea Tambaza Sec. School. Shule iliyotoa watawala wengi wa nchi hii. Shule iliyokuwa na waalimu mashuhuri Dar na Tanzania nzima. Tambaza ile ya kitambo. Enzi za akina mwalimu Dafa. Tuition zote bongo mashuhuri zilikuwa Tambaza. Hata Azania (tuliokuwa tunawapa mkong'oto kila tulipohitaji ku-release stimu kindondi) walikuwa wanatusifia kwa waalimu walio makini. Hata baadhi ya watoto wa IST walikuwa wanakuja kupigwa msasa wa tuition hapo. Though sikupata mwona Yo Yo na IST yake ya kufikirika!

Zanaki walikuwa mashori wetu. But kwa vile Tambazec ilikuwa taifa kubwa, tulikuwa hatuna upinzani hata pale tulipoamua kwenda kwa ngamia Jangwani (Azania simply couldn't square up to us). Forodhani watoto wa mama walikuwa wanatuachia njia tunapita huku mademu wao waki scream in excitement kana music fans kwenye concert ya MJ (RIP).

Watoto wa Misufuni Kinondoni pamoja na kujifanya watoto wa mjini bado walikuwa wananawa mikono wakituona. Zile kaptula za grey zilikuwa noma bana wee acha tu. Makonda wa mabasi hao ndiyo kabisaaa sitaongelea mengi kwa hawa. Maana hatuchelewi kuanza ibua mamabo ya akina Puza (RIP) na akina Nyau na akina Chuwa!! By the way hii ni ile Tambaza kama watoto wa mjini.

Tambaza kama wana academia pia ni kiwingu cha masafa ya mbali. History has it. Hamna ubishi katika hili. In fact, tangu enzi zile za 60s, 70s, 80s, hata hiyo 90s niliyosoma mimi Tambaza ni moto wa kuotea mbali kielimu, muulizeni Jasusi shahidi wetu wa enzi hizo hapa JF. Of course, mambo yalianza kuwa neutralised a bit hapo mid 90s, pale shule ilipoanza kuchanganywa na mademu na baada ya fujo spill out of control nakupelekea shule kufungwa kwa muda.

Btw kaptula yangu ya Daruweshi bado ninayo. Hebu ngoja nikanyonye picha kutoka kwenye blog ya kaka Mjengwa. Ni alumna mmojawapo huyu, alinitangulia aka kadhaa hivi... lol. Leteni mapicha mengineyo tukumbushane Taifa Kubwa la Tambaza wajomba! Ayeya!
 
Kumbe wewe ni Taifa kubwa, nakumbuka ATC. Mambo yote ilikuwa tukicheza mechi na wadogo zetu Azania (wakina Abdulhalim). Hivi yule Mzee muuza Karanga sijui yu wapi. Mzee alikuwa na stori kibao za wanafunzi waliopita Tambaza. Namkumbuka pia Mwalimu wa Biology Pepeyu na pia wa Historia Mama Kiwope. Bila kumsahau mkali wa Practical (Chemistry) Bwana Hassan Liana.

Marehemu Puza, yani kuingia tu Tambaza aliweza kupanda grorofa ya pili ambako kulikuwa na madarasa ya jamaa wa Kidato cha pili. Kwa utemi hakuteswa na mtu japo Kidato cha I walikuwa wanateswa zaidi na wa Kidato cha II. Ahhhh Tambaza.
 
Mama Shija alihamishiwa Azania, lakini Savimbi sijui yu wapi. Ila alinyoa yale Madevu.

Mama Shija na Tuition yake!! Tumetoka mbali sana enzi za Tambaza Boys..miaka ya 1980s!!

RIP H/M Mwalimu Kalumuna
 
duuh umenikumbusha mbali sana hasa fimbo za mwalimu Chale wa Chemistry balaa,

unamkumbuka okello yuko wapi yule?,msosi kupata lazima uvue shati sughuli yake pevu.

shani zinakaa toilet ,ATC saa tisa lazima iruke hakuna kusubiri kumi na moja,
 
Mama Shija na Tuition yake!! Tumetoka mbali sana enzi za Tambaza Boys..miaka ya 1980s!!

RIP H/M Mwalimu Kalumuna
nilimuona mwalimu hassan yule kiboko wa practical chemistry sometimes back , mie nilijiunga Advanced Level baada tu ya kuchanganywa jinsia. mwalimu wa biology alikuwa mama flani mnoko kichizi lakini alikuwa mshikaji wangu anaitwa Mama Mbele. naona wenzangu vikongwe kidogo maana enzi zangu mimi kulikuwa na WUTAMBA CLAN,walikuwa wanakoma billicanas maana kila ijumaaa lazima watu wakajipongeze
Dah mwana umenikumbusha mbali saaaana
 
duuh umenikumbusha mbali sana hasa fimbo za mwalimu Chale wa Chemistry balaa,

unamkumbuka okello yuko wapi yule?,msosi kupata lazima uvue shati sughuli yake pevu.

shani zinakaa toilet ,ATC saa tisa lazima iruke hakuna kusubiri kumi na moja,
hahhahahaha mwalimu chale nilikutana nae nilivyoendaga kuchukua vyeti vya ndugu yangu, alikuwa ame base kwenye lab ya biology, alikuwa kituko mdomo mziiito , unakumbuka mikwara yake?
 
Last edited:
na mama kalunga mlalamishi kichizi na mwenzake mdemu wa geography room...mjengwa akituandikia habari za kila mechi!
 
hahhahahaha mwalimu chale nilikutana nae nilivyoendaga kuchukua vyeti vya ndugu yangu, alikuwa ame base kwenye lab ya biology, alikuwa kituko mdomo mziiito , unakumbuka mikwara yake?

