Elections 2010 TAKUKURU yamkamata Magreth Sitta Tabora; Aachiwa kwa dhamana

Watakamatwa wengi na kampeni hizi!...

Mkuu hii issue ya TAKUKURU kukamata wagombea wa CCM mwisho ni tarehe 31 mwezi huu. Baada ya hapo hutosikia mgombea yeyote wa CCM anakamatwa na TAKUKURU kwa kutoa rushwa kwa wapiga kura, kununua shahada au kulisha watu wali. Kwani kwa kufanya hivyo kutakuwa ni kukosesha CCM jimbo. Tegemea wapinzani wengi kukamatwa na TAKUKURU wakati wa kampeni hasa maeneo CCM inapokuwa hoi bin taaban. Believe me haya ni maandalizi ya kuukandamiza upinzani wakati wa kampeni za kuelekea october. MARK THIS POST!!!!

Kwa nini TAKUKURU wanafanya hivi?

1. Kuudanganya ulimwengu kuwa CCM inapiga vita rushwa.

2. Majungu yanayoendelea miongoni mwa wana - CCM wenyewe kwa wenyewe

3. Part of revenge ya Hosea baada ya kumshikia bango, Huwezi kumkamata mtu akiwa na keshi au bahasha halafu useme alikuwa anataka. Unatakiwa kumkamata wakati anatoa rushwa. Kama bahasha zake na hela ni zake halali kuna kosa gani?

Unajua nilisoma jama eti wamemkamata mkuu wa wilaya ya kasulu betty Machangu akiwa chumbani hotelini, swala la kujiuliza ni kwamba kuna kosa gani mtu kukodi chumba hotelini na kukaa na wapambe wake wawili?. Yaani TAKUKURU ni big mchemko na inaonesha wazi kuwa wameshindwa mbinu za kikachelo matokeo yake wanatumia mbinu za kivamizi sasa. Tushangilie haya yanatokea sasa kwa CCM wenyewe kwa wenyewe lakini tujiandae kulia sana pale tutakapoona wagombea wenye nguvu wa upinzani wapoondolewa uwanjani - Kumbuka ya Shitambala

Wakati wa kuwakemea TAKUKURU ni huu. Baadae watasema mbona wana CCM walipokuwa wakikamatwa mlikuwa kimya?
 
Mkuu Mwanalugali unashangaa nchi inaendeshwaje?

Hapo ikiwa kweli Mh. Sitta amekamatwa na alikuwa na fikira za kurudi tena bungeni, je wanasheria mnaonaje suala la yeye kuwa na "Criminal Record" je ndio amemalizwa au?
 
Sasa hii imekaaje kwa hawa TAKUKURU mbona wanamoyo sana kukamata
au wamehaidiwa kitu manake ghafla wamefufuka kila siku sasa tunawasikia
mara huyu mara yule sijui hii imekaaje wadau naomba msaada.
Needs thinking... Ujio wa Slaa utasababisha baadhi ya watu wafikishwe mbele ya sheria haraka iwezekanavyo ili akose la kuongea kwenye kampeni maana JK atakuwa walau kawaonyesha watanzania kuwa 'anaweza kuthubutu'!

Lakini, hii kamatakamata isiishie hapo, hatua zichukuliwe, na wakimaliza kamatakamata yao tutakuja na video evidences za wale ambao hawakuwagusa kabisa na tutawaonyesha kwa kifupi tu via JF, wakibisha tutaleta FULL video clips ili kuwaonyesha kuwa wanaokamatwa ni vidagaa bado kwani kuna mapapa haswa!
 
Watanzania bwana!!! kwao hakuna zuri. Asingekamatwa halafu yakasikika mtaani kwamba ametoa rushwa, hapa zingetolewa lawama za kufa mtu kwamba PCCB haifanyi kazi au kazi yake inaifanya kwa upendeleo. Sasa amekamatwa, hoooo mbinu chafu.

Jamani waacheni PCCB wafanye kazi yao. Wewe mtu una bahasha 140 za khaki unataka za nini ilihali wewe siyo posta? Uzuri mwanakijiji katupa nakala ya sheria inayowabana hawa. Walizoea sana, naona mwaka huu wamepatikana. Let us get the real leaders we want na siyo viongozi wa kutuhonga kuku na pilau, halafu wakiingia madarakani wanafanya kazi ya kurudisha kile walichoiba.

Awe ni Sitta au ni Pinda au kikwete mkono wa sheria upo juu yake so far anatoa rushwa.
 
wanawanyima wananchi ulaji-ila vijijini hamana takukuru wala nini!! ndo mda wao wa kuvuna-acha wawape lkn wao c wanajua nani anawafaa?
 
Mkuu hii issue ya TAKUKURU kukamata wagombea wa CCM mwisho ni tarehe 31 mwezi huu. Baada ya hapo hutosikia mgombea yeyote wa CCM anakamatwa na TAKUKURU kwa kutoa rushwa kwa wapiga kura, kununua shahada au kulisha watu wali. Kwani kwa kufanya hivyo kutakuwa ni kukosesha CCM jimbo. Tegemea wapinzani wengi kukamatwa na TAKUKURU wakati wa kampeni hasa maeneo CCM inapokuwa hoi bin taaban. Believe me haya ni maandalizi ya kuukandamiza upinzani wakati wa kampeni za kuelekea october. MARK THIS POST!!!!

