Tamaduni Za Kipumbavu

Waridi

JF-Expert Member
Mar 30, 2008
1,025
172
Watanzania wenzangu,napendekeza tuachane na kuadhimisha sikukuu ya wajinga.

Mjinga ni mtu asiyejua kusoma au kuandika au vyote viwili.Namna nzuri ya kuadhimisha siku yake basi ingekuwa ni kumsaidia aonokane na ujinga wake na pengine kumsaidia hapate kila ambacho kwa sababu ya ujinga alionao anakikosa,matharani kushindwa kupata taarifa muhimu zilizoko katika maandishi nk.
Cha kusikitisha eti duniani kuna sikukuu ya wajinga na inaadhimishwa kwa kudanganyana-kupeana habari za uongo-kupumbazana.
Kwangu mimi maadhimisho ya namna hiyo ni upumbavu.Heri basi siku hiyo ingeitwa sikukuu ya WAPUMBAVU,kwa maana ya kwamba ni siku ambayo waongo na wapumbavu wanapata fursa ya kusema uongo wao hadharani.

Najiuluza ni nini kisa cha watanzania kushabikia sikukuu hii,hadi hata vyombo vya habari vinaamua kuwauzia wanunuzi wa magazeti na wasikilizaji wao habari za uongo.
Maadhimisho haya ni upuuzi,tamaduni ya kuachana nayo.
 
waridi nadhani tatizo liko kwenye sisi tuliotafsiri siku kuu ya "fools day" kuwa ni siku ya wajinga (ignorant). Sasa ingekuwa ni siku kuu ya wajinga basi suluhisho lako ni muhimu kwamba tunaelemishana, kwani ujinga hutoka; kwa bahati mbaya upumbavu hauotoki kwa elimu bali kwa mtu kuoneshwa upumbavu wake.
 
Back
Top Bottom