Taifa Tanzania lapinga sababu 51 za Kikwete kutogombea 2010!

Sumaku

Member
Feb 17, 2009
53
1
Wadau, mchomeko wa mada nyingine kwenye Taifa Tanzania inayohitaji kujadiliwa.

TUNAMJIBU M.M. MWANAKIJIJI:

Sababu 102 kwa nini Jakaya Kikwete agombee 2010 na aendelee kuongoza

MWANDISHI WETU


Wana CCM milioni 4 (kasoro Nungayembe wa kisiasa) na wapiga kura kwa mamilioni, wanatambua uongozi wa Rais Jakaya Kikwete. Hao waliopiga kura katika Uchaguzi Mkuu 2005, pamoja na wapiga kura wapya tuna hakika, hawajaona au hawategemei kuona mbadala kwa nafasi ambayo Kikwete anayoishikilia. Kwa nini tunaona hivyo?

Hali iliyopo kwa watu wanaofanya shughuli zao za kuzalisha mali na katika kujenga taifa inaridhisha tofauti na ramli za kutabiri mwisho wa dunia ya Tanzania yenye amani zinazopigwa na baadhi ya vyombo vya habari.

Kuna kundi dogo la watu ambao wana nongwa ya kuukosa Urais 2005 na wengine ambao hawana uwezo wa kuchambua matukio, michakato na mienendo ya kisiasa na kijamii wanaendeshwa na kuamini katika hisia zao, ambazo zinawatuma kuandika vitu vya kubuni na alnacha.

Walipofanikiwa kumg’oa Edward Lowassa hawakuridhika. Wamekuwa wakijidanganya kwamba wanaweza kutimiza ndoto yao ya kumng’oa na Kikwete na kuzika kizazi hicho cha uongozi. Katika Gazeti la Mwanahalisi, toleo Na. 167 Jumatano Desemba 16-22, 2009 makala ya M.M. Mwanakijiji (sababu 51 za kumkwamisha Kikwete) mwandishi anaonyesha alivyokosa cha kuandika, akalazimisha hoja na sababu kwa nini Rais Kikwete asigombee nafasi ya Urais mwaka 2010.

Kwanza kabisa hakuna mwanachama ndani ya CCM anayeweza kutaka kugombea na akawa tishio kwa Rais Kikwete. Kikwete alishapitia tanuru la moto mwaka 1995 na 2005.

Hakuna watu wenye nguvu na uwezo wa kila hali ambao wanaweza kujitokeza sasa kuliko wale ambao aliishashindana nao huko nyuma. Majina ya akina John Samwel Malecela, Frederick Sumaye, Profesa Mark Mwandosya, Cleopa Msuya, Benjamen Mkapa, Jaji mstaafu Mark Bomani, Salim Ahmed Salim na mengineyo ni majina makubwa. Alishindana nao na akawashinda.

Kikwete kugombea Urais siyo kwa maslahi ya wapambe, kuna mambo makubwa zaidi ya wapambe ambayo yanamfanya mtu agombee nafasi kuu ya Urais. Tamaa ya mtu katika nafsi yake kutaka kugombea uongozi ni kwamba ana uwezo fulani na anataka atekeleze mambo fulani nje ya nafsi yake. Wako watu wengi katika uwanja wa siasa ambao hawafikii hatua hiyo.

Ukweli wa mambo ni kwamba tangu achukue madaraka 2005, mambo mengi yamekuwa yanafanyika hapa nchini. Miradi imekuwa inatekelezwa na serikali watu katika sekta binafsi, mashirika makubwa ya kimataifa na mashirika ya kidini. Kusema kwamba wanaotaka Kikwete agombee ni wale ambao wanakariri kikasuku msemo wa “kuendeleza umoja, utulivu, amani na mshikamano” wa nchi yetu, ni fikra za mtu ambaye akili yake imedumaa na kukwama kutokana na kutotaka kujifunza mabadiliko yanavyotokea katika mazingira na nani analeta mabadiliko hayo.

