Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Mimi ni mshabiki mkubwa wa soka ya hapa Tanzania hali kadharika kutokana na utandawazi uliopo sasa na napenda pia soka ya nje ya Tanzania. Lakini kubwa nimekuwa nikifatilia kwa ukaribu mwenendo wa timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars). Kwa maoni yangu sielewi hasa kile wenzetu walipopewa dhamana ya kuendesha michezo nchini ikiwemo soka kama wanajua wanachokifanya. Tumekuwa wepesi wa kutamani mafanikio bila kuyatokea jasho. maneno mengi yanazungumzwa na viongozi wa vyama vya soka kuanzia ngazi ya wilaya, mkoa hadi taifa kuwa eti soka ya Tanzania imekuwa, mimi nasema hapana imeshuka tena kwa kasi kubwa ni kama gari iliyoshindwa kupanda mlima ikarudi nyuma.
Kwa maoni yangu hebu watanzania tuamke na tuwe serious na kile tunachotamani kufanikiwa nacho. Katika soka msingi wa mafanikio ni mipango ya kuandaa timu za watoto na vijana ambao mwishowe ndio hao huingia timu ya taifa. Siamini katika kubadirisha makocha kama nguo kuwa ndio suluhu. Hapa hata tungeletewa Sir Alex Furgeson, Jose Morinho au Carlo Ancelloti hakuna kipya kwani tatizo ni msingi mbovu. Karibu 80% ya wachezaji waliopo sasa katika timu a taifa ni wachezaji wasio na uwezo na kasi ya kucheza mpira wa sasa. Bila kubadirisha mitazamo yetu ili kujenga msingi imara na endelevu taifa stars itaendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu kama alivyowahi kusea raisi mstaafu wa awamu ya pili alhaji Ali HAsani Mwinyi kila mtu anajifunzia kunyoa kwetu. Naongea hili kama mtanzania ninayekerwa na hali ya timu yetu ya taifa. Viongozi wabadirike na kuwa na mtazamo chanya. Sasa hivi dunia imekuwa kama kijiji habari na mamb mbali mbali tunayapata kwa urahisi. Inashamgaza sana licha ya sasa hivi taifa stars kuwa na wafadhili wengi na wanaotoa fedha nyingi timu inadorora kila uchao. Miaka ya 80 ambapo suala la timu ya taifa walitupiwa FAT bado mpira ulionekana kiasi cha timu kukata tiketi kucheza mashindano ya Afrika.
Tusipoamka wenyewe hakuna atakayekuja kutuamsha tutabaki kubadirisha makocha tukidhani wao ndio wanaocheza mpira na kuleta mafanikio......naishi hapa kwa leo hebu tujadili wapenda soka.
Kwa maoni yangu hebu watanzania tuamke na tuwe serious na kile tunachotamani kufanikiwa nacho. Katika soka msingi wa mafanikio ni mipango ya kuandaa timu za watoto na vijana ambao mwishowe ndio hao huingia timu ya taifa. Siamini katika kubadirisha makocha kama nguo kuwa ndio suluhu. Hapa hata tungeletewa Sir Alex Furgeson, Jose Morinho au Carlo Ancelloti hakuna kipya kwani tatizo ni msingi mbovu. Karibu 80% ya wachezaji waliopo sasa katika timu a taifa ni wachezaji wasio na uwezo na kasi ya kucheza mpira wa sasa. Bila kubadirisha mitazamo yetu ili kujenga msingi imara na endelevu taifa stars itaendelea kuwa kichwa cha mwendawazimu kama alivyowahi kusea raisi mstaafu wa awamu ya pili alhaji Ali HAsani Mwinyi kila mtu anajifunzia kunyoa kwetu. Naongea hili kama mtanzania ninayekerwa na hali ya timu yetu ya taifa. Viongozi wabadirike na kuwa na mtazamo chanya. Sasa hivi dunia imekuwa kama kijiji habari na mamb mbali mbali tunayapata kwa urahisi. Inashamgaza sana licha ya sasa hivi taifa stars kuwa na wafadhili wengi na wanaotoa fedha nyingi timu inadorora kila uchao. Miaka ya 80 ambapo suala la timu ya taifa walitupiwa FAT bado mpira ulionekana kiasi cha timu kukata tiketi kucheza mashindano ya Afrika.
Tusipoamka wenyewe hakuna atakayekuja kutuamsha tutabaki kubadirisha makocha tukidhani wao ndio wanaocheza mpira na kuleta mafanikio......naishi hapa kwa leo hebu tujadili wapenda soka.