Tahadhari ya Polisi na RC Morogoro kuhusu Hukumu Kesi ya Uchaguzi kesho

Mkuu ccm kuna kitu inakitafuta kwenye nchi hii .
Aisee nikweli kabisa, ,maana mengine yanayofanyika hatujawai ona vpindi vyote vilivyopita ,tunavionaga tu kwa nchi za wenzetu huko majirani kusigina democracy, mungu atuepushe tusifike huko,,,,,maana kuna makesi makubwa mengi yaliyopita tena kwenye mahakama za juu, ila sijawai kuona inatolewa tahadhali kabla ya hukumu, labda ni taratibu mpya lakini hatuwezi jua
 
Hakuna haja ya kulia na kuomboleza,

Wewe unapofunga mlango huu, Mungu hufungua Milango mingine kumi kwa yule unayemfungia.

Na mimi nasema, Hukumu itoke na ikibidi Wabunge wa Chadema wote washindwe kesi hizo, mean WAVULIWE UBUNGE. Hapo ndipo utakapoona ni namna gani siasa za Nchi hii zinaendeswa.!!

Unajua nini, toka mwaka jana hakuna mikutano yoyote ya nguvu iliyofanywa na Upinzani kwa kisingizio kisichoeleweka. Kwahiyo ikitokea fursa hiyo ndipo tutakapopata midomo ya kusema.

Salamu zishatumwa kwa Mwenyekiti wa Kitongoji hapo juzi... You what iam saying??? !!!

BACK TANGANYIKA
 
Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro leo limetoa tahadhari kuwa halitasita kuchukua hatua kali kwa vikundi vya wanasiasa vitakavyokusanyika kesho kwenye mahakama ya Morogoro kusikiliza hukumu ya keshi ya uchaguzi kwenye majimbo ya Kilombero pamoja na Mrimba ambapo hukumu zote mbili zinatolewa Ijumaa wiki hii.

Wakati Polisi ikisema hivyo, RC nae amesema yoyote ambaye kesho hatakubaliana na uamuzi wa mahakama kuu akakate rufaa na asilete manung'uniko yasiyotarajiwa na wala asifanye mkusanyiko wowote ule kesho Ijumaa .

Kauli za wote hawa wawili binafsi zinanipa shaka kuwa kulikoni waanze na tahadhari za aina hii na kujipanga mapema kuonya wanasiasa kwa hukumu ambayo haijatoka. Je wanajua hukumu ina nini ndani yake hadi wameamua kutoa tahadhari hii?

Kwanini Mahakama isitoe tahadhari badalala yake Polisi na RC ndio watoe tahadhari hii? Kwanini itokee Morogoro tu na haijawahi kutokea mahala pengine popote tahadhari za aina hii?

Nimejiuliza sana na kesho nategemea bao la mkono Mahakamani.
Ndugu jifunze kukamilisha habari. Hao wabunge hawana majina?
 
Jeshi la Polisi Mkoani Morogoro leo limetoa tahadhari kuwa halitasita kuchukua hatua kali kwa vikundi vya wanasiasa vitakavyokusanyika kesho kwenye mahakama ya Morogoro kusikiliza hukumu ya keshi ya uchaguzi kwenye majimbo ya Kilombero pamoja na Mrimba ambapo hukumu zote mbili zinatolewa Ijumaa wiki hii.

Wakati Polisi ikisema hivyo, RC nae amesema yoyote ambaye kesho hatakubaliana na uamuzi wa mahakama kuu akakate rufaa na asilete manung'uniko yasiyotarajiwa na wala asifanye mkusanyiko wowote ule kesho Ijumaa .

Kauli za wote hawa wawili binafsi zinanipa shaka kuwa kulikoni waanze na tahadhari za aina hii na kujipanga mapema kuonya wanasiasa kwa hukumu ambayo haijatoka. Je wanajua hukumu ina nini ndani yake hadi wameamua kutoa tahadhari hii?