Kwa upande mwingine dhana ya utulivu wa kisiasa (political stability) imepitwa na wakati. Wanataaluma na watunga sera, sasa hivi wanazungumzia utulivu utokanao na mkusanyiko wa sababu mbalimbali za maendeleo katika sekta za uchumi na ustawi wa jamii (structural stability). Kwamba watu hawali maneno matupu na nadharia za siasa.

Utulivu kimfumo una nafasi kubwa kutokana na sekta mbalimbali kutegemeana ili kuleta maendeleo yenye ulinganifu, hivyo ni wazi kwamba sera zote zinazotungwa na miradi inayotekelezwa inakuwa imepangwa kimtambuka kiasi kwamba yanayotokea sekta moja yanaathiri maendeleo yatakavyokuwa katika sekta nyingine.

Kwa namna moja au nyingine watanzania walio wengi katika sekta mbalimbali wanaguswa na kufikiwa na miradi ya maendeleo ya kubadilisha maisha yao . Yawezekana kwamba kasi ya maendeleo inazidiana. Lakini kwa namna moja au nyingine kuna mabadiliko ya msingi kule wanapoishi watu.

Watu wasioelewa hali inavyobadilika wanakuwa wa kwanza kupiga mayowe jinsi serikali ilivyoshindwa kuwaletea watu maendeleo, bila kutambua ukweli wa mambo kwamba watu wenyewe ndiyo watajiletea maendeleo na kazi hiyo ndiyo wameshaianza. Kwa waandishi wapiga ramli, kwa sababu wanataka kuonyesha msimamo wao wa “kupinga kila kisemwacho au kufanywa na hasimu wao”, wanakuwa na watu wao ambao wanawaumba na kuwatengenezea mazingira.

Wanapoanzia siyo kuonyesha uwezo wa kiongozi wao wa kufikirika bali ni kubuni na kuzua mambo, na kujaribu kugeuza mkondo wa maji utoke ziwani na kupanda mlima. Kwa hili la Kikwete kugombea 2010 tunasema binadamu ana uwezo mkubwa, lakini hawezi kuzuia jua kuchwa!

Katika jamii inayokua kwa misingi ya kidemokrasi wapiga kura na raia kwa ujumla wana nafasi yao katika mchakato wa siasa, uchumi na maendeleo ya jamii. Nchi inaweza ikawa katika matatizo makubwa ya kiuchumi lakini hakuna matukio ya uvunjivu wa sheria wa makusudi kutoka kwa watu wengi. Tanzania ilipitia vipindi vigumu ambapo uchumi wa nchi ulikuwa mbaya. Hakuna fujo zilizotokea ambao zilitishia usalama wa watu na mali zao.
Kuna sababu 102 ambazo tunaona kwa nini Rais Kikwete agombee Urais 2010. Tutazitolea maelezo machache baadhi ya sababu kila panapokuwa haja.

Tunaanza na sababu 3:

Rais Kikwete amekuwa mstari wa mbele wa kutaka kuwepo utawala wa sheria. Utawala wa sheria ndiyo msigi mkuu wa utawala wa kidemokrasia, Tanzania ni nchi mojawapo miongoni mwa nchi changa kuwa na asasi zenye mamlaka zinazofanya kazi kwa uhuru kamili.

Hivi sasa ni wazi kwamba nchini Tanzania hakuna mtu anayekuwa juu ya sheria; awe ni raia wa kawaida, kiongozi mkuu serikalini au watendaji wakuu waandamizi. Matukio ya kutaka sheria ichukue mkondo, yako wazi na sasa tunaweza kusema sheria inatawala na watu wanaongoza. Tanzania haitumii utawala kwa sheria.

