Taifa stars na Brazil aliyecross uwanjani police walimpeleka wapi?

arasululu

Senior Member
May 13, 2010
135
1
Big thinkers naomba kuuliza swali! wakati mechi ya brazil na sisi ikiwa ndo imewiva kuna jamaa alikatiza uwanjani katikati na police wakawa wamemng'ang'ania! najiuliza hv! je wakati jamaa anazama ndani hao police walikuwa wp? na je! angekuwa na silaa kaka angepona? embu nisaidieni maana kwenye bilioni 3 moja kati ya sababu zilizotolewa ni usalama kuimarisha !!! ila pamoja na hayo yote namsifu yule jamaa kuingia uwanjani na jezz yake ya misri!!
 
tanzania tunajua maana ya neno usalama? hapa nakwambia tushasemwa na magazeti ya brazil kuwa walipofika airport mpaka police walowekkwa kuwapa ulinzi walikuwa wakiwapiga picha! huh
 
Kwani Tanzania kuna vyombo vya usalama basi?
Maaskari wetu ni wale mabwege darasani, waliokuwa wanakuwa wa mwisho na kufeli kila mtihani.
Ulinzi unataka watu walio na akili, sio mazembweta
 
Maaskari wetu ni wale mabwege darasani, waliokuwa wanakuwa wa mwisho na kufeli kila mtihani. Ulinzi unataka watu walio na akili, sio mazembweta

Huko mbali na ukweli kabisa.... ndo maana wao ukisha kamatwa huwa wana conlude kuwa tayari una makosa na wanakuhukumu... kinachofuata ni kujustify tu hukumu yao... hakuna kutaka kufikiri sana, maana hawawezi....:angry:
 
Police wa bongo huwa bize kuwatch mpira so jana jamaa walikuwa wanashangaa samba boyz na hapo jamaa kiulaini akapata nafasi ya kuingia uwanjani, mi nilishamuaona askari akishangilia kirungu juu na mapaka kofia ikadondoka siku simba walipofunga goli la nne dhidi ya yanga pale taifa, tusiwalaumu upenzi wa mapira ni hisia ya mtu na ni ngumu kuidhibiti.
 
:A S tongue: But we need to take measure about this security issues. Mpaka siku muungwana apigwe kichwa ndio labda watabadilisha mfumo. Frankly speaking just look at the internal security hierarchy those on top are mhhh Minister tunapiga nae gambe na offer anatupa, Mwema mhh I think he doesnt suit to be the IGP he is soft and politician, Kova duh hapa ndio hamna kitu cause he keep on threating without actual act on issues. Hawa wa chini ndio kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa:roll:
 
HAPANA BWANA,c upenzi wa mpira bali ni uchache wa uelewa walionao polisi wetu labda darasa nalo linachangia but ah wapi pengine hawajui wafanyayo ni makosa. kama ni mapenzi na mpira mbona polisi haohao huwapiga wapinzani wanapokuwa kwenye mikutano yao na wala hata ckumoja hutosikia wamewapiga wafuasi wa chama tawala? inamana hawana mapenzi na siasa pia ? nahisi reasoning yao ndogo coz kaz yao ni USALAMA WA RAIA NA MALI ZAO HIVYO MAPENZI YANAPASWA YAWEKWE PEMENI HAPA.
Cha muhimu hapa ni kuwawajibisha wale polisi walokuwa uwanjani coz hili si suala la kulichekea, hebu fikiria kama jamaa angekuwa na BOMU? SILAHA?
Mara nyingi mashabiki huwasha mishumaa,makaratas et kushangilia huku HUYO TUNAYEMWITA POLISI AKIWA KARIBUNAO AKIWAANGALIA.
Sasa kama hatuwez kujilinda ama mapolisi wetu ni wazembe kwa kiasi hiki bas NA tubinafsishe haka ka jeshi coz si tumezoez kuwa wazungu ndo wapo smart ktk kazi na sio cc? kama tilivyofanya viwandavyetu! AISEE ANASIKITISHAA!!
 
Bosi wao ni Mhe. Laurent Masha. Mnamjua vema, mnategemea nini kwa wafanyakazi walio chini ya wizara yake?:mad:
 
Ni kweli lazima kuongeza nguvu kwenye ulinzi - police wetu wanacheki game badala ya kucheki watu kama wenzetu wa nchi zilizoendelea. Lakini pia kumbukeni mambo kama haya huwa part of the game ukizingatia Brazil ni mabigwa wa dunia na wanaongoza FIFA ranking kucheza na sisi so mizuka kwa washabiki inakuwapo, Je mnakumbuka jamaa yule alivyokatiza katikati ya uwanja siku ya fainali ya UEFA kati ya Arsenal na Barca ? jamaa alikatiza na kumkimbilia Thiery Henry wakati huo akichezea arsenal na Kumpa Jezi ya Barca. nafikiri dogo huyu apigwe faini tu dogo wa watu wasichukulie kesi hii ya ajabu wataharibu dhana nzima ya mpira....na wakumbuke FIFA watafuatilia adhabu hii sababu imetokea wakati wa game.

