Maxence Melo
JF Founder
- Feb 10, 2006
- 4,230
- 13,415
Tahadhari
Kuanzia: Tarehe 30 Aprili 2012 Mpaka: Tarehe 04 Mei 2012
Aina ya Tukio Linalotarajiwa: Mvua Kubwa (zaidi ya milimita 50 katika kipindi cha saa 24 kila siku)
Kiwango cha Uhakika: 80%
Eneo: Mikoa ya Dar es Salaam, Mtwara, Lindi, Tanga, Morogoro, Pwani na visiwa vya Unguja na Pemba
Maelezo: Kuimarika kwa mgandamizo mdogo wa hali ya hewa katika maneo ya Bahari ya Hindi yanayopakana na Pwani ya kaskazini.
Angalizo: Wakazi wa maeneo hatarishi, watumiaji wa Bahari na nchi kavu wanashauriwa kuchukua Tahadhari. Aidha Taasisi zinazohusika na Maafa zinashauriwa kuchukua hatua stahiki.
Maelezo ya Ziada: Mamlaka inaendelea kufuatilia mifumo ya hali ya hewa na kutoa taarifa kila itakapobidi.
IMETOLEWA NA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA