Taifa likiingia vitani leo,Itakuwaje?

Dhaifu afunge safari akawaombe wawekezaji waje wapigane! Hivi raia wa Tz apigane kwa ajili ya nini hasa???
 
Nimejiuliza sana swali hili bila majibu. Nisaidieni.

Mwaka 1978 tuliingia vitani na Uganda chini ya Idd Amin, lakini tulipambana kama Taifa vita ile kwa pamoja yaani viongozi wetu, makamanda, askari, Taasisi mbalimbali na Raia wote hadi tukashinda.

Sasa hivi hatuna tena maelewano ya aina ile. Tunachokiona ni uhasama kati Bunge na Serikali, Serikali na Raia wake, Taasisi na Taasisi na hata Askari na Raia. Ufisadi umeshika kasi ndani ya Taasisi muhimu za Umma kiasi kufikia kununua vifaa vya kijeshi vinavyodhaniwa kuwa viko chini ya kiwango (fake) hasa tukikumbuka vitu kama Helicopter zinazoanguka hovyo na mabomu yanayolipuka hovyo.

Jee kwa hali kama hiyo, ikitokea nchi jirani kushambulia mipaka yetu tunao uwezo wa kuhimili mapigo kama ule wa mwaka 1978 kama Taifa? Ama tutaita wawekezaji wa kijeshi kutulindia mipaka yetu huku sisi tukiendelea kupiga soga la malumbano?

Umoja na Mshikamano wa Kitaifa kwa sasa hatuna kabisa na hii inatokana na Udhaifu wa Uongozi wa Juu hasa Rais ambaye ni Amiri Jeshi Mkuu wa Nchi. Tanzania inahitaji kiongozi mwenye uchungu na Nchi yetu ambapo kwa sasa hatuna viongozi wa namna hii. Tulionao wote ni viongozi wachumia tumbo tu. Natamani kama ningezaliwa Kenya au Rwanda.

Wanachoweza ni kupambana na haki za Wananchi bila sababu huku wakiunda sheria kandamizi bila sababu. Tukianzisha vita saa hizi lazima tuchapwe kichapo kitakatifu sana. Maana Nchi imejaa udini, ufisadi, watu kujichumia mali ya Nchi kama zao. Mungu utubariki tusipigwe mmpaka umoja na mshikamano utakapo fufuka tena.
 
Nimejiuliza sana swali hili bila majibu. Nisaidieni.

Mwaka 1978 tuliingia vitani na Uganda chini ya Idd Amin, lakini tulipambana kama Taifa vita ile kwa pamoja yaani viongozi wetu, makamanda, askari, Taasisi mbalimbali na Raia wote hadi tukashinda.

Sasa hivi hatuna tena maelewano ya aina ile. Tunachokiona ni uhasama kati Bunge na Serikali, Serikali na Raia wake, Taasisi na Taasisi na hata Askari na Raia. Ufisadi umeshika kasi ndani ya Taasisi muhimu za Umma kiasi kufikia kununua vifaa vya kijeshi vinavyodhaniwa kuwa viko chini ya kiwango (fake) hasa tukikumbuka vitu kama Helicopter zinazoanguka hovyo na mabomu yanayolipuka hovyo.

Jee kwa hali kama hiyo, ikitokea nchi jirani kushambulia mipaka yetu tunao uwezo wa kuhimili mapigo kama ule wa mwaka 1978 kama Taifa? Ama tutaita wawekezaji wa kijeshi kutulindia mipaka yetu huku sisi tukiendelea kupiga soga la malumbano?
Hilo halitakuwa jambo la kutuumiza kichwa sisi watanzania bali itakuwa vita ya nchi zote zenye uwekezaji wa kifisadi hapa Tanzania kupitia Makampuni yao ili kutetea maslahi yao. Tena nahisi Marekani kaenda Malawi kuchagiza hilo maana tunajifanya tumemsahau na kumkaribisha mchina kwa kishindo
 
Haaaapa tuombe tu vita istokee kwani tutachapwa hadi tutawaliwe na na kukaliwa juu na Malawi (Joyce Banda). Mwaka 1978 tuligangamala vijana wa mujibu wa sheria JKT, leo sijui mtampeleka nane frontline labda Nape na Ridhiwani
 
......ni mke na mume wapumbavu tu ndio watakao endelea na malumbano kuhusu uaminifu ktk ndoa yao huku wakimuona jambazi akivunja mlango na wasifanye kitu........
 
Back
Top Bottom