chiko
JF-Expert Member
- Feb 24, 2010
- 580
- 245
Showstopper... ni wale warembo ambao, wakipita barabarani waaacha waume domo zege, waume lazima wapinde shingo. Mwenyezi mungu kawaumba kwa MAKINI zaidi, nao wanajua, huongezea madaha. Warembo dizaini hii ni hatari sana sana!!!.
Napenda kutoa kisa kilinipata na pia ni ushauri kwa kina kaka, kwani damu ikiwa yachemka mtu akili hutupa jaani.
Ilikuwa wakati kama huu wa December, miaka kadhaa iliopita, kazini kwetu aliandikwa msichana mmoja 'Showstopper', kama mpokezi wa wageni na secretari. Wakati huo mimi sijao na damu yanichemka. Katokea mzee mmoja twafanya nae kazi, katika maongezi ya kazini, akatuasi..."Vijana wangu, mimi ni meishi sana na nimeona mengi, Wasichana kama huyu 'Showstopper', mchunge sana, watu hawa ni balaa!!.
Mimi nikiwa kwenye mashindano na wenzangu, nikajua hawanipati, ushauri nikatupa mbali, nikaanza kunyemelea, muda haukupita, 'showstopper' akawa wangu, tukirusha roho na kufunga mwaka. Haikuchukua muda, mimi pia nilikua si kidogo, nikaona mbio zake si wezi, nikamwachilia.
Kumbe Bosi wetu nae alikua ananyemelea, akaingia kwenye mtego!, Bosi alipelekwa mbio, kiasi hata kutumia hela za kampuni kumstarehesha kimwana. Mwisho Bosi na 'Showstopper' walipatikana na scandal ilio wafuta kazi.
Hii hadithi yoote, ni kwa masharobaro, wasichana hawa 'Showstopper' ni moto wakuotea mbali...chungeni sana , waweza kukupa kifo cha haraka, akufanye uibe ama kuachishwa kazi!!!
MWAKA MPYA MWEMA!!!!!
Napenda kutoa kisa kilinipata na pia ni ushauri kwa kina kaka, kwani damu ikiwa yachemka mtu akili hutupa jaani.
Ilikuwa wakati kama huu wa December, miaka kadhaa iliopita, kazini kwetu aliandikwa msichana mmoja 'Showstopper', kama mpokezi wa wageni na secretari. Wakati huo mimi sijao na damu yanichemka. Katokea mzee mmoja twafanya nae kazi, katika maongezi ya kazini, akatuasi..."Vijana wangu, mimi ni meishi sana na nimeona mengi, Wasichana kama huyu 'Showstopper', mchunge sana, watu hawa ni balaa!!.
Mimi nikiwa kwenye mashindano na wenzangu, nikajua hawanipati, ushauri nikatupa mbali, nikaanza kunyemelea, muda haukupita, 'showstopper' akawa wangu, tukirusha roho na kufunga mwaka. Haikuchukua muda, mimi pia nilikua si kidogo, nikaona mbio zake si wezi, nikamwachilia.
Kumbe Bosi wetu nae alikua ananyemelea, akaingia kwenye mtego!, Bosi alipelekwa mbio, kiasi hata kutumia hela za kampuni kumstarehesha kimwana. Mwisho Bosi na 'Showstopper' walipatikana na scandal ilio wafuta kazi.
Hii hadithi yoote, ni kwa masharobaro, wasichana hawa 'Showstopper' ni moto wakuotea mbali...chungeni sana , waweza kukupa kifo cha haraka, akufanye uibe ama kuachishwa kazi!!!
MWAKA MPYA MWEMA!!!!!