mariavictima
Senior Member
- Jul 8, 2010
- 179
- 39
True story hasa ma-Mercury(Hg) wa Iringa na Morogoro ni wanga sana!
Uchawi hauna kabila. Mimi mwenyewe yamewahi kunikuta. Nilikuwa na bahati mbaya ya ajabu kuwa na ma-HG watatu mfululizo wote wachawi. Wa kwanza alikuwa msukuma, alikaa kidogo na tulipomgundua na kuanza kumpeleka kwenye maombi akatoroka. Wa pili alikuwa Mnyaturu kutoka Singida. Huyu alianza kujieleza mwenyewe kabla hata hatujamgundua. Tulimpeleka kwenye maombi lakini ilipokaribia kufunguliwa naye akatoroka. Huyu alikuwa kila siku usiku anakwenda kwao Singida na kurudi. Alikuwa anachanjwa mwili mzima bila kumuona mchanjaji. Siku nyingine alikuwa anapigwa mihuri ya moto bila kumuona aliyempiga. Tulipomdadisi sana akasema kuwa bibi yake ni mchawi na anataka kumkabidhi vibuyu japo yeye hataki. Naye alipoona maombi yamezidi akatoroka. Wa tatu ndiye alikuwa balaa kabisa. Huyu alikuwa mchaga. Nusura aniulie kijana wangu wa sekondari. Tulipomgundua alikiri na kuweka ushahidi wa maandishi jinsi ambavyo anashirikiana na wachawi akiwemo mama yake mzazi, jinsi wanavyofanya kikao usiku nyumbani kwangu, na hata aliwataja watu wa huko kijijini Moshi ambao wamewala nyama. Pamoja na kumpeleka maombi, ilinitisha nikaamua kumrudisha kwao.
Nimewahi pia kukaa na ma-HG wa Iringa na Morogoro na walikuwa wasichana wazuri tu, wala hawakuwa na mambo ya kichawi. Sasa hivi nina Mgogo and she is okay kwa kweli namshukuru Mungu. Lakini kabla yake nilikaa mwaka mzima bila HG kwa kuwaogopa. Cha muhimu ni kuwa tu waangalifu na kujitahidi kuwachunguza kwa kina na siyo kuwaamini asilimia mia moja.