Napendekeza dogo ashitakiwa katika mahakama ya michezo na si hii ya jinai..... anyway mi si mwanasheria, wadau tuwekeni sawa kwa hili
 
Tatizo ni kuwa polisi nao wanaangali mechi badala ya kuangalia mashabiki. Yule jamaa hakuwa na jezi ya Brasil, unayemsema wewe ni Asst refree

KAKABRAZILNAJAMAA.JPG
 
Ni kweli lazima kuongeza nguvu kwenye ulinzi - police wetu wanacheki game badala ya kucheki watu kama wenzetu wa nchi zilizoendelea. Lakini pia kumbukeni mambo kama haya huwa part of the game ukizingatia Brazil ni mabigwa wa dunia na wanaongoza FIFA ranking kucheza na sisi so mizuka kwa washabiki inakuwapo, Je mnakumbuka jamaa yule alivyokatiza katikati ya uwanja siku ya fainali ya UEFA kati ya Arsenal na Barca ? jamaa alikatiza na kumkimbilia Thiery Henry wakati huo akichezea arsenal na Kumpa Jezi ya Barca. nafikiri dogo huyu apigwe faini tu dogo wa watu wasichukulie kesi hii ya ajabu wataharibu dhana nzima ya mpira....na wakumbuke FIFA watafuatilia adhabu hii sababu imetokea wakati wa game.

Napendekeza dogo ashitakiwa katika mahakama ya michezo na si hii ya jinai..... anyway mi si mwanasheria, wadau tuwekeni sawa kwa hili

Unachokisema ni kweli mkuu na tungependa kweli kama watamuhukumu wamuhukumu kimichezo na sio hizi mahakama zetu za jinai maana huko wataka kuoshea ful ful maana twawajua hao jamaaa na isngelikuwa watu kupiga makerere wange mfanyizia pale pale kwani hakuwa na hata siraha yeyote na alijisalimisha mwenyewe. ndio twakubali ndio part ya mchezo lazima kuwe na chakuongelea katika soka jamani, wamtende haki ipasavyo maana hao FIFA wasije wakatushangaaa jamani
 
Mi naona Jeshi la police wameachwa wajitafutie vipato vyao kupitia kutoza madreva michango ya sh 2,000 hadi 5,000 ili waweze ku-survive. Nchi yetu haijawapa umuhimu wa wao kujifunza mbinu za kulinda raia. Wakisha pigwa kwata na kupewa magwanda, wanadhani wamemaliza. Ukitaka kujua wanajua kuchukua fedha za madreva, hebu endesha gari la pick-up, pakia kama mbao mbili harafu endesha kuelekea Bagamoyo. Kwenye daraja la Bunju kabla ya Shule ya sekondari ya Bao bao, utajua kuwa hawa si askari wa usalama,bali ni VIBAKA.
 
Namsubiria kwa hamu Kamanda wetu wa kandaa maalum atuhabarishe maandalizi ya siku 2 ya security uwanjani ndio hayo??? hahahahha kazi kwelikweli
 
KAKABRAZILNAJAMAA.JPG


Mshkaji yuko juu kumkumbatia kaka live bila chenga.... potelea pote hata kama atapigwa virungu but keshankumbatia nia yake imetimia na ameingia uwanjani akionyesha vidole juu ishara ya amani hakutaka kumdhuru mtu
 
askari anatakiwa uso wake muda wote uwe kwa watazamaji: Upande wa pili wa shilingi, matukio ya kuingia uwanjani ni ya kawaida kutokea ulimwenguni kote. Tena tunabahati jamaa hakukimbia akiwa amevaa birthday suit!

photo_1262543235130-1-0.jpg
 
pamoja na mapungufu ya polisi wetu lakini kwa hilo la jamaa
kukatiza uwanjani sio kitu cha ajabu sana kutokea kwenye viwanja
vya michezo kwani hata huko majuu wasela huwa wanakatiza
uwanjani tena wengine wakiwa watupu a.k.a bila nguo kabisa
 
nilickia pia jamaa yupo ndani lakini bado anayofuraha ya kutosha kwa kutinga dimbani! haoni adhabu ya kuwekwa lupango kama ni shida kwake kazi yake aliyo taka kuifanya kafanya! kiukweli wadau vyombo vya usalama havipo makini coz kwanza kabisa kumuhoji tuu huyu jamaa ni kitendo cha masaa kwa wataalamu kweli wanaelewa mara moja tu dhamira ya huyu jamaa ilikuwa nzuri au mbaya.wangekuwa kweli ni wataalamu wa kuchunguza maswala ya kiusalama huyu jamaa wangemuachia cku ile ile! na hata FIFA wakifuatilia wanapewa tu info kwamba tumechunguza huyu jamaa hakuwa na nia mbaya hvo tume mrelease!!! atakaa ndani week 1 maskini tena utaskia kaundiwa tume!! tobah
 
wewe unae mjua vyema laurent Masha si utueleze yu koje, vinginevyo acha majungu!
Kama wewe humjui utendaji wake basi hauko well informed na mambo ya nchi hii, soma hata ile thread inayoelezea mahojiano yake Clouds alikoshindwa hata kujua Idadi ya magereza na hata data zingine kama waziri. Unajua maana ya neno majungu au unaandika tuu!
 
Back
Top Bottom