LINCOLINMTZA
JF-Expert Member
- Mar 15, 2011
- 1,639
- 516
Ndugu wana JF, Nimekuwa nikifuatilia tafsiri ya kujivua magamba kwa CCM ndani ya jamvi letu, naona wengi wetu tunaangalia kwa mtazamo wa hasi sana.
Mwenyekiti wa CCM taifa, Mh JK alitangaza rasimi kuwa CCM inahitaji kujivua gamba lake tarehe 5.2.2011 katika sherehe za CCM zilizofanyika Dodoma. Lengo lake lilikuwa ni kukibadilisha Chama Cha Mapinduzi ili kiwe na mvuto zaidi kwa wananchi. Na hilo halikupata publicity sana.
Katika vikao vya NEC na CC, CCM iliamua kuvunja sekreteriati nzima iliyokuwa chini ya Yusuph Makamba, uamzi ambao ni mngumu kwa kweli ikifuatiwa na kuwataka wanaodaiwa mafisadi kuchukuliwa hatua kama kuvuliwa nyazifa ndani ya chama. Haya maamuzi ndo yaliyopata publicity kubwa sana.
Pamoja na mambo yote hayo, wanajamvi wengi wamekuwa wakitoa tafsiri tofauti kwa kile JK alichokisema "Kujivua gamba" kwa kulinganisha na nyoka na kusahau kwamba huo ni msemo wa kiswahili wa kawaida kabisa. Mimi nafikiri tujadili zaidi lengo la kujivua gamba kwa taifa na siyo kuwa na tafsiri ya kila mtu bila kujali ushambiki.
Kama mtu hajaelewa maana ya kujivua gamba kwa CCM, ni vizuri kuwauliza wao wenyewe waseme walikuwa wanamanisha nini kisha tujadili ujumbe na siyo tafsiri potofu. Naomba kutoa hoja.
Mwenyekiti wa CCM taifa, Mh JK alitangaza rasimi kuwa CCM inahitaji kujivua gamba lake tarehe 5.2.2011 katika sherehe za CCM zilizofanyika Dodoma. Lengo lake lilikuwa ni kukibadilisha Chama Cha Mapinduzi ili kiwe na mvuto zaidi kwa wananchi. Na hilo halikupata publicity sana.
Katika vikao vya NEC na CC, CCM iliamua kuvunja sekreteriati nzima iliyokuwa chini ya Yusuph Makamba, uamzi ambao ni mngumu kwa kweli ikifuatiwa na kuwataka wanaodaiwa mafisadi kuchukuliwa hatua kama kuvuliwa nyazifa ndani ya chama. Haya maamuzi ndo yaliyopata publicity kubwa sana.
Pamoja na mambo yote hayo, wanajamvi wengi wamekuwa wakitoa tafsiri tofauti kwa kile JK alichokisema "Kujivua gamba" kwa kulinganisha na nyoka na kusahau kwamba huo ni msemo wa kiswahili wa kawaida kabisa. Mimi nafikiri tujadili zaidi lengo la kujivua gamba kwa taifa na siyo kuwa na tafsiri ya kila mtu bila kujali ushambiki.
Kama mtu hajaelewa maana ya kujivua gamba kwa CCM, ni vizuri kuwauliza wao wenyewe waseme walikuwa wanamanisha nini kisha tujadili ujumbe na siyo tafsiri potofu. Naomba kutoa hoja.