TAKUKURU, kuna kesi moja yenye ushahidi CHADEMA

acha uzabizabina ebu tueleze wewe na Slaa mulkutana wapi akakuamnia habari za mchange umeingia choo cha kike kamalizeni kwanza kujivua magamba ndio uje na uchuro wako sisi tunaendelea kujenga nchi yetu iliyowashinda ovyooooooooooo

soma tanzania daima la jumapili 29/5/2011 kabla hujakurupuka kuniita mzushi..
 
ninalo hilo gazeti TZ na halina habari hiyo wewe ni mwongo na mzushi labda useme umesoma maneno yaliyoandikwa hapa JF ambayo hakuna aliyeyathibitisha
 
Acha fitina kama mwana critical thinker huwezi kuandika upuuzi kama huu umetoka kwenye jamii ya magamba.
 
Hiki chama tumekipigania sana wana Arusha na wana Moshi, nyinyi si mnaendelea na sisiem yenu? Huyo mchange si anatoka pwani? Sasa pwani wapi na wapi na chadema? Tumegundua huyu ni Mamluki wa Kikwete wanaotoka mkoa mmoja. Yeye alisikia hata kuna mbunge viti maalum kutoka Pwani chadema? Aende ccm au agombee uongozi wa Madrasa huyo mchange kama anataka kuongoza, sio chadema chama cha mungu!
 
ninalo hilo gazeti TZ na halina habari hiyo wewe ni mwongo na mzushi labda useme umesoma maneno yaliyoandikwa hapa JF ambayo hakuna aliyeyathibitisha
soma heading"DR SLAA AJISALIMISHA"hadi mwisho inaendelea ukurasa wa pili..kwani unakuwa naharaka gani unaposoma gazeti
 
mkuu nimefuatilia post zako nimegundua wewe ni m2 wa kukurupuka na zimekaa kishebaki na hazina mshiko boya wewe jamaa kaonge ishu ya maana unakurupuka acha upumbavu
 
BARAZA la Vijana la Chadema (Bavicha), limepata viongozi wapya katika uchaguzi uliotawaliwa na mizengwe na vurugu zilizotishia usalama wa wapigakura.Habari zilizolifikia gazeti hili jana zilieleza kuwa, vurugu hizo zilichochewa na kitendo cha Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa kuonyesha visu alivyodai kuwa vilikamatwa na walinzi wa chama hicho jana asubuhi. Mbali na kuonyesha visu kadhaa, Dk Slaa alitangaza kuenguliwa kwa wagombea watatu wa nafasi ya uenyekiti; Bernard Saanane, Greyson Nyakarungu na Mtela Mwampamba kwa madai ya ukiukaji wa maadili.

Dk Slaa aliwaeleza wapigakura kuwa kamati ya ulinzi ya chama hicho pia ilibaini kuwapo kwa mabaunsa waliodaiwa kupandikizwa katika mkutano huo kwa lengo la kuuvuruga.Alisema watu hao waliletwa na baadhi ya wagombea wa nafasi za uongozi ambao kimsingi chama hicho kilikuwa kimebaini kuwa ni mamluki waliopandikizwa kwa lengo la kuvuruga uchaguzi huo. Kuhusu wagombea walioenguliwa, Dk Slaa alidai kuwa kuondolewa kwao kumetokana na kukiuka maadili.
 
Hiki chama tumekipigania sana wana Arusha na wana Moshi, nyinyi si mnaendelea na sisiem yenu? Huyo mchange si anatoka pwani? Sasa pwani wapi na wapi na chadema? Tumegundua huyu ni Mamluki wa Kikwete wanaotoka mkoa mmoja. Yeye alisikia hata kuna mbunge viti maalum kutoka Pwani chadema? Aende ccm au agombee uongozi wa Madrasa huyo mchange kama anataka kuongoza, sio chadema chama cha mungu!

Hapo mkiambiwa kuwa chama chenu ni cha wachaga mnakuja juu,hebu angalia upuuzi huo uliouandika hapo juu.
 
BARAZA la Vijana la Chadema (Bavicha), limepata viongozi wapya katika uchaguzi uliotawaliwa na mizengwe na vurugu zilizotishia usalama wa wapigakura.Habari zilizolifikia gazeti hili jana zilieleza kuwa, vurugu hizo zilichochewa na kitendo cha Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa kuonyesha visu alivyodai kuwa vilikamatwa na walinzi wa chama hicho jana asubuhi. Mbali na kuonyesha visu kadhaa, Dk Slaa alitangaza kuenguliwa kwa wagombea watatu wa nafasi ya uenyekiti; Bernard Saanane, Greyson Nyakarungu na Mtela Mwampamba kwa madai ya ukiukaji wa maadili.

Dk Slaa aliwaeleza wapigakura kuwa kamati ya ulinzi ya chama hicho pia ilibaini kuwapo kwa mabaunsa waliodaiwa kupandikizwa katika mkutano huo kwa lengo la kuuvuruga.Alisema watu hao waliletwa na baadhi ya wagombea wa nafasi za uongozi ambao kimsingi chama hicho kilikuwa kimebaini kuwa ni mamluki waliopandikizwa kwa lengo la kuvuruga uchaguzi huo. Kuhusu wagombea walioenguliwa, Dk Slaa alidai kuwa kuondolewa kwao kumetokana na kukiuka maadili.

Ngugu yangu nimefuatilia nimekufuatilia tangu jana na nimegundua kuwa unatuletea taarifa za ndani kabisa ya kilichokuwa kikiendelea katika vikao vya uchaguzi wa BAVICHA. Kwa mtazamo wangu ninakuona kama vile uko hasi katika yale uliyaona na kuyaeleza.

Ninaomba tu ufafanuzi kidogo juu ya hilo: Je, ni kweli kuwa ulikuwepo katika vikao /maeneo ya vikao hivyo?
 
Heche kuongoza Vijana Chadema
Imeandikwa na Lucy Lyatuu; Tarehe: 30th May 2011


JOHN Heche amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Taifa la Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Katika uchaguzi uliofanyika jijini Dar es Salaam, Heche amewabwaga wagombea wenzake sita waliokuwa wakiwania nafasi hiyo.

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk. Willibrod Slaa aliliambia gazeti hili jana kuwa wagombea wanne walienguliwa katika kinyang’anyiro hicho kutokana na kukosa maadili pamoja na rushwa, katika mkutano Mkuu wa Bavicha uliofanyika juzi.

Aliwataja walioenguliwa katika kinyanganyiro hicho kwa kampeni chafu, rushwa, kukosa maadili na uongo kuwa ni Grayson Nyakarundu, Bernard Saanane, Mtella Nampamba na Habib Mchange.

Dk. Slaa alisema Mchange alienguliwa na Kamati Kuu wakati wagombea wengine walienguliwa na Kamati ya Wazee baada ya kuagizwa na Kamati Kuu kuchukua hatua zozote zinazofaa dhidi ya wagombea wenye kutuhumiwa.

Alisema nafasi ya Mwenyekiti ilikuwa ikigombewa na Aidan Sadik, Bernard Mao, Saanane, Deogratias Kisandu, Edwin Soko, Nyakarungu, Mchange, Heche, Masood Suleiman na Mtela Mwampamba.

Kwa upande wa Makamu Mwenyekiti Bara, Dk. Slaa alisema ilichukuliwa na Juliana Shonza ambaye alikuwa akigombea pamoja na Emmanuel Somon, Gwakisa Mwakasendo, Joseph Patrick na Julieth Rushuli.

Dk. Slaa alisema kwa upande wa Zanzibar, alichaguliwa Sharifa Khamis na kuwabwaga Sharim Khamis, Zainab Bakari na Ally Akalipo Ally.

Alisema wagombea waliorudisha fomu kwa nafasi za Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Mratibu wa Uhamasishaji, Mweka Hazina watatangazwa katika ratiba ya baadaye.

Dk. Slaa alisema kwa nafasi ya Katibu Mkuu, Naibu Katibu Mkuu, Mratibu wa Uhamasishaji na Mweka Hazina, watapendekezwa na Kamati ya Utendaji ya Bavicha kwa mujibu wa ratiba itayopangwa baadaye na uteuzi wao utathibitishwa na Kamati Kuu ya chama, hivyo wataalikwa katika vikao vya baadaye.

Uchaguzi wa Bavicha ulikwama kufanyika mwaka jana kutokana na sababu mbalimbali na hivyo kuahirishwa hadi ulipofanyika Mei 28.
 
vijana wa jf kumbe na nyie mnatoa rushwa?
mtoto wa nyoka ni nyoka

mliotajwa hapo tuambieni imekuwaje tena.

hongera heche.
 
alisema mgombea mmoja bavicha kaenguliwa baada ya kutoa rushwa kwa m pesa na kunaushahd, sasa kwanini hakuwaita takukuru kuwakabdh mtu wao? narudia kusema cdm haipo salama na inachokikumba ccm sasa,bora ya ccm wameshapata uzoefu,cdm ikifikwa itakufa tu
kumbe ilitakukuru wafanye kazi inabidi waitwe...basi kazi ipo wasipoitwa wanakaa tu ofcn,hii serikali inaenda wapi,juzi rober manumba na yeye anataka wananchi wenye ushahidi wa kagoda waupeleke wakati yeye katulia ofn kusubiri ushahidi..kweli kazi ipo
 
Hiki chama tumekipigania sana wana Arusha na wana Moshi, nyinyi si mnaendelea na sisiem yenu? Huyo mchange si anatoka pwani? Sasa pwani wapi na wapi na chadema? Tumegundua huyu ni Mamluki wa Kikwete wanaotoka mkoa mmoja. Yeye alisikia hata kuna mbunge viti maalum kutoka Pwani chadema? Aende ccm au agombee uongozi wa Madrasa huyo mchange kama anataka kuongoza, sio chadema chama cha mungu!

ukisema Arusha na Moshi tu unakua unakosea.ni ubaguzi.
 
Ni nani Takukuru mwenye nia na uthubutu wa kumshika Mchange. Kama yupo na akamhoji maana Takukuru nayo ni chafu
 
Hongera Heche, Hongera Dr. Slaa kwa kusimamia unachoamini kwa haki.
 
Unategwa halafu unaingia kichwa kichwa, au una ID mbili? unapost na kujijibu mwenyewe?

ID yangu ni moja tu, na kama ulichemsha kusema kuwa Pwani na Chadema wapi na wapi basi ni bora ukiri tu kuwa umechemsha la sivyo ni yaleyale kuruka mkojo kukanyaga mavi.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom