Naelewa fika kuwa watu wengi wanafahamu kuwa jiji hili lina vibaka wa kutupwa, ila napenda kuwakumbusha watanzania wenzangu hasa wanaomiliki magari kuwa mara wanaposindikiza ndugu au jamaa zao na wakalazimika kuingia ndani ya standi ya mabasi yanayokwenda mkoani(ubungo) wahakikishe kuwa wameacha mtu wa kuangalia gari. Leo hii nilidamka mapema kumsindikiza ndugu yangu, niliamini kuwa nimepaki gari langu kwenye eneo lenye usalama, haikuwa hivyo kwani niliporudi nilikuta site mirror imeshanyofolewa, hivyo kulazimika kwenda gerezani ili kupata nyingine. Nimeona niwakumbushe watanzania wenzangu kuwa hali ya usalama standi ya Ubungo ni ndogo sana hivyo pamoja na kuwa gari lako lina alarm hiyo haitazuia vibaka waliosheheni kuchukua wanachotaka kwenye gari yako. hivyo umakini wa hali ya juu unahitajika unapoingia kwenye stand hiyo aidha hao wanaojiita wanausalama kama wanapitia humu JF nawaomba waimalishe ulinzi kweenye stendi hiyo kwani uhalifu upo wazi kabisa na hakuna mtu anayejali.