Nakumbuka chale na enzi zake pale chemistry utasikia wewe lete m@t@k0 bwana... weka vizuri... bado kimoja bado kimoja MTM si ukome kuafanya madudu hapa!!! ila alikuwa na mwandiko mzuri sana
 
Though sikupata mwona Yo Yo na IST yake ya kufikirika!
mtoto wa uswazi Abdulhalim alianza kupiga jungu na mie sijaozea majungu majungu nikasepa.......

yule dogo jenerali nyau yuko wapi?
 
mtoto wa uswazi Abdulhalim alianza kupiga jungu na mie sijaozea majungu majungu nikasepa.......

yule dogo jenerali nyau yuko wapi?

aaahhhh weweeeeeeee, wamo humu baadhi, kuna kajamaa kaliitwa no mbungi na nwenzake mmoja, walikuwa vituko mno... natamani ningewasiliana nao siku moja!!!

HIVI HAKUJAWAHI KUWA NA TAMBAZA THREAD BEFORE AISEE??
 
nilimuona mwalimu hassan yule kiboko wa practical chemistry sometimes back , mie nilijiunga Advanced Level baada tu ya kuchanganywa jinsia. mwalimu wa biology alikuwa mama flani mnoko kichizi lakini alikuwa mshikaji wangu anaitwa Mama Mbele. naona wenzangu vikongwe kidogo maana enzi zangu mimi kulikuwa na WUTAMBA CLAN,walikuwa wanakoma billicanas maana kila ijumaaa lazima watu wakajipongeze
Dah mwana umenikumbusha mbali saaaana
bibie ilikuweje ukasoma combination ngumu namna hio? PCB CBG unaonekana shori wa HKL HGK KLF hivi........

ila tambaza walikuwa machizi tu.....kujifanya magangwe gangwe usela wao ulizidi...kuna kijamaa kimoja eti alikuwa anajiita killer one......ukimuuliza kaua wangapi hata mbu hajaua.....
 
Kuna siku moja baada ya watu kufanya fujo Kinondoni Muslim, Julius Mushi akawaita watu, nbasi watu wakafikiri Mushi atawaua sana.Kitu cha kwanza Mushi akasema, "kila ninapoenda nasikia Tambaza hili, Tambaza lile, kama Tambaza jeshi gani sijui, mimi nachotaka kujua wa kwangu walioumia wako wapi". Basi Mushi na unoko wake wote watu walimshangilia sana siku hiyo.

Nakumbuka mpaka Lyatonga Mrema mwenyewe alitia timu na ku suspend fair proces ya kufukuza shule mwanafunzi on the fly in violation of Ministry of education policy.

Tambaza ilikuwa vita na makonda, wakiona grey shorts wanajua daladala linaweza kutekwa nyara kutoka njia ya kwenda Muhimbili likapelekwa mpaka Tambaza halafu wanafunzi wote wakashuka kabla halijasimama na kuingia mtini, machizi walishafanya hii.
 
Hassan hakuwa Mwalimu, ni lab technician ambae ilikuwa unalazimika kusoma tuition kwake kwa sababu mtihani wa practical chemistry ni yeye anaufungua kuu test siku mbili tatu kabla ya siku ya hukumu. Halafu anagawa kwa wana tuition. Fisadi mkubwa.

Azania walikuwa academically superior kuliko Tambaza, hilo tusibishe.

Puza alikuwa mgumu, one of the most roughneck kids in the history of Tambaza, lakini alijiua. Kumbe ndani alikuwa mlaini.

Mama Shija alikuwa fisadi, anafundisha madarasa jioni, ana miss vipindi asubuhi, anatumia majengo ya shule.

Makonda walikuwa wanatiwa adabu lakini kuna mmoja aliuawa siku ya mechi na Mgulani, uwanja wa Taifa. Shule likasambaratishwa, wakaletwa mademu, and that was the end of Tambaza as you knew it.
 
GT kasoma wapi? anasema yeye mtoto wa mjini shule zoote za town hayumo....IST miaka yoote niliosoma pale sikuwahi kuona shekhe yeyote
 
Azania walikuwa academically superior kuliko Tambaza, hilo tusibishe.

Inategemea kwa level ipi... O level yes for a few years after 1988 but for A level, you must be dreaming!!!!!! Kinega ulisoma wapi??
 
Mnanikumbusha enzi za Kalumuna na Mwaipopo hapo Tambaza, bila kusahau duka shop kwa yule muhindi kunywa juice chafu.
 
Inategemea kwa level ipi... O level yes for a few years after 1988 but for A level, you must be dreaming!!!!!! Kinega ulisoma wapi??

Ni kweli, A-Level Azania walikuwa vibonde. Lakini O-Level ni vizuri umekubali Tambaza walikuwa wanateswa.

Kulikuwa na pointi saba Azania kila mwaka, Abdil Rashid, Frank Minja, Omary Mtiga... just being objective
 
bibie ilikuweje ukasoma combination ngumu namna hio? PCB CBG unaonekana shori wa HKL HGK KLF hivi........

ila tambaza walikuwa machizi tu.....kujifanya magangwe gangwe usela wao ulizidi...kuna kijamaa kimoja eti alikuwa anajiita killer one......ukimuuliza kaua wangapi hata mbu hajaua.....
on the other hand,warushwa ukuta walikuwa wengi tuu Tambaza, ukianza na mwalimu wao Khan
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom