Jatropha
JF-Expert Member
- Apr 9, 2009
- 1,151
- 199
Kwa muda mrefu sana yamekuwepo malalamiko kuwa Tanzania imefika hapa ilipo kutokana na wasomi kushindwa kutimiza wajibu wao ipasavyo wa kutoa maoni na ushauri kwa mujibu wa taaluma hata kama havitawapendeza watawala. Hali hiyo imechangia kwa kiwango kikubwa Tanzania kuangukia mikononi mwa kikundo kidogo cha mafisadi.
Hivi karibuni hali hiyo imeanza kubadilika baada ya wasomi kutambua umuhimu wa kuwa wazalendo zaidi katika masuala yanayohusu taifa hili.
Mfano halisi ni maoni ya msomi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe aliyeamua kutoa maoni yake katika Gazeti la Mwanahalisi la Tarehe Okt 27- Nov 3 ,2010; kuhusu takwimu za idadi ya watu katika nchi mbali ikiwemo Tanzania ili kuunga mkono hoja yake kuwa Tanzania haiwezi kuwa na watu wenye sifa za kupiga kura wanaofikia Milioni 19.6 kama ambavyo Tume ya Uchaguzi imedai kuwa wamejiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
Kwa mujibu wa msomi huyo nchi za duni ya Tatu zinakuwa na tabia ya "Pyramid Demographic" kwa watu wa nchi hizi wanakuwa na tabia ya kuoa wake wengi hivyo watoto wengi huzaliwa.
Hivyo anadai kuwa Tanzania"s Demographic segments inaonyesha kuwa watu walioko katika kundi la umri wa siku moja hadi miaka 18 ni kati ya 65-70% ya watu wote. Hivyo wenye sifa ya kujiandikisha kupiga kura ni 35% ya watanzania Milioni 40, ambao idadi yao itafikia kama watu Milioni 14 tu. Kati ya hao anadai unawza kukuta wenye sifa za kuandikisha kupiga kura kutokana na sababu mbali mbali kama Milioni 12.5 tu. Ikiwa 75% yao ndio watajiandikisha utakuta watu wanaopaswa kuwa kwenye Daftari la Kudumu la Kupiga Kura ni watu Milioni 10.5 tu, na sio Milioni 19.6 kama Tume ilivyotangaza.
Ndipo msomi huyo anatoa changamoto ya kuundwa kwa Tume kuchunguza kulikoni iwepo idadi kubwa ya wapiga kura kuliko idadi ya watu wanaostahili kuwa na sifa za kunadikishwa kupiga kiura hapa nchini.
Hivi karibuni hali hiyo imeanza kubadilika baada ya wasomi kutambua umuhimu wa kuwa wazalendo zaidi katika masuala yanayohusu taifa hili.
Mfano halisi ni maoni ya msomi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe aliyeamua kutoa maoni yake katika Gazeti la Mwanahalisi la Tarehe Okt 27- Nov 3 ,2010; kuhusu takwimu za idadi ya watu katika nchi mbali ikiwemo Tanzania ili kuunga mkono hoja yake kuwa Tanzania haiwezi kuwa na watu wenye sifa za kupiga kura wanaofikia Milioni 19.6 kama ambavyo Tume ya Uchaguzi imedai kuwa wamejiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura.
Kwa mujibu wa msomi huyo nchi za duni ya Tatu zinakuwa na tabia ya "Pyramid Demographic" kwa watu wa nchi hizi wanakuwa na tabia ya kuoa wake wengi hivyo watoto wengi huzaliwa.
Hivyo anadai kuwa Tanzania"s Demographic segments inaonyesha kuwa watu walioko katika kundi la umri wa siku moja hadi miaka 18 ni kati ya 65-70% ya watu wote. Hivyo wenye sifa ya kujiandikisha kupiga kura ni 35% ya watanzania Milioni 40, ambao idadi yao itafikia kama watu Milioni 14 tu. Kati ya hao anadai unawza kukuta wenye sifa za kuandikisha kupiga kura kutokana na sababu mbali mbali kama Milioni 12.5 tu. Ikiwa 75% yao ndio watajiandikisha utakuta watu wanaopaswa kuwa kwenye Daftari la Kudumu la Kupiga Kura ni watu Milioni 10.5 tu, na sio Milioni 19.6 kama Tume ilivyotangaza.
Ndipo msomi huyo anatoa changamoto ya kuundwa kwa Tume kuchunguza kulikoni iwepo idadi kubwa ya wapiga kura kuliko idadi ya watu wanaostahili kuwa na sifa za kunadikishwa kupiga kiura hapa nchini.