Taliban Waanza Kukata Vidole Vya Wapiga Kura Afghanistan

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,080
2890074.jpg

Wanamgambo wa Taliban nchini Afghanistan

Baada ya kuwaonya watu wasijitokeze kupiga kura kwenye uchaguzi wa Afghanistan na kutishia kuvikata vidole vya watu wote watakaopiga kura, Taliban wameanza kuonyesha kwa vitendo vitisho hivyo kwa kukata vidole vya watu wawili. Awali kabla ya uchaguzi mkuu wa Afghanistan uliofanyika alhamisi, Taliban waliwataka wananchi wa Afghanistan wasusie uchaguzi mkuu wa nchi hiyo na kutishia kuvikata vidole vya watu wote watakaopiga kura.

Katika kutekeleza vitisho hivyo walivyovitoa, Taliban wamevikata vidole vya watu wawili ambao walikamatwa vidole vyao vikiwa bado vina wino usiofutika wa kupigia kura.

"Huu ni mwanzo tu, watu wote walioshiriki uchaguzi uliopita kwa kupiga kura watakatwa vidole vyao" ilisema taarifa ya Taliban baada ya watu hao wawili kukatwa vidole vyao.

Taasisi ya wasimamizi wa uchaguzi wa Afghanistan, Nader Nader ilithibitisha kwamba watu wawili toka kusini mwa Kandahar walikatwa vidole vyao na Taliban.

Ili kuepuka kukatwa vidole vyao baada ya uchaguzi, watu wengi waliopiga kura walikuwa katika harakati za kuhakikisha wanaufuta wino usiofutika wa kupigia kura kwenye vidole vyao.

Uchaguzi wa mkuu wa Afghanistan ulifanyika alhamisi chini ya ulinzi mkali wa majeshi ya kigeni yakisaidiana na yale ya serikali.

Hamid Karzai na mpinzani wake mkuu Abdullah Abdullah, kila mmoja anajigamba kuibuka kidedea katika uchaguzi huo pamoja na kwamba matokeo kamili ya uchaguzi huo yatatolewa mwezi ujao.

Source: nifahamishe.com
 
Hivi hasa Taliban wanataka nini? Kutawala nchi kwa njia ya mtutu wa bunduki au vipi. Kama kuna mtaalam wa maswala ya wa Taliban anifahamishe!!!Kukata watu vidole ni kukiuka misingi mikuu ya haki ya binadamu. Wapiga kura walikwenda kuchagua viongozi ambao watakao ongoza nchi ya Afghanistan
 
Hivi hasa Taliban wanataka nini? Kutawala nchi kwa njia ya mtutu wa bunduki au vipi. Kama kuna mtaalam wa maswala ya wa Taliban anifahamishe!!!Kukata watu vidole ni kukiuka misingi mikuu ya haki ya binadamu. Wapiga kura walikwenda kuchagua viongozi ambao watakao ongoza nchi ya Afghanistan

Hilo jambo sio geni kwa wafuasi wa Muhammad!
 
Hawajui wanachofanya hawa jamaa.Huo ni ushetani kama wakiamua kuufanya.Sio dini wala siasa
 
watakata pia makalio ya wale wafuasi wa paulo wanaochokoana vinyesi

Hiyo ni kabla au baada ya kumalizana wenyewe kwa wenyewe? Maana naona Taliban wana sulubu watu wao wenyewe, hapo hakuna cha Mmarekani wala Muingereza.
 
Mungu aiepushe Tanzania na all the Taliban likes. Mungu aiepushe dunia na watu hawa ambao wapo tayari kuua wananchi wao wenyewe wasio na hatia kwa ajili tu ya kuprove a point kwa watu wengine ambao hata hawa wagusi.
 
Mungu aiepushe Tanzania na all the Taliban likes. Mungu aiepushe dunia na watu hawa ambao wapo tayari kuua wananchi wao wenyewe wasio na hatia kwa ajili tu ya kuprove a point kwa watu wengine ambao hata hawa wagusi.

Ile mahakama ya KADHI ikianzishwa haiwezi kupelekea UTALIBANI mkuu?
 
Ile mahakama ya KADHI ikianzishwa haiwezi kupelekea UTALIBANI mkuu?

Sidhani mkuu. As much as I question mahakama ya kadhi I think utaliban is deeper than that. Nadhani utaliban una tokana na mila na desturi za watu. Mtu kakua ana fundishwa kitu fulani au kumchukia mtu fulani. Mtu ana kua kwa kufundishwa kuwa njia pekee ya kupata unacho taka ni kuua raia wenzio wasio na hatia. In short utaliban is a result ya mafundisho fulani fulani mtu anayo kua nayo tokea udogoni yanayo mfanya awe brainwashed. Yale yale ya mtu kuambiwa ukifanya hivi hata ukifa utaenda kupata hiki. Au ukiua kwa ajili fulani basi uta samehewa dhambi zako zote na kufika peponi. Simple propaganda to simple minded people can have a lot of harm. Lets just hope we in Tanzania have very few simple minded people who will be ready to do anything simply because they believe it's their ticket to heaven.
 
shukrani tumekujua wewe ni nani.