Rais Kikwete anajali mgawanyo wa madaraka kati ya mihimili mikuu mitatu

Sasa hivi mgawanyo wa madaraka kati ya utawala wa dola, mabaraza ya utungaji sheria na Mahakama uko wazi. Kila mhimili una eneo lake na mipaka yake utawala wa dola unafanya kazi ya utendaji katika mfumo wa dola. Utumishi wa umma, majeshi ya ulinzi na usalama na srikali za mitaa zote ni asasi za mamlaka. Uhuru wa Mahakama ni jambo lisilo la kubishaniwa. Tangu miaka ya 1960 bunge la Tanzania limekuwa linajaribu kuwa muhimili usiothibitiwa. Sasa hivi hilo limewezekana kutokana na Rais Kikwete kujali na kutaka kila mhimili uwe huru kufanya mambo yake na yote kwa maslahi ya taifa.

Rais Kikwete anajali na kutambua ulazima wa utawala bora kwa maendeleo ya taifa Utawala bora ni dhana mpya ambayo imebuniwa katika jitihada za dola kukabiliana na hali mpya inayotokana na matakwa mapya kadri mazingira ndani na nje ya jamii yanavyokuwa na matatizo mengi ya kijamii na kiuchumi. Utawala bora una maana ya ushirikishwaji wa wadau na dola kuwa chombo cha kuelekeza matumizi ya raslimali. Na hivyo utawala (bora) ni pamoja na njia zilizo bora za kudhibiti na kuratibu shughuli zinazolenga kuwapa watu uhuru zaidi na uwezo wa kuthibiti mazingira.

Rais Kikwete anathamini mashauriano kati ya wadau juu ya utungaji sera Rais Kikwete anajali usawa wa kijinsia.

Ametunza lengo la kuendeleza sera za kuvutia wawekezaji

Amekubali ushauri wa kufanya mabadiliko katika sera na sheria za madini (kuleta ulinganifu)

Ni kiongozi anayekubali ushauri katika miswada ya serikali inayopelekwa bungeni

Ni kiongozi mwenye kuwa na ubunifu katika utungaji sera za maendeleo mfano mzuri ukiwa ni sera ya Kilimo Kwanza.


Source: TAIFA Tanzania , Desemba 18, 2009
( Mambo yamepamba moto. Nyingine hii nimeinasa kutoka mtandao wa kwanzajamii.com)
 
Mwanakjj mnampaisha kinyama, lakini mnasahau kuwa ile thread alisherehesha tu Mkjj kisha wadau wengine wakaweka sumu zao, sasa kumpa credit Mkjj ni kupuuza juhudi za wengine walioweka, I mean tulioweka input zetu kule kwenye ile thread..

Ushauri: Acheni kukimbiza upepo. Hoja hujibiwa kwa hoja na sio hivi vioja mlivyoandika. You silly rebuttals are simply idiotic.
 
Kwanza ni nani hawa waliojibu?..Maana sidhani kama ni hao watu milioni 4
wanaosema.

Mwanakijiji, I await a rebuttal. Yangu macho tu.
 
Sijaona hiyo article ya Mwanakijiji kwa hivo nitaongea kutokana na kilicholetwa katika hii reply.

Kikwete mwenyewe amesema kwamba 70% ya Watanzania ni bendera kufuata upepo, huyu ndiye rais anayeshabikiwa?

Labda amesema kweli, maana wangekuwa si bendera kufuata upepo wasingemchagua yeye.Hapa kuna hao bendera kufuata upepo na wale wanaolinda/ kutafuta maslahi binafsi kwa kujikomba kwa wakubwa, style iliyowatoa kina Kikwete na Makamba.

Mwandishi anamsifia Kikwete kwamba amepitia tanuru la moto kwa kushindanishwa na magwiji kama vile Tanzania tuna system ya meritocracy na Kikwete kashinda on the merit (merit gani?).Tunajua Tanzania uongozi wa juu haufuati meritocracy, bali kuna Machiavellianism tupu na Kikwete was simply the best courtesant at stabbing his opposition in the back with a dagger and better at obtaining illegal funding.

Ndiyo maana nikasema rais ajaye atakuwa mbaya kuliko Kikwete kwa sababu system yetu haijakaa kum reward mtu mwenye uwezo na track record (meritocracy) ila the best deceiver kama Kikwete.
 