Kwa nini TAKUKURU wanafanya hivi?

1. Kuudanganya ulimwengu kuwa CCM inapiga vita rushwa.

2. Majungu yanayoendelea miongoni mwa wana - CCM wenyewe kwa wenyewe

3. Part of revenge ya Hosea baada ya kumshikia bango, Huwezi kumkamata mtu akiwa na keshi au bahasha halafu useme alikuwa anataka. Unatakiwa kumkamata wakati anatoa rushwa. Kama bahasha zake na hela ni zake halali kuna kosa gani?

Unajua nilisoma jama eti wamemkamata mkuu wa wilaya ya kasulu betty Machangu akiwa chumbani hotelini, swala la kujiuliza ni kwamba kuna kosa gani mtu kukodi chumba hotelini na kukaa na wapambe wake wawili?. Yaani TAKUKURU ni big mchemko na inaonesha wazi kuwa wameshindwa mbinu za kikachelo matokeo yake wanatumia mbinu za kivamizi sasa. Tushangilie haya yanatokea sasa kwa CCM wenyewe kwa wenyewe lakini tujiandae kulia sana pale tutakapoona wagombea wenye nguvu wa upinzani wapoondolewa uwanjani - Kumbuka ya Shitambala

Wakati wa kuwakemea TAKUKURU ni huu. Baadae watasema mbona wana CCM walipokuwa wakikamatwa mlikuwa kimya?
Hii vita dhidi ya rushwa haina shukrani! Mla rushwa anatetewa mchana kweupe, simply b'se ni mke wa Spika, kweli tuna safari ndefu!
 
mmeanza. wakiwakamata mnasema, wasipowakamata mnasema, wafanyaje sasa?

Mkuu huu ukamataji wa TAKUKURU Umekaa kisiasa zaidi ya kiusimamizi wa sheria. Hakuna evidence inayokusanywa ya kuweza kumfunga mtu kwa kosa. Jamaa hawa wanachofanya hapa ni "Uvuvuzela" wanapiga kelele tu. Ni kama vile mlevi anavyopita anaimba usiku au kufanya mazungumzo yeye mwenyewe kama vile wapo wengi kwa kubadilisha sauti ili kutisha wanyama na vibaka. Tokea nimeanza kusikia kukamatwa watu kwa rushwa sehemu zote zinasema alikuwa "anataka" Wewe una uwezo gani wa kuithibitishia mahakama nia ya mtu kiurahisi tu?. Kwa nini TAKUKURU wasitumie "covered electorate" na kupokea hizo rushwa ndiyo wakamate hao watuhumiwa?.

Huu ni mchezo mmbaya sana wa kutumia vyombo vya dola kwa masilahi ya kisiasa. Hapa hakuna kesi hata moja ya kumfunga mtu. Sasa basi kama TAKUKURU wanafanya hivi kwa CCM katika kutafuta wagombea, msitarajie itafanya hivi pindi wagombea watakapokuwa wameteuliwa kutetea majimbo. Ikifika hapo sasa CCM watakuja na uongo wa kusema walioteuliwa ni watu safi na TAKUKURU wataamliwa wabadili uwanja wa mapambano kuwavunja nguvu wapinzani wanaowatishia majimbo yao. MARK THIS POST!!!
 
Kamanda wa TAKUKURU Mkoa wa Kilimanjaro aliemkamata DC ahamishwa, ashushwa cheo.
Taarifa za uhakika zinasema kuwa kamanda wa TAKUKURU mkoa wa Kilimanjaro ambaye maafisa wake walimkamata Mkuu wa Wilaya ya Kasulu kwa tuhuma za kugawa rushwa hapo juzi, hivi leo amekabidhi barua ya kuhamishwa kituo chake cha kazi na kupelekwa mkoa mwingine lakini akiwa si kamanda tena bali afisa tuu wa kawaida. Hii inatosha kuashiria kwamba HOSEAH amebanwa na mkuu wa kaya kwamba kwanini anawazalilisha wateule wake wa kutoka chama tawala, HOSEAH kumbe hana ujanja, na huyo mama hata mchakato wa kumfikisha mahakamani umesimamishwa.

Kama unachoongea kimetokea basi ni dhahiri kuwa TAKUKURU inatumiwa kwa masilahi ya kisiasa zaidi miongoni mwa wagombea wa CCM. Hawajengi kesi bali wanavamia tu na kuanza kutangaza bila kuwa evidence ya kufungulia watu mashitaka. Huu ni uhuni!!!. Huwezi kumdhalilisha mtu kiasi hicho bila kufanya uchunguzi au kumshikisha mtu za moto.
 
jamani kama amekamatwa na vidhibitisho mbona mnaanza kuingilia kazi ya TAKURURU? mama Sitta na mumewe ni watu wawili tofauti! tunaomjua huyo mama si safi namna hiyo! Acheni TAKURURU ifanye kazi yake!
 