Well sorry if my opinions differ from you but if we all had the same views then there would be no point of JF. JF is not a place for getting simple yes or no answers. If you have noticed hamna thread yoyote iliyo isha kwa kila mtu kukubaliana. The purpose of JF is to look at both sides of the coin and to give each view an equal amount of time and space to voice their opinions. Kama wewe una taka kila mtu akubaliane na wewe I suggest you start a forum for people who simply think exactly like you. I'm sorry I don't share your opinions na hata siku moja I won't think killing innocent people, my own people, is for the greater glory.
 
Haya ni maamuzi ya kikundi kimoja cha kisiasa ambacho ukifatilia undani wake utakuta kuna nchi kubwa nyingi duniani zinazochochea vurugu za aina hii, ukweli wa mambo wanaujua wenyewe ila kikubwa kilichopo ni kwamba: Mataifa makubwa yanasababisha "political instability" kwa nchi za mashariki ya kati ili 1. Wauze silaha zao, 2. Wachukue resource zipatikanazo kwenye nchi husika 3. Wawagawe ili wawatawale kwa urahisi 4. Kuendelea kulinda maslahi yao kwa kuwasambazia silaha wanazotengeneza 5. Waweze kudumisha biashara zao za chakula, silaha na wataalamu wao na kujiongezea kipato.

Huo ni mtazamo wangu kwa upeo mdogo nilionao.
 
Haya ni maamuzi ya kikundi kimoja cha kisiasa ambacho ukifatilia undani wake utakuta kuna nchi kubwa nyingi duniani zinazochochea vurugu za aina hii, ukweli wa mambo wanaujua wenyewe ila kikubwa kilichopo ni kwamba: Mataifa makubwa yanasababisha "political instability" kwa nchi za mashariki ya kati ili 1. Wauze silaha zao, 2. Wachukue resource zipatikanazo kwenye nchi husika 3. Wawagawe ili wawatawale kwa urahisi 4. Kuendelea kulinda maslahi yao kwa kuwasambazia silaha wanazotengeneza 5. Waweze kudumisha biashara zao za chakula, silaha na wataalamu wao na kujiongezea kipato.

Huo ni mtazamo wangu kwa upeo mdogo nilionao.

Big up kisusi. Wanawafanya mhangaike na mambo yasiyo kichwa wala miguu na wao wanajichotea kiulaini. Angalia popote penye tifu duniani kwa asilimia kubwa lazima kuna hazina ya Mungu pale.sudan, Congo,Angola(zamani),Algeria, Nigeria,Msumbiji (zamani),etc
 
Suala la Taliban kukata watu vidole mimi ningependa lisihusishwe kabisa na suala la dini ya kiislamu.Maana haitaleta dhana nzima ya kuwa na huu uwanja wa kujimwaga.Taliban ni kundi kama makundi mengine yasiyopenda amani na si uislam.Waislam ndio wapenda amani wakubwa.Vikindi vichache visichukuliwe kuharibu DINI yetu.Wapo watu wanaotumia dini kujinufaisha wenyewe.Wapo mapandre ******* wanaotaka kutambulika na jamii ya kikristo kama watu wengine je tukiwaingingiza wakristo woote itakua sawa?Kuna mtu mmoja yupo Africa Mashariki hii hii.Joseph Konyi(Uganda) anataka kusimamisha amri kumi za dini yake.Hebu muangalie jamaa huyu anachokisema kinafanana na madai yake?Mbakaji yeye,muuaji yeye,mwizi yeye,Mnajisi yeye je tukiwahusisha wakristo kua ndio mambo yao ingependeza?
Naomba tuwe fair na Imani za wengine usikurupuke tu ukasema ooh ndio wa Muhhamad walivyo utakosea.Toa basi boriti jichoni mwako then ufauate kibanzi cha mwenzako.Haya si ndio maandiko jamani?Au huyaoni unaona kashfa tu ndio maisha?Ndio mafundisho ya Yesu mtoto wa Mariam hayo?Au ya Paulo?
Jiheshimu kijana yapo mengi sana yanayoendelea duniania yanayochafua dini zote kuu.Usiongee ushabiki.Unakumbuka yaliyotokea Bosnia?Au ulikua hujazaliwa?Ya Iraq juzi tu hapa wanajeshi walilazimisha watu kufirana wao wakishangilia na kupiga picha woote walikua wakristo wa kimarekani.
Kua mstaarabu na imani yetu we usie jitambua.
Hujawahi kujiuliza kuhusu Taliban na Amaerica uhusiano wao miaka ya 80?au ulikua hujazaliwa?
We wa wapi?
ACHA HIZOOOOOOOOOOOOOO NYAU We.
Suala la kadhi msiliongelee kabisa maana si busara kuongelea suala usilo lijua.Kama huna utafiti nalo usiliongelee.
Kwa heri babu!
 
Back
Top Bottom