Mwenda_Pole
JF-Expert Member
- Jul 5, 2008
- 281
- 66
WANAFUNZI wanne wa shule za sekondari wilayani Karagwe, wamehukumiwa kwenda jela miezi sita kila mmoja kwa kosa la kushindwa kuwataja waliowapa ujauzito na kusababisha washindwe kuendelea na masomo.
Wanafunzi hao kutoka shule za sekondari za Nyabiyonza, Nkwenda na Bugene ambao majina yao yamehifadhiwa, walihukumiwa kifungo hicho hivi karibuni na Mahakama ya Wilaya ya Karagwe.
Akizungumzia adhabu za wanafunzi hao, Mkuu wa Wilaya ya Karagwe, Kanali mstaafu Fabian Masawe, alisema wazazi wanapaswa kushirikiana na serikali kupiga vita watu wanaowakatisha masomo watoto walio chini ya umri, kwani hao ndio rasilimali ya taifa.
Masawe alisema mahakama ya wilaya imewahukumu watoto hao wa kike kwenda jela miezi sita kila mmoja, kutokana na kushindwa kuwataja waliowapa ujauzito na kushindwa kutoa ushirikiano kwa mahakama ili kuwatia hatiani wahalifu hao.
Alisema wanafunzi hao wamepelekwa katika mahakama za watoto watukutu ili iwe fundisho kwa watoto wengine wenye tabia kama hiyo.
Kwa mujibu wa Kanali Masawe, takwimu zilizopo ofisini kwake zinaonyesha kuwa wanafunzi tisa wa shule za sekondari wamepata ujauzito katika kipindi cha Januari hadi sasa.
Pia alisema asilimia 85 ya wanafunzi waliopimwa, wamekutwa na virusi vya ugonjwa wa ukimwi.
Kutokana na hali hiyo, amewaomba wananchi kuwafichua wazazi wanaowaozesha watoto wao walio chini ya umri, wanaowakatisha masomo wanafunzi kwa kuwapa ujauzito ili waweze kufikishwa mbele ya mikono ya sheria.
Source: Tanzania Daima, 21st September 2009
Hapo kwenye bold, huyu mwandishi atakuwa amekosea nini...???? au angetuambia tu ni wangapi jumla walipimwa kisha ikapatikana hiyo 85% otherwise hali inatisha...
Wanafunzi hao kutoka shule za sekondari za Nyabiyonza, Nkwenda na Bugene ambao majina yao yamehifadhiwa, walihukumiwa kifungo hicho hivi karibuni na Mahakama ya Wilaya ya Karagwe.
Akizungumzia adhabu za wanafunzi hao, Mkuu wa Wilaya ya Karagwe, Kanali mstaafu Fabian Masawe, alisema wazazi wanapaswa kushirikiana na serikali kupiga vita watu wanaowakatisha masomo watoto walio chini ya umri, kwani hao ndio rasilimali ya taifa.
Masawe alisema mahakama ya wilaya imewahukumu watoto hao wa kike kwenda jela miezi sita kila mmoja, kutokana na kushindwa kuwataja waliowapa ujauzito na kushindwa kutoa ushirikiano kwa mahakama ili kuwatia hatiani wahalifu hao.
Alisema wanafunzi hao wamepelekwa katika mahakama za watoto watukutu ili iwe fundisho kwa watoto wengine wenye tabia kama hiyo.
Kwa mujibu wa Kanali Masawe, takwimu zilizopo ofisini kwake zinaonyesha kuwa wanafunzi tisa wa shule za sekondari wamepata ujauzito katika kipindi cha Januari hadi sasa.
Pia alisema asilimia 85 ya wanafunzi waliopimwa, wamekutwa na virusi vya ugonjwa wa ukimwi.
Kutokana na hali hiyo, amewaomba wananchi kuwafichua wazazi wanaowaozesha watoto wao walio chini ya umri, wanaowakatisha masomo wanafunzi kwa kuwapa ujauzito ili waweze kufikishwa mbele ya mikono ya sheria.
Source: Tanzania Daima, 21st September 2009
Hapo kwenye bold, huyu mwandishi atakuwa amekosea nini...???? au angetuambia tu ni wangapi jumla walipimwa kisha ikapatikana hiyo 85% otherwise hali inatisha...