Huyu wandishi sijui kalamba ngapi mpaka akaja na haya majibu.....!!! No wonder tulishaambiwa only, I repeat only 15 % ndiyo wanajuwa walifanyalo 70 % ni wafuata upepo!!!!!!!!!!!
 
Hoja ni kikwete asigombee au asichaguliwe? Hakuna mtu mwenye mamlaka ya kumzuia mtu mwingine kugombea nafasi ya uongozi isipokuwa tu mtu huyu hana sifa za kikatiba. Sasa kugombea au kutogombea kwa Kikwete kunatuhusu nini sisi?

Sababu 51 za kikwete kutochaguliwa nakubaliana nazo. Wenye uwezo wa kumkataa mtu ni wananchi na sio makala ya mtu mmoja au watu kadhaa na wanaojibizana kama hawa Taifa Tanzania
 
Tatizo watu wanaangalia kukubalika na si uwezo.
Anaweza kukubalika lakini bado grade yake ni kwa ajili ya tea party tu kama alivyosema baba wa taifa.
 
"Kwa namna moja au nyingine watanzania walio wengi katika sekta mbalimbali wanaguswa na kufikiwa na miradi ya maendeleo ya kubadilisha maisha yao . Yawezekana kwamba kasi ya maendeleo inazidiana. Lakini kwa namna moja au nyingine kuna mabadiliko ya msingi kule wanapoishi watu. Watu wasioelewa hali inavyobadilika wanakuwa wa kwanza kupiga mayowe jinsi serikali ilivyoshindwa kuwaletea watu maendeleo, bila kutambua ukweli wa mambo kwamba watu wenyewe ndiyo watajiletea maendeleo na kazi hiyo ndiyo wameshaianza."

Kwa nini kuwepo serikali inayokusanya kodi?

Swala siyo tofauti ya maendeleo kati ya mtu na mtu hii ni dhana ya kifisadi kwa sababu fursa ya maendeleo inategemea fursa ya rasilimali ya taifa. Hili ndilo tatizo la Kikwete na kundi lake la Wanamandao kutumia fursa ya rasilimali ya taifa kuingia madarakani. Miaka minne sasa anajitahidi kuzima jitihada za wanamtandao wenzake waliokwapua kumwingiza madarakani.

Hakuna Sera ya Kilimo Kwanza. Taswira ya TANU/CCM ni chama cha wakulima na wafanyakazi, iweje sera ya kilimo ije 2009? Baada ya miaka 48 kama siyo kupenyeza ajenda kuondoa mjadala unaoendelea wa uadilifu wa watawala wetu. Vyombo vyote vya dola kwa sasa vina bei yakununulika na wenye pesa sio taratibu na kanuni za utendaji. Dhana ya utawala bora inapigiwa debe na kuimbwa kwa sababu hakuna utawala bora ila bora utawala. Ungekuwepo hata kufikiria utawala bora tu kusingekuwepo.

Mimi nina sababu 204 ya kutomtaka kikwete kugombea hata kenye serikali ya kijiji.
 
Hawa wanajikomba komba kama Mzee wa Kilalacha wanafikiria watapewa ukuu wa wilaya
 
"Babu yangu aliwahi kunisimulia hadithi ya Chura ambaye alikwenda kingoni mwa mto baada ya misele yake kadhaa nchi kavu, ili aweze kuvuka kwenda upande wa pili.Alipofika pale ukingoni alikutana na scorpion aliyekuwa ameduwaa baada ya kushindwa kuvuka mto.Scorpion baada ya kumuona chura alimsihi ambebe mgongoni ili aweze kumsaidia kuvuka.

Chura, alikataa kwa mantiki kwamba scorpion atamshindilia ule mkia wake wenye sumu kama akimruhusu apande mgongoni.

Scorpion yule alikataa katakata asingeweza kufanya vile na kwa ujasiri mkubwa alimshawishi chura kwamba akifanya hivyo basi wote watakutwa na mauti maana yeye hajui kuogelea.