Watoa/wala Rushwa lazima washughulikiwe bila kujali ni nani, kama kuna uthibitisho Mke wa Spika katoa rushwa kwa nini asishughulikiwe, lakini kama ni mipango fulani fulani inafanywa, njia ya mwongo ni fupi. Lakini pia nina wasiwasi na ushabiki hapa JF kwamba kwa sababu labda mtu fulani ameonyesha/alionyesha ni mpiganaji huko nyuma basi hawezi kutoa Rushwa. kumbuka hata kwenye dini kuna manabii wa uongo na tutawatambua kwa matendo yao. na sasa umefika wakati tuwa tambue kwa matendo yao. kama ni wasafi sasa tutawajua vizuri zaidi maana sheria ya uchaguzi imekaa kisanii, na wao ndo wameipitisha. wacha wajichome wenyewe.
 
22. The following persons shall be deemed to commit
unconscionable funding within the meaning of this Act:
(a) every person who corruptly gives, or provides,
or pays, wholly or in part, the expense of giving
or providing food, drink, entertainment or
provisions to or for any person, for the purpose
of influencing
that person, or any other person,
to vote or to refrain from voting at such
nomination process or election;
Asipochomokea kwenye tundu la "corruptly gives" atatokea kwenye "for the purpose of influencing."

Umejuaje nime "corruptly give"? Thibitisha nia ya moyo wangu kutoa "for the purpose of influencing."
 
Ni bora sheria ichukue mkondo wake, hata misahafu inasema inabidi uchague kuwa wamoto au wabaridi, huezi kuwa katikati.
 
Takukuru wanafanya kazi yao ,ila kama wanasema wamemkamata akitaka kutoa basi ni utata walitakiwa wasubiri atoe,au wadau mnaonaje?
Maana hapa ni rahisi kusema anafanyiziwa kutokana na mumewe.
 
Lakini mbona wanaokamatwa na rushwa ni watu wa CCM tu?. Hii imekaaje vile?
 
Takukuru wanafanya kazi yao, ila kama wanasema wamemkamata akitaka kutoa basi ni utata walitakiwa wasubiri atoe, au wadau mnaonaje?
Maana hapa ni rahisi kusema anafanyiziwa kutokana na mumewe.

Hakuna anayesema PCCB wasifanye kazi, tatizo ni kwamba wanatekeleza kazi yao kwa kuangalia maslahi ya mtu/watu/kikundi cha siasa na siyo kwa kufuata sheria ya Gharama za Uchaguzi wa wagombea wote pasipo kuangalia uso.

Hoja nyingine ni kwamba, Yusuf Makamba, alitamka wazi kwamba wale wote ambao wameshikwa na tuhuma za rushwa, wanajifuta automatically kwenye mchakato, lakini baadhi ya makatibu wa CCM wilaya na mikoa wameruhusu watu hao washiriki uchaguzi wa viti maalum, waki-cite mfano wa kesi ya Mramba kwamba ameruhusiwa kugombea ingawa ana kesi mahakamani.

Kumbukeni CCM hawa hawa walikata majina ya Elisa Mollel na Lekule Laizer kwenye uchaguzi wa CCM 2007, kwa kosa la kukutwa wako bar wanakunywa pombe na kula nyama choma wakiwa na shilingi laki nne.

Kwa hiyo tutarajie maajabu kwamba wapo ambao wameshikwa wakitaka kutoa rushwa wataachwa na kupeta na wako ambao watakatwa. Ndiyo maana nilisema primaries za CCM mwaka huu ni usanii mtupu wa kudai wanaimarisha demokrasia lakini hakuna kitu bali ni juhudi zile zile za kuendeleza kukumbatia ufisadi ambao wameshindwa kuupiga vita.

Kwa kuwa wote wanateuliwa kwa kutoa rushwa, ikija hoja ya ufisadi hakuna atakayenyua mkono ama kufungua mdomo kupinga ufisadi, maana dhamira itakuwa inamshitaki.
 
Hii vita dhidi ya rushwa haina shukrani! Mla rushwa anatetewa mchana kweupe, simply b'se ni mke wa Spika, kweli tuna safari ndefu!

Mkuu hapa hatetewi mtu bali ni mfumo mzima wa kuendesha zoezi umekakaa kisiasa zaidi ya kisheria. TAKUKURU hawakusanyi ushahidi wa kuwapeleka hawa watu mahakamani matokeo yake wamekuwa wanavamia tu kupewa signal na washindania. Yaani wamekuwa katikati ya fitina za kisiasa miongoni mwa wagombea, jambo ambalo ni dhahiri litaendelea baada ya kumaliza mchakato huu wa ndani na kupambana na wapinzani. Maana zambi hii haitaishia miongoni mwa wana-CCM tu bali itakuwa ni mbinu ya kuwaondoa wapinzani makini na wenye nguvu kwa kuwavamia na kuwazushia. Nyie ngojeni tu si tupo
 
Back
Top Bottom