punainen-red
JF-Expert Member
- Nov 18, 2010
- 1,731
- 450
Dhaifu afunge safari akawaombe wawekezaji waje wapigane! Hivi raia wa Tz apigane kwa ajili ya nini hasa???
Nimejiuliza sana swali hili bila majibu. Nisaidieni.
Mwaka 1978 tuliingia vitani na Uganda chini ya Idd Amin, lakini tulipambana kama Taifa vita ile kwa pamoja yaani viongozi wetu, makamanda, askari, Taasisi mbalimbali na Raia wote hadi tukashinda.
Sasa hivi hatuna tena maelewano ya aina ile. Tunachokiona ni uhasama kati Bunge na Serikali, Serikali na Raia wake, Taasisi na Taasisi na hata Askari na Raia. Ufisadi umeshika kasi ndani ya Taasisi muhimu za Umma kiasi kufikia kununua vifaa vya kijeshi vinavyodhaniwa kuwa viko chini ya kiwango (fake) hasa tukikumbuka vitu kama Helicopter zinazoanguka hovyo na mabomu yanayolipuka hovyo.
Jee kwa hali kama hiyo, ikitokea nchi jirani kushambulia mipaka yetu tunao uwezo wa kuhimili mapigo kama ule wa mwaka 1978 kama Taifa? Ama tutaita wawekezaji wa kijeshi kutulindia mipaka yetu huku sisi tukiendelea kupiga soga la malumbano?
Ahhh!! Hapa Kichapo kwa kwenda Mbele kwani mafisadi wameshajenga New Jesey
Hilo halitakuwa jambo la kutuumiza kichwa sisi watanzania bali itakuwa vita ya nchi zote zenye uwekezaji wa kifisadi hapa Tanzania kupitia Makampuni yao ili kutetea maslahi yao. Tena nahisi Marekani kaenda Malawi kuchagiza hilo maana tunajifanya tumemsahau na kumkaribisha mchina kwa kishindoNimejiuliza sana swali hili bila majibu. Nisaidieni.
Mwaka 1978 tuliingia vitani na Uganda chini ya Idd Amin, lakini tulipambana kama Taifa vita ile kwa pamoja yaani viongozi wetu, makamanda, askari, Taasisi mbalimbali na Raia wote hadi tukashinda.
Sasa hivi hatuna tena maelewano ya aina ile. Tunachokiona ni uhasama kati Bunge na Serikali, Serikali na Raia wake, Taasisi na Taasisi na hata Askari na Raia. Ufisadi umeshika kasi ndani ya Taasisi muhimu za Umma kiasi kufikia kununua vifaa vya kijeshi vinavyodhaniwa kuwa viko chini ya kiwango (fake) hasa tukikumbuka vitu kama Helicopter zinazoanguka hovyo na mabomu yanayolipuka hovyo.
Jee kwa hali kama hiyo, ikitokea nchi jirani kushambulia mipaka yetu tunao uwezo wa kuhimili mapigo kama ule wa mwaka 1978 kama Taifa? Ama tutaita wawekezaji wa kijeshi kutulindia mipaka yetu huku sisi tukiendelea kupiga soga la malumbano?