Chura akaridhika na maneno ya scorpion na akawa tayari kumpandisha juu ya mgongo wake na kuanza safari ya kuvuka mto.

Alipofika katikati ya mto yule scorpion alimuuma chura na kwa ukali wa sumu yake chura akaanza kuweweseka akilia kwa uchungu kwanini scorpion umefanya kitu ambacho uliahidi kutofanya na sasa kimetuletea sisi sote mauti? Scorpion alichomjibu kilikuwa kidogo tu...kwamba samahani chura najua tunakufa maana umeanza kuzama. Lakini nimekuuma kwasababu siwezi kuacha asili yangu.Ule mkao wa mgongo wako umenitia mshawasha nijaribu kuitumbukiza sumu yangu ndani ya ngozi yako"

Babu yangu yule alinisimulia hadithi ile akinikumbusha balaa ya kuishi huku nimeamua kwa makusudi kuudharau ukweli.

Ndugu mtoa thread, ukweli tu ndo utatuweka huru.Sio longolongo au ajenda zenye nia ya kutimiza malengo binafsi bila kujari wengi watapata nini.

Ni makosa kukubali kitu ambacho kiko dhahiri kuwa kina kasoro eti kwasababu ya guarantee ambazo sio guarantee katika standard yoyote ile.Kudharau ukweli kuna price inayolipiwa na tukiendelea kwamtindo huo, yatatupata yale yaliyompata chura kwa kuamua kudharau ukweli aliokuwa anaufahamu fika, kwamba yule scorpion angempa tu ile kitu yake tu mara baada ya kupata mgongoni maana ndio asili yake.

Kazi kweli kweli
 
Tanzania is no longer an ideological society it is a realistic society! hiyo data ya jk kushinda kishindo was it real au ni ya wizi kutokana na pesa za EPA? If that it is tru kwa utendaji wake can you please mention hata barabara moja yenye km 10 ambayo imejengwa kwa kiwango cha lami ambayo haikuwepo kwenye mpango kazi katika utawala uliopita/

ninyi vibaraka wa Makamba na Rostam, acheni uongo, semeni kweli!!!!!!
 
"Kwa namna moja au nyingine watanzania walio wengi katika sekta mbalimbali wanaguswa na kufikiwa na miradi ya maendeleo ya kubadilisha maisha yao . Yawezekana kwamba kasi ya maendeleo inazidiana. Lakini kwa namna moja au nyingine kuna mabadiliko ya msingi kule wanapoishi watu. Watu wasioelewa hali inavyobadilika wanakuwa wa kwanza kupiga mayowe jinsi serikali ilivyoshindwa kuwaletea watu maendeleo, bila kutambua ukweli wa mambo kwamba watu wenyewe ndiyo watajiletea maendeleo na kazi hiyo ndiyo wameshaianza."

Kwa nini kuwepo serikali inayokusanya kodi?

Swala siyo tofauti ya maendeleo kati ya mtu na mtu hii ni dhana ya kifisadi kwa sababu fursa ya maendeleo inategemea fursa ya rasilimali ya taifa. Hili ndilo tatizo la Kikwete na kundi lake la Wanamandao kutumia fursa ya rasilimali ya taifa kuingia madarakani. Miaka minne sasa anajitahidi kuzima jitihada za wanamtandao wenzake waliokwapua kumwingiza madarakani.

Hakuna Sera ya Kilimo Kwanza. Taswira ya TANU/CCM ni chama cha wakulima na wafanyakazi, iweje sera ya kilimo ije 2009? Baada ya miaka 48 kama siyo kupenyeza ajenda kuondoa mjadala unaoendelea wa uadilifu wa watawala wetu. Vyombo vyote vya dola kwa sasa vina bei yakununulika na wenye pesa sio taratibu na kanuni za utendaji. Dhana ya utawala bora inapigiwa debe na kuimbwa kwa sababu hakuna utawala bora ila bora utawala. Ungekuwepo hata kufikiria utawala bora tu kusingekuwepo.