Kwanini Mahakama isitoe tahadhari badalala yake Polisi na RC ndio watoe tahadhari hii? Kwanini itokee Morogoro tu na haijawahi kutokea mahala pengine popote tahadhari za aina hii?

Nimejiuliza sana na kesho nategemea bao la mkono Mahakamani.

Wamesha jua kitakacho tokea. Kwa hiyo ukiona hivyo mi dhuluma imeshapamgwa kwamba hao wabunge lazima ubunge wao utenguliwe.
 
Jana nimeshangaa sana kumsikia Rafiki yangu Kebwe Stephen Kebwe
Nilitazama kupitia Azam Tv on line nikiwa huku Ughaibuni...Ajabu ni kuwa RC na RPC wamesoma matamko yanayoshabihiana sana sana kana kwamba yameandikwa na mtu mmoja.

Lakina namna RC ambaye ni kada wa CCM na mbunge aliyepigwa chini Jimbo la Serengeti ni kama tayari anajuwa hukumu...Maana anasisitiza kuwa kuna watu hupenda sana kuandamana au kuja kusikiliza kesi,mimi kwenye mkoa wangu hakuna kukusanyika wala kujaa kusikiliza kesi..Sasa nikajiuliza,kwani siku hizi hata kusikiliza kesi Mahakamani ni hisani ya Mkuu wa Mkoa??

Namkumbuka Kabwe wakati akiwa MUCHS siku hizi MUHAS...Tulimpigania sana awe Rais wa Serikali ya MUCHS wakati huo DARUSO ikiwa moja kati ya Mlimani na Muhimbili...Alipita sbb ya misimamo yake,sijui ile hali na uelewa ule wa bila unafiki umeishia wapi??Aibu sana hii...

Kuna mahali hii nchi CCM wanataka kutupeleka...Watakipata tu wanachokitafuta
 
Acha kutudharau sisi waafrika, kwa sababu zako za kisiasa, rangi nyeusi tumepewa na mungu.
Weusi wetu ni halali yetu na ndivyo Mungu alivyotuumba. Kama ni dharau alishaifanya Mungu kwa alivyotuumba. Usijihisi kuwa wewe ni bora wakati ulishadharauliwa na Mungu.
 
Miaka 23 ya kupokea ruzuku na msaada kwa ndume wenu EU hata banda hamna

Kwanza nikujuze kuwa mm siyo mwanachama wa chama chochote cha siasa, ila ninachokijua hata ccm haijajenga ofisi mpya, inazodai kuwa ni ofisi zake zilijengwa na wanchi wakati wa chama kimoja, hivyo kuvichagiza vyama vingine kuacha kueneza sera zao na kutumia resources walizonazo kujenga ofisi siyo ajenda mwafaka kwa sasa.ndiyo maana kuna mikoa mingi imeanzishwa lakini majengo yanayotumiwa na ccm ni yaleyale yalikuwapo hivyo pamoja na ccm kupata mgao mkubwa zaidi wa ruzuku bado na wao shida ni ileile, lakini ujue kuendesha upinzani ktk nchi kama hii ni kazi ngumu sana. lakini kwa manufaa ya maendeleo ya nchi lazima upinzani UWEPO.
 
Kwanza nikujuze kuwa mm siyo mwanachama wa chama chochote cha siasa, ila ninachokijua hata ccm haijajenga ofisi mpya, inazodai kuwa ni ofisi zake zilijengwa na wanchi wakati wa chama kimoja, hivyo kuvichagiza vyama vingine kuacha kueneza sera zao na kutumia resources walizonazo kujenga ofisi siyo ajenda mwafaka kwa sasa.ndiyo maana kuna mikoa mingi imeanzishwa lakini majengo yanayotumiwa na ccm ni yaleyale yalikuwapo hivyo pamoja na ccm kupata mgao mkubwa zaidi wa ruzuku bado na wao shida ni ileile, lakini ujue kuendesha upinzani ktk nchi kama hii ni kazi ngumu sana. lakini kwa manufaa ya maendeleo ya nchi lazima upinzani UWEPO.
Dodoma convention center imejengwa wanananchi
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom