Taasisi ya kupambana na kuzuia rushwa{TAKUKURU} mkoani Arusha imewakamata watu wanne wanaodaiwa kwa ni wafuasi wa Chama Cha mapinduzi,CCM kwa tuhuma za kutoa rushwa kwa wajumbe wa mkutano wa jimbo la Arumeru
Mashariki Chama hicho kinarudia upigaji wa kura kutokana na uamuzi wa kamati kuu{CC} ya CCM kwa wagombea wawwili Sioi Sumari aliyepata kura 361 na Williamu Sarakikya alifanikiwa kupata kura 259.
Watu hao ambao inadaiwa kuwa ni wafuasi wa mmoja wa wagombea ubunge wa jimbo hilo wamekamatwa akiwemo katibu wa jumuiya ya vijana ya chama cha mapinduzi wilaya ya Monduli {UVCCM}Ezekiel Mollel.
Watuhumiwa hao inadaiwa kuwa waliwekwa ndani kwanza katika kituo cha polisi cha mji mdogo wa Usa river kabla ya kupelekwa makao makuu ya taasisi hiyo yaliyopo Jijini Arusha kwa mahojiano zaidi.
Kamanda wa Takukuru mkoani Arusha Mbengwa Kasomambuto amethibitisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao ambao ni wanachama wa UVCCM katika wilaya za Arumeru,Mondulu na Arusha.
Aidha taarifa za uchunguzi utoka Arumeru zimebaini kwamba vijana wawili wa UVCCM Arumeru na mmoja aliyewahi kuwa kiongozi wa jumuiya hiyo jijini Arusha walifanikiwa kutimua mbio na wanasakwa na Takukuru.
Mashariki Chama hicho kinarudia upigaji wa kura kutokana na uamuzi wa kamati kuu{CC} ya CCM kwa wagombea wawwili Sioi Sumari aliyepata kura 361 na Williamu Sarakikya alifanikiwa kupata kura 259.
Watu hao ambao inadaiwa kuwa ni wafuasi wa mmoja wa wagombea ubunge wa jimbo hilo wamekamatwa akiwemo katibu wa jumuiya ya vijana ya chama cha mapinduzi wilaya ya Monduli {UVCCM}Ezekiel Mollel.
Watuhumiwa hao inadaiwa kuwa waliwekwa ndani kwanza katika kituo cha polisi cha mji mdogo wa Usa river kabla ya kupelekwa makao makuu ya taasisi hiyo yaliyopo Jijini Arusha kwa mahojiano zaidi.
Kamanda wa Takukuru mkoani Arusha Mbengwa Kasomambuto amethibitisha kukamatwa kwa watuhumiwa hao ambao ni wanachama wa UVCCM katika wilaya za Arumeru,Mondulu na Arusha.
Aidha taarifa za uchunguzi utoka Arumeru zimebaini kwamba vijana wawili wa UVCCM Arumeru na mmoja aliyewahi kuwa kiongozi wa jumuiya hiyo jijini Arusha walifanikiwa kutimua mbio na wanasakwa na Takukuru.