Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,080
Wanamgambo wa Taliban nchini Afghanistan
Baada ya kuwaonya watu wasijitokeze kupiga kura kwenye uchaguzi wa Afghanistan na kutishia kuvikata vidole vya watu wote watakaopiga kura, Taliban wameanza kuonyesha kwa vitendo vitisho hivyo kwa kukata vidole vya watu wawili. Awali kabla ya uchaguzi mkuu wa Afghanistan uliofanyika alhamisi, Taliban waliwataka wananchi wa Afghanistan wasusie uchaguzi mkuu wa nchi hiyo na kutishia kuvikata vidole vya watu wote watakaopiga kura.
Katika kutekeleza vitisho hivyo walivyovitoa, Taliban wamevikata vidole vya watu wawili ambao walikamatwa vidole vyao vikiwa bado vina wino usiofutika wa kupigia kura.
"Huu ni mwanzo tu, watu wote walioshiriki uchaguzi uliopita kwa kupiga kura watakatwa vidole vyao" ilisema taarifa ya Taliban baada ya watu hao wawili kukatwa vidole vyao.
Taasisi ya wasimamizi wa uchaguzi wa Afghanistan, Nader Nader ilithibitisha kwamba watu wawili toka kusini mwa Kandahar walikatwa vidole vyao na Taliban.
Ili kuepuka kukatwa vidole vyao baada ya uchaguzi, watu wengi waliopiga kura walikuwa katika harakati za kuhakikisha wanaufuta wino usiofutika wa kupigia kura kwenye vidole vyao.
Uchaguzi wa mkuu wa Afghanistan ulifanyika alhamisi chini ya ulinzi mkali wa majeshi ya kigeni yakisaidiana na yale ya serikali.
Hamid Karzai na mpinzani wake mkuu Abdullah Abdullah, kila mmoja anajigamba kuibuka kidedea katika uchaguzi huo pamoja na kwamba matokeo kamili ya uchaguzi huo yatatolewa mwezi ujao.
Source: nifahamishe.com