Tayari serikali ya ccm iko mahututi. Ni ufisadi umewafikisha hapo walipo kiasi kwamba hawana hoja za kuwadanganya wananchi kuhusu ugumu wa maisha. Wananchi wanaelewa kinachoendelea. Lakini nionavyo mimi: Sasa watapata mahali pa kupumulia! Usanii wa kisiasa utatungwa ili kuwadanganya wananchi wasio na uelewa mpana kwamba ugumu wa maisha tulio nao ni kwa sababu ya kukataa kuruhusu ushoga ili tupate misaada! Subirini tu mtazisikia kauli za namna hiyo hivi karibuni.