Mimi nina sababu 204 ya kutomtaka kikwete kugombea hata kenye serikali ya kijiji.

Mwenzio alianzia huko akapanda mpaka hapo alipo. Hujui kuwa Mwinyi alimtoa kwenye U-District Party secritary Masisi na kumpa Unaibu waziri?? Sasa leo ukisema arudi alikotoka sijui una maana gani?? Kama meli imemshinda basi tutafute nahodha mwingine!!
 
mmm, mwanakijiji anatumiwa na wataka uraisi 2010 au nae ni mmojawapo. umelonga mkuu.
 
Majibu na kauli nyingi za viongozi wa CCM na hao wanaojiita wana CCM mwanzoni zilikua zinatia kichefuchefu lakini sasa zinakua vichekesho Kama kauli za Kinara mkuu wa Chama Makamba na viongozi wa juu wa chama akiwemo JK zinapingana ni upupu mtu iweje Sababu 102 zitaje walau 3!!!!!!! hawa.MUNU IBARIKI TANZANIA
 
(
Rais Kikwete anajali mgawanyo wa madaraka kati ya mihimili mikuu mitatu

Sasa hivi mgawanyo wa madaraka kati ya utawala wa dola, mabaraza ya utungaji sheria na Mahakama uko wazi. Kila mhimili una eneo lake na mipaka yake utawala wa dola unafanya kazi ya utendaji katika mfumo wa dola. Utumishi wa umma, majeshi ya ulinzi na usalama na srikali za mitaa zote ni asasi za mamlaka. Uhuru wa Mahakama ni jambo lisilo la kubishaniwa. Tangu miaka ya 1960 bunge la Tanzania limekuwa linajaribu kuwa muhimili usiothibitiwa. Sasa hivi hilo limewezekana kutokana na Rais Kikwete kujali na kutaka kila mhimili uwe huru kufanya mambo yake na yote kwa maslahi ya taifa.
Mhimili upi huo?

Mhimili unaotishwa na Chama?
Mhimili ambao mapendekezo yake yanabezwa na Serikali na wenyewe umenywea kama Mbwa Koko anayeona Chatu?
Mhimili ambao baadhi ya Watendaji kazi wake ni waajiriwa wa Serikali?

Au mhimili gani anaouzungumzia
 
Mwenzio alianzia huko akapanda mpaka hapo alipo. Hujui kuwa Mwinyi alimtoa kwenye U-District Party secritary Masisi na kumpa Unaibu waziri?? Sasa leo ukisema arudi alikotoka sijui una maana gani?? Kama meli imemshinda basi tutafute nahodha mwingine!!

Unajaribu kusema nini? Kwamba Kikwete anafaa kwa sababu kapanda ngazi kutoka chini?

Umeona nilivyoeleza mwanzo kwamba Tanzania uongozi si lazima uendane na uwezo?

Ikiwa Mwinyi mwenyewe aliyemteua Kikwete ni failure aliyejiuzulu, na akarudi tena kwenye system na kupanda ngazi mpaka urais (mtu alishajiuzulu kwa uzembe) unategemea nchi hii kupanda ngazi kuwe na maana ya kwamba kunatokana na utendaji mzuri?

Katika hili tusidanganyane.
 
Unajaribu kusema nini? Kwamba Kikwete anafaa kwa sababu kapanda ngazi kutoka chini?

Umeona nilivyoeleza mwanzo kwamba Tanzania uongozi si lazima uendane na uwezo?

Ikiwa Mwinyi mwenyewe aliyemteua Kikwete ni failure aliyejiuzulu, na akarudi tena kwenye system na kupanda ngazi mpaka urais (mtu alishajiuzulu kwa uzembe) unategemea nchi hii kupanda ngazi kuwe na maana ya kwamba kunatokana na utendaji mzuri?

Katika hili tusidanganyane.
hapa umemnyamazisha kijana!AMEELEWA SOMO HUYO
 
Back
Top Bottom