NO04
JF-Expert Member
- Jun 29, 2015
- 1,754
- 1,232
wakat naww naona unatafta...(kidding)HUYO DADA ANATUAIBISHA
wakat naww naona unatafta...(kidding)HUYO DADA ANATUAIBISHA
Me Simu sikupi yani umevaa Nguo za Gucci Bag la Louis Viutton Gaun la Dolce Gabanna halafu una Samsung ya Laki, 5 eti huna vocha Ma Sista Duu wezi ndo mana staki Shobo Nao
na geneza atanunua tu!!Pole ila usiige hiyo mbinu cha msingi shusha dau ukipata wengi utanunua ya kwanko
Hio style ya wizi mbona ya siku nyingi?!Juzi nimeenda Mlimani city kwa ajili ya kujipatia huduma katika maduka yaliopo pale, baada ya mihangaiko ya mda mrefu kutafuta ninachokitaka bila ya mafanikio, nikaamua kupata chakula katika mgahawa wa mary brown, wakati nasubiri chakula na kinywaji nilichoagiza, ghafla akatokea dada mmoja mrembo na alievaa nguo zinazoonekana za gharama kidogo alipofika alikuja kukaa meza karibu na yakwangu na kuanza kuchezea chezea simu, nikashangaa kwa nini hakuenda kutoa oda na amekuja straight kukaa!!!
mara akaniomba simu na hapa ninamnukuu "kaka samahani naomba kidogo uniazime simu nimpigie rafiki yangu ananitafuta na mm simu yangu imeisha chaji" kwa jinsi alivyo sikuwa na mashaka nae hata chembe, nikazama mfukoni na kutoa simu, kidogo akaanza kunyanyuka na kusogea kaunta akiwa na simu yangu kama anaenda kuagiza chakula akiwa bado anaongea kwa kutumia simu yangu niliompa wakati wote huo alikuwa anaongea na huku kila baada ya sekunde kadhaa ananiangalia mimi, na mimi kwa kumtoa wasi wasi nikaamua kuangalia upande mwengine ghafla kama niliepitiwa na mshangao kidogo sikumuona tena machoni mwangu,
nilichokifanya ni kukimbia mbio nikiwacha chakula mezani na kukimbilia nje kabisa ya eneo lile, nilienda kumkamata nje kabisa akijiandaa kupanda bodaboda. Nilikwapua simu yangu na kurudi ndani kuendelea na mambo yangu na sikutaka ugomvi. Tuchukue tahadhari sana wakuu.
Ni mdada mrefu kidogo mweupe, miaka kati ya 20 na 25, chini ya midomo ametoga na ana kito flani hivi cha silver, neno moja anaweka english, anavaa miwani rangi kama ya kahawia.
Me Mara nying nawapaga Vocha Simu yangu hapana aisee kuna mmoja jama tulikutana temeke hospital akaomba simu apige nikampa vocha mana nilihis jambazi
Roho mbaya mwingine anakudanganya imezima chaji
Mhhhh....Pole sana mkuu.
Wizi ni wa zamani ila umeboreshwa kidogo.
Mkuu....Miss natafuta kinachonishangaza kwa jinsi alivyo mrembo hata kama atakuwa na vyeti feki akienda kuomba kazi ofisini kwa mwanaume yoyote rijali atapata tu. Kwa nini anaamua kufanya kazi ile?
Kwahiyo.....magu ndio kasababisha haya yote kubana kila sekta mabosi sasa hv hawanunui dada kaona bora atafute ujanja wakuishi twn
Mhhhh.....Nyani Ngabu huenda anamjua kwani Ni mteja mzuri Sana wa pale jimmy jones na Mary Brown
Wanaume wa huko.. , yawezekana akasema aliacha chakula mezani, kumbe aliacha chips...Me mecheka hapo ulipoacha chakula tu.
Lol
Hii sasa dharau...Wizi mpya? Ebu badili title
Hivi.....Pole kk