VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
'Ziara' zangu ofisi za Serikali zinaelekea kubaya.Leo nilikuwa TAKUKURU ambapo mteja wangu mmoja anahojiwa akidaiwa kula rushwa ya shilingi laki tatu ili amwamishie mwanafunzi wake shuleni mwake.Nikawakuta maofisa wa TAKUKURU wametingwa na shughuli zao.Uchokonozi wangu ukaiponza.Nikamtwanga swali Afisa mmoja juu ya kuhojiwa na kupepelezwa kwa akina-MKULLO na TAKUKURU.
'Hao jamaa(Mkullo na wenzie) hawana tatizo lolote.Ni wasafi hadi tutakapopokea maelekezo mengine toka kwa wakuu wetu.Hadi sasa hatujaanza kuwapeleleza Waheshimiwa hao' alisema Afisa huyo. Wameanza taratibu za kuripoti kwao kila siku? nikamuuliza. 'Waripoti ili iweje? Wakuu hawajawapa amri hiyo.Mbona maswali yamekuwa mengi Wakili,unataka kuwatetea nini?' alisema akiniuliza swali la kichefuchefu Afisa huyo.
Nikatamani niingie Ofisi ya Mwalimu wangu(wakati ule pale UDSM),Dr.Edward Hossea,Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU hata nikapigane naye.Kiukweli,nikaogopa kesi.Hadi sasa,sijui nichukue hatua gani baada ya kukasirishwa na TAKUKURU...
'Hao jamaa(Mkullo na wenzie) hawana tatizo lolote.Ni wasafi hadi tutakapopokea maelekezo mengine toka kwa wakuu wetu.Hadi sasa hatujaanza kuwapeleleza Waheshimiwa hao' alisema Afisa huyo. Wameanza taratibu za kuripoti kwao kila siku? nikamuuliza. 'Waripoti ili iweje? Wakuu hawajawapa amri hiyo.Mbona maswali yamekuwa mengi Wakili,unataka kuwatetea nini?' alisema akiniuliza swali la kichefuchefu Afisa huyo.
Nikatamani niingie Ofisi ya Mwalimu wangu(wakati ule pale UDSM),Dr.Edward Hossea,Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU hata nikapigane naye.Kiukweli,nikaogopa kesi.Hadi sasa,sijui nichukue hatua gani baada ya kukasirishwa na TAKUKURU...